Magufuli alichelewa kuwa Rais wetu

Apr 24, 2011
29
542
"JPM ALICHELEWA KUWA RAIS WETU"

Tulitakiwa kuwa na JPM kabla ya miaka 20 iliyopita. Magufuli alichelewa kuwa Rais wetu kwa katiba ya kifalme/kisultan tuliyonayo. Miaka 5 na miezi 5 ilituonyesha rangi za udikteta. Ingawa rangi hiyo haikufika kwa mtu mmoja mmoja, wapo walioguswa

Bado tulihitaji kuwa na JPM kwa miaka mingi au tuseme kwa lugha rahisi kabisa, JPM alichelewa kuwa Rais wetu. Ndiyo. Kabla ya JPM, kuna masuala mengi ya hovyo hatukuwahi kuyaona au kupitia katika siasa za nchi yetu, lakini katika uwepo wake tumeona masuala mengi ya kuogofya.

JPM alikuwa daktari bingwa wa propaganda. Aliweza kuwaaminisha watu uchumi wetu ni imara na ukuaji wake ni wa kadi kubwa, watu waliamini ingawa bado walikuwa maskini wa kutupwa, hawana huduma za kijamii katika maeneo yao, hawana miradi ya maendeleo na kipato chao ni duni.

JPM aliweza kuwaaminisha watu ndiye mtetezi wao, mtetezi wa wanyonge. Akawapa jina hilo, umaskini ukatiwa nakshi-nakshi. Watu wakaamini, na kumuita Rais wa wanyonge, na kila alipokwenda hakusita kueleza kwa sauti kwamba haoni mwingine wa kumaliza kazi yake isipokuwa yeye.

Watu hawakujali, hata kuhamisha Serikali Dodoma bila bunge kuketi na kupitisha fedha hizo, ununuzi wa ndege bila bunge kurudhia, ujenzi wa uwanja wa ndege Chato bila bunge kuketi na kuridhia matumizi ya fedha za umma. Watu waliaminishwa kwamba Magufuli hakosei, wanyonge waliamini

Waliothubutu kuhoji walionekana ni wenye chuki na JPM, wakaitwa majina mabaya. Wakaambiwa ni vibaraka wa mabeberu. Walioendeleza ukosoaji walitafutwa na kuitwa wachochezi, wakashtakiwa kwa makosa ya uchochezi, madawa ya kulevya, uhujumu uchumi, utakatishaji fedha, ugaidi.

Upendeleo ulishamiri. Ubaguzi wa kisiasa ulikuwa ni dhahiri. Magufuli aliwahi kufika Vwawa, Mbozi na kuwaambia wananchi kwamba walichagua upinzani (CHADEMA) sasa wasitarajie kamwe atawapa maendeleo, wamuulize masuala ya maendeleo huyo mbunge waliyemchagua kutoka upinzani.

JPM akiwa Kinyerezi anazindua mradi wa umeme alisema hawezi kupeleka chakula kwa mtoto wa kambo (upinzani) na wakati nyumbani kwake wanahitaji hicho chakula. Akiwa na maana kwamba walipochagua wapinzani ni watoto yatima hawezi kuhangaika nao kamwe. Huu ulikuwa ubinafsi.

Ben Saanane hajulikani hata alipo hadi leo. Ni marehemu au bado yupo hai? Sasa awepo hai tangu 2016 kwamba wanamtunza? Siyo Kweli. Ben Saanane alikuwa mkosoaji mkubwa wa Serikali ya Magufuli. Alikosoa vilivyo pia upatikanaji wa PhD ya Magufuli. Nyakati hizo ndizo alizopotezwa.

Wakati ndugu wa karibu na viongozi wa Chadema wakitumia kila mbinu kujua aliko Ben, Desemba 24, 2016 siku moja kabla ya sikukuu ya Krismas, mtu asiyejulikana aliingia katika akaunti yake ya Facebook na kufuta baadhi ya maandishi yake yaliyokosoa viongozi wa juu serikalini.

Akwilina Akwilini, mnakumbuka kisa cha binti huyu wa chuo cha NIT? Akiwa katika daladala akitoka chuoni, alilelengwa na risasi iliyotupwa na Askari Polisi waliokuwa wakizuia Maandamano ya wafuasi wa CHADEMA eneo la Mkwajuni, Kinondoni, Dar es Salaam wakiongozwa na Freeman Mbowe

Kilichofuata? Freeman Mbowe na viongozi wenzake wa CHADEMA walishtakiwa kwa makosa mengi ikiwepo la kusabsbisha mauaji ya Akwilina Akwilini. Walihukumiwa kwenda gerezani au kulipa faini. Watanzania walichangia faini hizo, Shilingi 350 milioni. Muuaji wa Akwilina akabaki mtaani.

Wanasiasa wa upinzani walifanya biashara ya kisiasa. Walisema wanaunga juhudi za JPM mkono. Wabunge waliacha ubunge na kuomba ubunge. Madiwani pia na hata mameya. Ilifanyika biashara haramu kuaminisha macho ya umma Kwamba JPM anakubalika na wanasiasa wa upinzani. UONGO.

Ni wakati wa JPM tumeshuhudia COVID-19, janga kubwa la Dunia, likiumiza watu na kuondoka na maisha ya watu, lakini ilikuwa ni jinai kwa mamlaka za afya kutoa takwimu za ugonjwa. Waliacha. Uchumi uliharibika kutokana na COVID-19 lakini ilikuwa jinai wahusika kusema vinginevyo.

Ni wakati wa JPM kulikuwa na jaribio la kufuta Tanganyika Law Society (TLS) ambayo imeanzishwa kwa Sheria. Kisa? Ni wakati ule Tundu Lissu aligombea u-Rais wa TLS, awali ilionekana ni taasisi ambayo watawala na dola waliitumia kwa matakwa yao. Ujio wa Tundu Lissu uliwakera.

Ni katika utawala wa JPM, Mbunge halali wa watu wa Singida Mashariki, Rais wa chama cha Mawakili, Tundu Antiphas Mughwai Lissu alishsmbuliwa kwa risasi nyingi Mji wa Serikali Dodoma akitoka bungeni na wahalifu hawajawahi kutafutwa kamwe kama alipigwa risasi mnyama.

AZORY Gwanda? Ni kati ya wengi waliotoweshwa na kupotezwa kabisa. AZORY alikuwa mwandishi wa habari, akiandaa makala kuhusu mauaji yaliyokuwa yakifanyika katika eneo la MKIRU (Mkuranga, Kibiti, Rufiji). Raia wengi waliuwawa na habari za kwanini wanauwawa hazikuwahi kujulikana

AZORY Gwanda akachukua jukumu la uandishi wa habari za uchunguzi, akaandaa makala. Vikosi vya usalama vikamkamata, vikaenda naye hadi shambani kwa mkewe, akawapa funguo za nyumbani, wakafanya upekuzi, wakabeba vifaa kazi na kuondoka na AZORY hadi leo tangu mwaka 2017

Mdude Mpaluka Said Nyagali, ni mfano mzuri wa madhila ya utawala wa kidikteta. Ametekwa mara mbili kwa sababu za kumkosoa JPM. Ameteswa na kushtakiwa kwa kesi ya madawa ya kulevya. Alishinda kesi Mahakamani na ikaonekana ni kesi ya uongo kumuumiza Mdude Nyagali.

Gavana wa benki kuu alijitokeza hadharani akadiriki kuita hazina ya taifa kwamba ni chungu cha Rais. Huu ulikuwa ni mwisho kabisa wa kuona wataalam wetu, wasomi na wabobezi wamefika mwisho wao wa kufikiri kwa kutumia kichwa sasa wanatetea nyadhifa zao kwa kumlamba miguu mtawala

Mawaziri walianza kumuita JPM kwa jina la "Mheshimiwa Mungu" hadharani. Mkuu wa Mkoa wa Tabora akasema "Mungu sasa amshukuru JPM kwa niaba ya watu wa Tabora". Wote hao ni wakristo. Walifikia kiwango cha mwisho kabisa cha upambe. Na JPM hakuwahi kuwakanya wapambe wake.

Paul Makonda akiwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam akivamia Kituo cha luninga cha Clouds TV kwa mitutu ya bunduki na Askari, siku mbili baadae, JPM anasema hawezi kupangiwa mamlaka yake, hivyo Makonda achape kazi na asisikilize maneno ya wananchi. Kiburi cha hali ya juu

Lengai Ole Sabaya sasa ni mfungwa. Anatumikia kifungo chake katika gereza la Kisingo. Kifungo cha miaka 30 gerezani, alihukumiwa kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha. Ana kesi nyingine ya uhujumu uchumi. Huyu alikuwa ni mteule wa JPM. Unaweza kuona aina ya wateule wake

Mbaya zaidi, uchaguzi mkuu wa 2020, uliharibiwa na mamlaka za serikali, wagombea wa upinzani walienguliwa, maeneo mengi CCM wakajitangaza washindi, wagombea wa upinzani hadi sasa wanazo kesi za uhujumu uchumi, mauaji na wapo gerezani kutokana na uchaguzi huo.

Ni uchaguzi huo umelifanya bunge kuwa la chama kimoja. Bunge halina hata kambi rasmi ya upinzani bungeni. Walipogundua kwamba hata kamati za PAC na LAAC lazima ziongozwe na wabunge wa upinzani, wakawaomba ACT wapokee ofa na wale wabunge 19 wakaingizwa bungeni. Haramu.

JPM akiwa madarakani, wabunge 19 wasiokuwa na uwakilishi wowote wa chama cha siasa au kutokana na takwa lolote la katiba, waliapishwa, wakaitwa wabunge halali kwa kuapishwa na hadi sasa wapo bungeni. Ni matendo ya aibu kubwa sana yenye kuonyesha alama kubwa za udikteta.

JPM ametusaidia sana wanasiasa wa upinzani. Sasa tumefahamu umuhimu wa kuondokana na katiba hii mbovu inayompa mamlaka ya kikatili Rais. Ni lazima tupate katiba inayoendana na matakwa ya umma katika mfumo wa kisiasa wa vyama vingi na siyo Rais. Katiba mpya ni muhimu sasa.

Mwenyekiti wa UVCCM wakati fulani, Heri James alisema Jukwaani kwamba wao (CCM) ndiyo wanaamua wapi wapeleka maendeleo na wapi wasipeleke na wasipopeleka hakuna kitu watafanywa na yeyote. Hili lilipaswa kukemewa na JPM kama kweli siyo kweli. Lakini ndiyo ulikuwa mtazamo wa JPM.

JPM ametusaidia sasa tunafahamu kwamba kuna wanasiasa wanafiki, waongo na wazandiki katika siasa za nchi yetu, ambao wapo tayari kuuza UTU wao, kwa watawala ili watimize haja ya nafsi na matamanio yao. Wanapenda kuwa na vyeo bila kujali mahitaji ya wananchi. Wabinafsi.

JPM ametusaidia kuwafahamu 'political mercenaries' ambao Mwalimu Nyerere alisema tuwatambue kwa jina la "Malaya wa kisiasa". Wanayo bei. Wanajiuza. Hawana uvumilivu na hawa ndiyo wengi walihamia CCM wakisema wanaunga mkono juhudi za Rais. Hii ni shukrani kwa JPM .

Wafanyabiashara, ambao walikuwa ni tabaka kubwa linalounga na kufadhili shughuli za CCM, waliguswa, Walipewa mashtaka ya uhujumu uchumi, walifilisiwa. Hili ni moja kati ya makundi yaliyoguswa moja kwa moja. Hata wavuvi waliona moto. Nenda Chato, waulize wavuvi, JPM safi??

JPM ametuonyesha kwamba kwa katiba hii ukiwa na wapambe wengi bungeni, unaweza kuamua kujiongezea muda wa kubaki madarakani kisheria kabisa kwa Bunge kupitisha mabadiliko ys sheria na kuondoa ukomo wa muhula na Muda wa kuwa Rais. Tulianza kusikia minong'ono na vitendo.

JPM kwa muda wa miaka 5 na miezi 5 tu, alitufungua jicho, tulipaswa kuwa naye kwa miaka 20 kabla ili atusaidie kuwafungua watu akili, macho, masikio. Alituonyesha mkono wa chuma ukiwa madarakani, tusirudi huko, tuitengeneze katiba ya nchi yetu, asipatikane Magufuli mwingine.

