Mafunzo ya JKT yamepitwa na wakati

ego

JF-Expert Member
Apr 10, 2013
1,620
1,407
Naomba kutofautiana na watanzania wengi ambao bado wanaamini JKT inawajengea vijana, uzalendo n.k

Jana nimeshuhudia ki video kikitembea mitandao kikionyesha vijana waki "craw" kwenye tope.

kwa kweli nilikuwa very much shocked na kujiuliza kijana wa leo akipelekwa katika kambi na kupewa mafunzo haya yanamjenga vipi kukabiliana na changamoto za leo.

kama taifa ni lazima tujue zama zipi tulizopo na je ni elimu gani tuwape vijana wetu kujenga taifa letu kama jina linavyosema.

nikirudi katika historia ninaweza kusema miaka ya zamani jamii zilikuwa na elimu za jando na unyago. Vijana walipelekwa katika makambi kufundishwa mbinu za kuwa kijana bora katika jamii ikijumuisha jinsi ya kutimiza shughuli za kifamilia na ulinzi katika jamii.

Zama hizo zilipita tukaingia katika zama za ukombozi na hapa vijana walihitaji kufundishwa ukakavu na uzalendo ambao enzi hizo ulikuwa na kupelekwa msituni kupambana kukomboa nchi zao kutoka mikononi mwa watu. Baada ya kupata uhuru, serikali zetu nyingi hazikuwa na nguvu za kuajiri majeshi ya kutosha kulinda nchi zao na enzi hizo jamii zetu zilikuwa zimekumbwa na migogoro ya vita vya wenyewe kwa wenyewe na vita kati ya nchi moja na nyingine. Katika mazingira yale huo ndiyo ulikuwa uzalendo.

Lakini leo hii mazingira yamebadirika, jamii inakabiliwa na tatizo na kugawa rasilimali bila kufaidisha nchi zao, jamii zinakabiliwa na wingi wa wasomi kutoka katika mifumo ya elimu na kukosa ajira, tunakabiliwa na jamii ambazo masokoni kumejaa bidhaa za kigeni tena zinazoweza kutengenezwa kwa ujuzi kidogo tu.

bado tunakumbatia elimu ya miaka ya 60 na tukiamini tunajenga uzalendo.

Uzalendo wa miaka ya 60 ni mtu kwenda msituni kukomboa nchi yake lakini uzalendo wa mwaka 2000 ni mtu kuacha kuagiza nguo china na kufungua sehemu ya kushona nguo hizo hizo kwa ubora huohuo.

Uzalendo wa miaka ya 60 ilikuwa ni mtu kufundishwa kula chakula katika mazingira magumu maana hayo ndiyo vijana walitarajia katika kukomboa mataifa yao lakini uzalendo wa miaka ya 2000 ni kijana kuelimishwa kukataa kugawa rasilimali za taifa kwa vizawadi vidogo na jamii ielewe kuwa matajiri wanaotajirika kwa kugawa rasilimali zetu ni laana kwa taifa.

uzalendo wa miaka ya 60 ulikuwa wa kijeshi lakini uzalendo wa miaka ya 2000 ni wa uchumi zaidi maana tayari tuna uhuru wa bendera lakini bado tu watumwa kiuchumi.

Sioni ni kwa namna gani hizo program za JKT zinajenga taifa letu.

Wanasema zizi lisilokuwa na ndama halina "future" na nguzo ya taifa lolote ni vijana lakini iwapo vijana watajengwa katika kupeleka fikra zao kuendana na wakati ujao.

Je tumewahi kufanya utafiti hawa vijana wanaotoka jkt wanakuwa na impact gani katika jamii au tunatengeneza walinzi wa makampuni binafsi na ndivyo tunajenga nchi yetu?
 
Upo sawa kiasi Mkuu ila toa pendekezo kwa majeshi yetu yakitaka kuajili yatumie njia gani kuwafunza Askari wake bila kupitia jkt, pia jkt inawafundisha vijana mambo ya uzalishaji mali unajua hilo? Kwahiyo vijana unaowaona wametoka jeshini na hawana direction basi ujue ishu nyingine ni mitaji mkuu hamna ila vijana wana ujuzi vichwani mwao.
 
Ungeelezea kinachofanyika huko jkt kisha ufafanue jinsi kisivyokuwa na faida kwa mwendaji. Zaidi ya hii porojo uliyoandika. Kwanza ulienda jkt? Kama jibu ni ndio lini na intake gani?

Mbinu mojawapo ya kupima ubora unaopatikana huko ni kuwatazama wale waliotoka huko wamekuja na maarifa gani ukilinganisha na ambao hawajaenda. Lakini ukiona ubora unapimwa kwa kuulizwa wewe ni intake gani, ya lini? Hizi ndizo porojo

mimi ninachokisema vijana wafundishwe kufanya mapinduzi katika kilimo na tuone wanaotoka jkt wanaanzisha mashamba ya kilimo na kuonyesha umuhimu wa jkt katika jamii.

lakini kama tutabakia kuchukulia jkt kama pre intake ya kuingia jeshi na kama sifa za kuajiriwa katika makampuni ya ulinzi binafsi hatujengi taifa.

Ukipita mitaani sifa za vijana waliotoka jkt ni zipi? je ni kuwa wagomvi au wabuunifu?

bado nasisitiza jkt imepitwa na wakati na tunaweza kukomboa vijana wetu kwa kuwa na program za kuwajengea uthubutu wa kiuchumi, kuwajengea fikra za kiuchumi, kuchokonoa economic creativity n.k
 
Upo sawa kiasi Mkuu ila toa pendekezo kwa majeshi yetu yakitaka kuajili yatumie njia gani kuwafunza Askari wake bila kupitia jkt, pia jkt inawafundisha vijana mambo ya uzalishaji mali unajua hilo? Kwahiyo vijana unaowaona wametoka jeshini na hawana direction basi ujue ishu nyingine ni mitaji mkuu hamna ila vijana wana ujuzi vichwani mwao.
Sina shida na mfumo wao wa mafunzo kwa wanaoingia jeshini uweje shida yangu ni mfumo wa jkt ya hiari na vijana wanaomaliza kidato cha sita mafunzo wanayopewa siyo sahihi.
Wengi wanaingia huko wakiwa na matumaini ya ajira na nimeshudia wengi wakitoka huko bado wanakuwa na fikra zilezile kuhusu ajira. hakuna ubunifu unaoonekana kuongezeka au mtu kuupata na akitoka huko uone anajaribu kutumia fursa zilizoko katika jamii.

mfano mimi watu wengi ambao nilisoma nao waliojiajiri na kufanikiwa ni wale ambao walikuwa wanafanya kwenye makampuni ya sales na wakatoka wakaanza kufanya shughuli zilezile peke yao na kwa mafanikio makubwa. Kwa watu ambao wamekuwa wakifanya shughuli nyingine, wengi wameshindwa kuingia kwenye ujasiliamali.

Tulichotegemea ni vijana waende kufanyiwa incubation ambayo wakitoka huko wana mawazo kuanzia a kwenye production mpaka kufikia kwa customer mtaani na mtoto akitoka pale anaanza mtaani.

kama ni killimo tulitegemea mtoto akitoka jkt anaweza kuchukua ekari moja ya shamba, kuzalisha na kutafuta masoko

kama ni biashara tulitegemea mtoto akitoka jkt anajua kuzunguka katika saiti za ujenzi kutafuta supply ya vifaa na kujua vinakouzwa anapata commision kwa kujifanya mtu wa kati

kama vijana wote wanapita jkt tulitegemea wawe na uelewa sahihi wa historia ya nchi, siyo kukalili majina ya viongozi bali kuelewa dira ya tulikotoka na tunakoelekea

tulitegemea kama ni uzalendo vijana wafundishwe ni kwa jinsi gani mkulima anakuwa mzalendo kwa nchi yake, mfanyakazi anakuwa mzalendo kwa nchi yake, mfanyabiashara anakuwa mzalendo kwa nchi yake katika kutokupenda kuona nchi yake ikiharibikiwa kiuchumi, ki amani, kiustawi wa tamaduni na mila zetu n.k

lakini tusikae kupiga slogan ambazo ukizitazama on ground hakuna tunachokifanya na tunaendelea kujipongeza
 
Majeshi yote duniani mambo ya ku craw lazima ukutane nayo
Kukimbizwa mchakmchaka kurushwa viunzi, kichurachura hiyo ndiyo jeshini
Hapo unajengwa ukakamavu tu

Ova
 
Sina shida na mfumo wao wa mafunzo kwa wanaoingia jeshini uweje shida yangu ni mfumo wa jkt ya hiari na vijana wanaomaliza kidato cha sita mafunzo wanayopewa siyo sahihi.
Ni sahihi kwa mfumo wa kijeshi ila sio sahihi kwa vijana wa form six ile ya kwa mujibu ingawa kwao ina muhimu kidogo, jeshini bado wanatumia mfumo ule kwaajili ya kuhakikisha ukakamavu kwa vijana wao ambao wengine wanaweza kujiunga na majeshi mbalimbali.

Maana naona mkuu umejikita zaidi kwa vijana wanaoludi mitaani ila nao bado wanahesabika kama askari ndio maana mda wote wanahitajika kuwa wakakamavu na utayari wa kimwili pamoja na akili kwahiyo wapo sahihi sana katika mifumo ya kijeshi wala haina ubaya wowote mkuu
 
Naomba kutofautiana na watanzania wengi ambao bado wanaamini JKT inawajengea vijana, uzalendo n.k

Jana nimeshuhudia ki video kikitembea mitandao kikionyesha vijana waki "craw" kwenye tope.

kwa kweli nilikuwa very much shocked na kujiuliza kijana wa leo akipelekwa katika kambi na kupewa mafunzo haya yanamjenga vipi kukabiliana na changamoto za leo.

kama taifa ni lazima tujue zama zipi tulizopo na je ni elimu gani tuwape vijana wetu kujenga taifa letu kama jina linavyosema.

nikirudi katika historia ninaweza kusema miaka ya zamani jamii zilikuwa na elimu za jando na unyago. Vijana walipelekwa katika makambi kufundishwa mbinu za kuwa kijana bora katika jamii ikijumuisha jinsi ya kutimiza shughuli za kifamilia na ulinzi katika jamii.

Zama hizo zilipita tukaingia katika zama za ukombozi na hapa vijana walihitaji kufundishwa ukakavu na uzalendo ambao enzi hizo ulikuwa na kupelekwa msituni kupambana kukomboa nchi zao kutoka mikononi mwa watu. Baada ya kupata uhuru, serikali zetu nyingi hazikuwa na nguvu za kuajiri majeshi ya kutosha kulinda nchi zao na enzi hizo jamii zetu zilikuwa zimekumbwa na migogoro ya vita vya wenyewe kwa wenyewe na vita kati ya nchi moja na nyingine. Katika mazingira yale huo ndiyo ulikuwa uzalendo.

Lakini leo hii mazingira yamebadirika, jamii inakabiliwa na tatizo na kugawa rasilimali bila kufaidisha nchi zao, jamii zinakabiliwa na wingi wa wasomi kutoka katika mifumo ya elimu na kukosa ajira, tunakabiliwa na jamii ambazo masokoni kumejaa bidhaa za kigeni tena zinazoweza kutengenezwa kwa ujuzi kidogo tu.

bado tunakumbatia elimu ya miaka ya 60 na tukiamini tunajenga uzalendo.

Uzalendo wa miaka ya 60 ni mtu kwenda msituni kukomboa nchi yake lakini uzalendo wa mwaka 2000 ni mtu kuacha kuagiza nguo china na kufungua sehemu ya kushona nguo hizo hizo kwa ubora huohuo.

Uzalendo wa miaka ya 60 ilikuwa ni mtu kufundishwa kula chakula katika mazingira magumu maana hayo ndiyo vijana walitarajia katika kukomboa mataifa yao lakini uzalendo wa miaka ya 2000 ni kijana kuelimishwa kukataa kugawa rasilimali za taifa kwa vizawadi vidogo na jamii ielewe kuwa matajiri wanaotajirika kwa kugawa rasilimali zetu ni laana kwa taifa.

uzalendo wa miaka ya 60 ulikuwa wa kijeshi lakini uzalendo wa miaka ya 2000 ni wa uchumi zaidi maana tayari tuna uhuru wa bendera lakini bado tu watumwa kiuchumi.

Sioni ni kwa namna gani hizo program za JKT zinajenga taifa letu.

Wanasema zizi lisilokuwa na ndama halina "future" na nguzo ya taifa lolote ni vijana lakini iwapo vijana watajengwa katika kupeleka fikra zao kuendana na wakati ujao.

Je tumewahi kufanya utafiti hawa vijana wanaotoka jkt wanakuwa na impact gani katika jamii au tunatengeneza walinzi wa makampuni binafsi na ndivyo tunajenga nchi yetu?
Majukumu ya jkt Kwanza ni yepi mkuu

Ova
 
Sina shida na mfumo wao wa mafunzo kwa wanaoingia jeshini uweje shida yangu ni mfumo wa jkt ya hiari na vijana wanaomaliza kidato cha sita mafunzo wanayopewa siyo sahihi.

Majukumu ya jkt Kwanza ni yepi mkuu

Ova
Naomba nikukumbushe baadhi ya mambo kutoka katika historia

1. Mafunzo ya JKT yalivyonzishwa

"Kuanzishwa kwa JKT, kulitokana na mawazo ya Umoja wa Vijana wa Chama cha TANU (TANU Youth League), katika Mkutano wao Mkuu uliofanyika mjini Tabora tarehe 25 Aug 62, chini ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja huo, hayati Joseph Nyerere"


Tarehe 19 Apr 63, Baraza la Mawaziri la Tanganyika chini ya Rais wa Jamhuri ya Tanganyika na Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere, lilipitisha Azimio la umoja wa vijana wa TANU na kuamua kwa kauli moja kuazishwa JKT mnamo tarehe 10 Jul 1963. Kundi la kwanza lilipata mafunzo katika kambi ya Mgulani Dar es salaam likiwa na jumla ya vijana 11 toka wilaya 11 tofauti.



Vijana hao wa mwanzo walikuwa makatibu wa umoja wa vijana ambao walikwishapelekwa na TANU huko Yugoslavia mwaka 1962, kuchukua mafunzo ya uongozi wa vijana. Baadhi ya vijana hao watangulizi ni Bi. Z. Kiango, Bw. S. Chale, Bw. P. Lwegarulira, Bw. R. Kamba, Bw. H. Ngalason, Bw, J.Ndimugwango, Bi. M. Mhando (Senior Guide), Bw. D. S. Msilu (Master), Mr ES Mwakyambiki, (Senior Master) na Mr AI Msonge (Master), Mr LM Mitande.



Ulipofika mwezi Agosti, 1963 kikundi kingine cha watu watano kikiwa na Bw. S. Desai, Bw. E. Simkone, Bw. J. Mwanimlele (Asst Master) na Bw. A. A Moyo (Asst Master) kilijiunga na kupata pia mafunzo ya uongozi.



Kwenye uzinduzi wa JKT, Mwalimu Nyerere alisema Umuhimu wa JKT unatokana na Taifa kuhitaji huduma ya vijana na vijana kuitikia wito huo wa kulitumikia Taifa lao kwa jukumu lolote lihitajiwalo." Source ni website ya JKT


2. Unaweza kuona kuwa mafunzo haya yalianzishwa kwa Mahitaji ya wakati huo.

mwaka 1975 kulifanyika mabadiriko kutokana na mahitaji yaliyokuwepo wakati huo ya kuunganisha JKT na JWTZ

3. Hoja ya yangu ya leo ni je wazo hili la jkt liliasisiwa na vijana leo hii tunahitaji kufanya mabadiriko? au kuendelea na mfumo tulioutengeneza mwaka 1975? Nikukumbushe kuwa kwa mujibu wa kumbukumbu zinasema

"ili kuimarisha ulinzi wa Taifa, JKT liliungana rasmi na JWTZ mwaka 1975 hivyo kulifanya JKT kuwa moja ya Kamandi zilizochini ya JWTZ"

Swali la kujiuliza leo hii ni je kwa mahitaji ya vijana wa leo, maana vijana ndiyo walikuwa waasisi wa wa JKT, je bado tunahitaji JKT kuwa moja ya kamandi za JWTZ au chombo hiki tukiweke kukabiliana na hali ya sasa ya vijana kwa kukiweka kuwajenga vijana kiuchumi zaidi, kuwapa vijana uzoefu wa kiuchumi na uthubutu wa kiuchumi?
 
Nimepita jkt ,faida kubwa nilizozipata Ni kutumia bunduki kwa ufasaha,ukijichanganya naondoka na kichwa changu,nimefundishwa ukakamavu, skills za ulinzi na usalama nimezipatia jkt,,pia uzalishaji Mali nimefundishwa jkt

Sasa kwanini nisipasifu huko, Makutupola ndo ilikuwa kambi yangu miaka Ile, nilienjoy Sana kwakweli!!!
 
Naomba nikukumbushe baadhi ya mambo kutoka katika historia

1. Mafunzo ya JKT yalivyonzishwa

"Kuanzishwa kwa JKT, kulitokana na mawazo ya Umoja wa Vijana wa Chama cha TANU (TANU Youth League), katika Mkutano wao Mkuu uliofanyika mjini Tabora tarehe 25 Aug 62, chini ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja huo, hayati Joseph Nyerere"


Tarehe 19 Apr 63, Baraza la Mawaziri la Tanganyika chini ya Rais wa Jamhuri ya Tanganyika na Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere, lilipitisha Azimio la umoja wa vijana wa TANU na kuamua kwa kauli moja kuazishwa JKT mnamo tarehe 10 Jul 1963. Kundi la kwanza lilipata mafunzo katika kambi ya Mgulani Dar es salaam likiwa na jumla ya vijana 11 toka wilaya 11 tofauti.



Vijana hao wa mwanzo walikuwa makatibu wa umoja wa vijana ambao walikwishapelekwa na TANU huko Yugoslavia mwaka 1962, kuchukua mafunzo ya uongozi wa vijana. Baadhi ya vijana hao watangulizi ni Bi. Z. Kiango, Bw. S. Chale, Bw. P. Lwegarulira, Bw. R. Kamba, Bw. H. Ngalason, Bw, J.Ndimugwango, Bi. M. Mhando (Senior Guide), Bw. D. S. Msilu (Master), Mr ES Mwakyambiki, (Senior Master) na Mr AI Msonge (Master), Mr LM Mitande.



Ulipofika mwezi Agosti, 1963 kikundi kingine cha watu watano kikiwa na Bw. S. Desai, Bw. E. Simkone, Bw. J. Mwanimlele (Asst Master) na Bw. A. A Moyo (Asst Master) kilijiunga na kupata pia mafunzo ya uongozi.



Kwenye uzinduzi wa JKT, Mwalimu Nyerere alisema Umuhimu wa JKT unatokana na Taifa kuhitaji huduma ya vijana na vijana kuitikia wito huo wa kulitumikia Taifa lao kwa jukumu lolote lihitajiwalo." Source ni website ya JKT


2. Unaweza kuona kuwa mafunzo haya yalianzishwa kwa Mahitaji ya wakati huo.

mwaka 1975 kulifanyika mabadiriko kutokana na mahitaji yaliyokuwepo wakati huo ya kuunganisha JKT na JWTZ

3. Hoja ya yangu ya leo ni je wazo hili la jkt liliasisiwa na vijana leo hii tunahitaji kufanya mabadiriko? au kuendelea na mfumo tulioutengeneza mwaka 1975? Nikukumbushe kuwa kwa mujibu wa kumbukumbu zinasema

"ili kuimarisha ulinzi wa Taifa, JKT liliungana rasmi na JWTZ mwaka 1975 hivyo kulifanya JKT kuwa moja ya Kamandi zilizochini ya JWTZ"

Swali la kujiuliza leo hii ni je kwa mahitaji ya vijana wa leo, maana vijana ndiyo walikuwa waasisi wa wa JKT, je bado tunahitaji JKT kuwa moja ya kamandi za JWTZ au chombo hiki tukiweke kukabiliana na hali ya sasa ya vijana kwa kukiweka kuwajenga vijana kiuchumi zaidi, kuwapa vijana uzoefu wa kiuchumi na uthubutu wa kiuchumi?
Kwa sasa jkt majukumu yao wenyewe wanakuambia

1)nidhamu

2)uzalendo

3)ukakamavu

4)ujuzi

5)ulinzi wa taifa

6)maendeleo kiuchumi

Ova
 
Nimepita jkt ,faida kubwa nilizozipata Ni kutumia bunduki kwa ufasaha,ukijichanganya naondoka na kichwa changu,nimefundishwa ukakamavu, skills za ulinzi na usalama nimezipatia jkt,,pia uzalishaji Mali nimefundishwa jkt

Sasa kwanini nisipasifu huko, Makutupola ndo ilikuwa kambi yangu miaka Ile, nilienjoy Sana kwakweli!!!
Shida moja ya wanadamu ni kushindwa kujifanyia utathmini.

unakuta mtu anajigamba amefundishwa uzalishaji mali lakini ukimuuliza ni kitu gani umezalisha ambacho kwako kwenye jamii kinaonekana na nitofauti na wale ambao hawajapitia? unakuta hakuta ni slogan tu za mdomoni.

hakuna sehemu nimeenda nikakuta kitu cha tofauti na nikaambiwa ni vijana waliotoka jkt.

labda wewe una ushahidi tueleze umezalisha nini?
 
Mbinu mojawapo ya kupima ubora unaopatikana huko ni kuwatazama wale waliotoka huko wamekuja na maarifa gani ukilinganisha na ambao hawajaenda. Lakini ukiona ubora unapimwa kwa kuulizwa wewe ni intake gani, ya lini? Hizi ndizo porojo

mimi ninachokisema vijana wafundishwe kufanya mapinduzi katika kilimo na tuone wanaotoka jkt wanaanzisha mashamba ya kilimo na kuonyesha umuhimu wa jkt katika jamii.

lakini kama tutabakia kuchukulia jkt kama pre intake ya kuingia jeshi na kama sifa za kuajiriwa katika makampuni ya ulinzi binafsi hatujengi taifa.

Ukipita mitaani sifa za vijana waliotoka jkt ni zipi? je ni kuwa wagomvi au wabuunifu?

bado nasisitiza jkt imepitwa na wakati na tunaweza kukomboa vijana wetu kwa kuwa na program za kuwajengea uthubutu wa kiuchumi, kuwajengea fikra za kiuchumi, kuchokonoa economic creativity n.k
labda kwa kuwa sisi tz tulijengwa hivyo na wanasiasa wetu, lakini lengo kubwa ni kuwa na jeshi la akiba. nchi zingine vijana akifikisha miaka 21 ni lazima akalitumikie jeshi kwa mwaka1. so issue hapo sio kujifunza kilimo bora tu
 
Assume unampeleka jamaa anaye crow kwenye tope Ukraine!!
Tunazika siku hiyohiyo.
 
Hata makurutu wa Marekani wanacraw, chakuongeza labd tu wakitoka huko wapewe mitaji
 
Naomba kutofautiana na watanzania wengi ambao bado wanaamini JKT inawajengea vijana, uzalendo n.k

Jana nimeshuhudia ki video kikitembea mitandao kikionyesha vijana waki "craw" kwenye tope.

kwa kweli nilikuwa very much shocked na kujiuliza kijana wa leo akipelekwa katika kambi na kupewa mafunzo haya yanamjenga vipi kukabiliana na changamoto za leo.

kama taifa ni lazima tujue zama zipi tulizopo na je ni elimu gani tuwape vijana wetu kujenga taifa letu kama jina linavyosema.

nikirudi katika historia ninaweza kusema miaka ya zamani jamii zilikuwa na elimu za jando na unyago. Vijana walipelekwa katika makambi kufundishwa mbinu za kuwa kijana bora katika jamii ikijumuisha jinsi ya kutimiza shughuli za kifamilia na ulinzi katika jamii.

Zama hizo zilipita tukaingia katika zama za ukombozi na hapa vijana walihitaji kufundishwa ukakavu na uzalendo ambao enzi hizo ulikuwa na kupelekwa msituni kupambana kukomboa nchi zao kutoka mikononi mwa watu. Baada ya kupata uhuru, serikali zetu nyingi hazikuwa na nguvu za kuajiri majeshi ya kutosha kulinda nchi zao na enzi hizo jamii zetu zilikuwa zimekumbwa na migogoro ya vita vya wenyewe kwa wenyewe na vita kati ya nchi moja na nyingine. Katika mazingira yale huo ndiyo ulikuwa uzalendo.

Lakini leo hii mazingira yamebadirika, jamii inakabiliwa na tatizo na kugawa rasilimali bila kufaidisha nchi zao, jamii zinakabiliwa na wingi wa wasomi kutoka katika mifumo ya elimu na kukosa ajira, tunakabiliwa na jamii ambazo masokoni kumejaa bidhaa za kigeni tena zinazoweza kutengenezwa kwa ujuzi kidogo tu.

bado tunakumbatia elimu ya miaka ya 60 na tukiamini tunajenga uzalendo.

Uzalendo wa miaka ya 60 ni mtu kwenda msituni kukomboa nchi yake lakini uzalendo wa mwaka 2000 ni mtu kuacha kuagiza nguo china na kufungua sehemu ya kushona nguo hizo hizo kwa ubora huohuo.

Uzalendo wa miaka ya 60 ilikuwa ni mtu kufundishwa kula chakula katika mazingira magumu maana hayo ndiyo vijana walitarajia katika kukomboa mataifa yao lakini uzalendo wa miaka ya 2000 ni kijana kuelimishwa kukataa kugawa rasilimali za taifa kwa vizawadi vidogo na jamii ielewe kuwa matajiri wanaotajirika kwa kugawa rasilimali zetu ni laana kwa taifa.

uzalendo wa miaka ya 60 ulikuwa wa kijeshi lakini uzalendo wa miaka ya 2000 ni wa uchumi zaidi maana tayari tuna uhuru wa bendera lakini bado tu watumwa kiuchumi.

Sioni ni kwa namna gani hizo program za JKT zinajenga taifa letu.

Wanasema zizi lisilokuwa na ndama halina "future" na nguzo ya taifa lolote ni vijana lakini iwapo vijana watajengwa katika kupeleka fikra zao kuendana na wakati ujao.

Je tumewahi kufanya utafiti hawa vijana wanaotoka jkt wanakuwa na impact gani katika jamii au tunatengeneza walinzi wa makampuni binafsi na ndivyo tunajenga nchi yetu?
Sasa broo yale mashamba ya mahindi na maharagwe na zile ng'ombe bustani za mboga mboga na maua zitahudumiwa na akina nani
 
wenzako ukiteseka wao ndo furaha yao.
Sijawahi kupita huko.
Ila jeshi Kama una hasira hauliwezi
 
Nimepita jkt ,faida kubwa nilizozipata Ni kutumia bunduki kwa ufasaha,ukijichanganya naondoka na kichwa changu,nimefundishwa ukakamavu, skills za ulinzi na usalama nimezipatia jkt,,pia uzalishaji Mali nimefundishwa jkt

Sasa kwanini nisipasifu huko, Makutupola ndo ilikuwa kambi yangu miaka Ile, nilienjoy Sana kwakweli!!!
Yote hayo mimi nimeyapata nje ya JKT..

Acheni kupotezea vijana muda... Kwanza dunia hii kuandaa vijana kwa ajili ya vita ni kufikiri kijima.

Wapeni vijana vocational education wapeni mitaji waingie mtaani kupambana.

Mnaandaa mijambazi huko bure.
 
Back
Top Bottom