Madaktari: Hakuna anayerudi kazini kesho!

Madaktari: Hakuna anayerudi kazini kesho!

Serikali ya awamu ya nne inaongoza kuwa na watendaji viongozi magarasa,Pinda is a clown.
 
hata wewe?
Ulifikili yupo kwenye burn tu?
Sikutegemea jitu linalojiita toto la mkulima kutoa vitisho badala ya kutoa suruhisho watanzania wasiendelee kufa, kweli magamba wamechoka kichwani nadhani wamelogwa.
 
madaktari wasipoeenda kazini kesho, watakuwa wamejifukuzisha kazini halafu serikali itachukua madaktari kutoka jeshini,na maeneo mengine yenye ziada ya madaktari
 
Wawe na msimamo wao uleule wasijekuleta ulegelege kama ule wawalimu wakajakuishia kuganga njaa kama wagangavyo walimu sasa
 
Hao atakaoleta kutoka Cuba watakuja kutibu au kuuza cigar?
Au watakuja kutibu bure??
 
Ulifikili yupo kwenye burn tu?
Sikutegemea jitu linalojiita toto la mkulima kutoa vitisho badala ya kutoa suruhisho watanzania wasiendelee kufa, kweli magamba wamechoka kichwani nadhani wamelogwa.

upupu wako tu huu,hujamsikiliza pinda na kama umemsikiliza basi hujamwelewa,nenda you tube au soma magazeti ya kesho,sio tz daima lakini.
 
Inaeleweka wanaoumia zaidi ni watanzania wa kawaida ambao hawana uwezo wa kutafuta tiba sehemu nyingine; labda lingekuwa ni jambo la busara na ubinadamu kwa madaktari kuwatibu wagonjwa ambao wanahitaji matibabu ya dharura ili kuokoa maisha ya watanzania ambao wamejikuta wapo njia panda; na hili ni fundisho kwa watanzania wenzangu, haya yasingetokea kama tungetumia kura zetu vizuri, tumenunuliwa kwa pilau na fulana kuwaweka viongozi wabinafsi na wasiojali maisha ya watu wengine; wao wakiumwa hata na jino wanakwenda India. Ni vyema tutumie kura zetu vizuri tunahitaji viongozi wenye kujali maisha ya watanzania, haningii akilini kuona Taifa linakabailiwa na mgomo wa madaktari sekta nyeti na muhimu kwa maisha yetu ya kila siku mh. Raisi kasafiri nje ya nchi kuhudhuria forum, makamu wa Raisi yupo ziarani Tanga, hii inaonyesha hakuna wanachojali wamelikimbia tatizo na kumwachia mh. Pinda; watanzania hii ni dharura yetu viongozi hatuna.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
mmmmh! jambo la ajabu.
rais ndo huyo, kiranja mkuu nae ndo huyo.
safari tunayo ndefu hadi 2015.
 
shikirieni hapo hapo wala msiyumbe! Pinda siku zote anatafuta kuhurumiwa tu badala ajibu hoja anajidai innocent face kumbe wale wale tu! Mkirudi kazini ntajua makanjanja na nyie
 
hosipitali yangu ni muhimbili na mimi mwenyewe,lakini pia hata mimi nimepoteza ndugu wawili, juzi na jana.Ni lazima tujifunze kuheshimu taaluma na kuwapa sitahiki zao,kamwe sitabadili kauli yangu,wanahitaji kuthaminiwa na kusikilizwa kwa upendo nimewashuhudia wakifanya kazi kwa shida sana.

Mji Mkongwe, naomba ukajifunze maisha na mazingira magumu waliomo please,naomba tuungane nao japo wapate nusu ya kile wanachokiomba.
siyo kwamba Viongozi hawaelewi,bali Viongozi tulionao leo hawajui thamani ya watu wanaowaongoza.

Ndiyo maana wanaweza kupeana maagizo rahisi sana,na kwa wepesi sana.

nimesikitishwa na kauli ya waziri eti alikuwa na safari ya kwenda Arusha!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

NINI MAANA YAKE HAKUONA UMUHIMU WA MADAKTARI BALI ALIONA UMUHIMU WA MFU ALIYEMALIZA KAZI YAKE,NINI ALIPATA KULE MSIBANI?
LEO ANALALAMIKA NINI?

NDUGU ZANGU LET US BE SERIOUS.
sasa hata hiyo nusu watapata wapi wakati hawakwenda kwenye majadiliano?
 
Pinda kasahau kuna Private hospitals kibaooooooo na doctors wanapata job quickly, Pinda go & kaa naooo, ubabe kwa Drs ni vigumu kipata muafaka, i am out...
 
WAO WANATIBIWA NJE...halafu sasa hivi wanasema wanajitahidi!!! yani hawa jamaa wao wanajiona wako peponi na ni haki yao kula hii nchi kama watakavyo..Madaktari nawambia kazeni mkwiji Serikali hii chovuhaitapa Madaktari wa kujaza nafasi zenu ila mkisalitiana mjue mmekwisha!!!

Hapo mlipofikia ni point of No Return..so keep on Moving...
 
cjui ha2elew au yy PM ndo hajielewa!kesho ma-dr wacpoenda kazn hv ni nan kajifukuzisha kaz! PM au ma-dr!?
 
madaktari wasipoeenda kazini kesho, watakuwa wamejifukuzisha kazini halafu serikali itachukua madaktari kutoka jeshini,na maeneo mengine yenye ziada ya madaktari

Hao madaktari wengine ni waajiriwa na walikuwa wanahudumia na kutumikia waajiri wao, wakienda kwenye hospitali za serikali si huko walikotoka kutakuwa na ukosefu wa madaktari? Sioni Kama hii strategy itasolve tatizo, ni Public image strategy of solving problems, tatizo sasa litakuwa kwenye hospital za jeshi.
 
siatwalaumu maDr hata kama ni mtu wangu wa karibu yuko hatarini kufa kwa kukosa huduma. Serikali ndiyo yakulaumiwa. Lazima madactari wapate haki zao. Hii ni lazima. Kakuna kurudi kazini mpaka serikali iwajibike. Hakuan kurudi kazini hata kama mtafukuzwa kazi! Komaeni, wafundisheni waalimu na wafanyakazi wengine, kama vile mapolisi kwamba wanaweza kupata haki zao lkn wasitregemee kwamba watapata haki bila kufanya maamuzi magumu na yenye uthubutu.

Mungu yu pampoja nanyi siku zote!
 
Aaaaa we mtoto wanani tena!
Mnafki weee huna lolote, mnanyanyasa
watoto wa nani?
 
Huu ndio wakati muafaka wa kuonesha msimamo na ushupavu wenu madaktari. Kisheria, Pinda hana uwezo wa kukufukuzeni kazi kwa staili hiyo. Wala msihofu, wananchi tunafuata, na tunachohitaji ni kufikia hapo SYRIA ilipo.

Wapumbavu hawa wanafikiri wananchi hatujawachoka. Nadhani ule muda wa machafuko umefika. Wananchi tunaanza maandamano soon, just cling to your decision doctors.

Viva la medici.
:A S 465:
 
Back
Top Bottom