Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
- Thread starter
- #21
Uchambuzi:
· Kama tulivyokwisha ona, ‘concessional loans’ ina unafuu kwa maana ya riba (chini ya asilimia moja i.e 0.75%, fixed), deni linaiva baada ya miaka 40; na kunakuwa na grace period ya muda mrefu (miaka kumi) kabla deni halijaanza kudaiwa.
· Lakini tumeona pia kwamba kwa miaka ya hivi karibuni, vyanzo hivi vya mkopo vimekuwa vikizidi kupungua kutokana na ‘creditos’ kuamua kujiondoa taratibu kwa sababu mbalimbali. Reaction ya serikali imekuwa ni pamoja na kuhamia kwenye vyanzo vyenye gharama na pia masharti makubwa zaidi, na pia kutegemea sana soko la ndani la deni la taifa (Domestic Debt). Kwa mfano, Mwaka 2013, Serikali ilikopa DOLA milioni 600 kutoka Standard Bank ya Uingereza (Rejea sakata la EGMA na Benki ya Stanbic).
- Kwa mfano, tukiangalia gharama za mikopo (cost of debt), kwa mwaka 2010, Weighted Average Interest (Interest Rate) ya mikopo yote ya nje ilikuwa ni 0.4%. Kufikia mwaka 2015, Weighted Average Interest ilifikia 1.9%.
· Kwa mujibu wa Medium term Term Debt Management Strategy (2010), deni la nje lilifikia TZS takribani Trilioni saba. Kufikia Mwezi June 2015, deni la nje lilifikia USD 12.1 Billion, ambayo ilikuwa ni sawa na TZS takribani 25 trillion. Na kwa mujibu wa ripoti ya Benki Kuu (February 2016), deni la nje limefikia $15.6 Billion, ambayo ni sawa na takribani TZS Trilioni 33. Kwa mwaka 2010, deni la nje lilichukua 71% ya deni lote la taifa, na kufikia June 2015, takwimu hii ilishuka kidogo na kufikia (69%). Lakini kwa mujibu wa ripoti ya (BOT), kufikia mwezi Januari 2016, deni la nje limefikia 79% ya jumla ya deni lote la taifa. Masuala muhimu matatu hapa:
- Moja ni kwamba – katika kipindi cha miaka mitano tu, deni la taifa liliongezeka kwa karibia MARA SABA.
- Pili, ndani ya miezi sita tu (June 2015 hadi December 2016), deni la taifa liliongezeka kwa $1.4 Billion, sawa na karibia TZS Trilioni Tatu.
- Tatu, deni la nje linazidi kuchukua sehemu kubwa ya jumla ya deni lote la taifa. Jamno la kutoa wasiwasi katika hili ni kwamba, tofauti na zamani ambapo sehemu kubwa ya deni la taifa ilikuwa ni concessional loans (low interest, fixed interest rate, long grace period, long maturity), ongezeko la deni la nje katika kipindi kuanzia 2009, limeambatana na vyanzo vingi vya ‘non-concessional and commercial”.
· Kwa mujibu wa benki kuu (BOT), katika kipindi cha (January 2015 hadi January 2016), Serikali ya Rais Magufuli ililipa jumla ya $401 million ya deni la taifa (Debt servicing) (sawa na takribani TZS bilioni 870 za walipa kodi). Kati ya hizi, 58% ilikuwa ni malipo ya ‘principal’ peke yake, na kiasi kilichobakia ikiwa ni malipo ya interest. (Katika hili rejea athari zitokanazo na mabadiliko ya kuachana na mikopo yenye gharama na masharti nafuu i.e concessional loans).
· Katika kipindi hicho hicho cha January 2015 hadi January 2016 pekee, serikali ilikopa jumla ya $1.6 billion, sawa na karibia TZS Trilioni 3.5. Kati ya hizi, $1.3 (TZS karibia 2.8 trilioni) zilienda kwenye shughuli za serikali kuu, na kiasi kilichosalia $300 milion zilienda kwenye sekta binafsi (sawa na karibia TZS bilioni 600).
· Kwa mujibu wa ripoti ya BOT (February 2016), Kwa kipindi cha mwezi mmoja tu (December 2015 hadi January 2016), deni la nje liliongezeka kwa $67 (ikiwa ni karibia sawa na TZS bilioni 145). Kwa mwezi huo huo, serikali ililipa deni la nje $49 million (sawa na karibia TZS bilioni 105). Kwa maana hii, katika kipindi hicho hicho, TZS bilioni 145 ziliingia ndani ya nchi kama mkopo/deni la nje kwa mkono wa kushoto, na hapo hapo TZS bilioni 105 zikatoka kwa mkono wa kulia kama malipo ya deni la nje
4.12 Costs and Risks Indicators (Deni la Nje)
Jedwali #3
Risk Indicator
2010
2015
Cost of Debt:
1. Weighted Average Interest Rate.
0.4%
1.9%.
2. Refinancing Risk
*Debt Maturing in one year (out of total debt).
6.2%
4.7%
3. Interest Rate Risks
*Total Amoung of Debt Refixing (%)
*Average Time to Refixing (Interest Rates) – Number of years.
6.2%
19.3 Years
23%
14.7 years.
UCHAMBUZI WA JEDWALI #3:
· Cost of debt (Gharama za mkopo wa nje).
Hapo juu tunaona kwamba Weighted Average Interest Rate (wastani wa riba) kwa mwaka 2010 ulikuwa ni 0.4%. Wastani huu uliongezeka hadi 1.9% miaka mitano baadae (2015), ikiwa ni ongezeko la zaidi ya mara tano. Tukumbuke kwamba sehemu kubwa ya ongezeko hili ni la mikopo ambayo vyanzo vyake ni vya kibiashara kuliko ‘concessional’.
Refinancing Risk
Deni linaloiva katika kipindi cha mwaka mmoja kati ya deni lote kwa mwaka (2015) ilikuwa ni 4.7%, ikilinganishwa na mwaka 2010 ambalo ilikuwa ni 6.2% ya jumla ya deni lote kwa kipindi hicho. Hili ni punguzo la 1.5%. Kwa kuangalia juu juu inaonekana walipa kodi wamepata ahueni lakini uhalisia haupo hivyo. Jumla ya deni la nje (2010) ilikuwa ni takribani TZS 6.7 trilioni. Kwa maana hii, deni lililokuwa linaiva ilikuwa ni jumla ya TZS takribani 415 billioni. Kwa mwaka 2015, deni la nje lilifikia takribani TZS 25 trilioni. Kwa maana hii, deni lililokuwa linaiva ilikuwa ni karibia TZS 1.2 trilioni. Kwahiyo wakati kulikuwa na punguzo la 1.5% katika kipindi hicho, kwa upande wa fedha za walipa kodi, kulikuwa na ongezeko la zaidi ya TZS trilioni moja. Rejea mjadala wa refinancing risk huko juu.
Interest rate risk
Kufikia mwaka 2010, jumla ya deni ambalo lilikuwa linahitaji ‘refixing of interest rate’ kutokanana kuiva ilikuwa ni 6.2% ya jumla ya deni lote. Hii ilikuwa ni sawa na karibia TZS 415 billion. Kufikia mwaka 2015, kiwango hiki kilifikia 23%, ambayo ilikuwa ni sawa na karibia TZS trilioni 6 (trilioni sita). Tukirejea mjadala wa awali juu ya gharama/hatari ya ‘roll over of debt’, maana yake ni kwamba kufikia kipindi husika, TZS karibia trilioni Sita zilikuwa zinasubiri kuwa rolled over kwa riba ya juu zaidi kuliko awali wakati mikopo husika ilipochukuliwa na serikali.
Katika sehemu inayofuata tutajadili:
Kwanini tunapaswa kuwa na wasiwasi zaidi juu ya hali ya deni la nje.
Historia ya deni la nje.
· Kama tulivyokwisha ona, ‘concessional loans’ ina unafuu kwa maana ya riba (chini ya asilimia moja i.e 0.75%, fixed), deni linaiva baada ya miaka 40; na kunakuwa na grace period ya muda mrefu (miaka kumi) kabla deni halijaanza kudaiwa.
· Lakini tumeona pia kwamba kwa miaka ya hivi karibuni, vyanzo hivi vya mkopo vimekuwa vikizidi kupungua kutokana na ‘creditos’ kuamua kujiondoa taratibu kwa sababu mbalimbali. Reaction ya serikali imekuwa ni pamoja na kuhamia kwenye vyanzo vyenye gharama na pia masharti makubwa zaidi, na pia kutegemea sana soko la ndani la deni la taifa (Domestic Debt). Kwa mfano, Mwaka 2013, Serikali ilikopa DOLA milioni 600 kutoka Standard Bank ya Uingereza (Rejea sakata la EGMA na Benki ya Stanbic).
- Kwa mfano, tukiangalia gharama za mikopo (cost of debt), kwa mwaka 2010, Weighted Average Interest (Interest Rate) ya mikopo yote ya nje ilikuwa ni 0.4%. Kufikia mwaka 2015, Weighted Average Interest ilifikia 1.9%.
· Kwa mujibu wa Medium term Term Debt Management Strategy (2010), deni la nje lilifikia TZS takribani Trilioni saba. Kufikia Mwezi June 2015, deni la nje lilifikia USD 12.1 Billion, ambayo ilikuwa ni sawa na TZS takribani 25 trillion. Na kwa mujibu wa ripoti ya Benki Kuu (February 2016), deni la nje limefikia $15.6 Billion, ambayo ni sawa na takribani TZS Trilioni 33. Kwa mwaka 2010, deni la nje lilichukua 71% ya deni lote la taifa, na kufikia June 2015, takwimu hii ilishuka kidogo na kufikia (69%). Lakini kwa mujibu wa ripoti ya (BOT), kufikia mwezi Januari 2016, deni la nje limefikia 79% ya jumla ya deni lote la taifa. Masuala muhimu matatu hapa:
- Moja ni kwamba – katika kipindi cha miaka mitano tu, deni la taifa liliongezeka kwa karibia MARA SABA.
- Pili, ndani ya miezi sita tu (June 2015 hadi December 2016), deni la taifa liliongezeka kwa $1.4 Billion, sawa na karibia TZS Trilioni Tatu.
- Tatu, deni la nje linazidi kuchukua sehemu kubwa ya jumla ya deni lote la taifa. Jamno la kutoa wasiwasi katika hili ni kwamba, tofauti na zamani ambapo sehemu kubwa ya deni la taifa ilikuwa ni concessional loans (low interest, fixed interest rate, long grace period, long maturity), ongezeko la deni la nje katika kipindi kuanzia 2009, limeambatana na vyanzo vingi vya ‘non-concessional and commercial”.
· Kwa mujibu wa benki kuu (BOT), katika kipindi cha (January 2015 hadi January 2016), Serikali ya Rais Magufuli ililipa jumla ya $401 million ya deni la taifa (Debt servicing) (sawa na takribani TZS bilioni 870 za walipa kodi). Kati ya hizi, 58% ilikuwa ni malipo ya ‘principal’ peke yake, na kiasi kilichobakia ikiwa ni malipo ya interest. (Katika hili rejea athari zitokanazo na mabadiliko ya kuachana na mikopo yenye gharama na masharti nafuu i.e concessional loans).
· Katika kipindi hicho hicho cha January 2015 hadi January 2016 pekee, serikali ilikopa jumla ya $1.6 billion, sawa na karibia TZS Trilioni 3.5. Kati ya hizi, $1.3 (TZS karibia 2.8 trilioni) zilienda kwenye shughuli za serikali kuu, na kiasi kilichosalia $300 milion zilienda kwenye sekta binafsi (sawa na karibia TZS bilioni 600).
· Kwa mujibu wa ripoti ya BOT (February 2016), Kwa kipindi cha mwezi mmoja tu (December 2015 hadi January 2016), deni la nje liliongezeka kwa $67 (ikiwa ni karibia sawa na TZS bilioni 145). Kwa mwezi huo huo, serikali ililipa deni la nje $49 million (sawa na karibia TZS bilioni 105). Kwa maana hii, katika kipindi hicho hicho, TZS bilioni 145 ziliingia ndani ya nchi kama mkopo/deni la nje kwa mkono wa kushoto, na hapo hapo TZS bilioni 105 zikatoka kwa mkono wa kulia kama malipo ya deni la nje
4.12 Costs and Risks Indicators (Deni la Nje)
Jedwali #3
Risk Indicator
2010
2015
Cost of Debt:
1. Weighted Average Interest Rate.
0.4%
1.9%.
2. Refinancing Risk
*Debt Maturing in one year (out of total debt).
6.2%
4.7%
3. Interest Rate Risks
*Total Amoung of Debt Refixing (%)
*Average Time to Refixing (Interest Rates) – Number of years.
6.2%
19.3 Years
23%
14.7 years.
UCHAMBUZI WA JEDWALI #3:
· Cost of debt (Gharama za mkopo wa nje).
Hapo juu tunaona kwamba Weighted Average Interest Rate (wastani wa riba) kwa mwaka 2010 ulikuwa ni 0.4%. Wastani huu uliongezeka hadi 1.9% miaka mitano baadae (2015), ikiwa ni ongezeko la zaidi ya mara tano. Tukumbuke kwamba sehemu kubwa ya ongezeko hili ni la mikopo ambayo vyanzo vyake ni vya kibiashara kuliko ‘concessional’.
Refinancing Risk
Deni linaloiva katika kipindi cha mwaka mmoja kati ya deni lote kwa mwaka (2015) ilikuwa ni 4.7%, ikilinganishwa na mwaka 2010 ambalo ilikuwa ni 6.2% ya jumla ya deni lote kwa kipindi hicho. Hili ni punguzo la 1.5%. Kwa kuangalia juu juu inaonekana walipa kodi wamepata ahueni lakini uhalisia haupo hivyo. Jumla ya deni la nje (2010) ilikuwa ni takribani TZS 6.7 trilioni. Kwa maana hii, deni lililokuwa linaiva ilikuwa ni jumla ya TZS takribani 415 billioni. Kwa mwaka 2015, deni la nje lilifikia takribani TZS 25 trilioni. Kwa maana hii, deni lililokuwa linaiva ilikuwa ni karibia TZS 1.2 trilioni. Kwahiyo wakati kulikuwa na punguzo la 1.5% katika kipindi hicho, kwa upande wa fedha za walipa kodi, kulikuwa na ongezeko la zaidi ya TZS trilioni moja. Rejea mjadala wa refinancing risk huko juu.
Interest rate risk
Kufikia mwaka 2010, jumla ya deni ambalo lilikuwa linahitaji ‘refixing of interest rate’ kutokanana kuiva ilikuwa ni 6.2% ya jumla ya deni lote. Hii ilikuwa ni sawa na karibia TZS 415 billion. Kufikia mwaka 2015, kiwango hiki kilifikia 23%, ambayo ilikuwa ni sawa na karibia TZS trilioni 6 (trilioni sita). Tukirejea mjadala wa awali juu ya gharama/hatari ya ‘roll over of debt’, maana yake ni kwamba kufikia kipindi husika, TZS karibia trilioni Sita zilikuwa zinasubiri kuwa rolled over kwa riba ya juu zaidi kuliko awali wakati mikopo husika ilipochukuliwa na serikali.
Katika sehemu inayofuata tutajadili:
Kwanini tunapaswa kuwa na wasiwasi zaidi juu ya hali ya deni la nje.
Historia ya deni la nje.