Magoli matatu ya ushindi

Magoli matatu ya ushindi

Iko inaendelea vizuri tu ila ile story atupir ya kutosha tuumalizie
Kabisa uzuri JW hanaga mbambambaa kabisa kwenye story anatupia kitu roho inapenda mapemaa Story inaisha hakuna kuwekana!!
 
Sehemu ya 2
Ngurumo za radi zilisikika ishara ya kwamba mvua kubwa itanyesha muda si mrefu,mpaka wakati huo anilikuwa sijapata sehemu ya kulala!
Walianza kufunga hoteli huku wakiwa wanaongea lugha ambayo sikuielewa,ila kabla hawajafunga kabisa kuna mzee alikuja kutafuta chakula!
“Vipi huo ukoko haujaungua kama wa jana?”
“Leo uko vizuri babu!”
“Niletee si bei yetu ile?”
“Ndiyo babu!”
Yule mzee ilionekana ndiyo kawaida yake kuja kula ukoko kila siku wale wadada wakimaliza kuuza chakula!
Alikabidhiwa lile sufuria akaanza kulifakamia jungu lilikuwa na makoko mengi sana!
“Kijana karibu!”
“Ahsante mzee mimi tayari!”
Ulipita ukimywa kilichosikika ni sauti ya yule mzee akitafuna tu ukoko wake,baada ya nusu saa jungu lilikuwa jeupe kabisa!
Wale wadada walikuwa wamemaliza kuosha vyombo na kufunga,wakati yule mzee amemaliza akalipa anataka kuondoka mi bado nilikuwa pale,kitendo kile kiliwachanganya wale wadada ambao walianza kunifikiria labda nataka kuwatongoza,ila kilichowapa maswali ni begi nililokuwa nimebeba!
“Kaka si tunataka kufunga!”
Kauli ile ilikuwa kama msumari iliuchoma moyo wangu na kunipa mawazo mengi sana,ilibidi niseme ukweli kuliko kulala nje bora wanipe ruhusa nilale mle kwenye kile kibanda!
“Jamani mimi ni mgeni hapa!”
“MGENIIII?”
Walishtuka hadi yule mzee wa ukoko naye akageuka na kuniangalia kwa makini,bado sikujua kwanini watu wa kijiji hiki wanashtuka sana wakisikia neno “MGENI”.
“Ndiyo mi ni mgeni nimekuja hapa kufanya utafiti kuhusu tamaduni na maisha ya hapa,ni muandishi wa vitabu,naitwa Jack Mambo!
“Wewe kaka hiki kijiji hakipokei wageni kama nyie,tupishe tufunge sisi!”
Wale wadada walisema wakionekana kuwa hawana masikhara,nilijitetea lakini hakuna aliyenisikiliza kabisa,sikuwa na jinsi mpaka muda huo yule mzee wa ukoko alikuwa kimya hajasema kitu!
Nilijizoazoa taratibu na kibegi changu nikakiweka mgongoni,taratibu nkazipiga hatua zangu nikatoka nje!
Sikuwa najua pa kuelekea,sijui mtaa wowote sina mwenyeji wala mtu ninayemfahamu,nilishawahi kufanya tafiti mbali mbali ila kwa hii stori duh!
Nilianza kutembea nikiwa sijui naelekea wapi,wakati huo giza limeshaingia na mvua imeanza kunyesha taratibu!
Nilitamani kulia ila nilijikaza nikiamini ni changamoto ,japo kilichonipa hofu ni zile stori nilizosikia kuhusu Sumbawanga!
Nikiwa kwenye kuwaza ghafla nilishikwa mkono begani nikastuka sana,niligeuka nikakutana na yule mzee wa ukoko!
“Kijana unaenda wapi?”
“Sijui mzee wangu!”
“Nifuate!”
Alisema yule mzee kisha akaanza kuondoka,nilibaki nimesimama nikiwa na hofu kubwa lakini niliona hakuna jinsi!
Taratibu nilianza kuzivuta hatua zangu kumfuata yule mzee wa ukoko,haikuwa safari ndogo wala ndefu sana!
Mwisho tulifika sehemu ambayo kulikuwa na nyumba nyingi huku chache zikiwa zimeezekwa kwa bati!nyingi ziliezekwa kwa nyasi huku zingine zikiwa zimejengwa kwa nyasi kuanzia chini mpaka juu!
Safari ilitupeleka mpaka kwenye vijumba viwili vya udongo vilivyoezekwa kwa nyasi na vyote vilikuwa sehemu moja!
“Karibu kijana!”
“Ahsante sana mzee!”
“Ngoja nimgongee binti yangu atupe chakula!’
Nilishtuka kusikia yule mzee anataka chakula na huku ametoka kupakia jungu la ukoko tena mwingi tu!
Sikutaka kumuonyesha kuwa nimeshangaa nilitaka kiletwe hicho chakula nione yule mzee atakulaje na makoko aliyoyajaza tumboni!
Yule mzee alienda kwernye moja ya vile vijumba akagonga mlango,alitoka binti mmoja ambaye mwanga wa mbalamwezi ulisaidia kunionyesha urembo wa binti yule!
Alikuwa ni mrembo haswa!nakiri ni mmoja wa wanawake warembo niliyowahi kuwaona maishani!
Alifika akamsalimia ule mzee kwa kilugha chao kisha akanisalimia mimi pia kwa kilugha chao nikabakli nimeduwaa!
“Shikamoo!”
“Marahaba!”
Alipoona tu simuitikii akanisalimia kiswahili,kisha yule mzee akampa maelekezo akarudi kwenye kile kijumba chake!
Yule mzee alinichukua mpaka kwenye kile kijumba kingine,akawasha chemli,punde yule binti alikuja na chakula ambacho kilikuwa ni ugali na nyama!Nilikula kidogo tu nikawa nimeshiba,ila yule mzee alikula kama hajala ukoko nikabaki namshangaa tu,nikajiuliza au wako wawili!
Baada ya kumali
 
