Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,216
- 113,510
Mimi si kipofu wala si kiziwi.
Uwezo wangu wa kuona na kusikia upo juu.
Hivi hiki ninachokiona kwa macho yangu na kukisikia kwa masikio yangu ni uongo?
Nina maruerue labda? Hayo ninayoyaona ni mazingaombwe?
Kwa nyomi hizi zinazojipanga barabarani mwili wa Rais Magufuli unapopitishwa ndo tuamini kweli alikuwa anachukiwa sana na watu walio wengi zaidi?
Nahisi kuna watu wanakabwa na mafundo kooni wakiziona nyomi zimejipanga mabarabarani jijini Dar [na bado huko kwingine] zikimpa heshima za mwisho mwana udongo huyo. Hawa watu si aiabu wangependa kuona watu wachache wanaojitokeza kumuaga. La hasha.
Huwezi kupendwa na wote. Lakini pia, Rais hakuwa anachukiwa na idadi kubwa zaidi ya watu.
Licha ya mapungufu yake mengi, watu wengi walikuwa wanamkubali, hata kama si waziwazi. Na haitochukua muda watu wataanza kum miss.
Hii ni Manzese leo wakati akielekea uwanja wa Uhuru. Huyu ndo mtu anayechukiwa na watu?
Hapa ni Mwenge jana jioni mwili ukirudishwa spitali ya Lugalo. Huyu ndo mtu aliyekuwa anachukiwa? FOH.
Hapa ni jana jioni kwenye daraja la Kijazi.
Kote huko anapita. Hakuna vurugu. Watu wanamuaga kwa heshima kabisa.
Yawezekana wapo wachache wanaomtukana au kufurahia au vyovyote vile wajisikiavyo, lakini kwa hiki ninachokiona kwa macho yangu na kukisikia kwa masikio yangu, bado sijashawishika kwamba Rais Magufuli alikuwa anachukiwa na watu walio wengi.
Uwezo wangu wa kuona na kusikia upo juu.
Hivi hiki ninachokiona kwa macho yangu na kukisikia kwa masikio yangu ni uongo?
Nina maruerue labda? Hayo ninayoyaona ni mazingaombwe?
Kwa nyomi hizi zinazojipanga barabarani mwili wa Rais Magufuli unapopitishwa ndo tuamini kweli alikuwa anachukiwa sana na watu walio wengi zaidi?
Nahisi kuna watu wanakabwa na mafundo kooni wakiziona nyomi zimejipanga mabarabarani jijini Dar [na bado huko kwingine] zikimpa heshima za mwisho mwana udongo huyo. Hawa watu si aiabu wangependa kuona watu wachache wanaojitokeza kumuaga. La hasha.
Huwezi kupendwa na wote. Lakini pia, Rais hakuwa anachukiwa na idadi kubwa zaidi ya watu.
Licha ya mapungufu yake mengi, watu wengi walikuwa wanamkubali, hata kama si waziwazi. Na haitochukua muda watu wataanza kum miss.
Hii ni Manzese leo wakati akielekea uwanja wa Uhuru. Huyu ndo mtu anayechukiwa na watu?
Hapa ni Mwenge jana jioni mwili ukirudishwa spitali ya Lugalo. Huyu ndo mtu aliyekuwa anachukiwa? FOH.
Hapa ni jana jioni kwenye daraja la Kijazi.
Kote huko anapita. Hakuna vurugu. Watu wanamuaga kwa heshima kabisa.
Yawezekana wapo wachache wanaomtukana au kufurahia au vyovyote vile wajisikiavyo, lakini kwa hiki ninachokiona kwa macho yangu na kukisikia kwa masikio yangu, bado sijashawishika kwamba Rais Magufuli alikuwa anachukiwa na watu walio wengi.