Madaktari: Hakuna anayerudi kazini kesho!

Madaktari: Hakuna anayerudi kazini kesho!

Wakowapi wananchi na vyama vya kiraia na wanaharakati hii ndio sensitive issue ya kukaa barabarani sasa sijui mnasubili nini Jumanee na sisi jamani tukae barabarani kuanzia ubungo mpaka jangwani wakuu.
 
Madaktari na serikali wote ni vimeo. I hate them.

Nimeonja chungu ya jeuri yao unafikiri Mkuchika, Pinda, Kikwete n.k wanatibiwa humu nchini. Wanaoumia ni tabaka la chini kabisa ambalo pengine hakuna hata wa kuwasemea humu zaidi yangu mimi na wewe ambaye umeipenda comment hii.

Wengi tunaoingia JF tunao uwezo wa kwenda HINDU MANDAL, AGHAKAN, REGENCY n.k Lakini hao ambao wataumia kwa migomo ya madaktari hata uhakika wa milo miwili kwa siku hawana.

Hivi unafikiri kama kuna mtu ndugu yake atakufa; kwa hiyo migomo atawachukuliaje hao madaktari?
 
hilo tamko la pinda limezungumzia vifaa vya hospitali vitapatikana vipi?
 
mkuu kwani barua aliyopewa hakuiona au kiburi kama blandina
Lakini mwajiri wao ni serikali wanatakiwa kusikiliza Pinda atakutana nao lini na sio wao wanataka kukutana naye lini. Hao sasa hivi hawana kazi hawana majukumu ya kiserikali wakati Pinda anaendelea na kazi zake hivyo wakati alokuwa nao ni Jumapili na kawaomba wakutane leo. Wao wanachopinga kukutana leo ni nini haswa. kusubiri wengine wanaotoka bara?.. halafu wakifika ndio agenda zitabadilika au?.. Aaaah mimi naona mizinguo mitupu sii hawa madaktari wala serikali maana wanachokiomba hakiwezi patikana leo wala kesho pengine posho peke yake ndio inaweza kukubaliwa mara moja..

Dai mshahara mzuri nitakubaliana na wewe lakini posho? ambayo mimi sikubaliani na hata ya Wabunge halafu nikae hapa na kuwapa suipport wakati napinga posho za wabunge. Huu utakuwa unafiki wa nafsi yangu kubadilika kwa sababu ati wabunge wamepewa. Sikubaliani na posho ya vikao iwe kwa wabunge, watumishi wa serikali au madaktari. Na nitaendelea kupinga hadi siku haki yangu itakaposikilizwa na pande zote na kuwa sheria.
 
Lakini jamani mashindano ya nini?. Pinda kenda kuwaona leo madaktari wameingia kizani wao wanataka wakutane kesho... Hivi kuna tofauti gani kati ya kukutana leo na kesho ikiwa agenda zipo tayari?

tofauti ipo tena kubwa sana....l

JUMAPILI

1..siku ya mapumziko

2..wenye iman zao wanakwenda kanisana

3..siku ya kutulia na kupanga mipango na kuwatembelea ndugu na jamaa


jumatatu

ni siku ya kazi na kwesho huyo pinda angeweza kuwaona...........pinda amekurupuka...ametumia hasira kisa kaenda akawakuta hawajafika..ni mmoja wa mawaziri wakuu wapuuzi kabisa nchii hii imewahi kuwa nao........
 
When the cock stands on the big rock and begins to cock then the darkness disseapears and the sun rises its tantacles to welcome the better hopes,hopes for everyone...madocs naona mko kwenye ncha ya ushindi na umoja wenu ndo ushindi wenu na jukumu lenu kwa sasa ni kupingana na aina yoyote ya lobbying till the sun brings hopes for you

This is your time,do it now!
 
Sasa madaktari wadhihirisha immaturity tena. Wao wamesema hawawezi kukutana na waziri mkuu siku ya jumapili, lakini wameweza kukutana na waandishi wa habari!
Nadhani kuna madaktari wanapenda mgomo uendelee kwa sababu after all mshahara wao wanaendelea kupata na muda huu wa mgomo wanaendelea kufanya shughuli zao nyingine ikiwemo kwenda kutibia hospitali private...
hivi waandishi ndio wanaosikiliza madai ya madaktari??

kweli kabisa tuna safari.... Meeting with pinda is not a debriefing affair, it is a working session and needs high level of negotiation, patience and otehr readiness... kuongea na waandishi wa habari, tena wa tanzania huhitaji chochote, hasa wakiwa type ya makwaiya wa kuhenga!! just a brown envelope
 
sasa mimi dr wa wanyama sijui niwaunge mkono hawa jamaa..........\Orait, kesho siendi kuwatibu wale wadudu wa mzee Macha.
Nagomaaaa.........I am supporting you guys.........100% pamoja.

Yaani mkuu huwa nikisoma post zako nakoma sasa kama ukiacha kwenda kuwatibu wale mbuzi katoliki si watakufa na wengine wameshazoea kufukuzia majini?
 
mkuu waliokutana na press si viongozi.pinda anatakiwa madaktari ambao wengi wao wako safarini kuelekea dar.

kwa uelewa wake, kutoa updates na kufanya majadiliano ni sawa.... na pia anaona wanahabari na waziri mkuu ni sawa,
 
tofauti ipo tena kubwa sana....l

JUMAPILI

1..siku ya mapumziko

2..wenye iman zao wanakwenda kanisana

3..siku ya kutulia na kupanga mipango na kuwatembelea ndugu na jamaa


jumatatu

ni siku ya kazi na kwesho huyo pinda angeweza kuwaona...........pinda amekurupuka...ametumia hasira kisa kaenda akawakuta hawajafika..ni mmoja wa mawaziri wakuu wapuuzi kabisa nchii hii imewahi kuwa nao........
Mkuu hizi sio sababu kabisa mbona wamekutana leo wenyewe na kufikia maamuzi ya kutokutana na Pinda ila wamezungumza na waandishi wa habari. Hivi kweli mnafanya mchezo na maisha ya watu kwa kusema Jumapili ni siku ya kupumzika wakati hizo posho hupokea hata ktk vikao vya Jumapili?.. mbona siku zote wanakwenda kazini hadi Jumapili au unasahau hawa ni madaktari?..aaah sababu nyingine jamani mzijenge baada ya kuwauliza madaktari wenyewe kwa nini hawataki kukutana na Pinda.

Sijaona mwajiriwa akitoa masharti ya kukutana na mwajiri wake, iwe sehemu na saa kama vile Pirates wa Kisomali waloichukua nchi hostage!..Ni Ujinga mtupu miaka yote hawa madaktari hutaka wajkutane na fuilani sio fulani yaani wanaipangia serikali wakutane na nani.. wewe mwajiriwa tu unaweka masharti kwa serikali iliyokusomesha BURE, ukala chakula na kulala bure kwa kodi za wananchi leo unawaadhibu wao! leo wajiona mkuubwa kwa madai ya Posho sijui upuuzi gani..
Wekeni madai ya mshahara kuwa mdogo nitawaunga mkono lakini posho?... nooo way!
 
hivi jamani wekeni mweye official statent ya mgomo wa madatari watuwekee hapa tuone. Mmana tukisoma kwenye magaezeti naona sielewei elewi. mara wanafuzi , mara mazingiraya kazi .

Dr kingwala si member hapa Akisoma hapa tunaomba atuwekee offficial statemnte ya sababu za mgomo
 
Nilitegemea PM hatua yake ya kwanza ingekuwa kututangazia sisi waathirika kuwa Waziri, Naibu wake na Katibu wa wizara ya afya kuwa wamefukuzwa kazi au wajiuzulu kwa kushindwa kuchukua hatua ya kujadiliana na wawakilishi wa Madaktari mapema zaidi pale harufu ya mgomo ilipoanza kufukuta.

Pili nilitarajia Pm kutangaza kuwa yuko tayari kukutana na wawaklishi wa Madaktari kesho mapema huku akiwaomba wengine kuendela kutoa huduma na baada ya kikao chake na wawakilishi watapewa taarifa ya majadiliano na kama hawaridhiki majadiliano ya endelee ilikufikia muafaka.

Lakini hili la kuamuru kwamba kesho wote lazima warudi kazini kwa lazima na atakayeshindwa kazi basi kwa hakika wanasiasa sasa wamelewa madaraka naa nimuda muafaka kwa wananchi kuchukua hatua.

Wito wangu kwa madaktari waendelee na mgomo huku wakizingatia taratibu za mgomo ilikuepuka kupoteza haki za msingi, pale Serikali iliyolewa madaraka itakapo amua kiuwendawazimu kuwafukuza/kuwagawa.La muhimu kwa sasa ni kuwa inafaa manesi kuwa unga mkono kwenye madai yenu hatua hii ngumu na kuweza kuondoa jeuri hii ya Wanasiasa huko mbeleni.

Mungu awaongoze katika kudai haki kwa Busara
 
naunga mkono mgomo wenu..chonde chonde msiache kuwapa huduma mama wajawazito,watoto na wagonjwa walio ktk critical condition

all the best
 
Lakini mwajiri wao ni serikali wanatakiwa kusikiliza Pinda atakutana nao lini na sio wao wanataka kukutana naye lini. Hao sasa hivi hawana kazi hawana majukumu ya kiserikali wakati Pinda anaendelea na kazi zake hivyo wakati alokuwa nao ni Jumapili na kawaomba wakutane leo. Wao wanachopinga kukutana leo ni nini haswa. kusubiri wengine wanaotoka bara?.. halafu wakifika ndio agenda zitabadilika au?.. Aaaah mimi naona mizinguo mitupu sii hawa madaktari wala serikali maana wanachokiomba hakiwezi patikana leo wala kesho pengine posho peke yake ndio inaweza kukubaliwa mara moja..

Mkuu kama nimewaelewa vizuri hawa madaktari ni kwamba tatizo ni mtindo/efficiency ya mawasilano toka serikalini. Taarifa toka kwa Waziri mkuu zikiwataka madaktari wakutane naye (PM) Jumapili (leo) ziliwafikia jana Jumamasi saa 10 jioni! Na waliochosema viongozi ni kwamba kwa muda huo ingekuwa vigumu kuwapata madaktari hao. Pia wakasema wakati huo hata hata mkutano wa viongozi wa madaktari ulikuwa umeshaisha na watu wameshaingia uraini.

Nadhani Wizara ya Afya ndio yenye tatizo hapa. Kwanza kwa kuvurunda na kutoa kauli za kejeli, kauli ambazo ndizo ziliwapandisha maruhani hawa madaktari, na pili kutomshauri vizuri Waziri mkuu namna ya kutatua huu mtafaruku. Kama wangetumia busara kwa kuunda timu ndogo ili kuratibu mawasiliano kati ya serikali na madaktari na hakika barua ya mualiko wa kukutana na waziri mkuu ingefika kwa wakati. Hawajafanya hivyo na sasa mambo yanazidi kuharibika. Kumbuka hii sumu iko karibu nchi nzima kwa sasa. Hospitali nyingene hawasemi lakini huduma zimezorota kabisa. Nadhani wanaita mgomo baridi.
 
Hii ndiyo mnayo iita serikali sikivu ati.

Hivi angewasiliana na kiongozi wao kabla hajapanga muda wa kukutana nao nini kingeharibibika? Hata kukutana nao kesho kuna tatizo lipi gumu kihivyo?

Ninachojua haya madai ni serikali hii hii iliyoyapitisha sasa tatizo liko wapi, kwa nini wasikubali kukaa meza moja na kuyamaliza?
 
Wasiporipoti kazini kesho, Hapo ndipo itakapojulikana umuhimu wao. Kama Pinda ni mtoto wa Mkulima basi ajue sisi ni vibarua wa hao wakulima. Ashindwe kabisa nani arudi kwa vitisho?

Bravo doctors.
 
kama mdai haki zenu za msingi basi hata mimi nawaunga mkono. Msikubali vitisho vya serikali. Serikali inatakiwa kufanya mazungumzo na sio kutoa vitisho.
 
Huyo dada kwenye picha anatoa taswira ya kesho.
Hana matumaini tena,...
Hana kazi zaidi ya hiyo....

Akifukuzwa atakula wapi....
Akienda hela haitoshi,...

Bora warudi tu wakaue watu zaidi,...
Au kama ni huduma watoe kwa rushwa,...

Point ni kwamba,hakuna mgomo hapo labda hii sio tanzania.
Nime shiriki migomo kibao,...
Ila inapo fikia hatua hii ya kupuuzwa mgomo hua hauendelei,..this is no different.
 
sijuimheshimiwa pinda ana "plan b" iwapo agizo lake halitaheshimiwa?
naamini kabisa agizo hili limelenga kuvunja nguvu za wagomaji kwa kuweka nyufa
kwenye umoja wa wagomaji.

swali ni je iwapo mgomo utaendelea serikali itakuwa imetatua tatizo kwakuwafukuza
madaktari?

 
Back
Top Bottom