Mada maalum ya ndege toka FB

Mada maalum ya ndege toka FB

FARO - Mamlaka za Ureno zimetangaza kukamatwa rasmi kwa ndege aina ya Boeing 727-100 inayomilikiwa na Jean-Pierre Bemba, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Uchukuzi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Kukamatwa huko kunafanyika chini ya operesheni iitwayo "Operation Atlantic Route" inayolenga kukamata mali za viongozi wa zamani wa Kongo zinazoshukiwa kupatikana kwa njia isiyo halali.

Ndege hiyo imekuwa maegesho katika Uwanja wa Ndege wa Faro - Ureno kwa takriban miaka 19 bila matumizi yoyote. Kwa mujibu wa mamlaka za uwanja, Bemba alipewa siku 60 za kuiondoa ndege hiyo na kulipa deni la maegesho linalokadiriwa kufikia karibu euro milioni moja.
Baada ya muda huo kupita bila hatua kuchukuliwa, ndege hiyo ilitangazwa kuwa imekiuka sheria mpya ya Ureno kuhusu ndege zilizotelekezwa katika viwanja vya ndege.

Operesheni ya Atlantic Route inaendeshwa na Sekretarieti ya Usimamizi wa Mali ya Wizara ya Sheria ya Ureno.
Katika hatua ya hivi karibuni ya Februari 2026, operesheni hiyo ilikamata na kuuza kwa mnada nyumba ya kifahari iliyopo Quinta da Marinha, Cascais, inayomilikiwa na Waziri wa zamani wa Kongo Gilbert Ondongo.
Nyumba hiyo yenye vyumba saba, bwawa la kuogelea, ukumbi wa mazoezi na ukumbi wa sinema iliuzwa kwa zaidi ya euro milioni 10.9.

Kukamatwa kwa ndege ya Bemba si tukio la kwanza linalohusisha mali za viongozi wa Kongo nchini Ureno. Hata hivyo, tofauti na nyumba ya Ondongo, ndege ya Bemba haijauzwa bado bali imekamatwa rasmi na mamlaka kutokana na ukiukaji wa kanuni za uendeshaji wa viwanja vya ndege.

Wakati Bemba hajatoa kauli rasmi, watu wa karibu naye wanasema jukumu la gharama hizo linapaswa kubebwa na Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai. Wanadai kuwa mahakama hiyo ndiyo iliyoweka zuio kwenye mali zake wakati alipokuwa anakabiliwa na mashtaka, kabla ya kuachiliwa huru mwaka 2018 baada ya mashtaka hayo kufutwa.

Kando na hilo, Novemba 2025 ndege iliyobeba Waziri wa Madini wa sasa wa DRC, Louis Watum Kabamba, ilipata ajali ya kuteleza nje ya barabara ya kuruka na kuteketea kwa moto ingawa alitoka salama. Tukio hilo halihusiani moja kwa moja na operesheni ya Atlantic Route.
1778065108388.jpg
 
Tanzania - Mei 05, 2026.
Sekta ya anga imepata pigo kubwa kufuatia kifo cha rubani mkongwe Nahodha "Captain" Gaudioz Kusekwa, aliyefariki asubuhi ya Mei 04 akiwa anapata matibabu katika Hospitali ya Bugando.

Nahodha Kusekwa alikuwa rubani mwenye uzoefu mkubwa, akiwahi kuhudumu ATCL kabla ya kujiunga na Precision Air ambapo alishikilia nyadhifa tofauti ikiwemo Mkuu wa Uendeshaji wa Ndege na Mkuu wa Ubora, Usalama na Ulinzi.
Alikuwa anaheshimika kwa weledi wake na mchango wake katika maendeleo ya usafiri wa anga nchini.

Salamu za Rambirambi kwa familia na wadau wote wa sekta ya anga.
1778078638488.jpg
 
Uwanja wa Ndege wa Mtemere ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Nyerere umepokea ndege yake ya kwanza ya watalii Jumanne, 6 Mei 2026 tangu uzinduzi wake 11 Februari 2026.

Ndege ya Cessna 208 ilitua baada ya kukamilika kwa taratibu za usalama za ndani na za kimataifa.

Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Ephraim Mwangomo, alisema kiwanja hicho kinafungua fursa mpya za utalii hasa kuelekea msimu wa shighuli nyingi za Utalii (high season) na kimejengwa kwa tabaka gumu linalowezesha ndege kutua hata kipindi cha mvua.

Kiwanja hicho kina barabara ua kuruka na kutia ndege (runway) yenye urefu wa kilomita 1.8 iliyotengenezwa kwa tabaka la 'polyma' lisilonyonya maji na linalohifadhi mazingira, pamoja na mnara wa kuongozea ndege.
1778156577921.jpg
 
Airbus na shirika la ndege la AirAsia wametangaza kusaini mkataba wa ununuzi wa ndege 150 aina ya Airbis A220-300, ambalo ni agizo kubwa zaidi la ndege hizo lililothibitishwa tangu zianze kutengenezwa.

Kwa mujibu wa makubaliano hayo, agizo hilo linaifanya ndege ya A220 kuvuka idadi ya jumla ya maagizo 1,000 duniani.

AirAsia itakuwa shirika la kwanza kutumia muundo mpya wa ndani (Cabin) wa A220-300 unaoweza kubeba abiria 160.

Muundo huo umewezekana baada ya Airbus kuongeza mlango wa pili wa dharura juu ya mabawa katika kila upande wa ndege, mabadiliko yanayoruhusu kuongeza idadi ya abiria bila kupunguza viwango vya usalama.

Ndege ya A220-300 inajulikana kwa matumizi yake madogo ya mafuta na uwezo wa kuruka umbali mrefu katika njia za masafa ya kati.

Mkataba huu unatarajiwa kuimarisha zaidi nafasi yandege za Airbus A220 katika soko la ndege za kati za kisasa na kuongeza ushindani katika sekta ya usafiri wa anga.
1778263475768.jpg
 
Mtu mmoja aliyekuwa ametembea bila idhini kwenye njia ya kuruka aligongwa na kumezwa na injini ya ndege ya Frontier Airlines usiku wa Ijumaa katika Uwanja wa Ndege wa Denver, na kusababisha ndege hiyo kusitisha kuruka kwa dharura.

Ndege hiyo aina ya Airbus A321 nambari F94345 iliyokuwa ikielekea Los Angeles ilikuwa ikiongeza kasi ya kuruka kwenye Njia namba 17 kushoto (17L) wakati tukio hilo lilitokea, na rubani alisimamisha ndege mara moja baada ya tukio hilo.

Tukio hilo lilisababisha moto kwenye injini na moshi kuingia ndani, jambo lililomfanya Nahodha kuamuru abiria wote 224 na wafanyakazi 07 kuteremshwa kwa kutumia ngazi za dharura.

Huduma za dharura na uokoaji zilifika haraka kuzima moto na kuwapa huduma abiria, huku abiria mmoja akipata jeraha dogo wakati wa kuteremka kwa dharura

Hali na utambulisho wa mtu aliyegongwa bado haijafahamika, na Bodi ya Kitaifa ya Usalama wa Usafiri ya Marekani (NTSB) imeanza uchunguzi wa tukio hilo huku Njia namba 17L ikiendelea kufungwa.

Taarifa zaidi inasema mtu huyo aliruka uzio wa uwanja wa ndege
1778361755574.jpg
 
Kampuni ya Tata Advanced Systems Limited (TASL) kwa ushirikiano na Airbus imezindua rasmi ndege ya kwanza ya kijeshi ya C-295 iliyotengenezwa nchini India kutoka kwenye Kiwanda cha Ukusanyaji wa Mwisho - FAL huko Vadodara, Gujarat, tarehe Mei 11, 2026.

Hii ni hatua kubwa kwa sekta ya ulinzi ya India chini ya mpango wa “Make in India”. Ndege hiyo ni sehemu ya makubaliano ya uzalishaji wa ndege 40 za C-295 nchini India, baada ya India kupokea ndege 16 za kwanza zilizokamilika kutoka Uhispania.

C-295 ni ndege ya kijeshi ya usafirishaji yenye injini mbili, inayoweza kubeba wanajeshi, mizigo, magari na vifaa vya dharura kwa masafa ya kati.

Imeundwa kutua na kupaa hata kwenye viwanja vifupi na vya vumbi na inaweza kufanya kazi mbalimbali kama doria, uokoaji na usafirishaji wa wagonjwa.

Ni ndege imara inayofaa kwa hali ya hewa tofauti na maeneo magumu, hivyo inatumika sana katika shughuli za kijeshi na kibinadamu.
1778592689259.jpg
 
Dar es Salaam – Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kimetangaza uandikishaji wa kundi la tatu la mafunzo ya Leseni ya Urubani wa Kibinafsi (PPL) kozi iliyoidhinishwa na TCAA chini ya namba TCAA/ATO/010.

Waombaji wanatakiwa kuwa na cheti cha kidato cha nne au sawa na hicho wakiwa wamefaulu masomo ya Fizikia, Hisabati, Jiografia na Kiingereza, pia wawe na umri wa angalau miaka 17 na afya njema.

Maombi yaambatanishwe na cheti cha kidato cha nne, picha ya paspoti yenye mandhari ya bluu na cheti cha kuzaliwa.

Kozi itachukua takriban miezi sita (06) kuanza tarehe 13 Julai 2026, huku maombi yakifungwa tarehe 14 Juni 2026 jioni.

Gharama ya mafunzo ya kinadharia ni shilingi milioni 5.5/- na mafunzo ya kuruka shilingi 648,000/- kwa saa moja (kati ya saa 45 zinazohitajika)

Wanafunzi watakaohitimu wataweza kuendelea na kozi ya leaeni ya biashara CPL.

Maombi yanawasilishwa kupitia SIMS | Login.
1778915045261.jpg
 
Kamov Ka-26 ni Helikopta pekee duniani inayoonekana kama imeundwa kwa kutumia vipuri vya trekta na injini ya kifaru.

Helikopta hii ndogo ya Kirusi ilitengenezwa miaka ya 1960 na kampuni ya Kamov, inayojulikana kwa muundo wake wa kipekee wa kuwa na panga mbili zinazozunguka kinyume bila kuwa na panga ya mkia.

Helikopta hii ilitengenezwa kwa ajili ya kufanya kazi nyingi, kwani sehemu yake ya bodi ya chini nyuma inaweza kubadilishwa haraka kulingana na kazi inayohitajika, kama vile kunyunyizia dawa mashambani, kubeba mizigo, kubeba wagonjwa, kuzima moto au kubeba abiria wachache.

Ina injini mbili za pistoni na ina uwezo wa kuruka kwa kasi ya wastani pamoja na kuganda hewani kwa urahisi.

Ka-26 inasifika pia kwa urahisi wa kuitunza, uwezo mzuri wa kuinuka wima na kufanya kazi katika maeneo madogo, na hivyo ilitumiwa sana katika kilimo na huduma za kiraia katika Umoja wa Kisovieti na nchi jirani.


View: https://www.facebook.com/share/v/1CQS3dutQM/
 
Mountain Home, Idaho – Maonyesho ya anga ya Gunfighter Skies Air Show yalikatizwa ghafla siku ya Jumapili 17 Mei 2026 baada ya ndege mbili za jeshi la wanamaji la Marekani aina ya EA-18G Growler kugongana angani na kudondoka karibu na Kituo cha Jeshi la Anga cha Mountain Home.

Tukio hilo lilitokea majira ya alasiri wakati ndege hizo zilipokuwa zikifanya onyesho lao siku ya mwisho.

Video za mashahidi zilionyesha mgongano huo na baadaye parachuti nne zikijitokeza angani, zikithibitisha kuwa marubani wote wanne walifanikiwa kujifyatua nje salama.

Maafisa wamethibitisha kuwa marubani hao wamepatikana wakiwa hai na hakuna raia aliyejeruhiwa ardhini.

Kituo cha jeshi kilifungwa kwa muda huku maonyesho yote yaliyobaki yakifutwa mara moja.
1779078675713.jpg
 
Mtandao wa Flightradar24 umeripoti kuwa, anga ya dunia ipo katika hali ya shughuli nyingi leo, huku ndege zaidi ya 22,000 zikionekana kuwa angani kwa wakati mmoja kutoka kwenye mfumo wake wa kufuatilia ndege mubashara.

Idadi hiyo inatoa picha ya wazi ya jinsi usafiri wa anga unavyosalia kuwa na shughuli kubwa katika safari za ndani na za kimataifa, huku mashirika yakisafirisha abiria na mizigo pasipo mapumziko.
1779304268637.jpg
 
Airbus imetangaza kuwa itakata rufaa mahakama kuu ya Ufaransa baada ya mahakama ya rufaa ya Paris kuihusisha na kosa la mauaji inayohusu ajali ya ndege yake ya Air France Flight AF447 iliyotokea Juni 01, 2009.

Ndege ya Airbus A330 iliyokuwa ikisafiri kutoka Rio de Janeiro kuelekea Paris iliingia katika mawingu mazito ambapo vitambuzi vyake vya kasi (pitot tubes) kuzibwa na barafu.
Hiali hiyo ilisababisha mfumo wa ndege kujiendesha "Autopilot" kujizima na marubani kupokea data zenye taarifa zisizo sahihi kuhusu kasi ya ndege.

Kutokana na data hizo marubani walifanya mawasiliano duni kati yao, na kujikuta ndege imeingia kwenye hali ya kushindwa kupaa "Stall" na kushuka bila kudhibitiwa hadi kuanguka baharini, na kupoteza maisha ya abiria na wafanyakazi wote 228 waliokuwa ndani.
Uamuzi wa sasa unabatilisha hukumu ya kutokuwa na hatia iliyotolewa mwaka 2023.

Familia za waathirika zimesema hukumu hiyo inawapa faraja kuwa uzembe ulitambuliwa, huku Airbus ikisema bado itapigania kujisafisha kisheria.
1779421653521.jpg
 
Ndege ndogo ya Cessna 182H ilipata uharibifu mkubwa baada ya rubani kusahau kuondoa kifaa cha kufungia usukani kabla ya kupaa katika uwanja wa Three Forks, Montana.

Kulingana na ripoti ya Bodi ya uchunguzi wa ajali ya Marekani (NTSB), muda mfupi mfupi baada ya kupaa ndege hiyo iliinama kurudi chini na kudunda kisha kurejea tena angani kabla ya rubani kutambua kuwa hakufungua kufuli alilofunga usukani.

Taarifa inasema, kabla ya kufanikiwa kufungua kufuri hilo, ndege ilirudi chini tena kwa nguvu na kubomoa gurudumu la mbele na kutoka nje ya njia.

NTSB imehitimisha kuwa sababu kuu ya ajali hiyo ni ukaguzi duni wa kabla ya safari, ambao ulisababisha jaribio la kupaa huku udhibiti wa ndege ukiwa umefungiwa.

Ripoti hiyo ilitolewa Mei 2024 kama sehemu ya elimu kwa marubani ili kujifunza kutokana na makosa yaliyotokea.
1779423592328.jpg
 
Kapteni Ricosetta Mafella wa Batik Air alipata sifa baada ya tukio la tetemeko la ardhi na tsunami ya Palu, Indonesia, mwaka 2018.

Wakati akijiandaa kuondoka Uwanja wa ndege wa Mutiara SIS Al-Jufrie, alihisi wasiwasi usioelezeka.
Bila kujua kuwa tetemeko lilikaribia, aliamua kuondoa ndege mapema dakika tatu mbele ya ratiba. Uamuzi huo uliwezesha ndege yake kuondoka salama kabla ya uwanja kupigwa na janga la tetemeko kubwa la ardhi.

Baadaye alimsifu msimamizi wa mnara wa kudhibiti ndege, Anthonius Gunawan Agung, aliyemuita “malaika mlinzi” kwa kuhakikisha ndege hiyo iliondoka kabla ya Njia kuanza kupasuka na mnara kuanguka na kumjeruho muongoza ndege huyo ambaye alipoteza maisha baadae.

Kapteni Mafella alisimulia tukio hilo katika kipindi cha televisheni cha Indonesia, Mata Najwa, ambapo alieleza jinsi hisia yake ya ndani ilivyomwokoa yeye, wafanyakazi na abiria wake.
1779614047360.jpg
 
Boeing 777X ni toleo jipya la ndege za Boeing 777 zinazotengenezwa kuwa moja ya miradi mikubwa ya uhandisi katika usafiri wa anga wa kisasa.
Ndege hii inatumia mabawa yenye nyenzo za mchanganyiko wa plastiki na nyuzi za kaboni pamoja na injini kubwa za GE9X ili kuongeza ufanisi na umbali wa safari.

Sifa ya kipekee ni mabawa yake yanayokunja ncha, teknolojia ya kwanza katika ndege za abiria.

Wakati wa kuruka, mabawa hayo huwa na urefu wa futi 235, na kuifanya kuwa ndege ya injini mbili yenye mabawa makubwa zaidi duniani. Urefu huo husaidia kupunguza mburuto, kupunguza matumizi ya mafuta na kwenda umbali wa hadi kilomita 13,500 huku ikipakia abiria zaidi ya 420.

Lakini wakati wa kutua ncha za mabawa zenye urefu wa futi 11 hukunjwa juu, na kupunguza urefu wa mabawa.
Hii inaruhusu B777X kutumia viwanja vya kawaida vya Code E, bila kulazimisha viwanja kujenga milango maalum kama ilivyokuwa kwa Airbus A380.

Kwa sababu mabawa hayo ni sehemu ya muundo mkuu wa ndege, Boeing na mamlaka za anga zimeunda mfumo wa "Takeoff Inhibition System".
Mfumo huu unatumia sensa nyingi kuangalia kama ncha zimekunjuka vizuri.

Ikiwa hazijakunjuka vizuri, ndege automatiki haitaruhusu kuingia kwenye mwendo wa kupaa.
Hii ni hatua zaidi ya onyo la kawaida la ndege yenyewe kuepusha hatari kabla haijatokea.

Mfumo huo unadhibitiwa na marubani kupitia kitufe kwenye chumba cha marubani na mchakato wa kukunja au kukunjua mabawa unachukua sekunde 20 kwa kutumia mifumo ya "hydraulic".

Baada ya kutua, mbawa zinajikunja kiotomatiki ili kurahisisha kuingia kwenye maegesho.

Wataalamu wanaona teknolojia hii inaweza kuwa mwanzo wa ndege za baadaye: kupata faida za mbawa ndefu angani bila kupoteza urahisi wa kutumia viwanja vilivyopo duniani.
1779616284230.jpg
 
Tanzania imegundua madini muhimu adimu "Rare Earth Elements" katika kijiji cha Mkiu, wilayani Ludewa mkoani Njombe.
Madini hayo ya Neodymium na Praseodymium yamepatikana kupitia utafiti unaoendelea kati ya Serikali na kampuni ya Hongji Mining Co. Ltd ya China.

Kwa sekta ya usafiri wa anga ugunduzi huu una umuhimu mkubwa kwani madini hayo ndio yanayotumika kutengeneza sumaku zenye nguvu zinazohitajika katika injini za ndege za kisasa, mifumo ya umeme, rada, sensa na vifaa vya udhibiti.

Lakini pia madini hayo yanawezesha ndege na magari ya umeme na hybrid kufanya kazi kwa ufanisi zaidi huku zikipunguza uzito na matumizi ya mafuta.

Maafisa wa madini wanasema kama uchimbaji wa kibiashara utaanza, Tanzania inaweza kuingia kwenye ushindani na nchi kama Afrika Kusini na Madagascar ambazo tayari zinaongoza Afrika katika madini haya.

Afisa Mkazi wa Madini Mkoa wa Njombe, Mhandisi Lucas Mlekwa, alisema utafiti unaendelea kubaini ukubwa wa akiba na uwezo wa kiuchumi wa eneo hilo kabla ya kuanza uwekezaji mkubwa.