MMM, Martin Maranja Masese
 
Kwangu mimi naamini huyo JPM angekuwa Rais bora sana kuanzia mwaka 1977 mara baada tu ya kutengenezwa kwa hii katiba inayotumika mpaka sasa.

Kitendo cha yeye kuja miaka zaidi ya 40 baadaye, ndicho kilichotuletea mvurugano wa akili na nafsi baadhi ya Watanzania ambao hatukumsoma kuanzia mwanzo mpaka mwisho wa utawala wake.
 
Andiko limekaa kibavicha zaidi!
Hawa watu wa chadema wajinga sana. Hivi haya yanayoendelea sasa ndio wanayapenda?

Bora nyakati za Magufuli Ambazo kila mtanzania alijionea mwenyewe mambo makubwa aliyoyafanya. Kwa maendeleo ya watanzania wengi.

Nyie ni vipofu hamuoni kazi yenu ni vibarakatu na mnafuraia ugumu wa maisha wanaopitia watanzania kwa sasa.
 
Nilikuwa nasikia tu zamani madikteta wakiitwa wendawazimu, nikawa najiuliza sana hivi inakuwaje mtu anafikia madaraka hayo na awe na wazimu.

Kua uyaone, watanzania tulijionea rais anamwambia mwananchi live eti siku nyingine awe anaacha mavi yake nyumbani kwake?!!!

JPM alikuwa ni mtu, alikuwa mbaya na dikteta. CCM ni taasisi ina sifa zote za Magu
 
Hivi kuna nchi duniani imeshughulikia Covid-19 vizuri kuzidi Tanzania?
Imeshughulikia vizuri au imeshughulikiwa vizuri?

FB_IMG_1634495256250.jpg
 
Mzee Magufuli amesemwa sana, amesingiziwa maovu yote na kuchukiwa na wachache wenye sababu zao binafsi. Sasa hatuko naye tunaona Watanzania maisha wanayoishi lakini bado "wehu" fulani bado wanateseka na Marehemu. Binafsi na Watanzania hawa kwenye hii video tunamuombea mzee wetu aendelee kupumzika kwa amani.

Binadamu ndivyo walivyo, huwezi kupendwa na wote lakini siku ya msiba wake nadhani sote tuliona.


Continue resting in power Dr Magufuli my dady
 
"JPM ALICHELEWA KUWA RAIS WETU"

Tulitakiwa kuwa na JPM kabla ya miaka 20 iliyopita. Magufuli alichelewa kuwa Rais wetu kwa katiba ya kifalme/kisultan tuliyonayo. Miaka 5 na miezi 5 ilituonyesha rangi za udikteta. Ingawa rangi hiyo haikufika kwa mtu mmoja mmoja, wapo walioguswa

Bado tulihitaji kuwa na JPM kwa miaka mingi au tuseme kwa lugha rahisi kabisa, JPM alichelewa kuwa Rais wetu. Ndiyo. Kabla ya JPM, kuna masuala mengi ya hovyo hatukuwahi kuyaona au kupitia katika siasa za nchi yetu, lakini katika uwepo wake tumeona masuala mengi ya kuogofya.

JPM alikuwa daktari bingwa wa propaganda. Aliweza kuwaaminisha watu uchumi wetu ni imara na ukuaji wake ni wa kadi kubwa, watu waliamini ingawa bado walikuwa maskini wa kutupwa, hawana huduma za kijamii katika maeneo yao, hawana miradi ya maendeleo na kipato chao ni duni.

JPM aliweza kuwaaminisha watu ndiye mtetezi wao, mtetezi wa wanyonge. Akawapa jina hilo, umaskini ukatiwa nakshi-nakshi. Watu wakaamini, na kumuita Rais wa wanyonge, na kila alipokwenda hakusita kueleza kwa sauti kwamba haoni mwingine wa kumaliza kazi yake isipokuwa yeye.

