Mada maalum ya ndege toka FB

Mada maalum ya ndege toka FB

Kampuni ya Airbus Helicopters ilipiga hatua zaidi kwa kufanya mradi wa kubadilisha kabisa taswira ya usafiri wa anga kwa kuunda Helikopta aina ya Airbus RACER.

Huu ni mradi wa kimapinduzi wa Helikopta chotara unaochanganya uwezo wa Helikopta wa kupaa ma kutua wima (rotary wing) na kasi kubwa kama ya ndege za kawaida (Fixed wing)

Mradi huu unafadhiliwa chini ya mpango wa Ulaya wa Clean Sky 2, ukiwa na lengo la kutoa usafiri wa haraka, wenye gharama nafuu na unaolinda mazingira.

Helikopta hii inatofautiana kabisa na helikopta zilizozoeleka kutokana na muundo wake wa kipekee.

Helikopta hiyo inatumia panga ya juu (Rotor) kwa ajili ya kupaa na kutua, lakini ina mabawa maalumu ya pembeni yenye pangaboi zinazofanya kazi ya kama ndege ya kawaida ikiwa angani.

Kasi yake kubwa inatokana na pangaboi mbili zilizowekwa kwenye ncha za mabawa zinazoisukuma helikopta mbele.

Muundo huu unaondoa hitaji la panga la kawaida la mkiani na kuifanya helikopta kuwa na uthabiti mkubwa sana wakati wa kukata kona kali bila kuinama mbele.

Katika majaribio ya hivi karibuni yaliyovutia wengi kwenye maonyesho ya anga ya ILA Berlin Air Show, RACER imethibitisha kuwa chombo cha kipekee kwani ilifikia kasi ya rekodi ya kilomita 444 kwa saa na kuonyesha uwezo mkubwa wa kupaa kwenda juu kwa futi 10,000 ndani ya dakika mbili na sekunde 44 tu.

Zaidi ya hayo, helikopta hii inatumia mfumo wa kisasa wa Eco-Mode unaomruhusu rubani kuzima injini moja ikiwa angani ili kupunguza matumizi ya mafuta na uzalishaji wa kaboni kwa asilimia 20 hadi 25, huku injini hiyo ikiwa na uwezo wa kuwaka tena kwa sekunde chache ikihitajika.

Teknolojia hii ya hali ya juu inatarajiwa kuleta mapinduzi makubwa katika nyanja za usafiri wa dharura.

Kasi na uwezo wake wa kipekee unafanya RACER kuwa chombo bora kwa ajili ya operesheni za uokoaji, huduma za matibabu ya dharura, usimamizi wa majanga, na usafirishaji wa kijeshi ambapo kuwahi mapema ndio nguzo kuu ya kuokoa maisha ya watu.
1781842162140.jpg
 
Serikali ya Kenya imeweka wazi picha za muonekano mpya unaoonyesha mpango kabambe wa kuufanyia maboresho makubwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) ili uwe kitovu cha kisasa cha usafiri wa anga kikanda.

Mradi huo mkubwa wa mabilioni ya shilingi utahusisha ujenzi wa jengo jipya la abiria lenye uwezo wa kuhudumia watu milioni 10 kwa mwaka, huku majengo ya sasa yakifanyiwa ukarabati wa dharura kwa miezi 15 ili kuongeza uwezo wake kutoka abiria milioni 7.5 hadi milioni 12.

Muundo huo mpya unajumuisha pia barabara ya pili ya ndege yenye urefu wa kilomita 4.8, njia za dharura za kutokea ndege, na mifumo ya kisasa ya kuongozea ndege.

Aidha, uwanja huo utaunganishwa moja kwa moja na mifumo ya usafiri wa treni na mabasi ya haraka (BRT) ili kurahisisha usafiri wa abiria wanaoingia na kutoka uwanjani.

Mradi huu unakadiriwa kugharimu takriban shilingi bilioni 154.2 za Kenya na unalenga kukuza uwezo wa jumla wa uwanja huo kufikia kuhudumia abiria milioni 22 kwa mwaka pindi utakapokamilika kikamilifu.
1781873493402.jpg
 
Mwili wa mwanamume aliyesafiri kwa kificho umepatikana siku ya Jumanne, Juni 16, 2026, ndani ya sehemu ya gurudumu la ndege ya Air Arabia Maroc, aina ya Airbus A320.

Tukio hilo limegundulika majira ya saa tano na dakika arobaini na tano asubuhi katika Uwanja wa Ndege wa Gatwick jijini London, muda mfupi baada ya ndege hiyo kuwasili ikitokea mji wa Tangier nchini Morocco.

Wafanyakazi wa uwanja huo walibaini mwili huo wakati wakipakua mizigo, ambapo huduma za dharura na Polisi wa Sussex walifika haraka eneo la tukio kuanzisha uchunguzi.

Mpaka sasa utambulisho wa mtu huyo haujajulikana, huku mamlaka za Uingereza na Morocco zikishirikiana kubaini jinsi mwanamume huyo alivyofanikiwa kupita mifumo ya usalama.

Uzamiaji "stoway" wa namna hii kwenye sehemu za girudumu za ndege unatajwa kuwa hatari sana na mara nyingi husababisha vifo kutokana na baridi kali inayofikia nyuzi joto chini ya hamsini, ukosefu mkubwa wa hewa ya oksijeni, au kupondwa na mitambo ya matairi.
1781928995494.jpg
 
WASHINGTON - Rais Donald Trump amezindua rasmi ndege mpya ya rais itakayotumika kwenye msafara wa Air Force One, katika hafla iliyofanyika kwenye Kambi ya Jeshi la Anga ya Joint Base Andrews huko Maryland.

