winnerian
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 335
- 530
Madai ya muda kwa Tanroads yanayoongeza gharama za mradi, ucheleweshaji– Ripoti ya CAG
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, wakandarasi na washauri walikuwa na madai ya TZS 1.03 trilioni hadi Novemba 2019 kutokana na kuchelewa kulipwa hati za malipo ya muda.
“Ilibainika kuwa madai hayo yalisababishwa na kutotolewa kwa fedha na Wizara ya Fedha na Mipango; ambayo hatimaye ilizuia Tanroads kuwalipa wakandarasi kwa wakati na hivyo kusababisha kuzorota kwa maendeleo ya kazi pamoja na kupanda kwa gharama za mradi kutokana na tozo za riba,” inasomeka sehemu ya ripoti hiyo.
“Aidha, nina wasiwasi kuwa kutolipwa kwa wakati kwa madai ya wakandarasi na washauri kunaweza kuongeza kiasi cha deni kutokana na tozo za riba jambo ambalo linaweza kufanya miradi husika kukwama au kutokamilika hivyo kuwanyima wananchi manufaa yaliyokusudiwa ya miradi hiyo,” alibainisha CAG.
Muunganiko wa kandarasi na zabuni.
Serikali tunaishauri izingatie sana kulipa madeni yenye riba kwani kwa kufanya hivyo itajiondoa kwenye mzigo wa kulipa madeni ambayo haya tija kwenye miradi yake wala wananchi wake
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, wakandarasi na washauri walikuwa na madai ya TZS 1.03 trilioni hadi Novemba 2019 kutokana na kuchelewa kulipwa hati za malipo ya muda.
“Ilibainika kuwa madai hayo yalisababishwa na kutotolewa kwa fedha na Wizara ya Fedha na Mipango; ambayo hatimaye ilizuia Tanroads kuwalipa wakandarasi kwa wakati na hivyo kusababisha kuzorota kwa maendeleo ya kazi pamoja na kupanda kwa gharama za mradi kutokana na tozo za riba,” inasomeka sehemu ya ripoti hiyo.
“Aidha, nina wasiwasi kuwa kutolipwa kwa wakati kwa madai ya wakandarasi na washauri kunaweza kuongeza kiasi cha deni kutokana na tozo za riba jambo ambalo linaweza kufanya miradi husika kukwama au kutokamilika hivyo kuwanyima wananchi manufaa yaliyokusudiwa ya miradi hiyo,” alibainisha CAG.
Muunganiko wa kandarasi na zabuni.
Serikali tunaishauri izingatie sana kulipa madeni yenye riba kwani kwa kufanya hivyo itajiondoa kwenye mzigo wa kulipa madeni ambayo haya tija kwenye miradi yake wala wananchi wake