za kula ndipo akatoa kauli ambayo iliniacha kwenye wakati mgumu sana!
“Kijana mimi leo nalala na mama yako hapa,wewe kalale na binti yangu ila usimguse,kati ya vitu sitaki ukosee ni kufanya mapenzi na binti yangu!”
Kauli ile ilinishtua sana,kama ni mtihani ni ule,nilijiuliza nawezaje kulala na binti yule alivyo mrembo na nisimguse?
“Laikini mzee…!”
“Hakuna lakini kama huwezi nikurudishe nilipokutoa,nimekupa msaada sasa unataka nilale na mwanamke wangu na wewe humu ndani!?”
Mwisho niliamka na kuelekea kwenye kile kijumba cha yule binti nikagonga akanifungulia huku ananitazama kwa mshangao!
“Ni…ni….nimeambiwa nilale hu…huku!”
“Karibu!”

JE NINI KITAENDELEA?UNAHISI HUU MTIHANI UNAPITIKA KWELI?
 
Nilishafanya mitihani mingi hasa ya shule nikamaliza,sikujua kama ntakuja kukutana na mtihani mwingine kama huu!
Nilijiuliza nitawezaje kulala chumba kimoja na binti mrembo kaa yule nma nisiwaze kumgusa!
Baada ya kumwambia vile kuwa nimeambiwa nilale naye mle ndani,yule binti alinikaribisha ndani huku akionyesha kutokuwa na wasiwasi wowote jambo lililozidi kunitia wasiwasiw!
Yule binti alitandika chini kisha akataka mi nilale kwenye kile kitanda cha chuma chenye kigodoro cha pamba!
“Hapana wewe lala hapo juu mi ntalala chini!”
“hapana kaka wewe lala kitandani tu,wewe ni mgeni!”
Tulibishana sana ila sikukubali kulala kitandani,mwisho yule binti ambaye nilisikia yule mzee anamuita Regina akakubali kulala kitandani!
Nililala pale chini baridi lilikuwa kali kiasi cha kushawishi kumkumbatia yule dada tupeane joto!Ila nilipowaza kauli ya yule mzee kuwa nisifanye naye chochote nilituliza nyege zangu!
“Huku kutafutana ubaya tu,huyu mzee ananitafutia sababu tu aniroge anipeleke Gamboshi huyu!Anawezaje kumlaza Simba kwenye banda la swala?Ila hanipati kudadeki!”
Nilijisemea japo hisia zilikuwa kali,shetani alikuwa kazini anafanya kazi yake,usingizi ulikuwa mgumu sana siku ile!

