Magufuli akumbwa na kashfa nzito!

Magufuli akumbwa na kashfa nzito!

Status
Not open for further replies.
kwa hiyo kashfa iko wapi hapo? si usubiri ufafanuzi wa waziri wakati wa majumuisho

Hapo nadhani kuna technicalities juu ya ulipaji wa madeni na wala si ubadhirifu. Nasikia miaka ya karibuni serikali imekuwa ikiingia katika madeni makubwa na wakandarasi. Nitapenda kusikia ufafanuzi toka kwa Waziri wa Ujenzi Dr. John Joseph Pombe Magufuli wakati anahitimisha uchangiaji kwenye hotuba yake pamoja na wakati wa kupitisha bajeti kifungu kwa kifungu! Magufuli kama amekula MUKU vile manake akisimama kuongea hata kama ulikuwa unataka kumkamata pabaya unalegea na kumuacha atiririke. Ataanza kuongea kwa taratibu huku akiwa kama anaonyesha kuonewa kisha atashuka na data na kutaja barabara ambazo zipo kwenye jimbo la mbunge husika na mwisho kuwaambia niacheni nifanye kazi; hapo tena kila mtu kimya na matokeo yake ni kumuomba aangalie na barabara zao.

Magufuli kiboko; leo mtamsikia atakavyopangua hayo yote!
 
sure mkuu. kuna watu wanajaribu kumchafua kwa vile inasemekana akawa mgombea urais wa 2015. makandarasi wanamkoma
Acha kuingiza siasa kwenye kila kitu wewe, umewekewa data hapo za dummy projects wewe unaleta habari za kugombea urais. Ndio zenu maCCM kila kitu mnasingizia siasa huku mnakwapua kweli na nchi inazidi kudidimia kwa umaskini. Nakushauri uje na hoja kuonesha kuwa hizo hela hazijaibiwa kama ripoti ya CAG inavosema na sio kukimbilia kwenye siasa na kuchafuana. Data hukanushwa kwa data sio maneno we mngoni!
 
huu ni uzushi, hakuna ukweli wowote hapo...hizi ni takwimu za kupakana matope na hazitafanikiwa

Mkuu.
Acha kuweweseka! Hizo data zimetoka kwenye makarabrasha ya CAG mteule wa Magogoni. Walichofanya kambi rasmi ya upinzani bungeni ni kulinganisha data na kile pesa ilichoombewa kama zimefanya kazi iliyokusudiwa. Kazi haijafanika na CAG ameona ubadhirifu, una lalamikwa nini?! Tulia sindano iingie.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums.
 
Vote 98: Ministry of Works
Payment made through dummy project worth Shs.252,975,000,000
The Ministry paid a sum of Shs.252,975,000,000 through unspecified project with dummy code No.4168. It was alleged that this amount was used to pay previous year’s
contractual liabilities for projects which were implemented by TANROADS. However, we were not provided with a detailed analysis of these liabilities. In addition, the amount paid was not disclosed as a previous year’s liability in the financial statements.


Ina maana Magufuli hakuwa na majibu kwa Vijana wa CAG, ila hapa bungeni atapata majibu maana kule kwa CAG hakuna siasa ila bungeni ni mahala pake
 
Hii imetoka kwenye hotuba ya kambi ya upinzani. Sehemu hii inaonyesha ubadhirifu wa fedha kwenye wizara iliyooko chini ya Dr John Pombe Magufuli.

Mheshimiwa Spika,baada ya fedha hizi kupunguzwa kiasi cha shilingi bilioni 95 na kupelekwa wizara ya uchukuzi zilibakia kiasi cha shilingi bilioni 252.975 katika kifungu hiki, leo tumelazimika kulikumbusha Bunge kuhusiana na suala hili kwani kwa mujibu wa ripoti ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali ya mwaka husika wa fedha kuhusiana na kifungu hiki alisema, naomba kunukuu "malipo ya madeni ya mwaka wa nyuma yaliyolipwa kwa fedha za 2011/2012 kwa kutumia jina la mradi usiohalisi hs.252,975,000,000.

