Mada maalum ya ndege toka FB

Mada maalum ya ndege toka FB

WASHINGTON — NASA imebadili kidogo mpango wa safari yake ya kurejea Mwezini inayoitwa Artemis III.
Safari hiyo iliyipangwa kuzinduliwa mwaka 2027, lakini sasa Chombo hakitatua moja kwa moja Mwezini kama ilivyopangwa awali.
Badala yake, chombo cha angani cha Orion kitazunguka karibu na Dunia kwanza.

Chombo hicho kitarushwa kutoka Florida kwa kutumia roketi kubwa ya Space Launch System.

Kikiwa angani, Orion kitaungana na vyombo vingine vidogo vya kutua Mwezini ambavyo vinatengenezwa na kampuni za SpaceX na Blue Origin.

Wanaanga watakaa ndani ya vyombo hivyo, kukagua jinsi vinavyofanya kazi, kuangalia hewa na mawasiliano. Safari nzima itachukua kama wiki mbili, halafu chombo kitarudi kutua kwa usalama kwenye Bahari ya Pasifiki.

NASA imesema mabadiliko haya ni kwa ajili ya usalama. Wanaona ni bora kupima kila kitu karibu na Dunia kwanza kabla wanaanga hawajasafiri mbali zaidi.
Hii itawasaidia wahandisi kugundua na kutatua matatizo mapema.

Kwa safari hii NASA imechagua wanaanga wanne akiwemo Kamanda Randy Bresnik kutoka Marekani na Luca Parmitano kutoka Ulaya, pamoja na Frank Rubio na Andre Douglas ambao pia ni wa NASA.

Baada ya majaribio haya kukamilika, safari inayofuata ya Artemis IV ndiyo itajaribu kutua rasmi kwenye ncha ya kusini ya Mwezi.
1781311305753.jpg
 
Ndege ya Delta Air Lines ilichelewa kuondoka Cancun siku ya Alhamisi baada ya kundi kubwa la nyuki kukaa kwenye bawa la ndege yake aina ya Boeing 737. Wafanyakazi na abiria walishangaa kuona nyuki wamekusanyika pale kabla ya safari kuanza.

Kwa bahati nzuri tatizo hilo halikuchukua muda mrefu.

Marubani walipata suluhisho rahisi baada ya kuamua kuondoa ndege yao kwa kasi wakati wa kupaa.

Upepo wa kasi uliwafukuza nyuki wote na ndege ikaweza kuendelea na safari yake kwa usalama.

Video ya tukio hilo ilishirikiwa na @FerikaBoss na kuonyesha nyuki wakiwa wamezunguka bawa la ndege kabla ya kupaa.

 
𝗡𝗔𝗜𝗥𝗢𝗕𝗜, 𝗞𝗲𝗻𝘆𝗮 - Nahodha (Captain) Joseph Martin Ririani, aliyekuwa rubani wa shirika la ndege la Kenya Airways (KQ), ameweka historia nchini kwa kuacha kazi yake na kuanzisha Chuo cha Urubani cha Kenya (Kenya School of Flying) kwa lengo la kutoa mafunzo ya bei nafuu na ya kizalendo.

Hapo awali, gharama kubwa za mafunzo ziliwalazimu Wakenya wengi kwenda kusomea urubani nchini Afrika Kusini. Hatua ya Nahodha Ririani imebadilisha kabisa mwelekeo wa sekta ya anga ukanda huu na mapinduzi ya Mafunzo ya Urubani.

Historia ya chuo hiko kilianza rasmi Juni 1992, Ririani alipoweka misingi ya chuo cha kwanza cha urubani kinachomilikiwa na kuendeshwa na wazawa.

Ili kusimamia maono hayo kikamilifu, alichukua hatua ya kijasiri mwaka 1996 kwa kujiuzulu nafasi yake kama rubani wa ndege kubwa aina ya Airbus A310 ndani ya KQ.

Chuo hicho sasa kina miliki zaidi ya ndege 20 za mafunzo na mtambo wa kisasa wa kuiga urushaji wa ndege (flight simulator).

Katika mapambano ya Usalama wa Anga na mafunzo, Nahodha Ririani amekuwa mstari wa mbele kupigania usalama wa marubani wanaochipukia.

Mnamo 2025, alijifunga minyororo kwenye ndege katika Uwanja wa Ndege wa Wilson ili kutetea uwanja salama wa mafunzo.

Alikemea uvamizi wa ardhi ya uwanja wa ndege na maendeleo ya kyjenga magorofa kando ya eneo la uwanja wa ndege wa Wilson akionya kuwa majengo hayo yanahatarisha maisha ya wanafunzi inapotokea hitilafu za dharura za injini.
1781356563271.jpg
 
Ndege ya usafirishaji ya Jeshi la Anga la India aina ya Antonov An-32 imepata ajali jumamosi ya leo katika eneo la Jorhat, jimbo la Assam, kaskazini mashariki mwa India.

Jeshi la anga pa mchi hiyo limethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

Jumla ya Askari watano (05) wa Jeshi la Anga la India wamepoteza maisha katika ajali hiyo.

Tukio hili ni pigo kwa familia za askari hao na kwa Jeshi la Anga la India zima. Mamlaka zinaendelea kufuatilia sababu kamili ya ajali hiyo.
1781357079643.jpg
 
TOKYO, JAPAN - Shirika la Anga la Japan (JAXA) kwa kushirikiana na vyuo vikuu vikuu nchini humo limefanikiwa kufanya jaribio la kwanza la injini ya ndege inayokwenda kwa kasi ya sauti (hypersonic), hatua inayotajwa kuwa mapinduzi makubwa yatakayobadilisha sekta ya usafiri wa anga duniani kote.

Jaribio hilo la kihistoria lilifanyika katika Kituo cha Anga cha Kakuda mkoani Miyagi, lilihusisha mfano wa ndege hiyo yenye urefu wa mita mbili ikiwa imeunganishwa moja kwa moja na injini maalum inayotumia nishati ya haidrojeni.

Wakati wa jaribio hilo, wataalamu walifanikiwa kuchoma nishati hiyo kwa ufanisi mkubwa katika kasi iliyoiga mwendo wa Mach 5, ambayo ni sawa na kilomita 6,115 kwa saa au mara tano ya kasi ya sauti.

Kasi hii ina maana kwamba safari kati ya miji ya Tokyo na New York ambayo sasa huchukua takriban saa 12 itaweza kukamilika kwa chini ya saa 2 tu.

Changamoto kubwa ya usafiri wa kasi hii ni joto kali linalotokana na msuguano wa hewa, ambalo hufikia hadi nyuzi joto 1,000 na linaweza kuyeyusha vyuma vya kawaida.

Ili kukabiliana na hali hiyo, wanasayansi wa Japan walitengeneza ngao maalum ya kuzuia joto ambayo ilifanya kazi kwa mafanikio makubwa na kulinda mifumo ya ndani ya ndege hiyo kubaki katika kiwango cha joto cha kawaida.

Licha ya mafanikio haya makubwa, teknolojia hii bado ipo katika hatua za awali za utafiti ambapo hatua inayofuata itakuwa ni kurusha injini hiyo angani kwa kutumia roketi ili kuona uwezo wake halisi nje ya maabara.

Wataalamu wanakadiria kuwa itachukua takriban miaka 20 ya maboresho kabla ya ndege za kwanza za abiria kuanza kutumika rasmi, huku wakilenga miaka ya 2040 kuleta mabadiliko haya ya kudumu katika namna binadamu anavyosafiri duniani.
1781460165291.jpg
 
Katika operesheni hiyo ya usiku wa manane wa kuamkia leo anga ya mfereji wa Uingereza ilitawaliwa na helikopta kubwa za kijeshi zikiwemo Chinook, ambayo zilipaa kimya kimya juu ya meli ya mafuta ya kirusi huku marubani wakipambana na upepo mkali wa baharini.

Kutokea angani, makomando wapatao 40 wa Royal Marines walishuka kwa kasi ya ajabu wakitumia kamba maalum hadi kwenye sitaha ya meli hiyo iliyokuwa ikisonga mbele gizani.

Ili kufanikisha uvamizi huo bila kushtukiwa, marubani walilazimika kurusha helikopta hiyo bila kuwasha taa za nje, wakitegemea vifaa vya kisasa vya kuona gizani.

Wakati Chinook ikiwa imetua komando hao, ndege kubwa ya doria ya baharini aina ya RAF P-8 Poseidon ilikuwa ikipaa juu zaidi angani ikitazama eneo zima la operesheni kwa kutumia rada na kamera za joto ili kuhakikisha hakuna tishio lolote linalokaribia.

Wakati huo huo, helikopta za kivita aina ya Merlin na Wildcat zilikuwa zikipiga doria karibu na meli hiyo zikiwa zimejihami kwa silaha nzito ili kutoa ulinzi wa haraka wa anga endapo makomando wangerejeshewa mapigo na mabaharia.

