Mohammed Hamad
JF-Expert Member
- Jan 17, 2011
- 3,988
- 1,310
- Thread starter
-
- #121
mmh nikitizima huo ubeti wa mwisho nashindwa hata kukubembeleza uendelee kutupa company hapa jamvini.
haya asante,nanyi mkalale salama.
jamani jamani jamani sijui kwanini nimechelewa kwenye thread yako..... heheheh kumbe na mie nimoo ee kwa kuchangia jf....haya shukran mohammed.birthday yako ikifika nambie nikuletee bonge ya zawadi ukumbini,,, umeskia ee??..:msela::msela::msela::msela::msela::msela:
Huyu uliemtaja, hafui dafu jamani,
Ni dada mwenye viroja, amezidisha matani
Sifa zake nazitaja, upate kumbaini
Huyu ni mtu wa kuja, atokea milimani
Hawezi hata kungoja, subira haitamani
zingine nitazitaja, wala hutomtamani
Akikwambia "nakuja", kumbe yuko kitandani,
Si mtu alo na tija, amekosa shukurani,
Utakaa kumngoja, hayupo hata njiani
PJ congratulations
Nabofya kibodi yangu, salamu nazituma,
Kwenu marafiki zangu, natumai mu wazima,
Nawaombea kwa Mungu, mjaliwe yalo mema,
....................
Miss Judith huyo, ana UPANDE MWINGINE,
Yale ayaandikayo, hupendwa nao wengine,
Kwa mawazo si mchoyo, hufanya tushikamane,
..............................
Ambao sijawataja, lipo shairi jingine,
Sote tungali pamoja, kwa mema tuombeane,
Tusichoke zetu hoja, hivyo na tushikamane,
shosi wewe muwazi, hata kwa yako mavazi,
waona vyetu vivazi, kila upande kwa wazi,
hata Judith husazi, misi umemperuzi,
heri mejiweka wazi, filingi zako taenzi
wasema waja vingine, kwa wote ulosahau,
nusura mie nigune, mepozwa nazo nahau,
ingawa ni kama tone, chonde usinisahau
nitakodoa nione, tuko pamoja mdau
Nimeandika vizuri vina nimepangilia
Yale yaliyo ya kheri rahisi kuyagundua
Kwa anaefikiri vema kuyatambua
Tujitume kwa khiyari na jitihada pia
Tusitafute fahari kisha tukaumia
Zingatia shauri ujue wako wajibu
Usiingie kwenye hatari ukawacha ya wajibu
Mpongeze akupongezae, usimpongeze asokupongeza.
Asante mkuu, nilikuwa najaribu kukujibu kwa vina hapa lakini naona nachezea makaratasi tu ukizingatia nilikuwa na bifu na mwalimu wa kiswahili.
umejibu kwa wepesi, moyo wangu kusuza,
hata bila ya senkisi, heshima umenituza,
zi zako zote makisi, kwa yote ulonijuza
watunyosha kama pasi, vipaji vyetu kukuza
mkuu wewe kwa utenzi kiboko
Shukurani nazipokea, Jaluo mwana Nyeupe.
Mola mi sinizuie, namsifu kwa si kwamapepe
Urithi ni thamanie, tunzoni pepepe
Shairi ni kipaji,weka vina kibindoni
Nabofya kibodi yangu, salamu nazituma,
Kwenu marafiki zangu, natumai mu wazima,
Nawaombea kwa Mungu, mjaliwe yalo mema,
AfroDenzi, nakuzimia tangu MWANZONI,
Fikra zake ni huru, pia zina burudani,
Nami ninamshukuru, hachoki tangu zamani,
Mohammed Shossi, ooohh dear.
nimetamani kukuandikia shahiri
maneno matamu nimekosa..
nimetamani kutunga shairi
utenzi siiujui, kina ndo nini?
mistrari sijui yapangalia
lakini naamini maneno matamu
si lazima, shairi au Ngonjera,
naamini naweza kukuliwaza
na kukutuliza bila shairi..
napenda jinsi unavyo toa
maneno yako matamu
kwa kila anaye stahili
na ninashukuru kwa
michango yako mahiri..
samahani kwa kuchelewesha ujembe
lakini nadhani mlango bado u wazi..
Nilham
Kipaji ni jambo bora, amekupamba Rabana,
Tena umetia fora, posti hufana,
Basi usiwe mkora, akiba uweke sana,:A S 20::A S 20:
Sihadawe na unyange na unyange una mwisho
Asante Mohhamed Shossi, sasa naingia kichwa kichwa,
Ujinga kweli mkosi, hakika wapaswa kuachwa,
Najiunga rasmi na kikosi, chenye wachapa kazi kuliko mchwa.
Unikumbushe asubuhi nikiamka nijaribu tena kuandika.
Thanks Mohamed Shossi! This is so creative of u:clap2::clap2::clap2:
I will be back....
mohammed mi hivi siwezi nifanyeje jamani??
Nabofya kibodi yangu, salamu nazituma,
Kwenu marafiki zangu, natumai mu wazima,
Nawaombea kwa Mungu, mjaliwe yalo mema,
AfroDenzi, nakuzimia tangu MWANZONI,
Fikra zake ni huru, pia zina burudani,
Nami ninamshukuru, hachoki tangu zamani,
Mohammed Shossi, ooohh dear.
nimetamani kukuandikia shahiri
maneno matamu nimekosa..
nimetamani kutunga shairi
utenzi siiujui, kina ndo nini?
mistrari sijui yapangalia
lakini naamini maneno matamu
si lazima, shairi au Ngonjera,
naamini naweza kukuliwaza
na kukutuliza bila shairi..
napenda jinsi unavyo toa
maneno yako matamu
kwa kila anaye stahili
na ninashukuru kwa
michango yako mahiri..
samahani kwa kuchelewesha ujembe
lakini nadhani mlango bado u wazi..
Usingizi siupati, kkwa kuwa upo mbali,
Naghani kila wakati,mimi kwako sina hali,
Nakungoja kwa chati, nimeingiwa na muhali,
Jamvini nakungojea, kwa mahaba na bashasha,
Malenga ulobobea, kiu yangu ya tenzi kuishusha,
Furaha kuniletea, maishani kunitosha,
Pambo la mwangu jamvini, pekee kwenye dunia,
Busara zako jamvini, hakuna wa kufikia,
Jichoni mwangu u mboni, wewe wanonyesha njia,
Hata niwapo dhaifu, we wanifanya imara,
Tenzi yangu sadikifu, hakika watia fora,
Nami s'achi kukusifu, hata mara hamsa ashara,.
Ujembe wako umeshibashiba, bila ya choyo chochote,
Kwa hekima zako na huba, fikrazo tunashea wote
Umejawa na mahaba, nilikesha nikupate,
Najua fulani, amekasirika sikifani
Ila we mwandani usiache kughani
Tenzi zenye burdani kutumwagia jamvini
Siziwe za wastani zenye vina namizani
Akikumwa njiani me nitakuchukua nyumbani
Usiogope mwandani, wenzio waniwinda kwa ubani