Sijui nililala sangapi nilikuja kushtuka asubuhi jogoo anawika,nilifumbua macho nikaangalia kitandani sikumuona yule binti,nikajua tu alishaamka zamani,mabinti wa kijijini huamka mapema siyo kama wale wa mjini wanaokesha whatsap na insta!
Nilikurupuka nikajinyoosha,kwa mbali nilihisi mbavu zinauma sababu ya kulala chini,ila nilishukuru sababu nililala ndani kuliko kulala nje,halafu sehemu yenyewe ni Sumbawanga sasa!
Nilitoka nje nikamkuta yule mzee amewasha moto halafu amekaa pembeni yake,nilisogea pale sababu kulikuwa na baridi sana!
Nilichukua kigoda nikakaa pembeni ya yule mzee ambaye niligundua kwenye ule moto alikuwa anachoma viazi vitamu!
“Karibu kijana!”
“Ahsante sana shkamoo mzee wangu!”
“Marahaba kijana!”
Bado nilikuwa sijiamini amini,nilikuwa nawaza itakuwaje yule mzee akisema nimefanaya mapenzi na binti yake?
Ukimya ulitawala kati yetu muda huo yule mzee akatoa kiazi kimoja kwenye ule moto akanipatia!
Nilikipokea nikakiweka chini maana kilikuwa cha moto hatari,sijui hata yule mzee aliwezaje kukishika!
Muda huo yule binti alikuja akiwa amebeba maji,nikajua tu anatoka kisimani,nilipata muda sasa wa kumuona vizuri mrembo yule!
Dah!nilijisifu sana kuushinda mtihani ule,moyoni nilikiri nimekuwa sasa maana siyo kwa mtihani ule duh!
Nilipogeuza shingo kumuangalia yule mzee,nilikuta ananiangalia nikainama chini kwa aibu maana kaniona nilivyokuwa namtathimini binti yake!
“Hahahahahahah kijana!”
Alicheka yule mzee nisijue anacheka nini?nilikuwa mtu wa mashaka mashaka tu bado sikujiamini kabisa!
“Hongera kijana wewe ni mwanaume,uanaume siyo kufungua zipu tu hata ukijifunza kuifunga ni uanaume tena uanaume wa kweli!”
“Unamaanisha nini mzee wangu?”
“Namaanisha usiwe kama mbwa kila mgeni unambwekea tu ukiamni ni mtu mbaya!unaonekana utakuwa mgeni wa tofauti kuliko wageni wengine,kwa ajili yako naweza kuwaza kukishauri kijiji changu kianze kupokea wageni tena!”
“Wageni!!!!”
Niliuliza kwa mshangao cha ajabu yule mzee akaondoka zake huku anacheka,nilianza kuwaza namna nilivyopokelewa na wanakijiji wa pale,nilipounganisha na maneno ya yule mzee nilishindwa kuelewa,nikabaki na maswali mengi kichwani!
“WAGENI WANA NINI KWENYE HIKI KIJIJI?”
Licha ya kilichonileta nilitamani pia nifanye uchunguzi nijue kuna siri gani ya kile kijiji na wageni!
Yule binti alimaliza kuchota maji akachemsha uji na viazi tukanywa,muda ule yule mzee hakuwepo,alikuwa ameshaondoka zake!
Nilianza utafiti wangu kwa ajili ya kitabu changu kwa kumuuliza mambo mbali mbali yule binti ambaye alinipa ushirikiano wa kutosha kabisa!
Baada ya kumuuliza maswali yangu karibu yote ndipo nikaamua kumuuliza hili duku duku langu kuhusu wageni!
“Hivi Regina!”
“Rabeka!”
“Kuna kitu nataka nikuulize!”
“Kitu gani kaka halafu hujaniambia unaitwa nani?”
“Naitwa Jack Mambo!”
“Mmh aya unataka uniulize nini?”
“Oooh!nataka kujua kuna nini kwenye hiki kijiji mpaka wageni haw apokelewi vizuri?”
Swali lile lilimfanya Regina ainame chini na uso wake ukabadilika,ghafla akainuka akaacha kula na kuondoka!
Nilibaki njia panda yule mzee kasikia wageni kainuka akaondoka,Regina naye hataki kusema chochote,kuna nini katika kijiji hiki?wageni walikosea wapi?
JE NINI WAGENI WALIKOSEA WAPI HAPA KIJIJINI?USIKOSEEE
 
