Waziri wa Miundombinu na Ujenzi Mheshimiwa John Magufuli amesema kwamba atasimama na msimamo wake kuyapiga marufuku magari ya mazigo kutokugoma barabarani.Waziri Magufuli amesema kwamba anashangaa kutokana na lawama anazobebeshwa kufuatia mgomo unaoendelea na kudai kuwa amefanya hivyo kwa kufuata sheria na kuongeza kuwa analazimika kuchukua hatua hizo ili kulinda barabara zisiharibiwe Nchini.Na zaidi amewataka wamiliki wa malori kwamba milango iko wazi wanaweza kwenda mahakamani kama wanahisi wameonewa.