Madaktari: Hakuna anayerudi kazini kesho!

sasa mimi dr wa wanyama sijui niwaunge mkono hawa jamaa..........\Orait, kesho siendi kuwatibu wale wadudu wa mzee Macha.
Nagomaaaa.........I am supporting you guys.........100% pamoja.


Duuuh, Birigita umenivunja mbavu. Nyie mkigoma hakuna atakayewasikiliza. Kama ni mifugo ya kitoweo, wote tunakula mchicha tu!
 
Wataalamu wa mambo wanasema wakati wa hali tete ndo unaweza kugundua diagnositic skills za watawala. Upi ni mgomo bora kati ya active na passive? Namusihi Pm, Pinda kama ushauri wa bure kuwa meza ya mazungumuzo ni bora kuliko vitisho. Watanzania wenzangu tutarajie kudungwa sindano mafuta ya taa badala quinine, hii kada ni hatari sana. Viongozi wetu wanatibiwa nje ya nchi.
 
Pinda ni beneficiary wa posho... unajua anakunja shilingi ngapi kwa kikao?? hata cha leo alichoitisha yeye?
Cousin unajua serikali at times inapenda sana kudharau carrier za wengine wanaona kuwa kufukuza ndio suluhisho, sielewi wanaposema kuwa hawana hela miaka karibia mitano mfululizo Kikwete ametumia mamia ya hela za walipa kodi kwenda WEF (World Economic Forum) na hatujaona faida yoyote zaidi ya kufuja hela na misafara ambayo hizo hela zingefanyia mambo mengine
 
kweli wasaadizi wa raisi hawa msaidi, ndio maana Nyerere aliwaandikia kitabu watu fulani kwani wao badala ya kumshauri Raisi wana mpotosha, na vivyo hivyo kwa Pinda sasa hivi ajidhihirisha beyond resonable doubt kwamba hafai. naoni wakati muuafa wa kubadilisha waziri mkuu waacha tupate hiyo hasara ya kumlipa mafao lakini si ku na kiongozi asiye elewa utawala wa sheria wakati yeye mwenyewe kasomea sheria
 
Huyu PM angekuwa na busara angekubali ombi la madaktari kukutana nao kesho, uwaziri mkuu wake usingepungua na labda angejijengea heshima kwenye jamii. Kesho aibu itamshika pale madaktari watakapoendelea na mikutano yao.
labda kapewa order na bosi
 
Mh Pinda huwa ananifurahisha sana

PINDA.2.jpg


12_10_6scme1.jpg


Huyu Mkuu waziri anapenda sana maigizo

IMG_9046.jpg
 
Hapa ndiyo penyewe sasa. Mbona wabunge walipodai ongezeko la posho ya kukaa hapakutolewa amri? Zaidi tulipewa habari za kukubaliwa madai yao kwa kile kilicho elezwa gharama za maisha zimepanda mjini Dodoma.

MaDr. komaeni na msilegeze kamba. Haki haipigiwi magoti.

BRAVO kwa msimamo.

Nawasilisha.

Naungana na wewe mkuu.
 
Lakini jamani mashindano ya nini?. Pinda kenda kuwaona leo madaktari wameingia kizani wao wanataka wakutane kesho... Hivi kuna tofauti gani kati ya kukutana leo na kesho ikiwa agenda zipo tayari?
 
Kama ningekuwa Pinda ningejishusha hadi kesho kwenda pale wanapotaka niwasikilize hoja zao,kwa sababu madaktari walikua wanamtaka waziri mkuu.Ningeenda kesho nikawasikiliza kwa hali ya utulivu.Katika baadhi ya mambo ni ka side nao ili kuwa na empathy.Mengine magumu ningewaeleza ukweli na ugumu huo uko wapi,kuna mambo ya kisera ambayo huwezi kuyabadilisha overnight.

Kwa maamuzi ya Waziri mkuu ya leo kwa vyovyote vile sio suluhisho la matatizo kwa trade union yenye watu wachache kama ya madaktari ambao ni rahisi kuji organize sio kama walimu.Hata kama madaktari watarudi kazini hawatafanya kazi.Kujishusha huwa kunasaidia sana kwenye critical situations kama hizi.
 
Sasa madaktari wadhihirisha immaturity tena. Wao wamesema hawawezi kukutana na waziri mkuu siku ya jumapili, lakini wameweza kukutana na waandishi wa habari!
Nadhani kuna madaktari wanapenda mgomo uendelee kwa sababu after all mshahara wao wanaendelea kupata na muda huu wa mgomo wanaendelea kufanya shughuli zao nyingine ikiwemo kwenda kutibia hospitali private...
mkuu waliokutana na press si viongozi.pinda anatakiwa madaktari ambao wengi wao wako safarini kuelekea dar.
 
Lakini jamani mashindano ya nini?. Pinda kenda kuwaona leo madaktari wameingia kizani wao wanataka wakutane kesho... Hivi kuna tofauti gani kati ya kukutana leo na kesho ikiwa agenda zipo tayari?

mkuu kwani barua aliyopewa hakuiona au kiburi kama blandina
 
Wako wapi wananchi wenye hasira? wananchi mnachekelea tu mjue ninyi ndo mnatolewa kafala, pinda atatibiwa nje, madokta wataenda botswan, rwanda Zambia etc. Unganeni na madokta wanatetea haki yenu ya tiba, shauri yenu!!!!
 
Lakini jamani mashindano ya nini?. Pinda kenda kuwaona leo madaktari wameingia kizani wao wanataka wakutane kesho... Hivi kuna tofauti gani kati ya kukutana leo na kesho ikiwa agenda zipo tayari?

Mkuu Mkandara;

Tunaweza kuona kama hakuna tofauti hasa kama ni watazamaji wa hii ishu nzima.Madaktari hapo walipo wana hasira na wana tension.Kwangu mimi naona ingekuwa bora waziri mkuu kujishusha na kwenda kuwasikiliza kesho.Hiyo ingesaidia at least wao kujiona wanasikilizwa,na kesho angeweza kuwashawishi wakarudi kazini.Kwa maamuzi yake ya leo ambayo ni mwendelezo wa kuboronga kutokana na maamuzi yaliyopita utaendelea ku-prolong mgogoro huu.
 
Hapa ndiyo penyewe sasa. Mbona wabunge walipodai ongezeko la posho ya kukaa hapakutolewa amri? Zaidi tulipewa habari za kukubaliwa madai yao kwa kile kilicho elezwa gharama za maisha zimepanda mjini Dodoma.

MaDr. komaeni na msilegeze kamba. Haki haipigiwi magoti.

BRAVO kwa msimamo.

Nawasilisha.
Hapa patamu, ila pangenoga zaid kama na wananchi tungeingia barabarani kushinikiza maDK walipwe ili wakatibu wandungu zetu wenye wamelala mumahospitali bila kupatiwa huduma na madaktari. Yani hii ndo ilikuwa fursa ya kuuondoa huu utawala wa wababaishaji.
 
Madaktari shime wafanyakazi wa umma tupo nyuma yenu,ni bora tuingie kwenye mgomo wafanyakazi wote kama wakileta ujinga wao...shime madaktari tupo pamoja nanyi.
 
Nadhani suluhisho la huu mgomo linapashwa litoke kwa wananchi ambao ndo wenye nchi. Wananchi waamue kama wanawalipa madaktari wanachodai au hawawezi kulipa. Serikali ni wawakilishi tu kwa niaba ya wananchi lakini kwanini wao ndo wanajifanya ndo wenye maamuzi ya mwisho? Wananchi ndo tuamueni bana kama tuna aford hayo malipo kwanini tusiwalipe hawa jamaa wasije kutuOperate kichwa badala ya mguu?
Hela ni kodi zetu serikali inalinga nazo kama zake kwanini lakini?
Dhana hii ya kutufanya sisi wananchi ni wadogo kwa serikali ndiyo inayotufikisha hapa.

Watuulize wananchi kama tunakubali kulipa hizo hela basi mambo yaishe kama hatuwezi basi jamaa wasepe wakatafute ajira sehemu nyingine.

Kama serikali ingekuwa inajua kuwa wananchi ndo wenye maamuzi ya mwisho basi issue hii serkali ingewaomba wabunge ambao ndo wawakilishi wa wa wananchi waidhinishe au wakatae ongezeko hili hata kama ni kwa dharula. Sasa mambo ya serikali kujifanya kuwa wao ndo wakubwa kuliko wananchi ili hali si kweli ni matatizo. Sijui serikali za kiafrika zitawathamini lini wananchi wake ambao ndiyo waajiri wao.
 
Kazi pi mtakuwa mmejifukuzisha wenyewe.... fikirini kwa umakini... wengi wenu ni watoto wa wakulima ambao hata channel za kwenda kufanya kazi nnje ya nchi hamna.... mtaua watoto nandugu zenu jamani.
 
Siasa zitatufikisha mahala pabaya sana, Ifike mahala ambapo siasa haitakiwi kutumika basi na isitumike. Bado naendelea kusisitiza kuiona Taarifa ya Waziri mkuu na jinsi alivyowajibu madaktari.Kwa sababu sidhani kama kauli ya kwamba rudini kazini tutashughulikia matatizo yenu ndio kauli pekee aliyoitoa PM.
 
Back
Top Bottom