Ndege hiyo aina ya Boeing 747-8, ambayo ni zawadi ya kifahari kutoka kwa serikali ya Qatar yenye thamani ya takriban dola milioni 400, itatumika kama mbadala wa muda wakati kampuni ya Boeing ikiendelea kukabiliwa na ucheleweshaji wa kutengeneza ndege za kudumu za VC-25B.

Muonekano wa ndege hiyo umebadilishwa kabisa na kuacha rangi za kitamaduni za bluu na nyeupe zilizobuniwa na Jacqueline Kennedy miaka ya 1960, na badala yake sasa ina rangi ya bluu iliyoiva chini, nyeupe juu, na mstari mwekundu, huku mkia wake ukiwa na picha kubwa ya bendera ya Marekani iliyochorwa kwa mtindo wa kupepea.

Ndani ya ndege hiyo kuna samani za kifahari za ngozi ya rangi ya hudhurungi na mbao maalum zilizofanyiwa mapambo na kampuni ya Kifaransa, huku ikiwa na uwezo mkubwa wa kubeba mizigo mizito, kwenda kasi zaidi, na kusafiri umbali mrefu bila kuhitaji kuongeza mafuta njiani.

Hata hivyo, hatua ya kupokea mali hiyo kutoka kwa taifa la kigeni imeleta maswali mengi ya kimaadili na kiusalama kutoka kwa wakosoaji wa vyama vyote, huku serikali ikikabiliwa na gharama ya mamilioni ya dola kuifanyia marekebisho ili kuweka mifumo ya kijeshi ya mawasiliano ya siri na ulinzi.

Kwa mujibu wa sheria za Marekani zinazozuia viongozi kumiliki zawadi kubwa za kigeni, Ikulu imetangaza kuwa ndege hiyo itahamishiwa kwenye taasisi ya maktaba ya rais ya Trump baada ya muhula wake kuisha, huku kwa sasa ikijiandaa kwa safari za majaribio kabla ya kuonekana hadharani kwenye gwaride la maadhimisho ya miaka 250 ya uhuru wa Marekani hapo Julai 4, 2026.
1781963921903.jpg
 
Rais Donald Trump aliamua kubadilisha rangi za ndege ya kubeba Rais ya Marekani (Air Force One) ili kuipa muonekano wa kizalendo zaidi unaotumia rangi nyekundu, nyeupe, na samawati nzito, badala ya muonekano wa kihistoria wa rangi ya samawati hafifu na bluu uliokuwepo tangu enzi za Rais John F. Kennedy.

Trump alieleza kuwa mabadiliko hayo yalilenga kuilinda hadhi ya Marekani kupitia rangi zinazowakilisha bendera ya taifa hilo, akiamini kuwa muonekano mpya una nguvu na unafaa zaidi kwa ndege ya kiongozi wa nchi.

Aidha, muonekano huu mpya unashabihiana kwa karibu sana na muundo wa rangi wa ndege yake binafsi aina ya Boeing 757.

Ingawa uamuzi huo ulikabiliwa na changamoto hapo awali kutokana na ripoti za Jeshi la Anga zilizofanya tathmini kuwa rangi nzito zinaweza kuongeza joto kwenye ndege na kuhitaji mifumo mikubwa zaidi ya upozaji, hata hivyo agizo hilo lilitekelezwa kikamilifu.

Hivi sasa, muonekano huo mpya utatumika rasmi kwenye ndege mpya za kizazi kijacho za Boeing 747-8 (VC-25B) pamoja na ndege nyingine za msafara wa rais na makamu wa rais.
1781965502442.jpg
 
𝗪𝗔𝗦𝗛𝗜𝗡𝗚𝗧𝗢𝗡 - Rais wa Marekani Donald Trump jana ametoa sifa kedekede kwa mfumo wa mtandao wa satelaiti wa Starlink unaomilikiwa na Elon Musk, wakati akionyesha ndege mpya iliyotolewa na Qatar itakayotumiwa kama ndege ya mpito ya Rais ya Air Force One.

Akizungumza katika kituo cha jeshi la anga cha Joint Base Andrews huko Maryland, Trump amesifu maboresho makubwa ya kiteknolojia yaliyowekwa kwenye ndege hiyo, huku akitaja mfumo huo wa mtandao kuwa wa kiwango cha juu sana ambacho hakijawahi kushuhudiwa huko nyuma.

Katika hotuba yake, Trump alizua gumzo mitandaoni baada ya kukosea kwa muda jina la bilionea huyo na kumwita "Leon" kabla ya kujisahihisha haraka na kusema Elon atafurahi sana kusikia sifa hizo.

Ndege hiyo aina ya Boeing 747 iliyokarabatiwa inatumika kama suluhisho la mpito kuchukua nafasi ya ndege za zamani za rais za tangu mwaka 1990, wakati nchi hiyo ikisubiri kukamilika kwa ndege mpya kabisa kutoka kampuni ya Boeing zinazotarajiwa kiwa tayari baada ya miaka miwili.

Uamuzi wa kuweka teknolojia ya Starlink kwenye ndege hiyo ya urais unalenga kuhakikisha mawasiliano ya data ya kasi ya juu na mikutano ya video ya usalama wa hali ya juu inaendelea bila kukatika wakati rais akiwa anasafiri angani.
 

Attachments

  • 1781971300702.jpg
    1781971300702.jpg
    573.4 KB · Views: 4
Back
Top Bottom