Nguvu hii kubwa ya angani ilitumiwa na Jeshi la Uingereza baada ya kubainika kuwa meli hiyo ya Urusi ilikuwa ikisafirisha mapipa 700,000 ya mafuta ghafi kwenda nchini Misri chini ya bendera ya kughushi ya Cameroon.

Mafanikio ya operesheni hii ya angani yamepongezwa na viongozi wa Uingereza na Ukraine kama pigo kubwa kwa uchumi wa vita wa Urusi, huku Urusi ikilaani uvamizi huo na kuuita wa kijambazi.
1781509467907.jpg
 
Tukio hili linaonyesha helikopta ya kijeshi ya Marekani aina ya Sikorsky CH-53K King Stallion ikibeba ndege ya kivita ya F-35C Lightning II, huku ikiwa inajazwa mafuta angani na ndege ya tanki aina ya KC-130 Hercules.

Mazoezi haya yalifanywa na Kikosi cha Majini cha Marekani (U.S. Marines) kutoka kikosi cha majaribio cha VMX-1.

Helikopta hiyo ilisafirisha kiwiliwili hicho cha F-35C (ambacho hakikuwa na injini wala mifumo ya ndani) kwa kukifunga kwa kamba maalum chini yake kutoka Kituo cha Anga cha Patuxent River huko Maryland kwenda Kituo cha Pamoja cha McGuire-Dix-Lakehurst huko New Jersey kwa ajili ya majaribio ya mifumo ya uokoaji.

Operesheni hii ilionyesha uwezo mkubwa wa helikopta ya CH-53K King Stallion, ambayo ndiyo helikopta yenye nguvu zaidi katika jeshi la Marekani ikiwa na uwezo wa kubeba mizigo ya hadi tani 16.3.

Wakati ikisafirisha mzigo huo mzito, helikopta hiyo ilifanikiwa kujiunga na ndege ya KC-130 ili kujazwa mafuta ikiwa angani, jambo linaloruhusu kusafiri umbali mrefu zaidi bila kulazimika kutua.
1781539490804.jpg
 
Ndege ya shirika la Air Caraïbes, aina ya ATR 72-600, imeonekana ikifanya ujanja wa kipekee wa kurudi nyuma kwa kutumia nguvu zake yenyewe kwenye Uwanja wa Ndege wa Grand Case-Espérance uliopo kisiwani Saint Martin.

Kitendo hiki kinachojulikana kama "powerback" kinawezekana kwa sababu panga za propela zina uwezo wa kubadili mwelekeo wa upepo kwa kuabadili pembe za panga zake ili kwenda kinyume.

Mbinu hii inatumika sana katika uwanja huu kwa sababu barabara yake ya kuruka na kutua ni fupi sana na imezungukwa na maji, hali inayofanya nafasi ya kugeuka kuwa ndogo na kuzuia matumizi ya magari ya kawaida ya kuvuta ndege.

Video;
jet.nerd/instagram

View: https://www.facebook.com/share/v/18kirdLHZo/
 
Ndege ndogo iliyokuwa imebeba wanamichezo wa kuruka na miamvuli imeanguka na kulipuka kwa moto sekunde chache baada ya kupaa katika Uwanja wa Ndege wa Butler Memorial jimboni Missouri, nchini Marekani, na kusababisha vifo vya watu wote 12 waliokuwemo ndani yake, wakiwemo wapiga mbizi 11 na rubani mmoja.

Ajali hiyo ilitokea jana Jumapili asubuhi wakati ndege hiyo aina ya Pacific Aerospace 750XL inayomilikiwa na kampuni ya Skydive Kansas City ambapo ilionekana kishindwa kuongeza kimo, ikakata kona kali upande wa kushoto, na kisha kuanguka takribani mita 200 hadi 300 kutoka kwenye njia ya kurukia mbele ya macho ya baadhi ya ndugu wa wahusika waliokuwa uwanjani hapo.

Mamlaka za anga za FAA na NTSB zimeanza uchunguzi wa kina kubaini chanzo cha ajali hiyo, huku viashiria vya awali kutoka kwa usimamizi wa uwanja huo vikionyesha uwezekano wa injini kupoteza nguvu na kusababisha ndege hiyo kukwama angani kabla ya kuanguka chini kifudifudi.
1781540209209.jpg
 
Back
Top Bottom