Magufuli akumbwa na kashfa nzito!

Magufuli akumbwa na kashfa nzito!

Status
Not open for further replies.
Watanzania kwa kupenda matukio, ili suala tungesubiri waziri mwenye dhamana husika alitolee ufafanuzi kwenye majumuisho, kwa sasa ni mapema sana kusema ni kashfa kwa mhe. Magufuli.

Lakini jambo lingine, wapinzani kwa kukurupuka kwao mara kwa mara na kutoa taarifa za kupikwa bila kuwa na uthibitisho kamili na shutuma zao, refer ile shutuma ya Kinana, imani nao tena sina, hata kama ni kweli Magufuli kafisadi, sipo tayari kuamini kambi ya upinzani unless serikali ithibitishe.

Red ya kwanza: wapinzani wametumia report ya CAG kuhoji so hakuna kukurupuka mkuu
Red ya pili: Kumbe hata kama ni kweli huto amini? AJABU KWELI!!!!
 
mmmh hakuna jema kwa chadema. japo mbowe na nassari wanampenda magufuli..........chadema inampenda lowassa, sumaye anakuja huko soon
 
Tunasubiri kwa hamu majibu ya Magufuli, japo media leo zilihongwa matangazo hawakuona kama hii ni habari , lets wait and see,

Ila nimesikia atasema kuwa zilitumika kulipa madeni , atapaswa kusema ni madeni yapi na ya mwaka gani na vipi mbona alishindwa kumpa CAG taarifa za hayo madeni?
 
Msikilizeni Magufuli kaanza kujibu hotuba yake na ameanza kutaja Km Za uhuru , ngoja tuendelee kusubiria majibu ya kashfa hii.
 
Badala ya Magufuli kujibu hoja , yeye anafanya propaganda za kisiasa kuhusiana na TANROADS kuwa eti inasifiwa , ila anasahau kuwa wapinzani walinukuu taarifa ya PPRA iliyosema kwenye usimamizi walipata alama 0,
Anasema jamiiforums ni ya Chadema na ametaja link kuwa Mbowe alisifu kazi za ccm kwenye barabara , huyu jamaa bana .....
 
Majibu ya Magufuli , "Ni kwanini Arfi alikaa kimya mwaka jana kwenye bajeti aje azungumze leo kwenye bajeti hii" ......ameishia hapo

Hili ndio jibu la 252 bilioni shilings ,
 
Magufuli ni msanii wa kupindukia, badala ya kujibu hoja kwa vielelezo yeye anajibaraguza , na kama wabunge hawatahoji kuhusiana na fedha hizi watakuwa hawalitendei haki taifa hili kwani hizi fedha ni nyingi sana......
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom