Maelezo kwa ufupi juu ya clip ikionyesha wanajeshi katili wakiua raia

Hivi hawa washkaji wana familia kweli huko nyumbani yaani watoto au mke aseee !! Watu huwa wanasema kufanya kazi mochwari ni kipengele ila hii kazi ni ya moto asee naona bora hata anayenyonga wafungwa ana nafuu ! Hii kazi hata ukiiacha lazima upate Post Traumatic Disorder.

Hiki kitengo hata kwetu hapa kipo kweli ?
Cha ajabu ni kwamba kuna watu fulani walianza kumfuatilia Amjad ambae ni huyo muuaji, wakamfuatilia hadi wakagundua alikuwa anatumia mtandao wa kijamii, wakamuuliza kile amefanya anajisikiaje, jamaa akasema anajivunia na hajutii alichofanya. Baadae akapotea kabisa kwenye social media baada ya kugundua amefahamika, na akatoa vitisho. Baada ya clip kuvuja akakamatwa.

Kuna watu ni katili aisee.
 
Cha ajabu ni kwamba kuna watu fulani walianza kumfuatilia Amjad ambae ni huyo muuaji, wakamfuatilia hadi wakagundua alikuwa anatumia mtandao wa kijamii, wakamuuliza kile amefanya anajisikiaje, jamaa akasema anajivunia na hajutii alichofanya. Baadae akapotea kabisa kwenye social media baada ya kugundua amefahamika, na akatoa vitisho. Baada ya clip kuvuja akakamatwa.

Kuna watu ni katili aisee.
Duuh ila yeye si yupo kutekeleza maagizo anayopewa na wakuu wake maana yake huenda serikali imemficha tu kupooza umma ila uhalisia kuna God father nyuma yake /yao
 
Hivi hawa washkaji wana familia kweli huko nyumbani yaani watoto au mke aseee !! Watu huwa wanasema kufanya kazi mochwari ni kipengele ila hii kazi ni ya moto asee naona bora hata anayenyonga wafungwa ana nafuu ! Hii kazi hata ukiiacha lazima upate Post Traumatic Disorder.

Hiki kitengo hata kwetu hapa kipo kweli ?
Toka utawala wa JKN
 
Duuh ila yeye si yupo kutekeleza maagizo anayopewa na wakuu wake maana yake huenda serikali imemficha tu kupooza umma ila uhalisia kuna God father nyuma yake /yao
Sahihi hawezi fanya kitu kama kile pasipo order maalumu toka juu, ukizingatia alikuwa na wenzake, ni tukio liliandaliwa na wakubwa makusudi.
 
Demokrasia tatizo watu wanafahamu ni uongozi tu serikalini hasa uraisi, lakini demokrasia ni pana sana, kuanzia uongozi wa juu hadi maisha ya raia mmoja mmoja, hakuna balance of power kama hakuna demokrasia. Wanajeshi na askari wanakua na mamlaka ya juu kuliko raia. Mnaishi kama wanyama wafugwao.
Nchi gani kuna demokrasia duniani ?
 
Serikali zote duniani ni za kinyama gusa maslahi ya mapapa wa nchi ndio utajua moto haulambwi
Ni sawa lakini kuna nchi unaweza ongea mambo fulani ukabaki salama, kuna nchi ukimsema kiongozi hata kama ni ukweli, probability yako kuendelea kupumua masaa 72 yajayo ni 1/1000.

Siwezi kukubishia hata Snowden alikimbia US baada ya kutoa siri nzito, lakini kwa level waliopo America na Ulaya bado sana kwa nchi zingine nyingi kufika walipo katika free of speech na democracy.
 
Nchi za Ulaya na America wamejitahidi kwenye demokrasia.
Demokrasia gani waliyo jitahidi marekani Assange tu mpaka leo anaishi kama digi digi.

Hao ulaya unyama walio fanyia babu na bibi zako ni kwamba umesahau au hujui historia ?

Unyama anao fanya marekani hapo middle east kwa kushirikiana na dikteta mwenzake Israel huoni ?

Mauaji ya Marekani Vietnam unayafahamu ?
 
Hii clip nimeiona kutoka kwenye uzi alioanzisha mdau anaitwa GoldDhahabu wenye kichwa cha habari Hawa wanajeshi katili ni wa wapi? .

View: https://streamable.com/ly7v6f

Kuna maelezo mengi tofauti na sehemu kubwa si sahihi.

Tukio linaonyesha raia ambao wamefungwa mikono na kuzibwa macho wakikokotwa na askari, pasipo raia hao kujua wanaelekea wapi au pengine wakifahamu wanaelekea mahala salama wanaangukia kwenye shimo lililoandaliwa tayari na kupigwa risasi vichwani, baada ya askari hao kumaliza kuwapiga risasi mmoja baada ya mwingine, askari hao wakiwa wameshatanguliza matairi ya gari kwenye shimo, wanawasha moto na kuteketeza miili hio.



Hili tukio lilitokea 16 April 2013 nchini Syria katika mji mkuu Damascus, askari wanao onekana kutekeleza unyama huo wanatokea kitengo cha intelijensia katika jeshi la Syria (Military Intelligence Directorate (Syria)), na specifically hao askari wapo katika kitengo kinachohusika na ukatili, utesaji na mauaji pasipo huruma. Yaani kwenye Syrian Military Intelligence kuna hiki kitengo kwa ajili ya utesaji, mauaji na ukatili wa kila aina unaoufahamu.

Syrian Military Intelligence ipo chini ya raisi, inaendeshwa na Bashar Al Assad mwenyewe, kitengo hiki kimekuwa kimetumika pia kwenye siasa hasa kuwakandamiza wale wanaotaka kuleta upinzani lazima cha moto utakiona.

Hii clip imevuja mwaka 2022, inasemekana kuna mtu alipata access ya laptop iliyokuwa na clip hii, akacopy na kuihifadhi, inasemekana ni askari wa Syria.
Aliyetambulika kwenye hii clip ni Major Amjad Yousef ambae anaonekana kuwapiga risasi raia hao pasipo huruma, askari huyu katili inasemekana amejiunga na jeshi mwaka 2004, baadae baada ya mafunzo akajiunga na branch 227 katika Syrian Intelligence Service kitengo maalumu kwa ajili ya utekaji, kutesa na kuua hasa wapinzani katika serikali ya Syria.

Kwa ufupi hao raia wanauliwa kikatili inasemekana hawana kosa, kilikuwa ni kipindi cha mapigano ambapo waasi walikuwa wanakaribia eneo hilo, hivyo askari hao walitaka kuonyesha mfano kwa yeyote ambae atajaribu kuwa upande wa uasi. Raia hao inasemekana waliishi karibu kabisa na eneo ambalo kulikuwa na upinzani.

Raia waliouawa wakati huo ni 41, waliouawa kwenye hilo shimo. Hata hivyo inasemekana waliouawa wengine ni wanakadiriwa 200 au 300 katika maeneo mengine

Baada ya clip kuvuja, Amjad alikamatwa na serikali ya Syria 2022, Amjad amekamatwa pasipo warrant na hajafikishwa mahakamani, wachambuzi wa mambo wanasema kukamatwa kwa Amjad ni kuzuia waliojihusisha na unyama huo waliopo ngazi za juu wasifahamike.

Serikali ya marekani ilitoa sanctions juu ya Amjad Yousef mnamo March mwaka huu 2023 , secreatry of state Anthony Blinken alisema vikwazo hivyo ni kwa ajili ya mauaji hayo yaliyofanyika.

Hawa ndio FaizaFoxy umwambii kitu kuhusu Mwarabu, ndugu katika Imani.

Cc: MK254
 
Hizi nchi zilizopo mashariki ya kati mpaka huko uarabuni sijui zina watu wa aina gani. Kuua kwao ni kama kunywa chai.
Hapa tunawaonea. Haya yapo hata Afrika. Ni vile hizi zimevuja. Kusema kweli Afrika na Asia kuna mambo ya hovyo sana kutokana na haki za binadamu kutokua ishu pande hizo.
 
Ni sawa lakini kuna nchi unaweza ongea mambo fulani ukabaki salama, kuna nchi ukimsema kiongozi hata kama ni ukweli, probability yako kuendelea kupumua masaa 72 yajayo ni 1/1000.

Siwezi kukubishia hata Snowden alikimbia US baada ya kutoa siri nzito, lakini kwa level waliopo America na Ulaya bado sana kwa nchi zingine nyingi kufika walipo katika free of speech na democracy.
Hakuna nchi yenye hizo taka taka democracy na free speech kama propaganda ulizo lishwa na vyombo vyao vya habari nawe ukaaamini.

Futa mawazo ya free speech dunia hii ya kibepari, bepari hana huruma na anaye fichua maovu yake.
 
Hapa tunawaonea. Haya yapo hata Afrika. Ni vile hizi zimevuja. Kusema kweli Afrika na Asia kuna mambo ya hovyo sana kutokana na haki za binadamu kutokua ishu pande hizo.
Haya mambo yapo dunia kote sio Afrika,sio Asia, sio ulaya wala sio Amerika.

Serikali za dunia zimejaa damu za watu
 
Halafu kuna watu wanadiss western countries.
Kudadeki hakuna kitu sipendi kama kuuana bila hatia.
Kwangu ni mara 100 huo ushoga wanaoupromote western ila sio kuuana kama kuku.
Kuzikana kama mnyama aliekufa kwa ugonjwa, sote nchi moja, race moja lakini unaua na kumchoma moto, Really!!?
 
Back
Top Bottom