Maboresho ya JF - 2019

Maboresho ya JF - 2019

Halafu kuna zile post ambazo unakuta umechangia lakini baada ya muda unakuta imeamishwa na mods kwenye jukwaa lingine ambalo mimi sio member, uki click link inakwambia need valid post id, nilikua napendekeza kwanini yasiwekwe maelezo yenye kuelekeza mahala ambako post imeamishiwa ili tuweze kuifatilia

Sent using unknown device
 
Kuna ombi moja ambalo wadau wengi wameliomba kipindi cha maboresho yenu hapo awali lakini mlikataa, na mlikata kwa sababu maalum,,

Sasa Leo na mimi niombe kwa style tofauti,

Kuwe RECYCLE BIN STATUS. Humu kutapatikana THREAD zote ambazo ni-DELETED,

Kwenye ID yake isionekane ila itaonekana kule kwenye recycle bin na isionekane nani alipost ile thread, ili hata mtu akitafuta kitu chochote kile akipate huko,

Ila pia kuwepo na option mbadala ya kuirudisha tena iwe ya mtoa thread original endapo tu mtoa mada ataihitaji tena kuirudisha iwe ktk ID yake,,

Maswali ya kujiuliza je kule ktk recycle bin comments za mtoa thread na za wachangiaji zitaonekana pamoja na ID zao? Jibu zionekane comments tu ila ID zisionekane nani ali post na nani alichangia.


mwenye kuongezea aongezee tu, pia unaweza kukosoa.

NAWASILISHA OMBI.



Sent using Jamii Forums mobile app
Dili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Some years back, ilikuwa ukiwa kwenye thread fulani kwa chini unaona threads kadhaa ambazo zinafanana na hiyo.

Hivyo kama kuna kitu ulikuwa unatafuta na haujapata jibu unaweza kuclick thread iliyowekwa kwa chini, ni zaidi ya miaka miwili sasa hiyo kitu haipo. Nakumbuka niliwahi kuiulizia mkairudisha kwa siku chache tu.

Fanyieni kazi hiko kitu mkuu, kinasaidia sana kama kuna taarifa unatafuta.
Kweli kabisa mkuu walivyobadilisha walikera sana nilijikuta nimeshikwa na hasira sio ya dunia hii
 
Some years back, ilikuwa ukiwa kwenye thread fulani kwa chini unaona threads kadhaa ambazo zinafanana na hiyo.

Hivyo kama kuna kitu ulikuwa unatafuta na haujapata jibu unaweza kuclick thread iliyowekwa kwa chini, ni zaidi ya miaka miwili sasa hiyo kitu haipo. Nakumbuka niliwahi kuiulizia mkairudisha kwa siku chache tu.

Fanyieni kazi hiko kitu mkuu, kinasaidia sana kama kuna taarifa unatafuta.
Hii inarudishika tu, hata dakika hii 😊
 
Poa injinia. Tumeisoma hiyoo. Ila pia tangu mtoe vile vi emoj vya zamani, matumizi ya emojia mpya yamepungua sanaaa. Ni kama vile watu wamevisusa hivi vi emoji vipya. So ni bora m-bumbe vi emoji vingine au mrudishe vile vya zamani!
Emoji ruksa kutumia zilizo kwenye simu yako.

Tunaomba kitabu chenye orodha ya maadili ya kitanzania ili tuweze kukitumia kama mwongozo.
 
Wakuu,

Naomba kuwafahamisha kuwa siku si nyingi tutafanya maboresho kidogo kwenye mwonekano na matumizi ya JF.

Lengo ni kuzingatia mahitaji ya wadau (ambayo yamekuwa yakiombwa), kuendana na mabadiliko ya kiteknolojia na kuimarisha zaidi uimara wa platform.

Aidha, maboresho hayo yataenda hadi kwenye kuimarisha miundombinu (infrastructure) ili kuongeza uimara wa kukabiliana na hali yoyote.

Mabadiliko mengine ya aina hii yanaweza kufanyika 2021 au 2022.

Asante kwa ushirikiano mnaoendelea kutupa.
Hongereni sana. Mungu aendelee kuwapa afya njema JF idumu milele maboresho mema

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom