Magreat Thinkers ninaowafeel...........

Magreat Thinkers ninaowafeel...........

Hakuna aliezaliwa akajua ya bayana
Kila mmoja kapawa kipaji na Rabana
Jaribu kupangia vina usiseme hapana
Ghani kwa shairi kwa urefu na mapana
Usijishuke kifani wakauna uso maana

Nilham una elimu umewashinda watwana
Wewe bint rashed mwenye siha mwanana
Usingoje kuonyesha kipaji alokupa Maulana

Tungo nazisubiri kutoka kwako muhibu
Kiswahili safi wakijua usijigeuze bubu
Kilichobaki hivi sasa jivute taratibu
Utunge tungo za dawa tena zakitabibu
Uwasuuze nyoyo mabibi na mababu
ulijuwa kufariji, allah akakukareem.
ikawa mujib kuwapokea , wale walio muhimu
ukakupamba kwa huba , na ucheshi hakukunyima.

ukayapita mapana , kumridhisha kila muungwana..
ikawa ni tunu , kuwatunuku na siha kuwajulia..
hayupo mfano wako , ndani ya hii dunia..
akujaalia rahim , kwa siha na ukareem...



usinicheki ndio najifunza okay??) heheheh lol mpaka umenitia bilisi lol..

 
Baraza la kiswahili wanafanya nini sasa kumbe vipaji tunavyo humuhumu jamii forum ninyi ndio mlitakiwa muongoze kweli nimekupa saluti kipaji uacho mzee hongera sana man!

Nabofya kibodi yangu, salamu nazituma,
Kwenu marafiki zangu, natumai mu wazima,
Nawaombea kwa Mungu, mjaliwe yalo mema,

AfroDenzi, nakuzimia tangu MWANZONI,
Fikra zake ni huru, pia zina burudani,
Nami ninamshukuru, hachoki tangu zamani,

Yupo dadetu Festiledi, yeye hupenda MAISHA,
Kamwe hawezi kusita, mazuri kutuonesha,
Thanks tele azipata, maana huelimisha,

Michelle yupo, hutaka TUJIELEWE,
Daima aandikapo, vichwa vyetu tusuguwe,
Sifa zake zipo, muhimu apewe,

Dr W. Slaa nasaha tumepeyana, tena tukanufaika,
Mafumbo tukafumbana, kwa furaha na kucheka,
Na mara tukabishana, na wengine tukachoka
Kisha ukarudi tena, huku tumeshachamka.


Mzee Mwanakijiji, MZEE WA CHANGAMOTO,
Haishi kutuambia, mambo yalo motomoto,
Habari hutupatia, yenye midundo mizito,

Hashycool anza tangaza, ni kwako yamechimbuka
Watunzi waagiza, ushauri kuwataka
Yaseme kwenye baraza, hii ni mbiu ya mwaka.

Kaa la moto Chochote unachoweza,hima weka mchangoni
Hilo ndilo unalowaza,tukakawa hatulioni
Ila sala memaliza,ndio ukatia udhu

Madela wa Madilu keri hazi ghasi, nyimbounawaimbia
Mwenye kukerwa huhisi, hujali humuingia
Hawi zimwi asikisi, ikawa bure tabia.

[SIZE=-1]Pakajimmy amejieneza,sifa zakejamvini, [/SIZE]
[SIZE=-1]Jambo analoliwaza, taarifa kuwapeni, [/SIZE]
[SIZE=-1]Si vizuri kunyamaza, bora awajulisheni, [/SIZE]

Kaiza kaka yetu sote, jitu liloshiba,
Mengi hutaka tuyapate, yale yaliyoshiba,
Asichoke asisite, ajaze hata kibaba,

Gsana Naingia jamvini, hapana tena ajizi
Nazikubali shukrani, kwa juhudi zangu hizi
Kushajiisha jamvini, watunzi wa zama hizi
Kheri ipo kwa manani, Mpaji kanijaalia.


Katavi na LazyDog ipambeni JF wananeti mwasikia
Tenzi na mashairi nyeti, wengi watafurahia
Uridhi ndani ya beti mmfiche mmesikia?

Shishi na Mpevu hoja za kweli toeni, faida kutupatia
Aso ubavu wavuni, shimoni atakimbia
Mtenza mwenye nguvu makini, hadharani nawambia
M_bongotz acha woga, wananeti yetu hiba.

[SIZE=-1]Kuwa fundi si ajabu, hilo kwanza eleweni, [/SIZE]
[SIZE=-1]Kuwa fundi ni thawabu, aliyanena Manani, [/SIZE]
[SIZE=-1]Msijempa adhabu, kwa maswali ya kwa nini? [/SIZE]
[SIZE=-1]Drphone ameshasilimu, sasa naitwa FUNDI. [/SIZE]


Rose naye ni rafiki, hutumia DARUBINI,
Kazi yake haichoki, popote ulimwenguni,
Kwenye siasa na urafiki, hutujuza kulikoni,

Mwanajamvi Aspirin, hutuonesha MWANGAZA,
Makala zenye hekima, na mambo kuyachunguza,
Kwa ushairi ni vema, post zake zapendeza,

Zion Daughter Si wakuamsha daku,walo macho wameona
Hashindani na kuku,kula wanacho kiona
Wala havai kikuku,kuwaiga walonona


Miss Judith huyo, ana UPANDE MWINGINE,
Yale ayaandikayo, hupendwa nao wengine,
Kwa mawazo si mchoyo, hufanya tushikamane,

Gbolin umesibu, umenena ya hakika
Tena nimetaajabu, posti zako za haraka,
Wajibu tena wajibu, wanajamvi kukusanyika
Jamvini bila tabu, sote twaburudika.

Wa ndima Mgosi vipi unadhani, nasaha zipi azizi?
Nianze upande gani, kuepusha jinamizi?
Ni ipi ile ya ugoni, kutanguliza malezi?

MwanajamiiOne pia, hutuambia AMKENI,
Hachoki kutuletea, yatokeayo nchini,
Daima hukumbushia, tutoke usingizini,

October mwenzetu, utujuzaye maisha,
Wewe ni darasa kwetu, maarifa yaso kwisha,
Wafunza juu ya utu, mengi watuelimisha.

Teamo bado kuchoka, upo kwenye msafara,
Ungali kwenye pilika, kwa zako huru fikra,
Nakuombea baraka, uzidi kuwa imara,

Nilham usiyechoka, asubuhi na jioni,
Nyumbani kuwajibika, halafu pia kazini,
Kisha huachi andika, kutujuza kulikoni,

Mwenzetu ni mwanaharakati, daima usiyechoka,
Wautumia wakati, pasipo yoyote shaka,
Maisha kuwa na chati, daraja la uhakika,

Inkoskaz Upo kwenye mapambano, ujenzi walo taifa,
Hujalala kama pono, wastahili nyingi sifa,
Washika yetu mikono, ili tuzizibe nyufa,

Kiraka mwendo ukaze, usiache harakati,
Mawazo uyaeleze, tena kwa kila wakati,
Ili nasi tujifunze, nawe uwe katikati,

Voiceofreason, mapenzi umeandika,
tangu siku za zamani,
Yale yaliyokufika, na yale ya majirani,
Na kwako alozimika,umesema ya moyoni,

Ndugu yetu Preta, kabobea kwa MAVAZI,
Vitu vyake ni vizuri, hilo mbona lipo wazi,
Yupo kwenye mstari, hachoki kufanya kazi,

Fidel80 nayakumbuka, manenoyo jamvini,
Hakika niliridhika, nami nikakuamini,
Kwako hayakufichika, hata yale ya moyoni,
Hashima siku hizi hakuna labda zamani

Invisible tunamjua, mkuu wetu KIJIWENI,
Sheria apambanua, ili asitupige ban,
Sote tukajitambua, tujijue kina nani,


Mkuu Klorokwini, posti zake ni KITAMU,
Hatosahau daima, kutupa yote muhimu,
Ujuzi wake kisima, haisaliti elimu,


Mkuu Kashaijabutenge,nakuheshim zamani na sasa,
Yeye wala hajalala, mengi ameshayaasa,
Kabobea mijadala, ya jamii na siasa,

Kimokole moyoni nafarijika, malenga tukikutanika,
Ya haki kuyatamka, batili kuzifunika,
Kheri ikaminika jamvini tukanufaika.
Bwana Kimokole, nakushukuru hakika


Magulumangu mshairi, USHAIRI MAMBOLEO,
Mashairiye mazuri, tena yale ya kileo,
Huukuza ushairi, na kuupa mwelekeo,


Na Wiselady, siachi kumsifia,
Elimu kutugawia, na picha kutuwekea,
Mazuri hutuambia, ndani ya hii dunia,

Maria Roza
Posti zako laiti ni tarumbeta, kuvuma wakasikia
Lakini wapi ni nta, sikioni wametia
Lije kubwa la kivita, barugumu likalia

Ndugu yangu Rutashunyuma, sitokuwacha nyuma
Posti zako nii ghali sio kama uji
Zinawakuna wa mbali mbaka Tabora na Ujiji

Mjomba Bujibuji, mwingi wa burudani
Posti zako adhimu, zinatupa burudani
Sina wakufanisha hata na mmoja humu ndani.

Nakumiss mzee wa malivdavi ulie kaburini
Baada ya posti mbili wadau wakakupa bani
Kifo chako historia ndo mana nakutilia ubani

Ewe nawe The Finest usinung'unike,
Tena uingie ndani nawe ufarijike,
Utuambie amkeni, wanajamvi tubadilike
Tushikane kwa imani wanajamvi tunusurike.

Wozawoza wewe mshari jahili,
Kama huoni dalili, kebehi si jambo kupigania,
Twatetea kwa ukali, siambe tunatania
Kiwa sio zetu sisi, dini hizi ni za nani?

JF Moderator1 huyu wa ajabu, wala hataki mchezo
Kuwatia watu adabu, bila kuleta mizozo
Katoa watu ububu kukumbatia kuozo
Lazima tumpe thanks, Wanajamvi tumfurahie.

JF Moderator2 huyu ni hodari, Mtauni humkani
SIHABA baba jasiri, wala hataki utani
Hakuna kutafakari, mwanajamvi si muhuni
Pongezi tumpe na jamvi kulifurahia.

Mwenzetu huyu si mgeni, Samora10 mwamjua
Mwenzetu si limbukeni, kusema anayoyajua
Samora10 hana utani, kwenye uovu hufichua,
Ni kijana muadilifu si kijana wakuchakachua.

Jaluo Nyeupe mwamjua, bilashaka mwamuona
Ni yeye tunaemjua, hakika yupo bayana
Haki huitetea, bila kubaguana
Jaluo Nyeupe ni rafiki hana kubaguana.

Na Lizzy na Husniyo msisite, ikawa tusionane
Wala tusijikokote, mlonayo muyanene
Mllipo mji wowote, mambo tuelimishane
Abebwae hujikaza, ukumbi tuuchangie

Nyani Ngabu, Babaubaya, michango nileteeni
Ninyi ndugu pia, shime tujitokezeni
Muhimu ni zetu nia, na wala sio thamani

Lizzy fanya kuniandikia, wapi yako maskani
Ndipo nitapokwambia, mchango umpe nani
Na mimi tafatilia, nizitie kibwetani

Hongera niwatumie, Kibunango na Babu Atakasema sirisiri
Na duwa tuwaombee, Rabi awape kivuli
Mungu awazidishie, duniani na peponi

Masikini_Jeurina na Gurudumu hawa harambee, wapiga debe jamvini
Hawana ila ushee, imekuwa hamkani
Wamejifanya wazee, wao ndio makarani
Posti nyingi wanaandika hapa jamvini,

Muhogo mchungu kwa siri au dhahiri , atoae yujamvini
Uziitazo ghururi , mwenyewe amezibuni
Unenayo yafikiri, usijeitwa fatani

Mwaminifu thread ulozitunga,zitawafika wahunzi
Wale wasije kulonga,uloanza mwanafunzi
Wapita ukiwachonga,kwa vile una kurunzi

Ki Mey hutenda mengi ya dini, habanduki kanisani
na posti nyingi jamvini, hukaribisha na wageni
na ibada za nyumbani, hatutaki hata wageni.

WomanOfSubstance
Na kama wapendelea, usitajwe hadharani
Kwa kuwa unahofia, mambo fulani fulani
Ninakuhakikishia, taweka siri moyoni


Maxishimba uchunge mwenendo wako , wende mwendo wa kupima
Utunze twabiya zako , ujuwe baya na jema
Kama hujali wenzako , kutenda ya kuwauma
Ngoja nawe siku yako , utendwe bila huruma

Kakajambazi, yeye huyu si mwizi, na tena ye si jambazi
Kanilaghai kiujuzi, kwa jinale jamvini
Huyu yeye si jinamizi, akatuchuna na ngozi
Kakajambazi ni mwema mwenzetu jamvini.

Tatiana Kashika kuwasafisha, jamvini harufu waridi
Kutwa atuhamakisha, kuwa yeye ni shahidi
Posti zake zisokwisha, za tamu tena jadidi

Sulphadoxine Unasi ghamu ghalati, siugenini jamvini
Siraji ng'aza sirati, uongoze Furusani
Chifunaga kapaza sauti, Mwamuska si mwoga jamvini
MANYANZA taabani, hali hana hamu.


Mawazo1109 ni wetu sote, hima tusaidiane
Wa mbele tuwafuate, haya tusioneane
Kwa hili natusitete, bali tusikilizane
Abebwae hujikaza, ukumbi tuuchangie.

GT wake mdogodogo mwendo, wajulikana zamani
Mwendo usio vishindo, haufeli abadani
Asoweza huwa kando, awezae huwa ndani



Nami MWAJAMVI MIMI, Mohammed Shossi
Tungo zangu siwanyimi, nawapenda kiukweli,
Tena mara kumi kumi, tena na kwa kila hali,


Ambao sijawataja, lipo shairi jingine,
Sote tungali pamoja, kwa mema tuombeane,
Tusichoke zetu hoja, hivyo na tushikamane,
 
Realman wanichesha, meneja uso kitambi
Tungo hujasherehesha, usije niwacha kwa kumbi
Nadhani mdomo wakuwasha,ukazungumza kimatumbi
Kana unaumwimbi,si ungekula tambi?
Duh nimechoka maneno sina

Meneja kitambi cha nini, yeye wake weredi.
Kwa ujanja mjini, umahiri nawazidi.
Mapromota wa nini, kama meneja si fisadi?
Umeneja wanifaa, haki zako nizilinde.

Mo kipaji unacho, Maulana umshukuru
Wengine wana kijicho, wanapita hawashukuru
Utausahau mchacho, kipaji kukuweka huru
Umeneja wanifaa, haki zako nizilinde.
 
ulijuwa kufariji, allah akakukareem.
ikawa mujib kuwapokea , wale walio muhimu
ukakupamba kwa huba , na ucheshi hakukunyima.

ukayapita mapana , kumridhisha kila muungwana..
ikawa ni tunu , kuwatunuku na siha kuwajulia..
hayupo mfano wako , ndani ya hii dunia..
akujaalia rahim , kwa siha na ukareem...



usinicheki ndio najifunza okay??) heheheh lol mpaka umenitia bilisi lol..


Wala sitakucheka hilo shaka ondoa
Umenitahidi hoja kupangilia
Unataka kuwashinda malenga walotangulia
Maneno yako tiba yashinda za asilia
Ukarimu wako ni sifa alokupa Jalia

Haya sasa aamka ghani kutupatia
Uzipange kwa ubeti wala si zakutupia
Utujuze yako hali na aila yako pia
Usinisahau kwa dua pamoja na nabia
Mungu atkupe ya kheri na wanajamvi pia
Sitachoka kukutunza hadia


Kaditama namaliza kwa kuusia
Uwache kumcha Allah na mtume kumsalia
Uwarehemu wazazi wote walotangulia
Ulichona tugawane alokutunuku Jalia
Siwezi kukiweka bayana kila moja talila
Najua wengi wakitaka na wanakifatila.
 
Meneja kitambi cha nini, yeye wake weredi.
Kwa ujanja mjini, umahiri nawazidi.
Mapromota wa nini, kama meneja si fisadi?
Umeneja wanifaa, haki zako nizilinde.

Mo kipaji unacho, Maulana umshukuru
Wengine wana kijicho, wanapita hawashukuru
Utausahau mchacho, kipaji kukuweka huru
Umeneja wanifaa, haki zako nizilinde.

Mameneja mahasidi haki zetu kuziviza
Hamnatofauti na mafisadi pesa munazitukuza
Huwezi fanya mradi peso usio zaa
Lengo lako ufaidi, uniletee kizaazaa
Au ilikuwa midadi, umeneja kuukuza?
Sidhani kama umweledi, ujuzi wangu kuukuza
 
Baraza la kiswahili wanafanya nini sasa kumbe vipaji tunavyo humuhumu jamii forum ninyi ndio mlitakiwa muongoze kweli nimekupa saluti kipaji uacho mzee hongera sana man!

Mimi ningali mwanafunzi katika hii tansia
Bado singuli kutunga nje ya tanzania
Baraza watu mahiri Kimensera acha kutania
Ila umetoa wazo zuri kazi talifanyia
Sivibaya kuijenga lugha yetu sawia
Nawe pia umo njoo tupige kasia
Usijitoe kundini kusema utenzi ni kadhia
Tungo huleta faraja penye dhiki na ghasia
Malenga hutoa hoja za msingi na wosia
Namaliza kukuomba tunga japo kwa kukisia.
Wajuzi walo jamvini watakufunda kiintelejensia.
Utakuwa mahiri na kuwapiku na waasia.
 
Darlington wangu nini kimekusibu
Hekima zako zimwage usiwe kama bubu
Fikra zako mwanana tamu kama zabibu
Malenga wakusubiri wa dar na bububu
Hakuna asiekujua unaeng'aa kama balbu
Haya fanya hima utuletee majibu
Na upate wasaa ueleza kinachokusibu
Tungo utuletee ukivunje na kibubu
Zilizoficha za hemima ulizoridhi kwa mababu
 
Wadau nawauliza mbona mmeingia mitini
Au mwajipanga ili mnawiri jamvini
Ngongoja si mambo naona hamnithamini
Au nahau zimekishwa mnagoogle netini
Kama umalenga umewashinda nendeni uvuvini
Huko mliwe na papa na nyangumi baharini
 
Sasa umetamanisha, kujifunza mashairi
shabani robati amsha, tufunze yako shairi
medani nimechemsha, wapi vitabu shairi
 
Sasa umetamanisha, kujifunza mashairi
shabani robati amsha, tufunze yako shairi
medani nimechemsha, wapi vitabu shairi

Tena utumie fasihi hoja kusherehesha
Usije uneokana kioja ukajachekesha
Utume na nahau kiswahili kukisherehesha
Lete nyingi fakuri zile zenye bashasha
Usichokoze vigori ukadhaniwa ni basha
Vigori niwachiie mie nwape mshawasha
 
Mameneja mahasidi haki zetu kuziviza
Hamnatofauti na mafisadi pesa munazitukuza
Huwezi fanya mradi peso usio zaa
Lengo lako ufaidi, uniletee kizaazaa
Au ilikuwa midadi, umeneja kuukuza?
Sidhani kama umweledi, ujuzi wangu kuukuza

Hahahahahaaaaaaaaaaaaaaaaaaa,
Marijani ajuta meneja kukosekana,
Kazi za babaye mtaani zapatikana,
Familia haipati cha maana,
Usipuuze mameneja haki kuzikinga.

Lionel Mess wake ujuzi,
Lakini meneja hampuuzi,
Dunia leo sio ya juzi,
Mwenye kuijua njia mwache aongoze

CBE mikataba umefunzwa,
Muhimu sheria kujuzwa,
Ili njiani usije kwazwa,
Copy raiti wakumbuka?

Meneja mikataba najua,
Fungamtama anazingua,
Yake dowans tunajua,
Realman si Fungamtama.

Mo wewe kweli malenga,
Mashairi yako ni mwanga,
Mimi sijui vina kutunga,
Usibanie umeneja
 
Mkuu kazi njema kabisa!!:clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2:
 
Mkuu kazi njema kabisa!!:clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2:

Si kazi njema kabisa bali tungo za kisasa
Usinitie bashasha moto kuuendeleza
Wameingia mitini wanajmvi mpaka sasa
Simuoni PJ amniacha kwenye giza
Wiselady hakunijibu kile kisa
Nilimtaka ujira kisha akanyamaza
Na wewe ndugu upo wapi sasa
Nakumbuka ahadi utatembelea mbeza
Bado upo mjini au umepatwa na mkasa?
Sharifu akusubiri anamengi ya kukujuza.
Fanya hima wende safari unangoja nini sasa?
 
Hahahahahaaaaaaaaaaaaaaaaaaa,
Marijani ajuta meneja kukosekana,
Kazi za babaye mtaani zapatikana,
Familia haipati cha maana,
Usipuuze mameneja haki kuzikinga.

Lionel Mess wake ujuzi,
Lakini meneja hampuuzi,
Dunia leo sio ya juzi,
Mwenye kuijua njia mwache aongoze

CBE mikataba umefunzwa,
Muhimu sheria kujuzwa,
Ili njiani usije kwazwa,
Copy raiti wakumbuka?

Meneja mikataba najua,
Fungamtama anazingua,
Yake dowans tunajua,
Realman si Fungamtama.

Mo wewe kweli malenga,
Mashairi yako ni mwanga,
Mimi sijui vina kutunga,
Usibanie umeneja

Asante sana ndugu Mola akupe fanaka
Wala usijiweke nyuma twende utafika
Msingi bora unao njoo tulikomboe taifa

Ombi lako nafikiri jibu nitakupatia
Kama sheria najua labda mkzo kutia
Haki zangu haziibwi ataedhubu tajutia

Dunia imeharibika kila mmja mwogope
Anaweza jifanya mwema kumbe sawa na dope
Akakutia shimoni ukakwama kwenye tope
Subiri nifikirie na yawache mapepe.
 
Shukrani zangu za dhati kwenu waungwana
Hamkusita kunipongeza na kushia kuguna
Mimi muungwana nawaombea kwa Rabana
Yeye mstahiki mwenye sifa mwanana
Unadhani tungekuaje kama pumzi angebana?

Nyie ndio msingi nyie ndio kioo
Siwezi wadhikaki nikawaona kideo
Nistakuwa na ihsani nispowashukuru leo


Pongezi nawapa na wasiochangia pia
Wapo kashindwa kuchangia
Muda wao adhim si waliutumia
Wakasoma tungo na nahau pia
Shukrani wandugu wote mlochangia.
Mmoja mmoja kwa mafungu majina nimepangia.

The Following 32 Users Say Thank You to Mohammed Shossi For This Useful Post:
afrodenzi (Yesterday), Asprin (Yesterday), Bubu Ataka Kusema (Yesterday), engmtolera (Today), Fidel80 (Yesterday), Freestyler (Yesterday), Gurudumu (Yesterday), GY (Yesterday), Henge (Yesterday), Inkoskaz (Yesterday), Kaizer (Yesterday), KakaJambazi (Yesterday), Katavi (Yesterday), Kiraka (Today), LD (Yesterday), Mawazo1109 (Yesterday), Michelle (Yesterday), Miss Judith (Yesterday), MwanajamiiOne (Yesterday), Mzee Mwanakijiji (Yesterday), Nguruvi3 (Today), NILHAM RASHED (Today), RealMan (Yesterday), Rose1980 (Yesterday), Shapu (Today), Teamo (Yesterday), The Finest (Yesterday), VoiceOfReason (Yesterday), Wa Ndima (Yesterday), WiseLady (Yesterday), WomanOfSubstance (Yesterday), Yo Yo (Yesterday)​
 
Usingizi siupati, kkwa kuwa upo mbali,
Naghani kila wakati,mimi kwako sina hali,
Nakungoja kwa chati, nimeingiwa na muhali,

Jamvini nakungojea, kwa mahaba na bashasha,
Malenga ulobobea, kiu yangu ya tenzi kuishusha,
Furaha kuniletea, maishani kunitosha,

Pambo la mwangu jamvini, pekee kwenye dunia,
Busara zako jamvini, hakuna wa kufikia,
Jichoni mwangu u mboni, wewe wanonyesha njia,

Hata niwapo dhaifu, we wanifanya imara,
Tenzi yangu sadikifu, hakika watia fora,
Nami s'achi kukusifu, hata mara hamsa ashara,.

Ujembe wako umeshibashiba, bila ya choyo chochote,
Kwa hekima zako na huba, fikrazo tunashea wote
Umejawa na mahaba, nilikesha nikupate,

Najua fulani, amekasirika sikifani
Ila we mwandani usiache kughani
Tenzi zenye burdani kutumwagia jamvini
Siziwe za wastani zenye vina namizani
Akikumwa njiani me nitakuchukua nyumbani
Usiogope mwandani, wenzio waniwinda kwa ubani


nimekuwa bubu gafla
asante sana dear
kweli maneno yameni kimbia
:A S-rose::hug::busu
 
Hongereni ma great thinker mliotajwa, hakika mwastahili.
 
Hongereni ma great thinker mliotajwa, hakika mwastahili.

Nilingoja lako neno na wewe nikutaje
Mtoto uliye na hiba nikushau iweje
Mwenye ladha ya mapenzi na macho ya huba
Siku zote sikinai kwenye prof yako naganda kama luba
DaMie hupo nyuma kuchangia jamvini
Sasa noa panga na jembe tia mpini
Nani asojua mchango wako jamvini?


Napata tabu as natumia simu. Nikipost beti hjazikai inavyotakiwa I am out nikirudi nitaedit nakukupa sifa zako.
 
Hakika umetamba,
Tenzi kutaramba,
Mods kuwapamba,
Members kuwaimba,
Niaba ya Robot MTAMBA,
Shukurani kutoifumba,
Kwako tumeiumba,
Kwa tungo kujiramba
SHOSSI umebamba

Kanuni shika,
Hutoguswa hakika,
wale mlahaka,
walo na dhihaka,
JamiiForums siyo chaka,
Ni kiota kwa wahajaka,
SHOSSI umesomeka


 
Kweli kiswahili ni fani za watu Mohammed Shossi na JF Moderator na wengineo nawapeni heshima yenu maana kutunga shairi kama hili ni ngumu jamani. Vihisishi, vivumishi, vitenzi nawapeni sifa zenu. Hongereni sana!!!!
 
Back
Top Bottom