Mafanikio ya serikali ya AWAMU YA NNE katika MAPINDUZI YA KILIMO

...Hii inatia hata kichefuchefu kuisoma!!!! Eti mafanikio ya Serikali ya awamu ya NNE!!!! :puke:
 
Kweli aliyeshiba hamjui mwenye njaa!

Mafanikio mbona huku kwetu hungumalwa hata trekta moja silioni lililoletwa na hizo sera zenu watu wa Dar, mbona hiyo benki sijawahi hata kuona inafanana vipi zaidi ya kuisikia kwenkye hiki kiredio changu cha mkulima?

Mbona sijawahi kupata ruzuku kwa ajili ya kulima kishamba changu ambacho nacho nimeporwa na mwekezaji anayekuja na mradi wa ujenzi wa nyumba za mifuko ya mchanga eti za bei rahisi?

Mbona sijawahi kumuona hata mnunuzi mmmoja wa kuja kununua mahindi yangu hata nikivuna. Sera gani hizo ambazo mnazipangia dar wakati wakulima tupo huku hungumalwa tunateseka?
 
Huyu jamaa ni mchekeshaji sijui anataka kutwambia nini anaposema mafanikio, tungetegema kuona mafanikio katika uraisi wa upatikanaji wa pembejeo, mwaka huu huku mbozi mbolea ya kupandia imefika mwezi April 2012 badala ya September 2011 wakati watu wanajiandaa kuvuna jamaa hajui.

Achana na takwimu za kina profesa maghembe kama kweli unataka kujua mafanikio ya kilimo Tanzania hebu nenda kwa wakulima chukua hayo makabrasha wizarani ukafanye ulinganifu na kinachoendelea, ukirudi hapa utafuta hii thread yako na kama ni mzalendo hutaacha kulia kila utakapopita, yaelekea huijui nchi hii au unatumika vibaya pasipo kujua.
 
Mimi nimeipenda hii ya "rais shupavu." Kikwete ni shupavu kweli kweli. Kwa kutuuza Watanzania, wallahi hajambo.
 
Hizi taarifa na takwimu za kwenye mkabrasha hazimjengi Rais wala Serikali yake. Siku hizi hata wazito huko US na Ulaya wanadai kwamba ukuaji wa uchumi lazima udhihirike kwenye maisha halisi ya watu ili uwe na maana.
 
Nitaendelea kuwapa mafanikio mbalimbali ya serikali yetu ya awamu ya nne kadri siku zinavyoenda! We ukibisha au kutaka kupinga for sake ya kupinga just pinga tuu sikukatazi ni haki yako ya kidemokrasia
 
Ifike mahali tufanye mambo kama watu walioelimika na si vinginevyo.....pamoja maelezo yako yote ni vizuri ukajipange ili uweze kuwaonyesha WaTZ matokeo ya uliyoyaorodhesha hapo juu.

Ukinunua matrekta 100000 au 200,000,000 au Power tillers za Kilimo Kwanza maana yake nini? Je ukiongea fedha za ruzuku za pembejeo hata 10 fold je ina maana wakulima ndio wananufaika zaidi?
 
Heading the thread inasema mafanikio ya serikali katika kilimo. Post iliyowekwa inaonyesha juhudu zinazofanywa katika kuleta mapoinduzi ya kilimo. Sasa
1. Unataka kutuambia kuwa kwenu ninyi, kufanya juhudi tayari ni mafanikio?
2. Kwa nini Mods wasiifute thread hii kwa sababu inapotosha?

Sio kupotosha tu mkuu, inakera kweli kweli. Kila kukicha tunaona neno KILIMO KWANZA linazidi kusahaulika baada ya fedha za programu yenyewe kununulia magari ya kutembelea maafisa badala ya majembe. Huu upuuzi ndio unanifanyaga nashindwa kujizuia kutukana, hivi unaweza kuita MIKUTANO ni mafanikio kama sio kutaka kuonesha ujuha wako hapa?

Hizi sh kumi kumi mnazopewa Lumumba zisiwafanye muwe wajinga jamani. Asubuhi leo nimesikia Channel Ten kuwa Rais wetu kaweka rekodi ya dunia kwa kuwa mmoja kati ya viongozi wa kwanza kualikwa kuhudhuria mkutano wa G8, sasa hapo cha kujivunia ni nini? Mimi nilidhani anapongezwa kwa kuifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zinazounda G9 kumbe mnasifiana kupewa mwaliko wa kwenda kuchekacheka na kukuna kichwa na kidole
 
Nitaendelea kuwapa mafanikio mbalimbali ya serikali yetu ya awamu ya nne kadri siku zinavyoenda! We ukibisha au kutaka kupinga for sake ya kupinga just pinga tuu sikukatazi ni haki yako ya kidemokrasia

Excrement of the clan!


1. Kuimarika kwa reli ya kati
2. Kuimarika kwa bandari hasa za Tanga na Mtwara
3. Kuisha kwa tatizo la umeme
4. Udhibiti mzuri wa matumizi ya fedha za serikali
Ni vile sina tusi zito litakalokidhi kiwango cha ujinga unaoweka hapa jamvini kwa kuwa tu unalipwa. Mikataba mibovu inasainiwa kila leo halafu unaonesha madaha ya ubongo wako kuleta ujinga hapa.

Pambaf wewe, kilimo kwanza huku serikali inauza mashamba yake kwa wazungu na kuleta machafuko na wananchi kila uchao
 
Mnaojihangaisha kuitete serikali ya CCM mnapoteza muda wenu. Hilo dubwasha HALISAFISHIKI NA HALICHAGULIKI TENA, PEROD!
 
Kumbe mafanikio ya kilimo kwanza ni kufanya maonyesho ya powertillers,tractors kwenye yard mbalimbali huku mijini pamoja na kuchakachua mbolea kwa kumix na normal salt? Duu,the guy is vry superior,well done for that and keep on pressing
 
Mafanikio ya KILIMO KWANZA yataonekana kwa maisha ya wakulima sio takwimu.

Mafanikio ya KILIMO KWANZA yataonekana kwenye idadi ya exportation sio ripoti.

Mafanikio ya KILIMO KWANZA yataonekana kupitia jinsi kilimo kitakavyowezesha ukuaji wa sekta nyingi kama viwanda n.k na sio maneno ya Waziri, Katibu wa Wizara wala msemaji wa Ikulu.

ACHENI POROJO.

Mkuu wa kazi umemaliza. kitufe cha like ckioni tu mkuu wangu, yaani hii serikali ya awamu ya nne inapenda kuwaaminisha watu/wananchi vitu ambavyo havipo. Mleta mada anataka kutuaminisha kwamba jiwe ni mkate wakati sio.
 
hayo mafanikio ya kilimo kwanza ni yapi. maaana kuna yale ma landcruser V8 huwa naskia yanaitwa kilimo kwanza. naomba mwenye kujua kisa cha V8 kuitwa kilimo kwanza anijuze
 
hayo mafanikio ya kilimo kwanza ni yapi. maaana kuna yale ma landcruser V8 huwa naskia yanaitwa kilimo kwanza. naomba mwenye kujua kisa cha V8 kuitwa kilimo kwanza anijuze
 
hakuna mtu anayetaka kusifiwa, lakini pale inapotokea mtu mzima anakashifu hata yale mazuri yaliyofanyika na kwa namna moja ama nyengine amefaidika nayo then hatuna budi kuelezea mafanikio hayo

Lengo Mujumba sio kukashifu...hivi kama kila mtu anapata huduma muhimu na kula mkate wake wa kila siku bila bughuza, nani atakayekuwa na muda wa kulalamika? Tatizo linakuja kama wale waliopewa dhamana wanajisahau na kuanza kuhujumu Taifa kwasababu ya madaraka waliyopewa. Na hili limekuwa tatizo linalokua siku hadi siku. Awamu ya nne ni kama limepitiliza na kuwa kubwa zaidi.
Tukifanya kazi zetu vizuri, kazi ndio zitatupigia debe...hakuna sababu ya kununua spika na magari kuzunguka dunia nzima kueleza nini tunachofanya maana matendo yanaeleza zaidi kuliko maneno.
 
Majumba, umesihi tujadili bila jazba wala matusi. Hii ni kwa sababu umejua kabisa kwamba ulichokiandika kitapelekea jazba na hata matusi. Ninachokiona ni porojo na ushabiki wa kisiasa na uchambuzi wenye tija hata kidogo. Ni bora ukakaa kimya kuliko kupandisha watu jazba.
 
Back
Top Bottom