Mafunzo ya JKT kwa kujitolea kwa mwaka 2016

Mafunzo ya JKT kwa kujitolea kwa mwaka 2016

Vipi waliomaliza form four 2015 hawahusiki?
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, anawatangazia vijana wenye sifa za kujiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa kwa kujitolea kwa mwaka 2016.
Barua zilizoainisha sifa za kijana kujiunga na mafunzo ya JKT zimetumwa kwa Waheshimiwa Wakuu wa mikoa. Mchakato wa zoezi la kuwapata vijana wenye sifa unaanza Aprili 2016 hadi tarehe 20 Mei 2016.
Sifa za mwombaji ni kama zifuatazo:-
1. Awe raia halisi wa Tanzania.
2. Umri. Kwa vijana wenye elimu ya Darasa la saba hadi kidato cha sita ni miaka 18 hadi 23.Vijana wenye elimu ya Stashahada umri ni miaka 18 hadi 26 na Vijana wenye elimu ya Shahada na kuendelea umri ni miaka 18 hadi 30.
3. Awe na afya njema, akili timamu.
4. Asiwe na alama yeyote ya michoro mwilini (Tattoo).
5. Mwenye tabia nzuri, hajapatikana na hatia Mahakamani na hajawahi kufungwa.
6. Kwa vijana waliomaliza elimu ya Sekondari kidato cha nne wawe waliomaliza kuanzia mwaka 2010, 2011, 2012, 2013 na 2014 wenye ufaulu ufuatao:-
(a) Waliomaliza 2010 hadi 2012 wawe wamefaulu na wawe na alama (Points) zisizopungua 32.
(b) Waliomaliza 2013 wawe wamefaulu na wawe na alama (Points) zisizopungua 38.
(c) Waliomaliza 2014 wawe wamefaulu na wawe na GPA isiyopungua 0.6.
7. Awe na elimu ya msingi aliyehitimu darasa la saba.
8. Awe na cheti halisi cha kuzaliwa (Original Birth Certificate).
9. Awe na cheti halisi cha kumaliza shule (School Leaving Certificate)
10. Awe na cheti halisi cha matokeo (Original Academic Certificate/Transcript).
11. Asiwe ametumikia Jeshi la Polisi, Magereza, Chuo cha Mafunzo au KMKM wala kuajiriwa na Idara nyingine Serikalini.
12. Asiwe amepitia JKT Operesheni za nyuma.
13. Asiwe amejihusisha na matumizi ya madawa ya kulevya, bangi na yanayofanana na hayo..
Waombaji wenye sifa wapeleke maombi yao kwa Waheshimiwa wakuu wa mikoa. Makao Makuu ya JKT hayatapokea na hayapokei maombi yoyote, kwa vijana watakaoomba nafasi hizo wazingatie maelekezo yatakayotolewa kuepuka usumbufu.


Source: www.jkt.co.tz
Mbona kwenye website yao halipo hilo tangazo,ww umelitoa wap
 
Sasa mkuu cc wa kuanzia 2010 kurudi nyuma unakuwaje msaada tafari na anwan ya mkuu wa wilaya kinondon
 
Sasa mkuu cc wa kuanzia 2010 kurudi nyuma unakuwaje msaada tafari na anwan ya mkuu wa wilaya kinondon
Kama ulimaliza form 4 kurudi nyuma na una elimu kama ya Diploma na Degree basi ombea nafasi kupitia hiyo Diploma au Degree.
 
jamani mbona mimi nimefungua website ya JKT sioni tangazo? au wameshaliondoa? jaribuni kuingia kisha leteni mrejesho.
 
Mkuu Mwenye certificate za taharuma yyte ila wamenaliza kuanzia 2010 kurudi nyuma inakuwaje
 
ACHENI KUTAPELI WATU. NAFASI HAZIJATOKA. MPAKA BURGET 2016/2017.MUNAVUMISHA MAMBO ILIMUWAIBIE VIJANA WANAOZITAFUTA. NAFASI HIZO. TAJENI NI GAZETI GANI NA LA TARE. GANI.
 
ACHENI KUTAPELI WATU. NAFASI HAZIJATOKA. MPAKA BURGET 2016/2017.MUNAVUMISHA MAMBO ILIMUWAIBIE VIJANA WANAOZITAFUTA. NAFASI HIZO. TAJENI NI GAZETI GANI NA LA TARE. GANI.
me jana nilikuwa Msata kwenye kuhitimisha vijana waliokuwa wanachukua mafunzo pale na walisema nafasi zinaanza kutoka kwa vijana wanaotaka kujiunga na mafunzo
 
Back
Top Bottom