Kwa sasa dunia inaelekea zaidi kwenye teknolojia safi, na usafiri wa anga nao unafuata mwelekeo huo, hivyo kuwepo kwa madini haya hapa nchini kunafungua fursa kwa Tanzania kushiriki kikamilifu katika mnyororo wa ugavi wa sekta ya anga duniani.
1779705250492.jpg
 
HONG KONG – Watu 10 walijeruhiwa mapema asubuhi ya Jumamosi baada ya ndege ya Cathay Pacific kutoka Brisbane, Australia kukumbwa na hali mbaya ya hewa na msukosuko mkali, na kulazimisha timu za matibabu kukimbilia kwenye ndege hiyo ilipowasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hong Kong.

Tukio hilo lilitokea kwenye ndege ya nambari CX156, ya aina ya Airbus A350-900 yenye usajili B-LRV.
Kulingana na maelezo ya shirika hilo na baadhi ya abiria, ndege hiyo ilikumbana na dhoruba kali takriban masaa mawili kabla ya kutua, na kusababisha kushuka kwa ghafla na kwa nguvu kwa urefu.

Wahudumu sita na abiria wanne walipata majeraha madogo na michubuko, hasa kwa sababu walikuwa wamesimama ndani wakigawa chakula.

Ndege ilitua salama saa 12:45 asubuhi, na timu za matibabu zilishughulikia walioathirika uwanjani.
Cathay Pacific imesema itaendelea kuwafuatilia waliojeruhiwa.
1779707543046.jpg
 
Helikopta ya kijeshi aina ya AH-64E Apache Guardian ililazimika kutua dharura katika shamba la mpunga mapema mwezi huu baada ya rubani kupata onyo la joto kupita kiasi kwenye injini ilipokuwa ikiruka juu ya Pyeongtaek, Mkoa wa Gyeonggi, Korea kusini.

Kitendo hicho kilifanywa na marubani wawili waliokuwa ndani ya helikopta ili kuzuia hali isizidi kuwa mbaya.

Helikopta hiyo ilitua salama takriban kilomita 65 kusini mwa mji mkuu wa Seoul na takriban maili 9 sawa na kilomita 14 magharibi mwa Kambi ya Humphreys, kambi kubwa ya kijeshi ya Marekani nchini Korea Kusini.

Wanajeshi wawili waliokuwa wakirusha helikopta hiyo walitoka salama bila majeraha yoyote.

Tukio hilo linaangazia umuhimu wa itifaki za usalama wa anga ambapo marubani huchukua hatua za haraka kutua dharura mara tu onyo la kiufundi linapotokea, ili kulinda uhai na kuzuia uharibifu kwa ndege.

Mamlaka za kijeshi bado hazijatoa taarifa kamili kuhusu sababu halisi ya joto kupita kiasi kwenye injini, huku uchunguzi ukiendelea.
1780300146592.jpg
 
Kitendo cha kipekee cha ushirikiano wa kijamii kilitokea tarehe 28 Agosti 2020 katika kijiji kidogo cha Igiugig, Alaska, ambacho kiko umbali wa maili 280 kutoka Anchorage ambacho hakina barabara yoyote inayokiunganisha na dunia ya nje.

Katika eneo hilo usafirishaji wa anga ndiyo njia pekee ya kushughulikia dharura za kiafya.
Usiku saa chache kabla ya usiku wa manane, mtoto mmoja mdogo alihitaji kupelekwa hospitalini kwa dharura kwa ndege.

Lakini ndege ilipokaribia kijiji, wakazi waligundua kuwa mfumo wa taa wa uwanja mdogo wa ndege ulikuwa umeharibika kabisa na rubani hasingeweza kutua salama gizani.

Mmoja wa majirani haraka alipiga simu 32 ili kuwaamsha wakazi wote na ndani ya dakika chache, karibu wakazi wote 70 wa kijiji walifika kwenye njia ya kurukia ndege wakiendesha magari, malori na pikipiki za ATV.

Walipanga magari yao kwa makini kando zote mbili za njia ya kutua kisha kuwasha taa.
Taa hizo zilitengeneza mstari mkali wa mwanga ulioruhusu rubani kuona njia na kutua kwa usalama.
Ndege ilibeba mgonjwa na kurudi hospitalini ambapo mtoto huyo alipona baadae.
1780336326763.jpg
 
Back
Top Bottom