Ukiongeza na 29bilioni za Presidential Delivery Unit - Kitengo kipya chini ya Rais utagundua na kupata jibu lini maisha bora kwa mtanzania yatapatikana.


Pamoja na madudu hayo majamaa wale wa Kijani bado watasema ndiyooooooooo.............! alafu mama Mkubwa(Spika) atamaliza na nadhani waliesema ndiyooooooooooo......... wameshinda.

Sanaa ya namna hii kusema kweli ni Aibu kubwa kwa watu wanaotaka kuitwa waheshimiwa .

Uwizi huu wote una mambo makuu matatu.
1.Uchaguzi serikali ya Mtaa 2014
2.Kustaafu kwa vigogo kadhaa 2015.
3.Uchaguzi mkuu 2015
 
huyo ni bure zaidi kwa majigambo, akiwa raisi hana meno ya kuwang'ata ccm.
 
Vote 98: Ministry of Works
Payment made through dummy project worth Shs.252,975,000,000
The Ministry paid a sum of Shs.252,975,000,000 through unspecified project with dummy code No.4168. It was alleged that this amount was used to pay previous year's
contractual liabilities for projects which were implemented by TANROADS. However, we were not provided with a detailed analysis of these liabilities. In addition, the amount paid was not disclosed as a previous year's liability in the financial statements.


Ina maana Magufuli hakuwa na majibu kwa Vijana wa CAG, ila hapa bungeni atapata majibu maana kule kwa CAG hakuna siasa ila bungeni ni mahala pake

Daaaaah !
Yaaani sisi kule kwetu barabara ya Mkomazi - Same yenye km 54 tu haipitiki kipindi ya mvua lakini hawa wadudu wanakula Bil 252 kama hawana Wazazi ??

Sawaaa bhanaaaa
 
Magufuli ni mwizi wa kitambo kuanzia kujiuzia nyumba ya serikali na wizi mwingine mwingi utawekwa wazi soon.
Hivi hamshangai magufuli kila baada ya sentesi 2 lazima amtaje na kumsifia JK??

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Hebu ngoja kwanza bajeti ijadiliwe mpaka mwisho halafu ukweli utapatikana tu.
 
Makufuli sio wakuaminika hata siku moja ,angekuwa ana waledi wa uadilifu angetoka magamba ili aweze kuwarekebisha wenzie tokea enzi za Mkapa . Ila kwa kuwa ni mchumia tumbo anakichanga kama wenzie wa magamba
 
ni bora kuhangaika na mengine kuliko kupoteza muda kumchafua mtu asiyechafulika

Mkuu nakushauri wakati mwingine uongozwe na hoja pamoja na kupenda chama chako sana. Subiri basi majibu yatolewe
 
Makufuli sio wakuaminika hata siku moja ,angekuwa ana waledi wa uadilifu angetoka magamba ili aweze kuwarekebisha wenzie tokea enzi za Mkapa . Ila kwa kuwa ni mchumia tumbo anakichanga kama wenzie wa magamba

nakubaliana nawe katika hili
 
Huyo ni kati ya waadilifu walobaki Ccm!!!!!!!!! Sijui hii nchi ililogwa na nani, nadhani ndiyo maana hata Mungu ameamua kutupa mapigo mara majengo kuporomoka, mara meli kuzama, mara milipuko ya mabomu mara ugaidi ili mradi tukome kuchagua mafisadi.
 
Magufuli mbona mbabaishaji tu labda watu wa akili ndogo ndo huwa wanamkubali kwa sababu hawashughulishi akili yao hata kidogo wanakubali kila wanachoambiwa na kupiga makofi, ndo maana wengi eti wanasubiri kuona atakavyopangua hoja za upinzania. Sehemu ya kujibu hoja hizo kitaalamu ilikuwa ni kwa CAG na kwa kweli kama watanzania tungekuwa serious kitu cha kukipa uzito ni cha kitaalamu lakini kinyume chake tunakubali siasa na ubabaishaji mtupu. Ooooo Tanzania nchi yangu unayo safari ndefu ili kufikisha watu wako kwenye nchi ya ahadi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom