Nabofya kibodi yangu, salamu nazituma,
Kwenu marafiki zangu, natumai mu wazima,
Nawaombea kwa Mungu, mjaliwe yalo mema,
AfroDenzi, nakuzimia tangu MWANZONI,
Fikra zake ni huru, pia zina burudani,
Nami ninamshukuru, hachoki tangu zamani,
Mohammed Shossi, ooohh dear.
nimetamani kukuandikia shahiri
maneno matamu nimekosa..
nimetamani kutunga shairi
utenzi siiujui, kina ndo nini?
mistrari sijui yapangalia
lakini naamini maneno matamu
si lazima, shairi au Ngonjera,
naamini naweza kukuliwaza
na kukutuliza bila shairi..
napenda jinsi unavyo toa
maneno yako matamu
kwa kila anaye stahili
na ninashukuru kwa
michango yako mahiri..
samahani kwa kuchelewesha ujembe
lakini nadhani mlango bado u wazi..
Usingizi siupati, kkwa kuwa upo mbali,
Naghani kila wakati,mimi kwako sina hali,
Nakungoja kwa chati, nimeingiwa na muhali,
Jamvini nakungojea, kwa mahaba na bashasha,
Malenga ulobobea, kiu yangu ya tenzi kuishusha,
Furaha kuniletea, maishani kunitosha,
Pambo la mwangu jamvini, pekee kwenye dunia,
Busara zako jamvini, hakuna wa kufikia,
Jichoni mwangu u mboni, wewe wanonyesha njia,
Hata niwapo dhaifu, we wanifanya imara,
Tenzi yangu sadikifu, hakika watia fora,
Nami s'achi kukusifu, hata mara hamsa ashara,.
Ujembe wako umeshibashiba, bila ya choyo chochote,
Kwa hekima zako na huba, fikrazo tunashea wote
Umejawa na mahaba, nilikesha nikupate,
Najua fulani, amekasirika sikifani
Ila we mwandani usiache kughani
Tenzi zenye burdani kutumwagia jamvini
Siziwe za wastani zenye vina namizani
Akikumwa njiani me nitakuchukua nyumbani
Usiogope mwandani, wenzio waniwinda kwa ubani