Safari yangu ilikuwa ni kufanya utafiti wa kitabu changu lakini sasa shauku kubwa niliyonayo ni kujua siri iliyopo kati ya wageni na hiki kijiji!Nilitaka kujua kwanini wageni hawapokelewi vizuri katika kijiji hiki?Kwanini wageni wanachukiwa hapa!
Baada ya Regina kuacha kula na kungia ndani kisa nimemuuliza kuhusu mgeni,nilimfuata ndani nikamkuta kakaa kitandani kainama analia kwa sauti kubwa mpaka nikaogopa!
“Regina una nini?mbona unalia?”
“Dada yanguJack,pengine hasingekuja mgeni hapa ningekuwa na dada mimi!”
Kauli yake ilianza kunipa picha kidogo kuhusu mgeni,japo sijajua mgeni alikuwa muuwaji au alikuwaje!
“Kwani Regina kuna nini?mbona sielewi?”
“huwezi kuelewa niache Jck siko sawa!”
Nilimuacha Regina nikatoka zangu nje,nikiendelea kuangalia mazingira mazuri ya Sumbawanga,hakukuwa na joto kubwa kama la Dar,hali ya hewa iliruhusu kabisa kuujaza ulimwengu!
Nilichukua kiti nikakaa nikiwa na mawazo yangu kichwani,kwenye ule mji kuna njia ya watu kupita kwenda kisimani,nilidhani nimeshaona wanawake wazuri kumbe nilikosea aiseeh!
Kuna mabinti walipita wanaenda kisimani aiseeh!nilijiuliza sana kile kijiji kina nini?mbona kina warembo namna hii,mabinti wale walipita huku wakionyesha kunishangaa sana!
Regina alitoka ndani akanikuta nimekaa pale,akanisogelea akaniambia…..
“Kaka Jack usipende kukaa nje wageni wanachukiwa kwenye hiki kijiji,wanaweza wakakufanyia kitu kibaya!
“Kwani kuna nini Regina mbona unanitisha sasa!”
“Sikutishi nakuambia ukweli chukua tahadhali,wageni waliacha vita kwenye hiki kijiji ,wageni ni maadui wa hiki kijiji!”
Kauli yake ilinifanya nisimame ili niulize maswali kadhaa kuhusu uadui wa kile kijiji na wageni!
“Unasema wageni ni maadui?kivipi?”
“Ni historia Jack!”
“nisimulie tafadhali!”
“Ntakusimulia kesho maana tukianza asubuhi tutamaliza jioni au kesho yake asubuhi!”
“mmh!”
Niliishia kuguna Regina akaendelea na mambo mengine,niliingia ndani nikakaa maana tayari Regina alishanitisha kuhusu kile kijiji!
Niliingia mitandaoni nikaanza kukagua stori zangu nikipitia huku na kule kusoma komenti za wadau mwisho nikaposti stori nikatoka!
Mtandao ulikuwa chnini sana hivyo sikuweza kukaa sana mtandaoni,usingizi ulinichukua nikalala mpaka Regina alipokuja kuniamsha mchana kula!
Niliamka nikala nikarudi ndani tena,jioni alikuja Mzee wa ukoko akatukuta tumekaa nje tunaota moto!
Tulisalimiana kisha Regina akaingia ndani na kutuacha wawili,mimi na mzee wa ukoko!
“Kijana!”
“Naam!”
“Unatokea wapi?”
“nimetokea Dar!”
“Unaonekana mstaarabu sana kijana!”
“Kwanini mzee wangu?”
“Hhahahahah!kijana mimi ni mtu mzima najua kutofautisha maziwa na chokaa!”
Tuliendelea kupiga stori za hapa na pale huku akinipa majibu ya maswali yangu kuhusu kile
kijiji,japo sikumuuliza tena suala la wageni sababu nilihofia kumkwaza!
Yule mzee alikuwa mcheshi sana alitaka kuzivunja mbavu zangu,stori zake hasa za ujana ziliniacha hoi kwa kicheko!
Regina alileta chakula tukala,kisha mzee akaniambia kauli ile ile ya jana hapo nikachoka zaidi!
“Kijana utalala na binti yangu leo pia,kumbuka masharti ni yaleyale usimguse mimi nalala na mama yenu leo!”
Niliinama chini nikashika kichwa bado sikujua kwanini yule mzee ananifanyia vile,niliwaza pengine ananitega aniue!
“Huyu mzee anataka nikosee masharti aniloge huyu siyo bure kabisa!”
Niliinuka nikaenda kwenye kijumba cha Regina nikiwa nimenyong’onyea hadi akanishtukia.
“Vipi kuna nini?”
“Hivi Regina kwanini baba yako ananilaza huku ananitakia nini?”
“Kwani unaogopa!?”
“hivi we unaona kawaida?ujue wewe mwanamke mimi ni mwanaume itakuwaje?”
“Usiwaze Jack wewe lala kama jana tu,baba ana kidemu chake siku hizi kinakuja usiku tuu kwahiyo usiwaze!”
“Ikitokea nimeshindwa kuvumilia Regina itakuwaje?”
Swali lile lilimfanya Regina aangalie chini kwa aibu muda huo na mimi hisia zimenikaba,bakora ikasimama,mpaka hapo nilihisi nafeli kabisa maana kwa jinsi tulivyokuwa karibu nilijikuta natamani kumkumbatia Regina!”
“Jack usiwaze ujinga lala kesho nikupe stori un ayoitaka,maana najua hiki sicho unachotaka kwangu!
Ni kama masikio yaliziba nikamsogelea karibu zaidi Regina,mpaka nikagusana naye,bakora yangu liyokuwa imesimama ikamgusa huku chini akashtuka!
“Jack ni nini hiyo?”

JE NINI KITAENDELEA?ITAKUWAJE MASHARTI YAKIVU
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom