Rubani wa kike mwenye asili ya Kiafrika-Amerika aliyeitwa #Bessie_Coleman alizaliwa Texas, mnamo 1892 ambapo alikulia katika mazingira ya kifukara na Ubaguzi mkubwa wa rangi na jinsia.
Baadae alihamia #Chicago akiwa na miaka 23 kutafuta maisha lakini akiwa huko akapata nafasi ya kupiga soga na baadhi ya marubani waliopigana vita vya kwanza vya dunia (WW1).
Stori zao zilimchochea kupenda urubani, lakini alikabiliwa na unyanyapaa mara mbili zaidi katika ndoto hiyo, akiwa kama Mtu Mweusi na Mwanamke.
Huko akashahuriwa kwenda Ufaransa ambako anaweza kutimiza ndoto zake.
Haraka akaanza kujifundisha lugha Kifaransa kila jioni.
Mnamo 1920, Bessie Coleman alivuka bahari kwenda Ufaransa kwa kutumia akiba yake yote ya fedha alizodunduliza na kwa bahati nzuri akapata udhamini wa kifedha kutoka kwa #Robert_Abbott, mmoja wa mamilionea wa kwanza wa Kiafrika wa Amerika.
Kwa miezi saba iliyofuata, alijifunza kurusha ndege kwa umahiri na mnamo Juni 1921 Chuo cha kimataifa cha Urubani nchini Ufaransa #Fédération_Aéronautique_Internationale kilimtunuku Leseni ya kimataifa ya Urubani na kuwa mwanamke wa kwanza mwenye asili ya kiafrika ulimwenguni kupata leseni hiyo.
Kumbuka hata Rubani wa kike Mmarekani aliyejizolea umaarufu Amelia Earhart alipata Leseni yake miezi 06 baadae mnamo Disemba mwaka huo.
Aliporudi Amerika, waandishi wa habari walijikosha na kujitokeza kwa wingi kumlaki kutaka kujua habari zake kitu ambacho hakikuwa kawaida kwa wakati huo.
Coleman alianza kutumbuiza katika maonyesho mengi ya anga kwa miaka mitano mfululizo akikonga nafsi na kusisimua maelfu kwa jinsi anavyocheza sarakasi za kuchungulia kifo kwa kupinduka na ndege angani ambazo wanaita 'Death Defying Stunts".
Hapo akabatizwa jina la "Queen Bessie "
Haikuwa kitu rahisi sana hasa ukivuta picha ya ndege zilizoundwa miaka ya 1920 ukizingatia ilipita miaka 17 tu na tangu wakina #WrightBrothers kuvumbua ndege ya kwanza kutumia injini.
Kwakuwa Teknolojia ilikuwa bado haijakua vizuri, ndege nyingi za wakati huo zilikuwa zimeundwa kwa Chuma, Mbao, Turubai ngumu na baadhi ya Bati.
Kurusha ndege wakati huo ilihitaji ujasiri, akili na nguvu kiasi kwasababu hakukuwa na masuala ya 'Hydraulics', 'autopilots' wala vifaa vya kusaidizia ndege kupaa.
Hii ilikuwa ngumu mfano wa kufanya michezo ya 'Drift' na Landrover 109.
'Queen Bessie' alikuwa na akihimiza Wamarekani wengine wenye asili ya Kiafrika kufuata nyayo zake ili kupunguza unyonge katika vita ya ubaguzi.
Pia alikuwa na msimamo mkali wa kukataa kufanya maonesho sehemu ambazo watu weusi walizuiwa kushiriki.
Lakini kwa bahati mbaya, vizuri havidumu.
Bossie Coleman alipoteza maisha katika ajali ya ndege mnamo 1926 akiwa na miaka 34.
Kifo chake kilitokea wakati akiwa kaketi kiti cha abiria wakati ndege moja ikifanyiwa majaribio.
Mwandishi mashuhuri na mtetezi wa haki sawa #Ida_Wells alisimamia mazishi yake.
Mhariri mmoja katika gazeti maarufu wakati huo "#Dallas Express"aliandika,
"Kuna sababu ya kuamini kwamba, umma kwa ujumla haukuelewa kabisa ukubwa wa mchango wake katika mafanikio ya kupinga ubaguzi"
#Admin
aviationmediatz@gmail.com.