SULEIMAN ABEID
JF-Expert Member
- Feb 26, 2013
- 390
- 385
HALMASHAURI ya Wilaya ya Meatu kama ilivyo maeneo mengine ya
Serikali za Mitaa inasimamiwa na kuongozwa kwa kuzingatia
Sheria mbalimbali za nchi ikiwemo Sheria ya Serikali za Mitaa ya
mwaka 1982 na Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Wilaya ya
Meatu za Mwaka 2014 ambazo zinaelekeza mambo mbalimbali ya
kuzingatia.
Kwa kipindi kirefu sasa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya
Meatu Mhe. Antony Philipo Athumani na Mkurugenzi Mtendaji
wa Halmashauri Ndugu. Msoleni Juma Dakawa wameshindwa
kumudu nafasi zao kwani kumekuwepo na usimamizi dhaifu wa
shughuli za Halmashauri, uzembe, upendeleo na matumizi
mabaya ya fedha za umma hali inayopelekea kurudisha nyuma
maendeleo ya wana Meatu.
Aidha kumekuwepo na ukiukwaji mkubwa wa Sheria, Kanuni na
Taratibu zilizowekwa katika usimamizi na uendeshaji wa shughuli
za Serikali hali ambayo inaiweka halmashauri pabaya kila leo
ikiwemo ubadhirifu wa fedha za umma, miradi kutelekezwa,
kukosekana kwa uwiano wa miradi ya maendeleo na gharama
kubwa za miradi.
CHANGAMOTO ZA USIMAMIZI NA UENDESHAJI WA
HALMASHAURI YA WILAYA YA MEATU
1. Usimamizi na utekelezaji dhaifu wa miradi ya maendeleo
Utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwenye fedha za Serikali na
wahisani kwa mwaka wa fedha 2021/22 kuna miradi ambayo
imetekelezwa kwa kiwango cha chini sana, kuchelewa kwa
utekelezaji wa miradi, fedha kupelea na miradi kutelekezwa na
kuachwa magofu, baadhi miradi hiyo ni kama ifuatavyo:-
(i) Ujenzi wa Kituo cha Afya Iramba Ndogo na Mwasengela
ilikuwa ukamilike tangu Aprili 2022 kwa awamu ya kwanza lakini
hadi sasa miradi hiyo haijakamilika na fedha zimepelea
kukamilisha miradi hiyo pia tangu fedha za awamu ya pili kiasi
cha Tsh 500,000,000 ziletwe Mwezi Mei, 2022 hadi leo ujenzi
haujaanza katika vituo hivyo vya afya.
Sababu za kupelea fedha na kukwama kwa ujenzi wa miradi hiyo
hazieleweki hadi sasa na hazikuwahi kutolewa taarifa hapo awali.
(ii) Ujenzi wa Sekondari mpya za Mwandu Itinje na Mwamanimba
ambazo zililetewa fedha kutoka Serikali Kuu kwa awamu ya
kwanza kiasi Tsh 940,000,000 yaani kiasi cha Tsh 470,000,000
kwa kila shule. Fedha za utekelezaji wa miradi hii zimepelea na
ujenzi umesimama na kuacha magofu. Awali menejimenti licha ya
kujua kuwa fedha zitapelea lakini haikutoa taarifa Wizarani,
Baraza la Madiwani wala uongozi wa Kata husika ambako mradi
unatekelezwa na hakuna mkakati wowote uliowekwa kumalizia
miradi hiyo.
(iii) Miradi ya WASH- ujenzi wa vyoo inayotekelezwa katika
Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kwa miradi mingi fedha
zimepelea na ujenzi umesimama na kuacha magofu ya miradi
hiyo ambayo haitoi huduma iliyokusudiwa. Hakuna taarifa
iliyotolewa juu ya kupelea na kusimama kwa miradi hiyo na
hakuna mkakati uliowekwa wa kukamilisha miradi hiyo.
Kitendo cha kuanza kutekeleza miradi kwa fedha pungufu,
kuchelewa utekelezaji wa miradi bila sababu za msingi,
kukosekana kwa mikakati madhubuti ya kumalizia miradi hiyo na
Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kushindwa kutoa
taarifa sahihi kwa Wahisani, Wizarani, Baraza la Madiwani na Kata
husika kunazua maswali mengi yasiyo na majibu. Lakini pia
kwanini mradi usitekelezwe kwa awamu na kwa ukamilifu badala
ya kubaki na gofu lisilotumika.
2. Kubadilisha mpango wa bajeti bila idhini ya Baraza la
Madiwani
Mnamo Tarehe 8.02.2022 Baraza la Madiwani lilifanya kikao
maalum kwa ajili ya kupitia na kupitisha bajeti ya halmashauri ya
mwaka wa fedha 2022/23 bajeti ya Halmashauri hupitishwa kwa
kuzingatia Sheria ya Fedha ya Serikali za Mitaa namba 9 ya
mwaka 1982 kifungu cha 43 (i), ilani ya uchaguzi ya CCM ya
mwaka 2020 na ahadi za viongozi za wakati wa uchaguzi.
Katika vikao vya Kamati za Kudumu za Halmshauri ya Wilaya vya
robo ya kwanza imeonekana kuna ukiukwaji mkubwa sana wa
sheria na kanuni katika utekelezaji wa bajeti ambapo imeonekana
miradi mingi iliyopitishwa na baraza la madiwani haikupangiwa
fedha na kupendekezwa kupewa fedha miradi mingine mipya
ambayo haikuidhinishwa na kupangiwa fedha na Baraza la
Madiwani katika kikao halali cha kupitisha bajeti mwaka wa fedha
2022/2023. Baadhi ya maeneo hayo ni kama ifuatavyo:-
(i) Baraza la Madiwani lilipitisha fedha za lishe Tsh 109,000,000
na Fedha za Kilimo na Ushirika za Mapato ya ndani Tsh
50,000,000 jumla ya Tsh 159,000,000 Baraza lilipitisha fedha hizi
ziende kukamilisha miundombinu katika Zahanati 10 ili ziweze
kufunguliwa na kutoa huduma kwa wananchi na kila zahanati
ilipangiwa Tsh 15,900,000 kila moja Zahanati hizo ni (i) Itaba, (ii)
Mwanzugi, (iii) Mwageni B, (iv) Semu, (v) Malwilo Mnadani, (vi)
Igushilu, (vii) Makomangwa, (viii) Tindabuligi, (ix) Nata (x)
Itongolyangamba. Fedha hizi hazikupangwa katika bajeti kama
Baraza la Madiwani lilivyoamua kinyume na bajeti ilivyopitishwa.
(ii) Katika kupitisha Bajeti ya mwaka 2022/2023 Baraza la
Madiwani lilipitisha Tsh 500,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa mradi
wa Kituo cha Afya cha Iramba ndogo na Mwasengela yaani kila
kituo cha afya kilipangiwa kiasi cha Tsh 250,000,000. Fedha hizi
hazikuingizwa katika bajeti na badala yake zilibadilishiwa
matumizi bila idhini ya Baraza la madiwani na kupangiwa maeneo
mengine kama ifuatavyo:-
(a) Ujenzi wa nyumba ya mtumishi Zahanati ya Masanga Tsh
50,0000,000
(b) Ujenzi wa nyumba ya mtumishi zahanati ya Mwandu Kisesa
Tsh 50,000,000
(c) Ujenzi wa nyumba ya Mtumishi zahanati ya Semu Tsh
50,000,000
(d) Ujenzi wa nyumba mtumishi Zahanati ya Mwabagalu Tsh
50,000,000
(e) Ununuzi wa vifaa tiba kwa ajili vituo vya afya Tsh 300,000,000
Miradi hii iliyoonyeshwa (a) hadi (e) yenye thamani ya Tsh
500,000,000 haikupitishwa na Baraza la Madiwani na wala Baraza
halijawahi kupewa taarifa ya mabadiliko hayo ya mpango wa
Bajeti hadi hii leo Oktoba 2022, uamuzi uliofanywa na
Menejimenti wa kubadilisha mpango wa bajeti bila kibali na idhini
ya Baraza la Madiwani ni kinyume cha Sheria ya Fedha na Sheria
ya Bajeti.
3. Kutokutolewa kwa fedha za miradi ya maendeleo 40%
ya mapato ya ndani
Taarifa ya Mapato na matumizi ya kipindi cha Julai hadi Septemba
2022 inaonyesha kuwa fedha ya maendeleo 40% ya mapato ya
ndani iliyokuwa imetolewa ilikuwa kiasi cha Tsh 259,856,910
badala ya kiasi cha Tsh 481,984,136 iliyopaswa kutolewa kwa
kipindi hicho.
Kiasi cha fedha kilichokuwa kimekutumika ni Tsh. 103,000,000
kwa ajili ya mikopo ya akina mama, vijana na wenye ulemavu kati
ya fedha Tsh 259,856,910 zilizokuwa zimepokelewa huku Tsh.
156,856,910 zikibaki kwenye akaunti ya maendeleo.
Hapa kuna zua maswali mengi bila majibu sababu ya fedha za
miradi ya maendeleo 40% ya mapato ya ndani kukusanywa na
kutokupelekwa kwenye akaunti ya maendeleo ni zipi? Sababu ya
fedha kukusanywa na kuachwa kwenye akaunti badala ya
kupelekwa kutekeleza miradi ya maendeleo ni nini? Kwa miezi 4
sasa miradi inayotekelezwa kutokana na 40% ya mapato ya ndani
haijapelekewa fedha na utekelezaji wa miradi hiyo ni Sifuri.
Sababu za kutokutekeleza miradi ya maendeleo kama baraza
lilivyoidhinisha hazijulikani na hazijawahi kutolewa. Ingawa katika
vikao vya hivi karibuni mkurugenzi amekuja kuwasilisha
mapendekezo ya kubadili matumizi ya fedha za miradi ya
maendeleo kiasi cha zaidi ya Tsh 405,000,000 na kupendekeza
ziende kwenye kuanzisha miradi ya biashara ya ufyatuaji matofali,
shule ya chekechea na ujenzi wa maghala ya chumvi.
Hivyo kwa kipindi cha miezi 4 Mkurugenzi Mtendaji amekaidi
kupeleka fedha za maendeleo katika miradi iliyopitishwa kwenye
bajeti kwa lengo la kufanikisha nia yake ya kubadili matumizi ya
fedha hizo kwa malengo anayoyajua yeye.
4. Upendeleo na mipango mibovu katika ugawaji wa
fedha za maendeleo
Mwenyekiti na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
wamekuwa na tabia ya kuzipendelea baadhi ya kata kuzipa fedha
nyingi za miradi ya maendeleo huku kata zingine zikibaguliwa kwa
kuwa madiwani wa kata hizo hawaendani na mtizamo wa
viongozi hao. Pia kuna upendeleo wa dhahiri wa wajumbe wa
Kamati ya Fedha hapa ipo mifano mingi kama ifuatavyo:-
(i) Kata ya Mwangudo inayoongozwa na Mwenyekiti wa
Halmashauri Mhe. Anthony Philipo Athumani miradi iliyopewa ni
ujenzi wa kituo cha afya Iramba ndogo Tsh 500,000,0000, ujenzi
wa Ofisi ya Kata Mwangudo Tsh 11,000,000, Ukamilishaji wa
Bweni Shule ya Sekondari Makao Tsh 20,000,000, ukamilishaji wa
Bwalo la Chakula Shule ya Sekondari Makao Tsh 30,000,0000,
ukalimishaji wa nyumba ya mtumishi Shule ya Msingi Mbuyuni
50,000,000
(ii) Kata ya Mwasengela inayoongozwa na Mwenyekiti wa Kamati
ya Uchumi, Ujenzi, Hifadhi na Mazingira, Mhe. Mlangale Sakumi
Sayi miradi iliyopewa ni Ujenzi wa Kituo cha Afya Mwasengela Tsh
500,000,000, Ujenzi wa Bweni la Wasichana Lingeka Sekondari
Tsh 73,000,000, ujenzi wa madarasa mawili Shule ya Msingi
Ng’hanga Tsh 25,000,000, ujenzi wa madarasa mawili Shule ya
Msingi Ng’hanga Tsh 40,000,000, ukamilishaji wa Jengo la OPD
na nyumba ya mtumishi katika Zahanati Mwamhongo Tsh
148,000,000.
(iii) Kata ya Lingeka inayoongozwa na Mjumbe wa Kamati ya
Fedha, Mhe. Joseph Nyanza Sayi miradi iliyopewa ni ukamilishaji
madarasa 4 na ofisi 2 Tsh 50,000,000, ukamilishaji wa madarasa
2 na ofisi 1 Shule ya Msingi Masanga Tsh 40,000,000, ujenzi wa
maabara Shule ya Sekondari Masalinge Tsh 73,000,000, Ujenzi
wa Sekondari mpya Masalinge (Maalum) Tsh 600,000,000
Na hii haingii akilini katika bajeti Shule mpya ya Sekondari
Masalinge (Lingeka) imepangiwa kiasi cha Tsh 600,000,000 kwa
ajili ya ujenzi wa madarasa na miundombinu mingine ikiwemo
maabara lakini wakati huo huo tena inapangiwa kiasi cha Tsh
73,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya maabara. Pia Kata
ya Lingeka imepangiwa kiasi cha Tsh 100,000,000 kwa ajili ya
ujenzi wa OPD na nyumba ya mtumishi katika Zahanati ya
Masanga.
(iv) Kata ya Mwandoya ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Fedha,
Mhe. Basu Kayungilo imetengewa Tsh 130,000,000 kwa ajili ya
ujenzi wa Wodi ya wazazi katika Kituo cha Afya Mwandoya wakati
Kituo cha Afya cha Mwandoya kina wodi ya Wazazi haya
yanafanywa kukiwa na mahitaji makubwa ya miundombinu ya
afya katika maeneo mbalimbali. hiyo ni mifano michache tu ya
baadhi tu ya kata zilizopendelewa
Baadhi ya Kata zinazobaguliwa na kutokupangiwa miradi
inavyostahili ni Kata ya Kabondo, Kata ya Mbugayabanhya, Kata
ya Mbushi, Kata ya Mwabuzo, Kata ya Mwabusalu, Kata ya
Tindabuligi, Kata ya Mwakisandu, Kata ya Imalaseko, Kata ya
Nghohoboko n.k
Kata ya Mbushi kwenye Bajeti Baraza lilipitisha Tsh 600,000,000
kwa ajili ya ujenzi wa Sekondari ya Kata na fedha hizo
zimeondolewa na hazijulikani zilipo.
Kata ya Mbugayabanhya kata hii haina sekondari mpya katika
kupitisha bajeti ya mwaka wa 2022/2023 Baraza la Madiwani
lilipangia Tsh 80,000,000 kwa ajili ya kuanzisha Sekondari mpya
lakini fedha hizo zimeondolewa.
Kata nyingine ni Tindabugili ina magofu mengi na yalikuwa
yamepangiwa fedha katika Bajeti lakini kwa sasa fedha
hazionekani tena. Hii ni mifano michache lakini ziko baadhi ya
kata nyingi zilizobaguliwa kwenye miradi ya maendeleo.
5. Ukiukwaji wa taratibu za uundwaji wa Kamati ya
Fedha, Utawala na Mipango.
Katika kuunda Kamati ya Fedha, utawala na mipango, Mwenyekiti
wa Halmashauri na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya
Meatu wamekiuka Kanuni Namba 40(5) kinachosema Mwenyekiti.
wajumbe wa Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango na kuyaleta
ndani ya Baraza la Madiwani na kupitishwa kwa kura na baraza la
madiwani lakini kamati iliyochaguliwa ndani yao wajumbe 6
walipaswa kupigiwa kura na baraza la madiwani lakini mwenyekiti
na mkurugenzi hawakufanya hivyo na kamati hiyo
iliyopendekezwa na mwenyekiti wa halmashauri hadi sasa
inaendelea na vikao na ziara kama kawaida na wanalipwa stahili
zao kama kawaida hapa kuna ukiukwaji mkubwa sana wa kanuni
tajwa hapo juu.
Kwa mantiki hiyo Mwenyekiti wa Halmashauri hakuleta orodha ya
wajumbe aliowapendekeza kwenye baraza la halmashauri ili
yapigiwe kura kama kanuni zinavyoelekeza badala yake ameteua
yeye hivyo kukiuka kanuni na kutumia madaraka yake vibaya.
6. Matumuzi mabaya ya fedha za Serikali
Mwenyekiti na Mkurugenzi wa Halmshauri wamekuwa na desturi
ya kutumia vibaya fedha za Halmshauri bila idhini ya Baraza la
Madiwani kinyume na Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa. Ipo
mifano kama ifuatavyo:-
(i) Katika miradi ya UVIKO-19 Mwenyekiti wa Halmshauri na
Mkurugenzi wametumia vibaya fedha za Serikali kwa kuagiza
mabati katika miradi yote bila idhini ya Baraza la Madiwani na bati
moja lilinunuliwa kwa Tsh. 40,000 na wakati huo bei ya juu kwa
bati hizo katika soko ilikuwa ni Tsh 35,000 kwa kila bati la gage
28 maamuzi haya yalikiuka Sheria, Kanuni na miongozo
iliyowekwa.
(ii) Katika ujenzi wa Zahanati 4 za Makomangwa, Mwanyahina,
Sapa na Mwandu Kisesa ambapo kila zahanati ilipewa Tsh Milioni
50 na jumla ya Tsh Milioni 200 zilitumika kwa kukiuka utaratibu
wa Force Account ambapo mikataba ya ujenzi huo ilisainiwa na
Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya badala ya Kamati
za vijiji husika zilizopewa hiyo miradi.
(iii) Katika utekelezaji wa bajeti ya Mwaka 2021/2022 Mwenyekiti
na Mkurugenzi wamekiuka kanuni kwa kuhamisha fedha Tsh
Milioni 25 kutoka Igushilu na fedha Tsh Milioni 25 toka Mwanzugi
ambazo zilikuwa za ukamilishaji wa miundombinu ya Zanahati
katika vijiji hivyo na badala yake fedha hizo zote Tsh Milioni 50
zilipelekwa Kijiji cha Dakama kujenga nyumba ya mtumishi katika
zahanati hiyo ambayo haikuwa katika bajeti.
(iv) Kuanza kutekeleza majukumu na kulipwa posho wajumbe 6
wa Kamati ya Fedha ambao si wajumbe halali wa Kamati ya
Fedha, Utawala na Mipango kwani wajumbe hao hawakupigiwa
kura na Baraza la Madiwani hivyo kutumia vibaya jumla ya Tsh
Milioni 4.8 kwa mchanganuo ufuatao:-
(a) Kikao (i) @ 250,000 x 6 = 1,500,000
(b) Ziara (i) @ 550,000x 6 = 3, 300,000
7. Utoaji holela wa mikopo ya akina mama, vijana na
walemavu
Kumekuwepo na utoaji holela na upendeleo wa mikopo ya akina
mama, vijana na wenye ulemavu kwa vikundi vinavyopata mikopo
katika Halmashauri ya Wilaya ya Meatu hali inayopelekea vikundi
vingi vya uzalishaji mali kukosa mikopo huku vichache vikinufaika
kinyume na malengo ya kuanzishwa kwa utaratibu wa mikopo ya
aina hii. Baadhi ya mifano katika mwaka wa fedha 2021/2022
mikopo iliyotolewa kwa vikundi ni kama ifuatavyo:-
(i) Kikundi cha vijana cha Heroes Group chenye wanachama
watano kimepewa mkopo wa kununua Min Bus yenye thamani ya
Tsh 72,000,000 huku muda wa kurejesha ni miaka 4
(ii) Kikundi cha akina Mama cha Hapa Kazi Tu chenye wanachama
watano kimepewa mkopo wa Trekta wenye thamani ya Tsh
74,150,000 umri wa mkopo ni miaka 7
(a) Mkopo huu ni mkubwa sana kutolewa kwa kikundi kimoja
kulingana na mapato yanayopatikana kila mwaka katika
halmashauri, wastani wa 4% ya mapato ya ndani kwa mikopo ya
vijana ni Tsh 100,000,000 tu hivyo ukitoa mkopo kwa kikundi
kimoja cha Tsh 72,000,000 umebakiwa na Tsh 28,000,000 tu kwa
vikundi vyote kutoka vijiji vyote vya Wilaya ya Meatu.
(b) Kutolewa kwa mkopo huu kwa kikundi kimoja cha vijana
kutoka Kijiji cha Mwanhuzi Bomani na kikundi kimoja cha
wanawake kutoka Kijiji cha Bukundi kulipelekea vikundi vingi vya
akina mama, vijana na wenye ulemavu kukosa mikopo katika
Wilaya ya Meatu. Vikundi vingi viliomba mkopo lakini
havikufanikiwa kwa maelezo ya upungufu wa fedha, sababu za
kupendelewa vikundi viwili kwa gharama za wana Meatu wote ni
nini?
(c) Gharama ya kununua Min Bus ni Tsh 62,000,000 kwa nini
mkopo umetolewa wa Tsh 72,000,000? Imekuwa ikohojiwa
kwenye vikao mbalimbali vya halmashauri lakini hakuna majibu
ya uhakika yanayotolewa.
(d) Sababu ya vikundi hivi kujipatia Mikopo ya Min Bus na
Matreka kupitia mikopo ya akina mama, vijana na wenye ulemavu
ilikuwa ni nini kwani mikopo ya aina hiyo ingewezwa kuombwa
kupitia Taasisi za Fedha badala ya kupitia halmashauri ambazo ni
fedha kidogo kwa ajili ya wananchi wanyonge.
(e) Tathimini ya utoaji wa mikopo hiyo inaleta mashaka makubwa
kama vikundi hivyo vitaweza kurejesha mikopo hiyo kwani uimara
na muda wa uchakavu kwa mashine na mitambo ni wastani wa
miaka 3 mpaka miaka 5 hayo marejesho ya miaka 7
yatarejeshwaje wakati mitambo itakuwa haipo.
(f) Hakuna uthibitisho wa tathmini ya kitaalamu uliyofanywa
kujiridhisha uwezo wa vikundi hivyo kurejesha mkopo kwa muda
uliowekwa. Hakuna maoteo ya taarifa za fedha yanayothibitisha
vikundi hivyo kumudu kurejesha mkopo huo. Kushindwa kufanya
marejesho kwa vikundi hivyo kutaleta hasara kubwa kwa
Halmashauri na Serikali kwa ujumla lakini pia itazorotesha zoezi la
utoaji wa mikopo kwa wananchi.
Haya mambo yote yamefanywa na Divisheni ya Maendeleo ya
Jamii kwa kibali na Baraka za Mkurugenzi Mtendaji na Mwenyekiti
wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu.
3.0 HITIMISHO
Halmashauri ya Wilaya ya Meatu inaendeshwa kwa ukiukwaji
mkubwa wa Sheria, Kanuni na Taratibu na matumuzi mabaya ya
madaraka hali inayopelekea upotevu mkubwa wa fedha za umma
na hasara kubwa kwa taifa.
Kuchelewa na Kukwama kutekelezwa kwa miradi ya maendeleo
kunachelewesha utoaji wa huduma kwa wananchi, udhaifu huu
unathibitisha kuwa kwa kiwango kikubwa Mwenyekiti na
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
wamepwaya na wameshindwa kumudu majukumu yao.
Lakini pia kutokana na udhaifu huu mkubwa wa usimamizi na
uendeshaji CAG afanye ukaguzi maalum kwa Halmashauri ya
Wilaya ya Meatu.
Mwisho.
ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI WANAOUNGA
MKONO HOJA HII:-
Serikali za Mitaa inasimamiwa na kuongozwa kwa kuzingatia
Sheria mbalimbali za nchi ikiwemo Sheria ya Serikali za Mitaa ya
mwaka 1982 na Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Wilaya ya
Meatu za Mwaka 2014 ambazo zinaelekeza mambo mbalimbali ya
kuzingatia.
Kwa kipindi kirefu sasa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya
Meatu Mhe. Antony Philipo Athumani na Mkurugenzi Mtendaji
wa Halmashauri Ndugu. Msoleni Juma Dakawa wameshindwa
kumudu nafasi zao kwani kumekuwepo na usimamizi dhaifu wa
shughuli za Halmashauri, uzembe, upendeleo na matumizi
mabaya ya fedha za umma hali inayopelekea kurudisha nyuma
maendeleo ya wana Meatu.
Aidha kumekuwepo na ukiukwaji mkubwa wa Sheria, Kanuni na
Taratibu zilizowekwa katika usimamizi na uendeshaji wa shughuli
za Serikali hali ambayo inaiweka halmashauri pabaya kila leo
ikiwemo ubadhirifu wa fedha za umma, miradi kutelekezwa,
kukosekana kwa uwiano wa miradi ya maendeleo na gharama
kubwa za miradi.
CHANGAMOTO ZA USIMAMIZI NA UENDESHAJI WA
HALMASHAURI YA WILAYA YA MEATU
1. Usimamizi na utekelezaji dhaifu wa miradi ya maendeleo
Utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwenye fedha za Serikali na
wahisani kwa mwaka wa fedha 2021/22 kuna miradi ambayo
imetekelezwa kwa kiwango cha chini sana, kuchelewa kwa
utekelezaji wa miradi, fedha kupelea na miradi kutelekezwa na
kuachwa magofu, baadhi miradi hiyo ni kama ifuatavyo:-
(i) Ujenzi wa Kituo cha Afya Iramba Ndogo na Mwasengela
ilikuwa ukamilike tangu Aprili 2022 kwa awamu ya kwanza lakini
hadi sasa miradi hiyo haijakamilika na fedha zimepelea
kukamilisha miradi hiyo pia tangu fedha za awamu ya pili kiasi
cha Tsh 500,000,000 ziletwe Mwezi Mei, 2022 hadi leo ujenzi
haujaanza katika vituo hivyo vya afya.
Sababu za kupelea fedha na kukwama kwa ujenzi wa miradi hiyo
hazieleweki hadi sasa na hazikuwahi kutolewa taarifa hapo awali.
(ii) Ujenzi wa Sekondari mpya za Mwandu Itinje na Mwamanimba
ambazo zililetewa fedha kutoka Serikali Kuu kwa awamu ya
kwanza kiasi Tsh 940,000,000 yaani kiasi cha Tsh 470,000,000
kwa kila shule. Fedha za utekelezaji wa miradi hii zimepelea na
ujenzi umesimama na kuacha magofu. Awali menejimenti licha ya
kujua kuwa fedha zitapelea lakini haikutoa taarifa Wizarani,
Baraza la Madiwani wala uongozi wa Kata husika ambako mradi
unatekelezwa na hakuna mkakati wowote uliowekwa kumalizia
miradi hiyo.
(iii) Miradi ya WASH- ujenzi wa vyoo inayotekelezwa katika
Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kwa miradi mingi fedha
zimepelea na ujenzi umesimama na kuacha magofu ya miradi
hiyo ambayo haitoi huduma iliyokusudiwa. Hakuna taarifa
iliyotolewa juu ya kupelea na kusimama kwa miradi hiyo na
hakuna mkakati uliowekwa wa kukamilisha miradi hiyo.
Kitendo cha kuanza kutekeleza miradi kwa fedha pungufu,
kuchelewa utekelezaji wa miradi bila sababu za msingi,
kukosekana kwa mikakati madhubuti ya kumalizia miradi hiyo na
Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kushindwa kutoa
taarifa sahihi kwa Wahisani, Wizarani, Baraza la Madiwani na Kata
husika kunazua maswali mengi yasiyo na majibu. Lakini pia
kwanini mradi usitekelezwe kwa awamu na kwa ukamilifu badala
ya kubaki na gofu lisilotumika.
2. Kubadilisha mpango wa bajeti bila idhini ya Baraza la
Madiwani
Mnamo Tarehe 8.02.2022 Baraza la Madiwani lilifanya kikao
maalum kwa ajili ya kupitia na kupitisha bajeti ya halmashauri ya
mwaka wa fedha 2022/23 bajeti ya Halmashauri hupitishwa kwa
kuzingatia Sheria ya Fedha ya Serikali za Mitaa namba 9 ya
mwaka 1982 kifungu cha 43 (i), ilani ya uchaguzi ya CCM ya
mwaka 2020 na ahadi za viongozi za wakati wa uchaguzi.
Katika vikao vya Kamati za Kudumu za Halmshauri ya Wilaya vya
robo ya kwanza imeonekana kuna ukiukwaji mkubwa sana wa
sheria na kanuni katika utekelezaji wa bajeti ambapo imeonekana
miradi mingi iliyopitishwa na baraza la madiwani haikupangiwa
fedha na kupendekezwa kupewa fedha miradi mingine mipya
ambayo haikuidhinishwa na kupangiwa fedha na Baraza la
Madiwani katika kikao halali cha kupitisha bajeti mwaka wa fedha
2022/2023. Baadhi ya maeneo hayo ni kama ifuatavyo:-
(i) Baraza la Madiwani lilipitisha fedha za lishe Tsh 109,000,000
na Fedha za Kilimo na Ushirika za Mapato ya ndani Tsh
50,000,000 jumla ya Tsh 159,000,000 Baraza lilipitisha fedha hizi
ziende kukamilisha miundombinu katika Zahanati 10 ili ziweze
kufunguliwa na kutoa huduma kwa wananchi na kila zahanati
ilipangiwa Tsh 15,900,000 kila moja Zahanati hizo ni (i) Itaba, (ii)
Mwanzugi, (iii) Mwageni B, (iv) Semu, (v) Malwilo Mnadani, (vi)
Igushilu, (vii) Makomangwa, (viii) Tindabuligi, (ix) Nata (x)
Itongolyangamba. Fedha hizi hazikupangwa katika bajeti kama
Baraza la Madiwani lilivyoamua kinyume na bajeti ilivyopitishwa.
(ii) Katika kupitisha Bajeti ya mwaka 2022/2023 Baraza la
Madiwani lilipitisha Tsh 500,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa mradi
wa Kituo cha Afya cha Iramba ndogo na Mwasengela yaani kila
kituo cha afya kilipangiwa kiasi cha Tsh 250,000,000. Fedha hizi
hazikuingizwa katika bajeti na badala yake zilibadilishiwa
matumizi bila idhini ya Baraza la madiwani na kupangiwa maeneo
mengine kama ifuatavyo:-
(a) Ujenzi wa nyumba ya mtumishi Zahanati ya Masanga Tsh
50,0000,000
(b) Ujenzi wa nyumba ya mtumishi zahanati ya Mwandu Kisesa
Tsh 50,000,000
(c) Ujenzi wa nyumba ya Mtumishi zahanati ya Semu Tsh
50,000,000
(d) Ujenzi wa nyumba mtumishi Zahanati ya Mwabagalu Tsh
50,000,000
(e) Ununuzi wa vifaa tiba kwa ajili vituo vya afya Tsh 300,000,000
Miradi hii iliyoonyeshwa (a) hadi (e) yenye thamani ya Tsh
500,000,000 haikupitishwa na Baraza la Madiwani na wala Baraza
halijawahi kupewa taarifa ya mabadiliko hayo ya mpango wa
Bajeti hadi hii leo Oktoba 2022, uamuzi uliofanywa na
Menejimenti wa kubadilisha mpango wa bajeti bila kibali na idhini
ya Baraza la Madiwani ni kinyume cha Sheria ya Fedha na Sheria
ya Bajeti.
3. Kutokutolewa kwa fedha za miradi ya maendeleo 40%
ya mapato ya ndani
Taarifa ya Mapato na matumizi ya kipindi cha Julai hadi Septemba
2022 inaonyesha kuwa fedha ya maendeleo 40% ya mapato ya
ndani iliyokuwa imetolewa ilikuwa kiasi cha Tsh 259,856,910
badala ya kiasi cha Tsh 481,984,136 iliyopaswa kutolewa kwa
kipindi hicho.
Kiasi cha fedha kilichokuwa kimekutumika ni Tsh. 103,000,000
kwa ajili ya mikopo ya akina mama, vijana na wenye ulemavu kati
ya fedha Tsh 259,856,910 zilizokuwa zimepokelewa huku Tsh.
156,856,910 zikibaki kwenye akaunti ya maendeleo.
Hapa kuna zua maswali mengi bila majibu sababu ya fedha za
miradi ya maendeleo 40% ya mapato ya ndani kukusanywa na
kutokupelekwa kwenye akaunti ya maendeleo ni zipi? Sababu ya
fedha kukusanywa na kuachwa kwenye akaunti badala ya
kupelekwa kutekeleza miradi ya maendeleo ni nini? Kwa miezi 4
sasa miradi inayotekelezwa kutokana na 40% ya mapato ya ndani
haijapelekewa fedha na utekelezaji wa miradi hiyo ni Sifuri.
Sababu za kutokutekeleza miradi ya maendeleo kama baraza
lilivyoidhinisha hazijulikani na hazijawahi kutolewa. Ingawa katika
vikao vya hivi karibuni mkurugenzi amekuja kuwasilisha
mapendekezo ya kubadili matumizi ya fedha za miradi ya
maendeleo kiasi cha zaidi ya Tsh 405,000,000 na kupendekeza
ziende kwenye kuanzisha miradi ya biashara ya ufyatuaji matofali,
shule ya chekechea na ujenzi wa maghala ya chumvi.
Hivyo kwa kipindi cha miezi 4 Mkurugenzi Mtendaji amekaidi
kupeleka fedha za maendeleo katika miradi iliyopitishwa kwenye
bajeti kwa lengo la kufanikisha nia yake ya kubadili matumizi ya
fedha hizo kwa malengo anayoyajua yeye.
4. Upendeleo na mipango mibovu katika ugawaji wa
fedha za maendeleo
Mwenyekiti na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
wamekuwa na tabia ya kuzipendelea baadhi ya kata kuzipa fedha
nyingi za miradi ya maendeleo huku kata zingine zikibaguliwa kwa
kuwa madiwani wa kata hizo hawaendani na mtizamo wa
viongozi hao. Pia kuna upendeleo wa dhahiri wa wajumbe wa
Kamati ya Fedha hapa ipo mifano mingi kama ifuatavyo:-
(i) Kata ya Mwangudo inayoongozwa na Mwenyekiti wa
Halmashauri Mhe. Anthony Philipo Athumani miradi iliyopewa ni
ujenzi wa kituo cha afya Iramba ndogo Tsh 500,000,0000, ujenzi
wa Ofisi ya Kata Mwangudo Tsh 11,000,000, Ukamilishaji wa
Bweni Shule ya Sekondari Makao Tsh 20,000,000, ukamilishaji wa
Bwalo la Chakula Shule ya Sekondari Makao Tsh 30,000,0000,
ukalimishaji wa nyumba ya mtumishi Shule ya Msingi Mbuyuni
50,000,000
(ii) Kata ya Mwasengela inayoongozwa na Mwenyekiti wa Kamati
ya Uchumi, Ujenzi, Hifadhi na Mazingira, Mhe. Mlangale Sakumi
Sayi miradi iliyopewa ni Ujenzi wa Kituo cha Afya Mwasengela Tsh
500,000,000, Ujenzi wa Bweni la Wasichana Lingeka Sekondari
Tsh 73,000,000, ujenzi wa madarasa mawili Shule ya Msingi
Ng’hanga Tsh 25,000,000, ujenzi wa madarasa mawili Shule ya
Msingi Ng’hanga Tsh 40,000,000, ukamilishaji wa Jengo la OPD
na nyumba ya mtumishi katika Zahanati Mwamhongo Tsh
148,000,000.
(iii) Kata ya Lingeka inayoongozwa na Mjumbe wa Kamati ya
Fedha, Mhe. Joseph Nyanza Sayi miradi iliyopewa ni ukamilishaji
madarasa 4 na ofisi 2 Tsh 50,000,000, ukamilishaji wa madarasa
2 na ofisi 1 Shule ya Msingi Masanga Tsh 40,000,000, ujenzi wa
maabara Shule ya Sekondari Masalinge Tsh 73,000,000, Ujenzi
wa Sekondari mpya Masalinge (Maalum) Tsh 600,000,000
Na hii haingii akilini katika bajeti Shule mpya ya Sekondari
Masalinge (Lingeka) imepangiwa kiasi cha Tsh 600,000,000 kwa
ajili ya ujenzi wa madarasa na miundombinu mingine ikiwemo
maabara lakini wakati huo huo tena inapangiwa kiasi cha Tsh
73,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya maabara. Pia Kata
ya Lingeka imepangiwa kiasi cha Tsh 100,000,000 kwa ajili ya
ujenzi wa OPD na nyumba ya mtumishi katika Zahanati ya
Masanga.
(iv) Kata ya Mwandoya ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Fedha,
Mhe. Basu Kayungilo imetengewa Tsh 130,000,000 kwa ajili ya
ujenzi wa Wodi ya wazazi katika Kituo cha Afya Mwandoya wakati
Kituo cha Afya cha Mwandoya kina wodi ya Wazazi haya
yanafanywa kukiwa na mahitaji makubwa ya miundombinu ya
afya katika maeneo mbalimbali. hiyo ni mifano michache tu ya
baadhi tu ya kata zilizopendelewa
Baadhi ya Kata zinazobaguliwa na kutokupangiwa miradi
inavyostahili ni Kata ya Kabondo, Kata ya Mbugayabanhya, Kata
ya Mbushi, Kata ya Mwabuzo, Kata ya Mwabusalu, Kata ya
Tindabuligi, Kata ya Mwakisandu, Kata ya Imalaseko, Kata ya
Nghohoboko n.k
Kata ya Mbushi kwenye Bajeti Baraza lilipitisha Tsh 600,000,000
kwa ajili ya ujenzi wa Sekondari ya Kata na fedha hizo
zimeondolewa na hazijulikani zilipo.
Kata ya Mbugayabanhya kata hii haina sekondari mpya katika
kupitisha bajeti ya mwaka wa 2022/2023 Baraza la Madiwani
lilipangia Tsh 80,000,000 kwa ajili ya kuanzisha Sekondari mpya
lakini fedha hizo zimeondolewa.
Kata nyingine ni Tindabugili ina magofu mengi na yalikuwa
yamepangiwa fedha katika Bajeti lakini kwa sasa fedha
hazionekani tena. Hii ni mifano michache lakini ziko baadhi ya
kata nyingi zilizobaguliwa kwenye miradi ya maendeleo.
5. Ukiukwaji wa taratibu za uundwaji wa Kamati ya
Fedha, Utawala na Mipango.
Katika kuunda Kamati ya Fedha, utawala na mipango, Mwenyekiti
wa Halmashauri na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya
Meatu wamekiuka Kanuni Namba 40(5) kinachosema Mwenyekiti.
wajumbe wa Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango na kuyaleta
ndani ya Baraza la Madiwani na kupitishwa kwa kura na baraza la
madiwani lakini kamati iliyochaguliwa ndani yao wajumbe 6
walipaswa kupigiwa kura na baraza la madiwani lakini mwenyekiti
na mkurugenzi hawakufanya hivyo na kamati hiyo
iliyopendekezwa na mwenyekiti wa halmashauri hadi sasa
inaendelea na vikao na ziara kama kawaida na wanalipwa stahili
zao kama kawaida hapa kuna ukiukwaji mkubwa sana wa kanuni
tajwa hapo juu.
Kwa mantiki hiyo Mwenyekiti wa Halmashauri hakuleta orodha ya
wajumbe aliowapendekeza kwenye baraza la halmashauri ili
yapigiwe kura kama kanuni zinavyoelekeza badala yake ameteua
yeye hivyo kukiuka kanuni na kutumia madaraka yake vibaya.
6. Matumuzi mabaya ya fedha za Serikali
Mwenyekiti na Mkurugenzi wa Halmshauri wamekuwa na desturi
ya kutumia vibaya fedha za Halmshauri bila idhini ya Baraza la
Madiwani kinyume na Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa. Ipo
mifano kama ifuatavyo:-
(i) Katika miradi ya UVIKO-19 Mwenyekiti wa Halmshauri na
Mkurugenzi wametumia vibaya fedha za Serikali kwa kuagiza
mabati katika miradi yote bila idhini ya Baraza la Madiwani na bati
moja lilinunuliwa kwa Tsh. 40,000 na wakati huo bei ya juu kwa
bati hizo katika soko ilikuwa ni Tsh 35,000 kwa kila bati la gage
28 maamuzi haya yalikiuka Sheria, Kanuni na miongozo
iliyowekwa.
(ii) Katika ujenzi wa Zahanati 4 za Makomangwa, Mwanyahina,
Sapa na Mwandu Kisesa ambapo kila zahanati ilipewa Tsh Milioni
50 na jumla ya Tsh Milioni 200 zilitumika kwa kukiuka utaratibu
wa Force Account ambapo mikataba ya ujenzi huo ilisainiwa na
Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya badala ya Kamati
za vijiji husika zilizopewa hiyo miradi.
(iii) Katika utekelezaji wa bajeti ya Mwaka 2021/2022 Mwenyekiti
na Mkurugenzi wamekiuka kanuni kwa kuhamisha fedha Tsh
Milioni 25 kutoka Igushilu na fedha Tsh Milioni 25 toka Mwanzugi
ambazo zilikuwa za ukamilishaji wa miundombinu ya Zanahati
katika vijiji hivyo na badala yake fedha hizo zote Tsh Milioni 50
zilipelekwa Kijiji cha Dakama kujenga nyumba ya mtumishi katika
zahanati hiyo ambayo haikuwa katika bajeti.
(iv) Kuanza kutekeleza majukumu na kulipwa posho wajumbe 6
wa Kamati ya Fedha ambao si wajumbe halali wa Kamati ya
Fedha, Utawala na Mipango kwani wajumbe hao hawakupigiwa
kura na Baraza la Madiwani hivyo kutumia vibaya jumla ya Tsh
Milioni 4.8 kwa mchanganuo ufuatao:-
(a) Kikao (i) @ 250,000 x 6 = 1,500,000
(b) Ziara (i) @ 550,000x 6 = 3, 300,000
7. Utoaji holela wa mikopo ya akina mama, vijana na
walemavu
Kumekuwepo na utoaji holela na upendeleo wa mikopo ya akina
mama, vijana na wenye ulemavu kwa vikundi vinavyopata mikopo
katika Halmashauri ya Wilaya ya Meatu hali inayopelekea vikundi
vingi vya uzalishaji mali kukosa mikopo huku vichache vikinufaika
kinyume na malengo ya kuanzishwa kwa utaratibu wa mikopo ya
aina hii. Baadhi ya mifano katika mwaka wa fedha 2021/2022
mikopo iliyotolewa kwa vikundi ni kama ifuatavyo:-
(i) Kikundi cha vijana cha Heroes Group chenye wanachama
watano kimepewa mkopo wa kununua Min Bus yenye thamani ya
Tsh 72,000,000 huku muda wa kurejesha ni miaka 4
(ii) Kikundi cha akina Mama cha Hapa Kazi Tu chenye wanachama
watano kimepewa mkopo wa Trekta wenye thamani ya Tsh
74,150,000 umri wa mkopo ni miaka 7
(a) Mkopo huu ni mkubwa sana kutolewa kwa kikundi kimoja
kulingana na mapato yanayopatikana kila mwaka katika
halmashauri, wastani wa 4% ya mapato ya ndani kwa mikopo ya
vijana ni Tsh 100,000,000 tu hivyo ukitoa mkopo kwa kikundi
kimoja cha Tsh 72,000,000 umebakiwa na Tsh 28,000,000 tu kwa
vikundi vyote kutoka vijiji vyote vya Wilaya ya Meatu.
(b) Kutolewa kwa mkopo huu kwa kikundi kimoja cha vijana
kutoka Kijiji cha Mwanhuzi Bomani na kikundi kimoja cha
wanawake kutoka Kijiji cha Bukundi kulipelekea vikundi vingi vya
akina mama, vijana na wenye ulemavu kukosa mikopo katika
Wilaya ya Meatu. Vikundi vingi viliomba mkopo lakini
havikufanikiwa kwa maelezo ya upungufu wa fedha, sababu za
kupendelewa vikundi viwili kwa gharama za wana Meatu wote ni
nini?
(c) Gharama ya kununua Min Bus ni Tsh 62,000,000 kwa nini
mkopo umetolewa wa Tsh 72,000,000? Imekuwa ikohojiwa
kwenye vikao mbalimbali vya halmashauri lakini hakuna majibu
ya uhakika yanayotolewa.
(d) Sababu ya vikundi hivi kujipatia Mikopo ya Min Bus na
Matreka kupitia mikopo ya akina mama, vijana na wenye ulemavu
ilikuwa ni nini kwani mikopo ya aina hiyo ingewezwa kuombwa
kupitia Taasisi za Fedha badala ya kupitia halmashauri ambazo ni
fedha kidogo kwa ajili ya wananchi wanyonge.
(e) Tathimini ya utoaji wa mikopo hiyo inaleta mashaka makubwa
kama vikundi hivyo vitaweza kurejesha mikopo hiyo kwani uimara
na muda wa uchakavu kwa mashine na mitambo ni wastani wa
miaka 3 mpaka miaka 5 hayo marejesho ya miaka 7
yatarejeshwaje wakati mitambo itakuwa haipo.
(f) Hakuna uthibitisho wa tathmini ya kitaalamu uliyofanywa
kujiridhisha uwezo wa vikundi hivyo kurejesha mkopo kwa muda
uliowekwa. Hakuna maoteo ya taarifa za fedha yanayothibitisha
vikundi hivyo kumudu kurejesha mkopo huo. Kushindwa kufanya
marejesho kwa vikundi hivyo kutaleta hasara kubwa kwa
Halmashauri na Serikali kwa ujumla lakini pia itazorotesha zoezi la
utoaji wa mikopo kwa wananchi.
Haya mambo yote yamefanywa na Divisheni ya Maendeleo ya
Jamii kwa kibali na Baraka za Mkurugenzi Mtendaji na Mwenyekiti
wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu.
3.0 HITIMISHO
Halmashauri ya Wilaya ya Meatu inaendeshwa kwa ukiukwaji
mkubwa wa Sheria, Kanuni na Taratibu na matumuzi mabaya ya
madaraka hali inayopelekea upotevu mkubwa wa fedha za umma
na hasara kubwa kwa taifa.
Kuchelewa na Kukwama kutekelezwa kwa miradi ya maendeleo
kunachelewesha utoaji wa huduma kwa wananchi, udhaifu huu
unathibitisha kuwa kwa kiwango kikubwa Mwenyekiti na
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
wamepwaya na wameshindwa kumudu majukumu yao.
Lakini pia kutokana na udhaifu huu mkubwa wa usimamizi na
uendeshaji CAG afanye ukaguzi maalum kwa Halmashauri ya
Wilaya ya Meatu.
Mwisho.
ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI WANAOUNGA
MKONO HOJA HII:-
- Seni Sitta - Diwani Kata ya Itinje - Simu Na. 0621 139 000
- Daudi M. Sollo – Diwani Kata ya Mwakisandu – Simu Na. 0621 944 915
- Masumbuko Pesa – Diwani Kata ya Mbugayabanhya – Simu Na. 0712 342 564.
- Charles Lunjini – Diwani Kata ya Mwabuzo – Simu Na. 0785 542 427.
- Tabu Magembe – Diwani Kata ya Tindabuligi – Simu Na. 0626 131 569.