Watu hawakujali, hata kuhamisha Serikali Dodoma bila bunge kuketi na kupitisha fedha hizo, ununuzi wa ndege bila bunge kurudhia, ujenzi wa uwanja wa ndege Chato bila bunge kuketi na kuridhia matumizi ya fedha za umma. Watu waliaminishwa kwamba Magufuli hakosei, wanyonge waliamini

Waliothubutu kuhoji walionekana ni wenye chuki na JPM, wakaitwa majina mabaya. Wakaambiwa ni vibaraka wa mabeberu. Walioendeleza ukosoaji walitafutwa na kuitwa wachochezi, wakashtakiwa kwa makosa ya uchochezi, madawa ya kulevya, uhujumu uchumi, utakatishaji fedha, ugaidi.

Upendeleo ulishamiri. Ubaguzi wa kisiasa ulikuwa ni dhahiri. Magufuli aliwahi kufika Vwawa, Mbozi na kuwaambia wananchi kwamba walichagua upinzani (CHADEMA) sasa wasitarajie kamwe atawapa maendeleo, wamuulize masuala ya maendeleo huyo mbunge waliyemchagua kutoka upinzani.

JPM akiwa Kinyerezi anazindua mradi wa umeme alisema hawezi kupeleka chakula kwa mtoto wa kambo (upinzani) na wakati nyumbani kwake wanahitaji hicho chakula. Akiwa na maana kwamba walipochagua wapinzani ni watoto yatima hawezi kuhangaika nao kamwe. Huu ulikuwa ubinafsi.

Ben Saanane hajulikani hata alipo hadi leo. Ni marehemu au bado yupo hai? Sasa awepo hai tangu 2016 kwamba wanamtunza? Siyo Kweli. Ben Saanane alikuwa mkosoaji mkubwa wa Serikali ya Magufuli. Alikosoa vilivyo pia upatikanaji wa PhD ya Magufuli. Nyakati hizo ndizo alizopotezwa.

Wakati ndugu wa karibu na viongozi wa Chadema wakitumia kila mbinu kujua aliko Ben, Desemba 24, 2016 siku moja kabla ya sikukuu ya Krismas, mtu asiyejulikana aliingia katika akaunti yake ya Facebook na kufuta baadhi ya maandishi yake yaliyokosoa viongozi wa juu serikalini.

Akwilina Akwilini, mnakumbuka kisa cha binti huyu wa chuo cha NIT? Akiwa katika daladala akitoka chuoni, alilelengwa na risasi iliyotupwa na Askari Polisi waliokuwa wakizuia Maandamano ya wafuasi wa CHADEMA eneo la Mkwajuni, Kinondoni, Dar es Salaam wakiongozwa na Freeman Mbowe

Kilichofuata? Freeman Mbowe na viongozi wenzake wa CHADEMA walishtakiwa kwa makosa mengi ikiwepo la kusabsbisha mauaji ya Akwilina Akwilini. Walihukumiwa kwenda gerezani au kulipa faini. Watanzania walichangia faini hizo, Shilingi 350 milioni. Muuaji wa Akwilina akabaki mtaani.

Wanasiasa wa upinzani walifanya biashara ya kisiasa. Walisema wanaunga juhudi za JPM mkono. Wabunge waliacha ubunge na kuomba ubunge. Madiwani pia na hata mameya. Ilifanyika biashara haramu kuaminisha macho ya umma Kwamba JPM anakubalika na wanasiasa wa upinzani. UONGO.

Ni wakati wa JPM tumeshuhudia COVID-19, janga kubwa la Dunia, likiumiza watu na kuondoka na maisha ya watu, lakini ilikuwa ni jinai kwa mamlaka za afya kutoa takwimu za ugonjwa. Waliacha. Uchumi uliharibika kutokana na COVID-19 lakini ilikuwa jinai wahusika kusema vinginevyo.

Ni wakati wa JPM kulikuwa na jaribio la kufuta Tanganyika Law Society (TLS) ambayo imeanzishwa kwa Sheria. Kisa? Ni wakati ule Tundu Lissu aligombea u-Rais wa TLS, awali ilionekana ni taasisi ambayo watawala na dola waliitumia kwa matakwa yao. Ujio wa Tundu Lissu uliwakera.

Ni katika utawala wa JPM, Mbunge halali wa watu wa Singida Mashariki, Rais wa chama cha Mawakili, Tundu Antiphas Mughwai Lissu alishsmbuliwa kwa risasi nyingi Mji wa Serikali Dodoma akitoka bungeni na wahalifu hawajawahi kutafutwa kamwe kama alipigwa risasi mnyama.

AZORY Gwanda? Ni kati ya wengi waliotoweshwa na kupotezwa kabisa. AZORY alikuwa mwandishi wa habari, akiandaa makala kuhusu mauaji yaliyokuwa yakifanyika katika eneo la MKIRU (Mkuranga, Kibiti, Rufiji). Raia wengi waliuwawa na habari za kwanini wanauwawa hazikuwahi kujulikana

AZORY Gwanda akachukua jukumu la uandishi wa habari za uchunguzi, akaandaa makala. Vikosi vya usalama vikamkamata, vikaenda naye hadi shambani kwa mkewe, akawapa funguo za nyumbani, wakafanya upekuzi, wakabeba vifaa kazi na kuondoka na AZORY hadi leo tangu mwaka 2017

Mdude Mpaluka Said Nyagali, ni mfano mzuri wa madhila ya utawala wa kidikteta. Ametekwa mara mbili kwa sababu za kumkosoa JPM. Ameteswa na kushtakiwa kwa kesi ya madawa ya kulevya. Alishinda kesi Mahakamani na ikaonekana ni kesi ya uongo kumuumiza Mdude Nyagali.

Gavana wa benki kuu alijitokeza hadharani akadiriki kuita hazina ya taifa kwamba ni chungu cha Rais. Huu ulikuwa ni mwisho kabisa wa kuona wataalam wetu, wasomi na wabobezi wamefika mwisho wao wa kufikiri kwa kutumia kichwa sasa wanatetea nyadhifa zao kwa kumlamba miguu mtawala

Mawaziri walianza kumuita JPM kwa jina la "Mheshimiwa Mungu" hadharani. Mkuu wa Mkoa wa Tabora akasema "Mungu sasa amshukuru JPM kwa niaba ya watu wa Tabora". Wote hao ni wakristo. Walifikia kiwango cha mwisho kabisa cha upambe. Na JPM hakuwahi kuwakanya wapambe wake.

Paul Makonda akiwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam akivamia Kituo cha luninga cha Clouds TV kwa mitutu ya bunduki na Askari, siku mbili baadae, JPM anasema hawezi kupangiwa mamlaka yake, hivyo Makonda achape kazi na asisikilize maneno ya wananchi. Kiburi cha hali ya juu

Lengai Ole Sabaya sasa ni mfungwa. Anatumikia kifungo chake katika gereza la Kisingo. Kifungo cha miaka 30 gerezani, alihukumiwa kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha. Ana kesi nyingine ya uhujumu uchumi. Huyu alikuwa ni mteule wa JPM. Unaweza kuona aina ya wateule wake

Mbaya zaidi, uchaguzi mkuu wa 2020, uliharibiwa na mamlaka za serikali, wagombea wa upinzani walienguliwa, maeneo mengi CCM wakajitangaza washindi, wagombea wa upinzani hadi sasa wanazo kesi za uhujumu uchumi, mauaji na wapo gerezani kutokana na uchaguzi huo.

Ni uchaguzi huo umelifanya bunge kuwa la chama kimoja. Bunge halina hata kambi rasmi ya upinzani bungeni. Walipogundua kwamba hata kamati za PAC na LAAC lazima ziongozwe na wabunge wa upinzani, wakawaomba ACT wapokee ofa na wale wabunge 19 wakaingizwa bungeni. Haramu.

JPM akiwa madarakani, wabunge 19 wasiokuwa na uwakilishi wowote wa chama cha siasa au kutokana na takwa lolote la katiba, waliapishwa, wakaitwa wabunge halali kwa kuapishwa na hadi sasa wapo bungeni. Ni matendo ya aibu kubwa sana yenye kuonyesha alama kubwa za udikteta.

JPM ametusaidia sana wanasiasa wa upinzani. Sasa tumefahamu umuhimu wa kuondokana na katiba hii mbovu inayompa mamlaka ya kikatili Rais. Ni lazima tupate katiba inayoendana na matakwa ya umma katika mfumo wa kisiasa wa vyama vingi na siyo Rais. Katiba mpya ni muhimu sasa.

