Magufuli akumbwa na kashfa nzito!

Magufuli akumbwa na kashfa nzito!

Status
Not open for further replies.
Ukitaka kujua kimiundombinu tulivyochoka,achana na barabara za mijini na barabara kuu.utajuta kuzaliwa tanzania.TEMBELEA HAYA MAENEO KAMA SAMPLE UELEWE NINACHOKIANDIKA..
Tuanzie same mashariki,
ludewa,
mbozi mash/magh
nzega kwenda tabora mjini,
simiyu,
tabora MJINI hadi manyoni (ITIGI),
katavi
mpanda,
same magharibi,
mwanga kusini,
njombe magharibi,
meatu,
kongwa dodoma,
ismani,
kilolo,
korogwe,
lushoto.n.k
hii ni mifano tu ya zile sehemu ambazo hutamani kupeleka gari zaidi ya trekta na greda.tz bado hakuna barabara ni kero..magufuli anajisifia badala ya kusema ukweli?.72.12% barabara zilizojengwa tumesaidiwa na wahisani hususani ujenzi unaoendelea dodoma mjini na arusha isitoshe kiasi cha fedha kilichotolewa kimechakachuliwa.
 
...malipo ya madeni ya mwaka wa nyuma yaliyolipwa kwa fedha za 2011/2012 kwa kutumia jina la mradi usiohalisi hs.252,975,000,000.

Miradi katika wizara ilipewa namba 4168 kwa ajili ya kupitisha malipo ya madeni ya miaka ya nyuma kwa miradi inayotekelezwa na TANROADS. Namba hii sio halisi” (chanzo: taarifa ya CAG uk.160,fungu 98)

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums.

Mkuu kamanda Mohamedi Mtoi ukweli wa mambo ni kuwa sasahivi magamba yanatumia kila mbinu na kila upenyo kujikusanyia fedha za kuhonga wananchi katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015.

Na ukitazama kwa makini utagundua kuwa wizara ya ujenzi ni mojawapo ya wizara chache sana zinazopokea fedha kutoka hazina bila kuchelewa kama wizara nyengine, tena wao hupokea mafungu yote waliyotengewa.

Na kwakutumia mwanya huo huo basi ccm wanajichotea mabilioni ya fedha na kuyatunza kwa ajili ya kutoa rushwa katika uchaguzi mkuu ujao kwakuwa wametambua kwamba hawana sera tena ya kuwahadaa watanzania.

Mwisho, tusisahau kuwa Magufuli hajaanza leo kuchakachua, ni bahati mbaya kwamba anapiga sana kelele kiasi kwamba watu wanashindwa kuzingatia ufisadi wake. Magufuli aliwahi kumuuzia nyumba ya serikali mdogo wake aliyekuwa akisoma chuo kikuu kipindi cha utawala wa Mkapa wakati walipoamua kuuziana nyumba za serikali.
 
Last edited by a moderator:
Hebu ngoja kwanza bajeti ijadiliwe mpaka mwisho halafu ukweli utapatikana tu.

Mkuu betlehem tuna ripoti ya mtaalamu CAG, unataka usubiri siasa tena? Kama alikuwa na majibu mujarabu ilibidi ayawasilishe mbele ya wataalamu bungeni ni siasa na ubabaishaji tu
 
Mkuu.
Acha kuweweseka! Hizo data zimetoka kwenye makarabrasha ya CAG mteule wa Magogoni. Walichofanya kambi rasmi ya upinzani bungeni ni kulinganisha data na kile pesa ilichoombewa kama zimefanya kazi iliyokusudiwa. Kazi haijafanika na CAG ameona ubadhirifu, una lalamikwa nini?! Tulia sindano iingie.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums.

Threads zenye figures kwa Buku Saba FC ni tatizo, ungeleta umbea hapa pangechimbika
 
Technical issue inaendaje kwenye politic, CAG ni taaluma tupu na taaluma maana yake facts bungeni ni bla bla bla bla.....
Vote 98: Ministry of Works
Payment made through dummy project worth Shs.252,975,000,000
The Ministry paid a sum of Shs.252,975,000,000 through unspecified project with dummy code No.4168. It was alleged that this amount was used to pay previous year’s
contractual liabilities for projects which were implemented by TANROADS. However, we were not provided with a detailed analysis of these liabilities. In addition, the amount paid was not disclosed as a previous year’s liability in the financial statements.


Ina maana Magufuli hakuwa na majibu kwa Vijana wa CAG, ila hapa bungeni atapata majibu maana kule kwa CAG hakuna siasa ila bungeni ni mahala pake
 
Huyu jamaa nilimshuhudia kwa macho yangu akichukua kipisi cha Nondo anaikagua barabara kwakuigongagonga, na hakuridhika na kumwambia Mkandarasi aliyeijenga barabara hiyo anampa miezi 6 awe ameibomoa na kuirudia upya na kua na kiwango kinachoridhisha ama sivyo anamtimua na hela arudishe!

Chezea John Pombe weyee!

Kwahiyo akifanya hivyo ndio anakuwa MUADILIFU ? Tanzania tuna hali mbaya sanaa ya kuamka kifikra...

Kwani mbona hata Lowassa kule Same mjini alishamfukuza Mkurugenzi wa halmashauri jukwaani kwa kosa la kutopeleka chakula cha msaada kwa wakati !

Kwani hizo staili za kufanya kazi ndio zinakufanya umuone mtu MUADILIFU ???
 
huu ni uzushi, hakuna ukweli wowote hapo...hizi ni takwimu za kupakana matope na hazitafanikiwa

Mbona Watazania mnakuwa na akili kama za samaki (Karume Jr 2012)

Huyu Pombe Magufuri aliwahi kumuuzia hawala yake (read Kimada) nyumba ya serikali wakati huo kimada wake huyo (Sundi) hakuwa mtumishi wa serikali, alikuwa mwanafunzi wa chuo cha Ardhi, wakati ule wa uzauza nyumba za serikali enzi ya Mkapa.

Sasa watanzania mnataka mtu awafanyie nini ndio muamini??!! Hata Pharaoh enzi zile za Mussa hakuwa na moyo MGUMU kama nyinyi Watanzania!
 
Kweli Magufuli anaweza kuwa ni msafi lakini kwa jinsi serikali ilivyochafuka kuanzia kichwani (soma Ikulu) hadi unyayo (soma serikali ya mtaa/kijiji) hakuna namna akabaki msafi peke yake. Kwa kawaida system ikishaharibika inatema kile kisafi kwa hiyo angeshatemwa tu sema nae anafanana na system. Hauna kitu hapo!! mbwembe tu. Huwa nashangaa sana unakuta mtu baki tu na njaa yake anatetea wakuu serikalini utadhani anajua jinsi mambo yanavyoendeshwa humo serikalini. Yaani, humu serikalini ni kupiga deal tu kwa kwenda mbele!! Usipopiga deal unaambiwa pisha njia!! Ukiziba njia unakufa!! chezea mafisadi wewe!!
 
Kwahiyo akifanya hivyo ndio anakuwa MUADILIFU ? Tanzania tuna hali mbaya sanaa ya kuamka kifikra...

Kwani mbona hata Lowassa kule Same mjini alishamfukuza Mkurugenzi wa halmashauri jukwaani kwa kosa la kutopeleka chakula cha msaada kwa wakati !

Kwani hizo staili za kufanya kazi ndio zinakufanya umuone mtu MUADILIFU ???
Kwahiyo unapendekeza tuwe na viongozi wezi kama kina Chenge sio?
 
Threads zenye figures kwa Buku Saba FC ni tatizo, ungeleta umbea hapa pangechimbika

Mkuu!

Nimecheka sana! Maneno yako kama ya kweli vile?! Na kibaya zaidi data zimetoka kwenye ripoti ya CAG.

Samahani! Kwani pale Lumumba wamekatwaza kujifunza kuja kujibu data kwa data hapa JF?
 
Jamani eeee , Msisahau na Zile Nyumba za Wananchi ( siyo za serikali ) alizoziuza kwa bei Ubwete ! na ile moja inayosemekana ilipewa NYUMBA NDOGO .
 
Mohamedi Mtoi,
siku hizi ameanza kuwa kama mpare,
Anatoa taarifa nusu nusu bila kutoa taarifa kamili.
Mgosi hebu funguka tukuelewe

Halafu mkiambiwa nyinyi mna dharau na wabaguzi mnabisha! Ona ulivyo andika "... Kama MPARE..." Hii ni dharau kwa wapare! Utajifuunza lini ustaarabu wewe?! Kabila bora kwako ni lipi?! Umejivua nguo sana mkuu.
 
Huyu jamaa nilimshuhudia kwa macho yangu akichukua kipisi cha Nondo anaikagua barabara kwakuigongagonga, na hakuridhika na kumwambia Mkandarasi aliyeijenga barabara hiyo anampa miezi 6 awe ameibomoa na kuirudia upya na kua na kiwango kinachoridhisha ama sivyo anamtimua na hela arudishe!

Chezea John Pombe weyee!

Baada ya hapo ulifuatilia kama jamaa alibomoa au alirudisha chenji?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom