Madaktari wa Mwanza wanaipima Serikali?

Madaktari wa Mwanza wanaipima Serikali?

Haya mambo yamepitwa na wakati kutegemea huruma ya daktari kuhudumia mgonjwa au panga la wanasiasa kutishia madaktari ndio wafanye kazi.

Dunia nzima sasa hivi hospitali zimefungwa systems ambapo mgonjwa akisajiliwa hospitalini tu inajulikana ni saa ngapi na kuonyesha amepangiwa daktari nani. Akihudumiwa na daktari kwenye system inasoma, akipangiwa kwenda maabara inaonyesha na kapima vipimo gani na majibu ni yepi hadi siku mgonjwa anatoka hospital na inabaki kwenye medical records. Kufanya kazi kisisiemu sisiemu kwa kutegemea huruma na kutishiana imebakia Tanzania tu na hata hao akina Majaliwa na Magufuli hawataweza kufika hospitali zote Tanzania, lakini MIS zinaweza kufungwa kila hospitali na kituo cha afya. Dunia imebadilika nyie maccm, wekeni MIS kwenye mahospitali, wekeni CCTV mabarabarani maisha yawe mazuri. Mbona kodi mnatukamua sana
 
Ndugu inaonekana kama kuna mass mobilization dhidi yao sasa, nani kamobilize jamii dhidi ya watu wa afya?......... sikatai kuwa afya kuna matatizo, nadhani njia wanazo zitumia kuwajibisha watovu wa nidhamu ndo zenye matatizo .
Mkuu ukitazama undani wa tatizo hili utaona kuna chuki imejengeka muda mrefu kati ya jamii na watumishi wa afya. Sasa huu uhasama umeanzia wapi? Utakuta ni pale watumishi wa afya walipowabadilikia wananchi kutoka kuwa wafariji wao wanapokuwa katika hali ya ugonjwa na kuwa makatili kama wanajeshi vitani.
 
Ok! palipo na neno mhudumu nilimaanisha "mtumishi" ili kuleta collectiveness.
Kuna madaktari na manesi wanahudumia wananchi kwenye preventive care na hao unawajumuisha huko?
 
Haya mambo yamepitwa na wakati kutegemea huruma ya daktari kuhudumia mgonjwa au panga la wanasiasa kutishia madaktari ndio wafanye kazi.

Dunia nzima sasa hivi hospitali zimefungwa systems ambapo mgonjwa akisajiliwa hospitalini tu inajulikana ni saa ngapi na kuonyesha amepangiwa daktari nani. Akihudumiwa na daktari kwenye system inasoma, akipangiwa kwenda maabara inaonyesha na kapima vipimo gani na majibu ni yepi hadi siku mgonjwa anatoka hospital na inabaki kwenye medical records. Kufanya kazi kisisiemu sisiemu kwa kutegemea huruma na kutishiana imebakia Tanzania tu na hata hao akina Majaliwa na Magufuli hawataweza kufika hospitali zote Tanzania, lakini MIS zinaweza kufungwa kila hospitali na kituo cha afya. Dunia imebadilika nyie maccm, wekeni MIS kwenye mahospitali, wekeni CCTV mabarabarani maisha yawe mazuri. Mbona kodi mnatukamua sana
Kuna wakati watu tunasahau kama tupo Tanzania na tunaongea kama tupo Ulaya! Tunawaza kufunga MIS ilihali vifaa tiba bado ni matatizo.
 
Habari wana JF, hivi karibuni tumeona tukio moja likitokea huko Mtwara la Kusimamishwa Daktari mmoja aliyehusika katika kuomba rushwa kutoka kwa mgonjwa aliyetakiwa kufanyiwa upasuaji.
Japo ushahidi ni mgumu wa mazingira ya hiyo rushwa, ni ukweli usio na kificho kuwa Wahudumu wa afya walio wengi wamekuwa si waaminifu tena wasiokuwa na chembe ya huruma kwa binadamu wenzao kiasi cha kutojali uhai wa wagonjwa wanaowahudumia.
Tukio la Mtwara limefuatana na matukio mawili ya kusikitisha yaliyotokea katika jiji la Mwanza, wilaya ya Nyamagana kwenye hospitali ya wilaya ya Nyamagana (Butimba) na hospitali ya mkoa ya Sekou Toure.
Likitangulia la hospitali ya Butimba, mama mmoja alijifungulia chooni watoto mapacha na wakafariki kwa kile kilichodaiwa ni uzembe wa manesi waliokuwa wakimtolea kauli chafu mjamzito huyo kuwa awaite Majaliwa na Magufuri waje wamhudumie.
Tukio jingine lililofuatia ni kufariki kwa mama na watoto wake mapacha katika hospitali ya mkoa (Sekou Toure) kwa kucheleweshwa kuongezwa damu.
Kutokana na matukio hayo, kuna manesi na madaktari wametiwa nguvuni kutokana na kasi iliyopo sasa ya kurejesha nidhamu na uwajibikaji katika utumishi wa umma. Sasa Madaktari wamefanya mgomo katika hospitali ya Butimba kwa madai wanaogopa usalama wa kazi yao kwa kuwa wao hawawezi kuzuia kifo kwa mgonjwa pale muda wake unapokuwa umefika.
Mheshimiwa Rais, sichelei kusema hawa madaktari wanataka kutunishiana misuli na serikali yako kwa kile kilichotokea Mtwara. Kwanini Wananchi wote wanaokumbwa na masahibu haya kutoka kwa wahudumu wa afya katika maelezo yao wanaambiwa wawaite Majaliwa na Magufuli wawahudumie?
Mheshimiwa watumie vijana wako wa TISS wakupe taarifa kamili ili ujue utapambana vipi na udhalimu wa baadhi ya watumishi wa afya ambao wanafikiri kuwa wao ni bora katika jamii kuliko watu wengine wakisahau kuwa wao pia ni product ya mwalimu, hivyo tunaishi kwa kutegemeana.
Sasa wacha tuone mwisho wa hiyo Vita ya taasisi
 
Kuna tatizo pia la uwiano wa wagonjwa na madaktari na manesi kwa ujumla.Lisipoangaliwa vyema litaleta shida.Kuna kuchoka sana iwapo uwiano haupo vyema.

Then,mtendaji anayehangaika hivyo inapofikia mwisho wa mwezi kwenye account yake hakiingii kulingana na wajibu wake,ila mwanasiasa awepo bungeni au asiwepo,aongee au asiongee mshahara wake ni mkubwa sana.Kwenye utendaji chini ya kiwango,wizi na rushwa na kashfa nyinginezo,mtendaji anakamatwa na kupelekwa mahakamani ila mwanasiasa ni exceptional,haguswi wala hazungumziwi.Itaunda TABAKA la wenye haki na wasio na haki baadae INAKATISHA TAMAA na watu kutokuwa morali ya kufanya kazi kwa weledi hata pale wanapozidiwa na majukumu yao.

Ngoja niulize,nipate jibu.Hivi kuna wanasiasa wenye madeni serikalini??Jumla ya madeni yao yanaweza kufikia sh.ngapi??
Nakuunga mkono wananchi lazima waamke unakuta mwanasiasa anafika kwenye kituo cha afya na gari la million mia mbili na suti kali. uzeni hayo magari mlete vifaa tiba na kuboresha maslahi ya watumishi wa afya kama mnavyofanya kwenye mashirika ya umma watoto wenu wanapofanya kazi i.e tra bot ewura nhif Sumatra n.k. Wananchi waache kubweteka kwa maneno ya wanasiasa wafanye uchunguzi na kujua ni kiasi gani cha fedha kinachotengwa kwa ajili ya afya zao. Na waandishi wa habari fanyeni utafiti wa kina juu ya Medical Services in Tanzania zinatengewa kiasi gani na halisia wanapokea kiasi gani, tuache siasa tufanye kwa vitendo. Ningefurahi mwanasiasa anapotembelea kituo cha afya aulize kiasi cha fedha zilizo tolewa kwa ajili ya matibabu sio kuwalaumu wafanya kazi kwa mambo ambayo yako uwezo wao
 
Daktari anafanya kazi masaa mangap kwa siku? siku ngapi kwa week??
Daktari analipwa sh. Ngap? anakatwa sh. Ngap?
daktari anapaswa kuwa na familia au laaaah?? akiwa nayo mke wa daktari anakaa na mumewe au mkewe lini? watoto wake wanapataje wasaa wa kukaa na wazazi wao??
most of u guys mnalala jumamosi na jumapili. Weekdays mnatoka kazin sa. 11 Maximum.
Most of us tunakaa hospital mpaka sa 2, na usiku tunaamshwa kuja kuwahudumia nyie kama ndugu zetu. We work 7days a week, and our timetable always accomodate room ya kuitwa hata kama usiku sa. 10 Niko natengeneza mtoto... u think we get paid fo that? Well we dont. Our children wanakua with pride wazaz wao madr. But we are poorest parents ever, its not a choice is default kwenye system yetu.. sio kwamba nilichagua niwe daktari so as kutake every crap ambayo utakuja nayo kwakuwa we ni mgonjwa. And sisi ni watu pia, nina familia, nina ndugu... mshukuru mungu ukienda kazini unaenda kuhesabu hela au Kuandika kwenye makaratasi.. nataman siku moja ungejua inakuaje unaamkia kuwasikiliza watu ambao wengi wao sio waekewa na hawajali wenzao bali wao wenyewe..
Ofisi ya serikali ikifika sa. 7-8 Ni muda wa kula ila dr. Akiacha clinic muda huo kwenda kula utaambiwa tumekuja sa. 12 Bila hata kujua wewe upo pale tangu jana.. you dont ask, you never ask.. doctors are most non-selfish people out there but hamuwez kujua kwakua mnaangalia mambo mnayoyafanya kwenye 24 hours nakuzan tinalingna..
fine, ni vizuri kuwaza mnavyowaza kwakua scope ya what mmewitness haiwaruhusu kuwaza beyond that..
Anf no, drs. Hawana lugha mbaya but kama human akiwa na bad mood learn kuongea naye pia..
We work in most difficulty environments, tunajitoboa kuhudumia wagonjwa wa HIV, personally nishawah kumzalisha mtoto kwa mikono mitupu 5years ago wakati hamna gloves. I risked my life mom was positive, alafu leo mnakuja kuongea ujinga without hata kusikiliza mazingira yakoje..
Its shame nchi kama yetu inamadaktar wachache na tuko 45 mil.
mnazan madakatari wenye vyet wanafika hata elfu 20???
Fine, we bleed for ua relatives, we abandon our husbands, wives for you.. tunachoka pia, tutachoka one day.. its not fair, u may not see these but one day mtajua.. NIMEIKUTA MAHALI!!
Madaktari wetu wanapenda mno kutukuzwa,wanapenda mno wao kuchukuliwa kama ni watu muhimu kuliko mtu mwingine yeyote jambo ambalo sio sahihi,tuheshimiane kwani hakuna kazi ambayo haina umuhimu,unaweza dharau kazi fulani lakini siku moja mfanya kazi wa kazi hio unayoidharau anaweza akakukwamisha kwenye jambo ambalo kwako ni muhimu sana kulifanikisha wakati huo,kudhihirisha umuhimu wa kila kazi kila idara kuna rushwa,sasa kwanini watu watoe rushwa wakati inalohitaji afanyiwe halina umuhimu?
 
Ukifuatilia uhusiano kuwa mbovu kati ya watumishi wa afya na jamii Mwanza, chanzo ni hao watumishi wa afya kutokana na rushwa iliyokithiri. Waulize watu wa Mwanza wakuambie hali rushwa ilivyo mahospitalini.
Nakubaliana na ww mkuu RUSHWA ni tatizo ili kuchukiana na kuhaiwezi kuondoa tatizo hili hapa inabidi sheria na kanuni za utumishi zikae vizuri ili ziwabane hawa jamaa kuitumikia jamii
 
Nakubaliana na ww mkuu RUSHWA ni tatizo ili kuchukiana na kuhaiwezi kuondoa tatizo hili hapa inabidi sheria na kanuni za utumishi zikae vizuri ili ziwabane hawa jamaa kuitumikia jamii
Mimi nafikiri mindset ya watumishi wa afya ibadilike ili kuleta mutual understanding na jamii.
 
Madaktari wetu wanapenda mno kutukuzwa,wanapenda mno wao kuchukuliwa kama ni watu muhimu kuliko mtu mwingine yeyote jambo ambalo sio sahihi,tuheshimiane kwani hakuna kazi ambayo haina umuhimu,unaweza dharau kazi fulani lakini siku moja mfanya kazi wa kazi hio unayoidharau anaweza akakukwamisha kwenye jambo ambalo kwako ni muhimu sana kulifanikisha wakati huo,kudhihirisha umuhimu wa kila kazi kila idara kuna rushwa,sasa kwanini watu watoe rushwa wakati inalohitaji afanyiwe halina umuhimu?
Hii mindset ya baadhi ya madaktari kuona wao ni bora kuliko wengine inaanzia hata vyuoni wakati bado wanasoma, huwa wanaona kozi zao ni bora kuliko kozi zingine.
 
Acheni kuingiza siasa kwenye taaluma zenye akili, madaktari wamekua Mungu kuzuia vifo..!!?
 
Sipendi dhana inayoanza kujengwa ya kutengeneza uadui kati ya watumishi wa umma na wananchi.
 
Yaani*

Kweli mkuu jamii inawadharau hao madaktari kama Mwanza nilisikia Dr.fulani akisema kuna uhusiano mbaya kati ya jamii na watumishi wa hosp.hiyo

Sijui tunapoelekea katika hili
Hata Serikali inauhusiano mbaya na watumishi wake: Serikali inajua kuwa citizens wake wanawachukuia watumishi wake, Serikali inashiriki kwenye mob justice ya kumsurubu daktari kwa mere allegations za mtummoja, Serikali inaamua ku create scarcity ya madsktar ili ijisafishe kwa wananchi, Serikali haioni kuwa sasa imeawaumiza wote- mzigo mzito kwa waliobaki na kuchelewesha huduma kwa wananchi wake, poor we.
 
Sipendi dhana inayoanza kujengwa ya kutengeneza uadui kati ya watumishi wa umma na wananchi.
uhasama lazima uwepo kama wataendelea kutuacha tujifungulie kwenye mabeseni, wabake binti zetu na watudhulumu viwanja.
 
Hey Tanzanians! You shall reap what you are sowing now! Be careful.
 
Hebu dadavua hoja yako in detail, kwamba what exactly happenned. Umekuwa biased zaidi kuwalaumu hao watumishi wote wa afya wa Mwanza bila kusema ni kitu gani hasa kimewafanya kuchukua maamuzi ya kufanya kitu kama mgomo hivi.

Mimi nimesikia kupitia vyombo vya habari haya kuhusu baadhi ya madaktari, manesi na wauguzi wa Mwanza;

1. Kwamba RC Mwanza alisikia malalamiko ya baadhi ya wagonjwa kutohudumiwa vizuri ikiwemo huyo mjamzito kujifungulia (sina hakika ni ktk mazingira gani na kwa nini, lakini inasemekana alijifungua mtoto/watoto ambao walifariki). Kwa incident hii wananchi walikasirika na kuona kuwa kuna uzembe flani ulitokea ndiyo maana hilo likatokea. Kelele hizi zikasikika na RC akafika ktk hospitali hiyo na kuamuru baadhi ya madkatari na manesi kusimamishwa kazi kwa malalamiko tu ya wananchi kupitia camera za TV!

2. Jana juma4 au juzi juma3 nikasikia tena kupitia vyombo vya habari kuwa madaktari, manesi na wahudumu wa afya wa hospitali nadhani ya Butimba ambayo ni DDH ya manispaa ya Nyamagana "wanatishia" = "kugoma" kutukuendelea na majukumu yao kwa sbb ya usalama wao kazini kutolindwa na pia kutotendewa haki especially kuadhibiwa pasipo kufuata taratibu na kusikilizwa.

Nadhani hoja ya msingi iko hapo yaani KUADHIBIWA PASIPO KUFUATA TARATIBU ZA KIUTUMISHI NA KUSIKILIZWA. Hii inadhalilisha, kuogepesha na kukatisha tamaa sana!

Aidha, watumishi wa afya kwa ujumla wao wanalalamikia mazingira duni ya utoleaji huduma kwa wagonjwa ikiwemo ukosefu kabisa wa vitendea kazi kwa maana ya vifaa tiba, upungufu wa madaktari, manesi na wahudumu wengine wa afya to the extent kwamba mtumishi mmoja analazimika kufanya kazi masaa mengi kuliko kawaida kuhudumia
wagonjwa, malipo duni nk

Swali ni je, tunafikiria haya kabla ya kuchukua hatua ya kuwalaumu?

Kingine mimi nadhani matatizo mengine yapo kwa wagonjwa wenyewe na watu wao wanaowauguza kutokuwa na elimu ya kutosha juu ya haki na wajibu wao.

Mfano kwa mama mjazito, amebeba mimba akakaa tu nyumbani na hata siku moja hakuwahi kuhudhuria kliniki ili kuwezesha daktari kufanyia monitoring ya ujauzito huo.

Muda wa kujifungua ukafika ikashindikana kujifungulia nyumbani kama walivyotarajia na sasa uamuzi ukafikiwa wa kupeleka hospitali. Ni lazima mama huyu na ujauzito wake atakuwa kwenye risk kubwa ya kupoteza maisha au mtoto wake.

Maswali yangu ni haya, kuwa was this considered kabla ya kufikia maamuzi yoyote?

Au ni kwa sbb tu wananchi wamepiga kelele, then na sisi viongozi kwa sbb tunatekeleza majukumu yetu kwa "mzuka" tu pasipo kuzingatia taratibu, kanuni na sheria zilizopo?

Je, wananchi hawa wana elimu ya kutosha juu ya wajibu na haki zao au ni kwa sbb tu wamelishwa kasumba na kuaminishwa kuwa watumishi wa umma madaktari na manesi wakiwemo ni wala rushwa na kwa hiyo popote mlipo pigeni kelele na serikali itachukua hatua? Na je, tutakwenda na kufika salama kweli kwa mtindo huu wa ufanyaji kazi?

Hakuna anayebisha kuwa kuna baadhi ya watumishi wa umma kweli walikuwa wamejisahau na walikuwa hawatekelezi wajibu wao ipasavyo.

Mimi ninachojaribu kusisitiza hapa ni kuwa, katika kurudisha maadili na nidhamu katika utumishi wa umma ni lazima kufanyike kwa uangalifu mkubwa ili tusije kuwatia hofu hata wasio na matatizo na kushindwa kutekeleza majukumu yao na wakati huohuo taratibu, kanuni na sheria za utumishi wa umma zikizingatiwa ipasavyo.

Haiwezekani RC au DC au Waziri yeye ndiye awe mtoa amri tu ya fukuza huyu, simamisha kazi huyu au hamisha huyu na peleka kule. Itakuwa ni chaos

Aidha serikali nayo itende na itekeleze majukumu yake na isiwe ni chanzo cha watumishi hawa kuonekana hawafanyi kazi zao ipasavyo wakati haijawajengea mazingira bora ya kuhudumia watu.

Mfano ipeleke vitendea kazi na pesa ktk hospitali zake kwa wakati ili hawa watumishi wasiwe na visingizio vya kutotenda yawapasayo kutenda.

Mimi niko Shinyanga. Juzi kati mwanangu alikuwa ana kohoa na homa, nikampeleka ktk kituo cha afya cha serikali kilicho jirani nami. Akapimwa na kukutwa anasumbuliwa na minyoo na U.T.I.

Daktari akamwandikia dawa hizi kentrax, erythromicine na panadol. Amini usiamini, nilipata panadol pekee hapo na zingine zote nilikwenda kununua ktk maduka ya madawa mitaani licha ya kuwa natumia NHIF card na kila mwezi nakatwa ktk mshahara wangu takribani Tshs 60,000/= kuchangia bima ya afya!

Sasa ktk mazingira haya, who is to blame? Serikali au wauguzi naadaktari?

Haiwezekani focus iwe ktk hospitali za Muhimbili tu na kuzisahau zahanati na vituo vya afya vijijini ambako huko pia ndiko kuliko matatizo makubwa!!
 
Wakati kila jambo linapofanywa siasa na kutafuta sifa Taaluma huonekana si kitu Tubadilike Hawa wanasiasa hawataumia kama sie tunaehemka mitaani mazingira ya watumishi ni duni sana hospital dawa Hamna mgonjwa kafa unafukuza daktari badala ya kuleta dawa siasa hizi
 
kitu kimoja serikali ya majipu ilichokosea na inachokosea,ukiacha naufanyaji kazi wao kwa mihemko, vigeregere na vifijo serikali hii haikutaka kujua yanayo wakabiri watumishi wa umma ikiwemo madaktari,narudia kabla ya kufukuzana na kuwajibishana kulitakiwa kuwepo na utengamano kati ya serikali na watumishi ambao ndio walipa kodi halali wa serikali.
Dactari anachelewa ulisha wahi kuuliza kwanini anachelewa,dactari anaomba rushwa,jiulize kwanini anaomba rushwa!!
watumishi wa serikali hasa madakitari na waalim walisha ilili mara kadhaa serikali kusikiliza stakihiki zao,ikiwemo kuthaminihuduma wanayotoa lakini badala ya serikali kutumia meza ya mazungumzo,kutumia demokrasia imekuwa katili kwa watendaji hawa muhimu,yote yanayo tokea ni sababu ya mfumo mbovu na ubabe usio na tija wa serikali ya chama cha mapinduzi,nao wananchi tulivyo wajinga badala ya kuinyooshea serikali kushindwa kufanya kazi yake tuna walaumu watendaji mahala ambapo hata wafanyenini hawawezi kutoa huduma stahiki..

leo mama Tibaijuka anadaiw milioni miatano(500) na TRA na kagoma kulipa hakuna wakumshika,hebujiulize milioni miatano ingetosha kujenga labor ward ngapi na kununulia vifaa tiba kiasi gani?mnao walaumu watumishi wa afya ni nyie ambao hamjawahi ku experience maisha yao ya kazi wala hamjawahi kupata huduma katika hospitali hizi za umma,kwa asilimia sabini matokeo mabovu ya huduma katika hizi ofisi za umma chanzo ni serikali
 
Back
Top Bottom