Mwenyekiti wa UVCCM wakati fulani, Heri James alisema Jukwaani kwamba wao (CCM) ndiyo wanaamua wapi wapeleka maendeleo na wapi wasipeleke na wasipopeleka hakuna kitu watafanywa na yeyote. Hili lilipaswa kukemewa na JPM kama kweli siyo kweli. Lakini ndiyo ulikuwa mtazamo wa JPM.

JPM ametusaidia sasa tunafahamu kwamba kuna wanasiasa wanafiki, waongo na wazandiki katika siasa za nchi yetu, ambao wapo tayari kuuza UTU wao, kwa watawala ili watimize haja ya nafsi na matamanio yao. Wanapenda kuwa na vyeo bila kujali mahitaji ya wananchi. Wabinafsi.

JPM ametusaidia kuwafahamu 'political mercenaries' ambao Mwalimu Nyerere alisema tuwatambue kwa jina la "Malaya wa kisiasa". Wanayo bei. Wanajiuza. Hawana uvumilivu na hawa ndiyo wengi walihamia CCM wakisema wanaunga mkono juhudi za Rais. Hii ni shukrani kwa JPM .

Wafanyabiashara, ambao walikuwa ni tabaka kubwa linalounga na kufadhili shughuli za CCM, waliguswa, Walipewa mashtaka ya uhujumu uchumi, walifilisiwa. Hili ni moja kati ya makundi yaliyoguswa moja kwa moja. Hata wavuvi waliona moto. Nenda Chato, waulize wavuvi, JPM safi??

JPM ametuonyesha kwamba kwa katiba hii ukiwa na wapambe wengi bungeni, unaweza kuamua kujiongezea muda wa kubaki madarakani kisheria kabisa kwa Bunge kupitisha mabadiliko ys sheria na kuondoa ukomo wa muhula na Muda wa kuwa Rais. Tulianza kusikia minong'ono na vitendo.

JPM kwa muda wa miaka 5 na miezi 5 tu, alitufungua jicho, tulipaswa kuwa naye kwa miaka 20 kabla ili atusaidie kuwafungua watu akili, macho, masikio. Alituonyesha mkono wa chuma ukiwa madarakani, tusirudi huko, tuitengeneze katiba ya nchi yetu, asipatikane Magufuli mwingine.

MMM, Martin Maranja Masese
LA maana hapa uliloandika ni katiba basi!

Mengine umeandika ujinga uliokujaa kichwani mwako!

Kwamba JPM aliwahadaa hadi WB kutuweka uchumi wa kati?

Pimbi wewe!
 
Nimesoma huo utumbo nilipofika kwenye civid ndio nikajua kweli chadema ni kama kuku, akili hawana na ni wepesi wa kusahau ama wanafanya maksudi.

Kwenye covidi hata waume zenu wamekubali kua huu ugonjwa hauondoki na wameshajiandaa kuishi nao kama ilivyo mafua na magonjwa mengine, jambo ambalo alilisema JPM.

Kwa kua alisema JPM na waume zenu hawakusema basi hamtaki kukubali kua JPM alikua mbele ya wakati.

Uharo Mwingine sikutaka hata kusoma.
 
Kwangu mimi naamini huyo JPM angekuwa Rais bora sana kuanzia mwaka 1977 mara baada tu ya kutengenezwa kwa hii katiba inayotumika mpaka sasa.

Kitendo cha yeye kuja miaka zaidi ya 40 baadaye, ndicho kilichotuletea mvurugano wa akili na nafsi baadhi ya Watanzania ambao hatukumsoma kuanzia mwanzo mpaka mwisho wa utawala wake.
nazani kauli ya nang'atuka isinge kuwepo...
 
Huyo wa pili toka kulia bado yupo na sasa RC wa Kilimanjaro na alikuwa na bahati sana ile kutolewa ikulu na kupelekwa kuwa katibu wa bunge ingekosa hivyo labda na yeye angesepa na wenzake hao.
Sio kweli sio mkuu wa mkoa wakilimanjaro huyo ,
 
Back
Top Bottom