Shebbydo
JF-Expert Member
- Feb 12, 2015
- 1,176
- 1,939
- Thread starter
- #41
Mkuu unaposema malipo kidogo sidhani kwa hali halisi ilivyo kwa watumishi wa umma hapa nchini upande wa mishahara ni sahihi kusema hivyo. Nadhani ukitoa wanasiasa na ma-CEO na ma-DG watu wakada hii wana unafuu kuliko wenzao. Hizi hospitali mbili za Mwanza, yaani ya Butimba(DDH) na hiyo ya Sekou Toure kumekuwa na matatizo ya rushwa iliyokithiri ambayo imejenga chuki kubwa kati ya watumishi na wananchi.Hebu dadavua hoja yako in detail, kwamba what exactly happenned. Umekuwa biased zaidi kuwalaumu hao watumishi wote wa afya wa Mwanza bila kusema ni kitu gani hasa kimewafanya kuchukua maamuzi ya kufanya kitu kama mgomo hivi.
Mimi nimesikia kupitia vyombo vya habari haya kuhusu baadhi ya madaktari, manesi na wauguzi wa Mwanza;
1. Kwamba RC Mwanza alisikia malalamiko ya baadhi ya wagonjwa kutohudumiwa vizuri ikiwemo huyo mjamzito kujifungulia (sina hakika ni ktk mazingira gani na kwa nini, lakini inasemekana alijifungua mtoto/watoto ambao walifariki). Kwa incident hii wananchi walikasirika na kuona kuwa kuna uzembe flani ulitokea ndiyo maana hilo likatokea. Kelele hizi zikasikika na RC akafika ktk hospitali hiyo na kuamuru baadhi ya madkatari na manesi kusimamishwa kazi kwa malalamiko tu ya wananchi kupitia camera za TV!
2. Jana juma4 au juzi juma3 nikasikia tena kupitia vyombo vya habari kuwa madaktari, manesi na wahudumu wa afya wa hospitali nadhani ya Butimba ambayo ni DDH ya manispaa ya Nyamagana "wanatishia" = "kugoma" kutukuendelea na majukumu yao kwa sbb ya usalama wao kazini kutolindwa na pia kutotendewa haki especially kuadhibiwa pasipo kufuata taratibu na kusikilizwa.
Nadhani hoja ya msingi iko hapa yaani KUADHIBIWA PASIPO KUFUATA TARATIBU ZA KIUTUMISHI NA KUSIKILIZWA.
Aidha, watumishi wa afya kwa ujumla wao wanalalamikia mazingira duni ya utoleaji huduma kwa wagonjwa ikiwemo ukosefu kabisa wa vitendea kazi kwa maana ya vifaa tiba, upungufu wa madaktari, manesi na wahudumu wengine wa afya to the extent kwamba mtumishi mmoja analazimika kufanya kazi masaa mengi kuliko kawaida kuhudumia
wagonjwa, malipo duni nk
Swali ni je, tunafikiria haya kabla ya kuchukua hatua ya kuwalaumu hawa?
Kingine mimi nadhani matatizo mengine yapo kwa wagonjwa wenyewe na watu wao wanaowauguza.
Mfano kwa mama mjazito, alibeba mimba akakaa tu nyumbani na hata siku moja hakuwahi kuhudhuria kliniki ili kuwezesha daktari kufanyia monitoring ya ujauzito huo,muda wa kujifungua ukafika ikashindikana kujifungulia nyumbani na sasa uamuzi ukafika wa kupelekwa hospitali, ni lazima mama huyu na ujauzito wake atakuwa kwenye risk kubwa ya kupoteza maisha au mtoto wake.
Swali langu ni hili, kuwa was this considered kabla ya kufikia maamuzi yoyote? Je, ni kwa sbb tu wananchi wamepiga kelele, then na sisi viongozi kwa sbb tunatekeleza majukumu yetu kwa "mzuka" tu pasipo kuzingatia taratibu, kanuni na sheria zilizopo? Wananchi hawa wana elimu ya kutosha juu ya wajibu na haki zao au ni kwa sbb tu wamelishwa kasumba na kuaminishwa kuwa watumishi wa umma madaktari na manesi wakiwemo ni wala rushwa na kwa hiyo popote mlipo pigeni kelele na serikali itachukua hatua? Tutakwenda na kufika salama kweli kwa mtindo huu wa ufanyaji kazi?
Hakuna anayebisha kuwa kuna baadhi ya watumishi wa umma kweli walikuwa wamejisahau na walikuwa hawatekelezi wajibu wao ipasavyo.
Mimi ninachojaribu kusisitiza hapa ni kuwa, katika kurudisha maadili na nidhamu katika utumishi wa umma ni lazima kufanyike kwa uangalifu mkubwa ili tusije kuwatia hofu hata wasio na matatizo na kushindwa kutekeleza majukumu yao na wakati huohuo taratibu, kanuni na sheria za utumishi wa umma zikizingatiwa ipasavyo.
Haiwezekani RC au DC au Waziri yeye ndiye awe mtoa amri tu ya fukuza huyu, simamisha kazi huyu au hamisha huyu na peleka kule. Itakuwa ni chaos
Aidha serikali nayo itende na itekeleze majukumu yake na isiwe ni chanzo cha watumishi hawa kuonekana hawafanyi kazi zao ipasavyo.
Mfano ipeleke vitendea kazi na pesa ktk hospitali zake kwa wakati ili hawa watumishi wasiwe na visingizio.
Mimi niko Shinyanga. Juzi kati mwanangu alikuwa anaumwa na nikampeleka ktk kituo cha afya cha serikali kilipo jirani nami. Akapimwa na kukutwa anasumbuliwa na minyoo na U.T.I.
Daktari akamwandikia dawa hizi kentrax, erythromicine na panadol. Amini usiamini, nilipata panadol pekee hapo na zingine zote nilikwenda kununua ktk maduka ya madawa mitaani licha ya kuwa natumia NHIF card na kila mwezi nakatwa ktk mshahara wangu takribani Tshs 60,000/= kuchangia bima ya afya!
Sasa ktk mazingira haya, who is to blame? Serikali au wauguzi naadaktari?
Haiwezekani focus iwe ktk hospitali za Muhimbili tu na kuzisahau zahanati na vituo vya afya vijijini ambako huko pia ndiko kuliko matatizo makubwa!!
Mkuu chuki huwa haizuki ghafla tu, lazima inakuwa na chanzo. Hivi kweli mwananchi atakuwa na chuki dhidi ya daktari au nesi aliyemhudumia vizuri ili iweje? Kwa hali ya rushwa ilivyofikia hapa nchini, sasa hawa viongozi ambao wametaka kurejesha imani kwa wananchi dhidi ya serikali iliyochukiwa kwa kiwango cha hali ya juu wamelazimika kutumia nguvu kubwa sana ambayo sasa imelipua hasira za wananchi.
Mimi nadhani kuna haja ya kila mmoja wetu kujitathmini na kuanza upya lakini hali ya kutunishiana misuli haitotufikisha popote zaidi ya kuangamia.