Mada maalum ya ndege toka FB

Mada maalum ya ndege toka FB

Saa 3 asubuhi ya tarehe 14 Agosti 2005, Boeing 737 ya Helios Airways iliondoka Larnaca ikiwa na lengo la kuwasili Prague. Hakuna aliyejua ndani ya dakika chache baadae, ndege ingebadilika kuwa chumba cha ukimya (ghost room).

Kabla ya kupaa, mhandisi mmoja aliwasha mfumo wa shinikizo la kipupwe ndani (Cabin pressurization) kwenye “manual” kwa majaribio lakini alisahau kurudisha kitufe hicho kwenye “auto”.

Rubani na msaidizi wake walipitwa na kosa hilo. Ndege ilipopanda, mgumo wa hewa ulianza kutoka polepole sababu uliachwa kwenye 'manual' upungufu wa Oksijeni ukatokea kwenye ubongo wa abiria, macho yakaanza kuzimika abiria mmoja baada ya mwingine.

Ingawa Kengele ya onyo ililia, lakini walidhani ni onyo la kawaida.
Ndani ya dakika chache, watu 121 walikuwa wamelala usingizi wa milele.
Ndege ikabaki peke yake. Ilipaa kwa mduara kuzunguka anga ya Athens karibu mara sita kama ndege iliyopotea.

Jeshi la Ugiriki lilituma ndege mbili za F-16. Marubani wa kijeshi walipofika karibu, waliona msaidizi wa rubani amelala juu ya usukani kiti cha nahodha kikiwa tupu, na vinyago vya oksijeni vinining’inia bila mtu.

Ndege nzima ilikuwa na mzimu, hakuna aliyekuwa macho, mhudumu mmoja wa kiume alichelewa kusinzia sababu alivaa kinyago cha hewa ya dharura (Portable Oxygen mask) na kujaribu kutambaa kwenda chumba cha marubani, lakini pia nae hakuweza kuokoa jahazi.

Saa tatu baadaye angani mafuta yalikata kwenye ndege hiyo ya Helios 522 na kwenda kuanguka Grammatiko.
Ilikuwa ni ajali mbaya zaidi katika historia ya Ugiriki.

Ajali hii ilifundisha dunia kuwa kosa dogo la binadamu, kama kusahau kubadilisha kitufe kimoja, linaweza kusababisha janga lisilofikirika mfano wa hii ndege ya Helios 522 iliyopata umaarufu kama ndege ya mizimu (Ghost Plane)

Tangu mwaka huo wa 2005, sekta ya anga imeimarisha mapitio ya uendeshaji zaidi (“checklist discipline”).

Sasa mifumo ya shinikizo la kipupwe lazima ithibitishwe mara mbili kabla ya kupaa, na sauti au kengele za onyo zimebuniwa zitofautiane wazi ili rubani asichanganyikiwe.

Kwa sababu kila kengele ina maana yake, na kutoisikiliza kunaweza kuwa gharama ya maisha.
1782031437767.jpg
 
𝗛𝗢𝗨𝗦𝗧𝗢𝗡 - Safari ya ndege ya United Airlines 'Flight 404' iliyokuwa ikitokea Houston jioni ya Jumapili iligeuka kuwa adha ya saa 14 kwa abiria baada ya rubani kulazimika kusitisha safari dakika moja tu kabla ya kuruka kutokana na kufikia kikomo cha muda wa kazi kisheria.

Ndege hiyo ambayo ililazimika kutua kwa dharura katika uwanja wa ndege wa Washington Dulles kutokana na hali mbaya ya hewa, baada ya dhoruba kutulia, wafanyakazi walipata idhini ya kuendelea na safari na walianza kuiongoza ndege kuelekea njia ya kurukia.

Hata hivyo, zikiwa zimesalia sekunde 60 tu kabla ya kupaa, saa ya kisheria ya rubani inayofatiliwa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya Marekani (FAA) iligonga kikomo chake cha juu cha kufanya kazi.

Kutokana na sheria kali za usalama wa anga, rubani hakuwa na chaguo lingine zaidi ya kuigeuza ndege na kurudi langoni majira ya saa tisa usiku.

Hatua hii iliwaacha abiria wakiwa wamegubikwa na uchovu mkubwa, ambapo baadhi yao, wakiwemo watangazaji wa Kombe la Dunia, walilazimika kukodisha gari ili kukamilisha safari yao baada ya kukwama uwanjani hapo hadi asubuhi.

Tukio hili limeibua mijadala mikubwa kuhusu uwajibikaji katika sekta ya anga. Upande mmoja unampongeza rubani kwa kufuata sheria kikamilifu, wakidai kuwa viwango vya muda wa kazi vipo ili kuzuia ajali zinazotokana na uchovu wa marubani na kwamba sheria hizo hazipaswi kulegezwa kwa sababu yoyote ile.

Upande mwingine unaisukumia lawama kampuni ya United Airlines kwa kupanga ratiba inayowasukuma marubani karibu kabisa na ukomo wa muda wao kisheria, huku wakijua fika kuwa changamoto za hali ya hewa na ucheleweshaji wa uwanjani ni mambo yanayoweza kujitokeza wakati wowote.
1782053488485.jpg
 
Kuzama kwenye tenki la mafuta la ndege (Aircraft fuel tank diving au rasmi inajulikana kama Fuel Tank Entry au Confined Space Fuel Tank Inspection) ni utaratibu muhimu sana wa matengenezo ambapo mafundi hulazimika kuingia kimwili ndani ya mabawa au kiwiliwili cha ndege ili kufanya ukaguzi na matengenezo ya ndani.

Kazi hii inafanywa kwa sababu matenki ya mafuta yameundwa ndani ya muundo wenyewe wa ndege na hayawezi kufikiwa au kukaguliwa kwa urahisi kutoka nje.

Mafundi huingia humo ili kuangalia nyufa za muundo, kuzuia kutu, kubadilisha gundi maalum inayozuia mafuta kuvuja, na kurekebisha mifumo ya ndani kama vile pampu na nyaya za umeme.

Kwa sababu mazingira haya yana hatari kubwa ya moto, ukosefu wa hewa safi, na uwepo wa mivuke yenye sumu ya mafuta ya ndege, usalama mkali unapaswa kuzingatiwa kabla na wakati wa kazi.

Ndege lazima imwagwe mafuta yote na kuunganishwa na mfumo wa kuzuia cheche za umeme, huku hewa safi ikipulizwa ndani mfululizo ili kuondoa mivuke hatari.

Kabla ya fundi kuingia, vipimo maalum hufanywa ili kuhakikisha kiwango cha oksijeni kiko salama na hakuna hatari ya mlipuko.

Fundi anayeingia huvaa mavazi maalum ya kujilinda yasiyopitisha kemikali na vifaa vya kupumulia, huku fundi mwingine akibaki nje ya tundu la kuingilia ili kufuatilia usalama wake wakati wote na kuwa tayari kutoa msaada wa dharura ikibidi.
1782296277146.jpg
 
Back
Top Bottom