Mada Moto Channel Ten: Julius Mtatiro vs Humphrey Polepole

Mada Moto Channel Ten: Julius Mtatiro vs Humphrey Polepole

Umesema kweli. Polepole alinishangaza aliposema makosa ya Magufuli anayetakiwa kuwajibika ni waziri mkuu kwa sababu Magufuli anatumwa tu. Lakini hakusema kwa Lowassa nani alipaswa kuwajibika, hilo alikaa kimya! The guy was biased!

Lowassa ndio alikua waziri mkuu sasa Nani angewajibika kama sio yeye alieshindwa kujitetea akakimbilia kuachia ngazi,mnafikiri tumesahau kilichotokea,video zipo u tube.Muulizeni lowassa kwanini hakuitumia nafasi waliyompa kina mwakyembe kujitetea?muulizeni hilo
 
Nilimkubali sana Julius Mtatiro, jamaa alimzidi sana Polepole kwa hoja
 
yaani wewe ujielewi kabisa, kabla ya lowassa kuingia ukawa ulikuwa unamwita lowassa fisadi papa, sasa hivi unamsifia(haujielewi wewe ni bendera fuata upepo), pili ulikuwa unamsifia sana polepole wakati akitetea rasimu ya katiba ya tume(leo hii unamkana japokuwa yeye bado ajabadilisha msimo wake(unafuata upepo unakovuma)

mwache polepole afanye anachofanya kwani kila mtu yuko huru, polepole go ahead usiyumbe na upepo km hwa wanaokulaumu
 
  • Thanks
Reactions: cpt
Wasiomjua huyu HP huwa wanafikiri ni mtu genius saaana na muadilifu saaaana lakini wanaomjua wanasema ana makashfa ya kula pesa na infact ashawahi pata hata grant ya kujiongezea elimu na still aliitafuna na shule hakwenda! Halafu form 6 si alipataga 0 huyu!

Tatizo la jamaa ni opportunist sana otherwise angeweza kuwa mweledi sana kwenye mambo ya social development, social change.Huyu ni watu wa calibre ya akina Nape, Makonda yuko tayari kujitoa ufahamu as long as puesa inaingia kwake!

Na nyie mnaoshinda humu kumsafisha lowassa mnatarajia mini kutoka kwake umesahau kutuambia
 
Kanaudhi kweli jinsi kalivyokomaa usoni,kanajifanya kanajua kuliko watanzania amini katapotea kama akina zito na jeri muro
 
Huyu Dogo sikujua kama anaweza kuwa mnafiki kiasi hicho
huyu dogo si alikua mtu wenu mkimmwagia sifa kemkem. sasa mmekula matapishi yenu amewageuka..hivi kweli nyie ukawa mnataka mabadiliko, mageuzi, au mmenunuliwa?
 
toka kupata uhuru hatujawahi kuongozwa na chama cha siasa bali chama dola ccm nikama maNAZI wa ujerumani au BAATH hizi elimu za kukariri zinafanya tuone hili wengine wana pandishwa vyeo kwa ufisadi au kuminya demokrasia au kuua wapinzani hata maNAZI walifanya hivyo hivyo.
 
Hata mimi namshangaa sana humphrey,nilimuamini sana kumbe hana lolote.Hii njaa itatuua:A S confused:
 
Acheni kumjadili huyo mjinga polepole mnazidi kumpa publicity.Zaidi sana huyo mwizi wa laki sita anatafuta kujipatia walau ukuu wa wilaya iwapo alcohol atashinda urais.Alishakariri kuwa kila anayemtukana Lowassa anapata cheo serikalini na kwenye chama. Mwacheni atapetape akija huku mikoani nitamuuliza laki sita alizoiba alizipeleka wapi.
 
jana ndio nimejua unafiki wa bwana pole pole,

hapo mwanzo wakati akijipambanua mpigania rasimu ya warioba,watu walimwelewa kama mpambanaji wa ukweli, kumbe alikua mnafiki mkubwa!

Jana katika kipindi cha mada moto pale chanel ten ndio nikamgundua huyu bwana ni wakuogopa kama ukoma,

anataka kutuaminisha kwamba kwa sasa chama cha mapinduzi ni kizuri sana tena hakuna mfano wake na magufuli na samia suluhu ni watu wakuchaguliwa?

Maali nilipo mdharau ni pale aliposema mgombea wa ukawa asichaguliwe kwa sababu alikataa katiba ya warioba.

Huku hakisahau magufuli tena alichangia kuisigina rasimu ya warioba?

Mbaya zaidi mgombea mwenza samia suluhu hasani, ndiye alikua makamu mwenyekiti wa bunge la katiba na kwa kiasi kikubwa yeye kwa maelekezo ya chama alitumika kuminya na kuchana chana maoni ya wananchi!

Sasa pole pole anakuja kutuaminisha nini? Ndani yake amekua na chuki ya wazi wazi kwa lowassa!

Nampongeza sana ndugu julius mtatiro uameongea vitu vya msingi sana,

ushauri wangu kwa pole pole, unajidhalilisha sana mgodo wangu wacha kutumika simamia ukweli hakuna msafi ndani ya ccm kama unavyotaka kuwa aminisha watanzania, wewe siyo MUNGU hata ugeuke kumwukumu lowassa, bila ushahidi wowote,

kama unao ushahidi wa tuhuma unazo zisema peleka mahakamani ili mahakama iamue lowassa ni mkosaji hau la. Tusilete vituhuma vya kisiasa kuchafuana kisiasa,

wadau naomba kuwasilisha:

Nilichojifunza toka kwa Polepole:

CCM katika mchakato wake wa kupata wagombea urais imefanikiwa kuwaondoa mafisadi wake wakubwa waliokuwa na matumizi makubwa ya fedha ili kushawishi wajumbe wawapitishe katika uteuzi. CCM wangeshindwa kuliona hilo nchi ingekuwa imeuzwa.

Mfumo ni zaidi ya CCM. Mfumo ni utendaji mzima wa Watumishi wa Umma, Sekta binafsi, Mahakama, vyombo vya ulinzi na usalama na taasisi zake. Kumuondoa Rais au chama peke yake Hakuondoi mfumo.

Watanzania hawahitaji mabadiliko (Change of regime), wanahitaji Mageuzi (Transformation). Mageuzi ndiyo yanayoweza kubadili mfumo na ambao ukibadilishwa hauwezi kurudiwa tena lakini change of regime inaweza kuwa reversed.

Lowassa si mtu binafsi bali ni taasisi yenye wafanya biashara wakubwa ndani yake, isiyoweza kudhibitiwa kwa maamuzi yake. Ila yeye anaweza kuwadhibiti wengine kama inavyotokea sasa katika baadhi ya viongozi wa vyama vya ukawa kudhibitiwa. Taasisi hii ndiyo ikiwa ndani ya CCM ndiyo iliyopambana kuzuia mabadiliko ya Katiba mpya sababu ina athari katika maslahi yao ya kibiashara.

Magufuri katika utumishi wake wote, amehudumu wizara zisizo za muungano ambazo msimamizi wake ni Waziri mkuu. Maana yake majukumu yake ni ya utekelezaji wa maagizo ya Bosi wake, Waziri mkuu. Mfano uuzwaji wa nyumba za serikali.
 
Polepole alisema ccm wakichagua wagombea mafisadi atazunguka tz nzima kuwapinga,namsubiria kuzunguka maana wamewachagua watuhumiwa wa ufisadi.
 
Acheni mihemko, Jana alizidi kujidhihirisha kuwa ana kazi moja tuu aliyotumwa nayo ni kumchafua Lowasa. Mtatiro Jana amesaidia sana kumsababisha Polepole akae uchi na kueleweka has a malengo take ni nini?
Hapo ndio linakuja swali, jee kazi hii ya ghafla ya kupambana na Lowasa mwanzo mwisho anaifanya bure au kwa malipo? Haiwezi kuwa Bure, sasa nani anamlipa? Tuendelee kufuatilia tutamjua tuu.
 
yaani wewe ujielewi kabisa, kabla ya lowassa kuingia ukawa ulikuwa unamwita lowassa fisadi papa, sasa hivi unamsifia(haujielewi wewe ni bendera fuata upepo), pili ulikuwa unamsifia sana polepole wakati akitetea rasimu ya katiba ya tume(leo hii unamkana japokuwa yeye bado ajabadilisha msimo wake(unafuata upepo unakovuma)

mwache polepole afanye anachofanya kwani kila mtu yuko huru, polepole go ahead usiyumbe na upepo km hwa wanaokulaumu

Ni bora tumuingze fisad mmoja ktk taasis ya urais ktkat ya wasafi kuliko kupitsha mafisad milion ktkat ya msafi mmoja ambaye tayar ameshaanza kuwa under someone hata kabla ya kuingia.
Ni zamu ya Fisadi mmoja utak kale malimao
 
Back
Top Bottom