Magufuli akomaa na wenye Malori

Magufuli akomaa na wenye Malori

TECH WIZ

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2013
Posts
1,675
Reaction score
555
Waziri wa Miundombinu na Ujenzi Mheshimiwa John Magufuli amesema kwamba atasimama na msimamo wake kuyapiga marufuku magari ya mazigo kutokugoma barabarani.Waziri Magufuli amesema kwamba anashangaa kutokana na lawama anazobebeshwa kufuatia mgomo unaoendelea na kudai kuwa amefanya hivyo kwa kufuata sheria na kuongeza kuwa analazimika kuchukua hatua hizo ili kulinda barabara zisiharibiwe Nchini.Na zaidi amewataka wamiliki wa malori kwamba milango iko wazi wanaweza kwenda mahakamani kama wanahisi wameonewa.
 
kwani ishu kwa sasa ni kugomea barabarani au ni faini wanayotakiwa walipe wakizidisha mzigo?
 
Waziri wa Miundombinu na Ujenzi Mheshimiwa John Magufuli amesema kwamba atasimama na msimamo wake kuyapiga marufuku magari ya mazigo kutokugoma barabarani.Waziri Magufuli amesema kwamba anashangaa kutokana na lawama anazobebeshwa kufuatia mgomo unaoendelea na kudai kuwa amefanya hivyo kwa kufuata sheria na kuongeza kuwa analazimika kuchukua hatua hizo ili kulinda barabara zisiharibiwe Nchini.Na zaidi amewataka wamiliki wa malori kwamba milango iko wazi wanaweza kwenda mahakamani kama wanahisi wameonewa.

source?
 
Barabara ya Mandela imejengwa miaka michache iliyopita, na sasa imeanza kuharibika kwa sababu ya uzito wa mizigo kwenye magari. Hapa Mh.Magufuli lazima ajue kitu kimoja, pamoja na uzito unaozidi, lakini pia, wanaojenga hizi barabara wanazijenga kwa kiwango cha chini sana!
 
Magufuli wewe ni kiongozi makini japo wasiojua sheria wanazani unakurupuka lkn sisi wachache tunaeshimu kazi yako,usikate tamaa songa siku moja watanzania watakuelewa, maana wenye malori ni walewale tabaka lilelile.
 
Barabara ya Mandela imejengwa miaka michache iliyopita, na sasa imeanza kuharibika kwa sababu ya uzito wa mizigo kwenye magari. Hapa Mh.Magufuli lazima ajue kitu kimoja, pamoja na uzito unaozidi, lakini pia, wanaojenga hizi barabara wanazijenga kwa kiwango cha chini sana!

Kwenye ujenzi anajitaidi sana kusimamia lkn watanzania sisi ndo shida,rushwa za watu wa mizani na mizigo kuzidi ndo tatizo,tusimkatishe tamaa bali tumtie moyo kwa faida ya vizazi vijavyo.
 
Hii kauli ni outdated. Maamuzi yameshafanywa na Waziri Mkuu, inabidi aongee na hao wenye malori na wala hawaendi mahakamani.
 
Barabara ya Mandela imejengwa miaka michache iliyopita, na sasa imeanza kuharibika kwa sababu ya uzito wa mizigo kwenye magari. Hapa Mh.Magufuli lazima ajue kitu kimoja, pamoja na uzito unaozidi, lakini pia, wanaojenga hizi barabara wanazijenga kwa kiwango cha chini sana!

Mandela road kiwango cha chini, una uhakika? Halafu pesa zilitoka European Union, wakaleta Mhandisi Mshauri wenyewe, Tanroads walihusika tu kama Clerks of works! Ikumbukwe kuwa kazi iliyofanyika Mandela Road ni kazi bora kabisa kwa uwezo wetu, huku tukizingatia kama tungekuwa na uwezo tungeongeza ili kuongeza tabaka la materials zile, lakini hatukuweza kuongeza, basi design imebaki ya tani angalau 40 hivi! Kwa kifupi Mandela road waliweka overlay, na siyo ujenzi from the scratch/beginning.
 
kuna wendawazimu wachache wasio na fadhila kama hao waliocomment kama hao juu hao hapo!!!
 
Umeona ee,kwanini watanzania tusimsuport magufuri,ukiachana na barabara ya mandela hebu angaria barabara ya morogoro(morogoro road) maeneo ya kukaribia chalinze utaona ni nini anachokipigania magufuri
 
Mandela road kiwango cha chini, una uhakika? Halafu pesa zilitoka European Union, wakaleta Mhandisi Mshauri wenyewe, Tanroads walihusika tu kama Clerks of works! Ikumbukwe kuwa kazi iliyofanyika Mandela Road ni kazi bora kabisa kwa uwezo wetu, huku tukizingatia kama tungekuwa na uwezo tungeongeza ili kuongeza tabaka la materials zile, lakini hatukuweza kuongeza, basi design imebaki ya tani angalau 40 hivi! Kwa kifupi Mandela road waliweka overlay, na siyo ujenzi from the scratch/beginning.
mi namshauri magufuli aweke mzani bandarini ili kunusuru barabara ya mandela
 
Magufuli nnchizi.
huwezi kukomalia sheria inayovuruga jamii nawe unajisifu kusimamia sheria.
 
Waziri wa Miundombinu na Ujenzi Mheshimiwa John Magufuli amesema kwamba atasimama na msimamo wake kuyapiga marufuku magari ya mazigo kutokugoma barabarani.Waziri Magufuli amesema kwamba anashangaa kutokana na lawama anazobebeshwa kufuatia mgomo unaoendelea na kudai kuwa amefanya hivyo kwa kufuata sheria na kuongeza kuwa analazimika kuchukua hatua hizo ili kulinda barabara zisiharibiwe Nchini.Na zaidi amewataka wamiliki wa malori kwamba milango iko wazi wanaweza kwenda mahakamani kama wanahisi wameonewa.

Nadhani muafaka utapikana tu.
 
Waziri wa Miundombinu na Ujenzi Mheshimiwa John Magufuli amesema kwamba atasimama na msimamo wake kuyapiga marufuku magari ya mazigo kutokugoma barabarani.Waziri Magufuli amesema kwamba anashangaa kutokana na lawama anazobebeshwa kufuatia mgomo unaoendelea na kudai kuwa amefanya hivyo kwa kufuata sheria na kuongeza kuwa analazimika kuchukua hatua hizo ili kulinda barabara zisiharibiwe Nchini.Na zaidi amewataka wamiliki wa malori kwamba milango iko wazi wanaweza kwenda mahakamani kama wanahisi wameonewa.

Kama umeangalia ITV Jioni umeingia chaka hizo zilikuwa habari za wiki na Pinda alishatoa order kuwa utaratibu wa zamani utumike na ndiyo mgomo ukaishia hapo.
 
Magufuli nnchizi.
huwezi kukomalia sheria inayovuruga jamii nawe unajisifu kusimamia sheria.

Ni mapema kumlaumu Maghufuli, ingefaa walaumiwe waliotunga sheria hiyo
 
Back
Top Bottom