Magreat Thinkers ninaowafeel...........

Magreat Thinkers ninaowafeel...........

Hakika umetamba,
Tenzi kutaramba,
Mods kuwapamba,
Members kuwaimba,
Niaba ya Robot MTAMBA,
Shukurani kutoifumba,
Kwako tumeiumba,
Kwa tungo kujiramba
SHOSSI umebamba

Kanuni shika,
Hutoguswa hakika,
wale mlahaka,
walo na dhihaka,
JamiiForums siyo chaka,
Ni kiota kwa wahajaka,
SHOSSI umesomeka

Mkuu umesomeka, Kanuni nitazifata
JF si kichaka, hilo nimelipata
Hakika nimefarijika, kwa shukrani zako kuzipata
Kumbe wewe mshairi, mbona ulikaa kimya?
Au uliiunda safari, kukifungua kinywa?

Beti zako murua mistari yako hatari
Tungo yako ni muwa, wenye utamu wa sukari
Kaditama namaliza nakuombea ya kheri
Mwaka tuumalize bila kupata ya shari
 
duh bado upo wakwetu.............ngoja niandae shairi sasa.........:coffee:
 
Kuna wakati nimechoka natamani nijiliwaze
Nikiwa kwetu Tanga hakuna upweke
napakumbuka sana Tanga nikiwa mpweke
Inshallah nitarudi kuijenga Tanga yetu

Nimejifunza mengi nikiwa safarini
Natamani nirudi kwetu niyaenzi
Nyumbani ni nyumbani
Inshallah nitarudi kuijenga Tanga yetu

Nakumbuka sana ngoma zetu
Kamwe sikuwahi kosa la kufanya kwetu
Sijaona na sitaona kama Tanga kwangu
Inshallah nitarudi kuijenga Tanga yetu

Shossi ndugu yangu nafurahi kukufahamu
Dunia bila ndugu waweza pata wazimu
JF napapenda pamenifunza mengi muhimu
Inshallah nitarudi kuijenga Tanga yetu
 
Kuna wakati nimechoka natamani nijiliwaze
Nikiwa kwetu Tanga hakuna upweke
napakumbuka sana Tanga nikiwa mpweke
Inshallah nitarudi kuijenga Tanga yetu

Nimejifunza mengi nikiwa safarini
Natamani nirudi kwetu niyaenzi
Nyumbani ni nyumbani
Inshallah nitarudi kuijenga Tanga yetu

Nakumbuka sana ngoma zetu
Kamwe sikuwahi kosa la kufanya kwetu
Sijaona na sitaona kama Tanga kwangu
Inshallah nitarudi kuijenga Tanga yetu

Shossi ndugu yangu nafurahi kukufahamu
Dunia bila ndugu waweza pata wazimu
JF napapenda pamenifunza mengi muhimu
Inshallah nitarudi kuijenga Tanga yetu

Michelle nimefurahi kutangaza yako nia
Karibu tena nyumbani uje kuhamia
Tena uje kwa kasi ilizidi spidi mia
Uje tule bada, ngogwe na bamia

Tanga imekuwa takujengea sahare
Uione bahari na samaki narenare
Tuijenge Tanga jetu tusicheze segere

Mimi ndugu yako umejiwahi mapema
Ingekuwa sijajua ningekutongoza zamani
Wewe ni dada yangu tumeshea mama
Tusitupane ndugu tukajenge nyumbani
 
Mbona mi simo au kwa vile ni mwana ccm

Mzambia kasema nani umetengwa kichama
JF memba wote ndgu fungua macho tazama
Acha yako majungu ukajaleta zahama
Sisi sote ndugu Hawa ndio mama

Siasa hutumika watu kutugawa
Wenye wakikutana wanakunywa kahawa
Sisi mitaani kwa maradhi twauwawa
Tia akili fikiri sio unachachawa.
 
i see asante sana Mohammed shossi
Kumbe uwepo wangu unautambua
Nashukuru sana kwa kompulimentaliri
Naombi maalumu kwako hili lifanyie kazi
Na mimi ninatamani kuwa mtunzi wa shairi
2011 naweka nadhiri moyoni
Kuwa mtunzi mzuri wa shairi ,
nikienda sambamba na MJ1, Asprin,Teamo
Mzee Mwanakijiji,Michelle ,wewe mwenyewe na wengine wengi
walo katika fani hii
 
Aisee ngoja nikakariri mistari, nikujibu kishairi.

Kwa sasa wacha nikugongee senksi kwanza.

BRB!

Mkuu bado unakariri mistari? maana tangu juzi ulivyosema unakariri mistari hujatia maguu tena kulikoni?
 
Mwana nipo mbali ila mwaka huu namaliza so tutakua pamoja man ila umenifuraisha sana kweli nchi inavipaji sana ila wanavipoteza sababu siku hizi sio kama zamani zamani kulikua na mashindano kuanzia mtaa kwa mtaa mpaka mashuleni kwenye makata na tarafa then kimkoa na kitaifa ndio maana tulikua tunafanya vizuri kwenye mambo mengi sana ila naona toka ilipoingia serikali ya awamu ya 3 chini ya mungai ndipo mambo yalipoanza kufa yaani ukienda wilaya za pembeni huko kuna vipaji vingi sana vimejificha man nimefeel sana na utaalamu wako sijajificha sema nashindwa sababu nipo mbali but inshallah nadhani huu ni mwaka wa mwisho so tutakua pamoja kuanzia miezi ya august!kila la kheri man!
Mimi ningali mwanafunzi katika hii tansia
Bado singuli kutunga nje ya tanzania
Baraza watu mahiri Kimensera acha kutania
Ila umetoa wazo zuri kazi talifanyia
Sivibaya kuijenga lugha yetu sawia
Nawe pia umo njoo tupige kasia
Usijitoe kundini kusema utenzi ni kadhia
Tungo huleta faraja penye dhiki na ghasia
Malenga hutoa hoja za msingi na wosia
Namaliza kukuomba tunga japo kwa kukisia.
Wajuzi walo jamvini watakufunda kiintelejensia.
Utakuwa mahiri na kuwapiku na waasia.
 
duh humu malenga mko wengi mnaenda kimashairi na tenzi hongereni

Superfisadi sasa aamka, tenzi kutupatia
Uzipange kwa ubeti wala si zakutupia
Utujuze yako hali na aila yako pia
Usinisahau kwa dua pamoja na nabia
Mungu akupe ya kheri na wanajamvi pia
 
duh humu malenga mko wengi mnaenda kimashairi na tenzi hongereni

Superfisadi sasa amka, tenzi kutupatia
Uzipange kwa ubeti sio za kutupia
Utujuze hali yako na aila yako pia
Usinisahau kwa dua pamoja na nabia
Mungu akupe ya kheri na wanajamvi pia.
 
Nilingoja lako neno na wewe nikutaje
Mtoto uliye na hiba nikushau iweje
Mwenye ladha ya mapenzi na macho ya huba
Siku zote sikinai kwenye prof yako naganda kama luba
DaMie hupo nyuma kuchangia jamvini
Sasa noa panga na jembe tia mpini
Nani asojua mchango wako jamvini?


Napata tabu as natumia simu. Nikipost beti hazikai inavyotakiwa I am out nikirudi nitaedit nakukupa sifa zako.

Asante kwa kweli
nami nasubiri,
beti zenye sifa zaidi,
ili kunipa ahueni.
 
i see asante sana Mohammed shossi
Kumbe uwepo wangu unautambua
Nashukuru sana kwa kompulimentaliri
Naombi maalumu kwako hili lifanyie kazi
Na mimi ninatamani kuwa mtunzi wa shairi
2011 naweka nadhiri moyoni
Kuwa mtunzi mzuri wa shairi ,
nikienda sambamba na MJ1, Asprin,Teamo
Mzee Mwanakijiji,Michelle ,wewe mwenyewe na wengine wengi
walo katika fani hii

Mchango wako mkubwa tena wenye umakini
Wewe ni mjenga hoja mkubwa hapa jamvini
Tunakukarisha kwa shangwe tena kwa kujiamini
Tutakuvisha taji na koja la asumini
Karibu wetu malenga FistLady wani
Uwashinde manguli Mwanakijini na Aspirini
 
Asante kwa kweli
nami nasubiri,
beti zenye sifa zaidi,
ili kunipa ahueni.

Nimedit hapo juu na kuweka beti hii.........

DaMie nimeona na wewe nikutaje
Mtoto uliye na hiba nikushau iweje
Posti zako ni dawa zimeshinda mvuje
Zina toa wosiwa dar mpak kivinje
Usirudi nyuma jamvi usilikunje
 
Michelle nimefurahi kutangaza yako nia
Karibu tena nyumbani uje kuhamia
Tena uje kwa kasi ilizidi spidi mia
Uje tule bada, ngogwe na bamia

Tanga imekuwa takujengea sahare
Uione bahari na samaki narenare
Tuijenge Tanga jetu tusicheze segere

Mimi ndugu yako umejiwahi mapema
Ingekuwa sijajua ningekutongoza zamani
Wewe ni dada yangu tumeshea mama
Tusitupane ndugu tukajenge nyumbani


Sahare Sahare nitafurahi kujengewa
Nitajiona wa thamani sahare ukinijengea
Niko njiani ndugu yangu Tanga ntarejea
Kufurahi na kusahau magumu ya ugenini
 
Sahare Sahare nitafurahi kujengewa
Nitajiona wa thamani sahare ukinijengea
Niko njiani ndugu yangu Tanga ntarejea
Kufurahi na kusahau magumu ya ugenini

Nakusubiri kwa hamu siku hiyo ifike
Imeisha yake hamu Hashcool amekupiga teke
Rudi nyumbani ndugu mwambie una kwenu
Ufisadi kaufanya kunipoka changu kishunu
Nilham wamjua ameshau hisanu

Amezisahau tenzi zote nilomtungia
Amezinguliwa kwa kizungu tele akaingia

Dunia naiona chungu njoo dada uniliwaze
Unifute machozi nibembele ninyamaze
 
Aisee mheshimiwa Muddy sikujua kama unanifeel asee?

Sijui nikujibu kwa ushairi au hii inatosha?

Nimekugongea senksi kule, kakague.
 
Back
Top Bottom