Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 371,076
- 859,173
- Thread starter
- #1,001
๐๐ถ๐ด๐ผ๐บ๐ฎ, ๐ง๐ฎ๐ป๐๐ฎ๐ป๐ถ๐ฎ - Ukarabati na maboresho ya uwanja wa Ndege wa Kigoma umefikia asilimia 60 ya utekelezaji hadi kufikia Juni 2026.
Mradi unaotekelezwa na kampuni ya China Railway Construction Engineering Group kwa gharama ya shilingi bilioni 51.4 unajumuisha ujenzi wa jengo jipya la abiria lenye uwezo wa kuhudumia watu 500 kwa wakati mmoja.
Njia ya kurukia ndege yenye urefu wa kilomita 1.8 tayari imekamilika, huku ujenzi wa mnara wa kuongozea ndege, ofisi za Mamlaka ya Hali ya Hewa TMA, na jengo la mitambo ya umeme kwa ajili ya Taa za uwanjani ukiendelea.
Pia kumefanyika upanuzi wa eneo la maegesho ya magari pamoja na ujenzi wa uzio kuzunguka uwanja mzima.
Mradi unatarajiwa kukamilika rasmi Julai 2026 na huduma zianze kutolewa kikamilifu kuanzia Novemba mwaka huu.
Maboresho haya yanalenga kuufanya uwanja wa Kigoma kuwa kitovu cha usafiri wa anga katika ukanda wa magharibi, kukuza biashara na nchi jirani kama Burundi na DRC, pamoja na kuimarisha sekta ya utalii.
Mradi unaotekelezwa na kampuni ya China Railway Construction Engineering Group kwa gharama ya shilingi bilioni 51.4 unajumuisha ujenzi wa jengo jipya la abiria lenye uwezo wa kuhudumia watu 500 kwa wakati mmoja.
Njia ya kurukia ndege yenye urefu wa kilomita 1.8 tayari imekamilika, huku ujenzi wa mnara wa kuongozea ndege, ofisi za Mamlaka ya Hali ya Hewa TMA, na jengo la mitambo ya umeme kwa ajili ya Taa za uwanjani ukiendelea.
Pia kumefanyika upanuzi wa eneo la maegesho ya magari pamoja na ujenzi wa uzio kuzunguka uwanja mzima.
Mradi unatarajiwa kukamilika rasmi Julai 2026 na huduma zianze kutolewa kikamilifu kuanzia Novemba mwaka huu.
Maboresho haya yanalenga kuufanya uwanja wa Kigoma kuwa kitovu cha usafiri wa anga katika ukanda wa magharibi, kukuza biashara na nchi jirani kama Burundi na DRC, pamoja na kuimarisha sekta ya utalii.