MKUU
Maxence Melo post ni ndefu lakini soma yote tafadhari
Muendelezo wa API ...
==========<<<<<>>>>>>=========
Mifano ya matumizi ya API ya JF
ni kama nikitaka kukusanya (query) michango threads na/au posts zinazo husu mada flani toka kwa user flani au wote au za kwangu kwa interval ya muda na tarehe flani n.k.
JF inaweza kutumika kama data source ya tafiti za kijamii, kisayansi, na kibiashara.
Mfano kampuni flani inaweza kuwa na project ya kutengeneza product ya deep learning na AI ikatumia baadhi ya data kutoka JF kwa kuilipa JF kiasi flani au kuwa acknowledge JF na kuvutia watu wengi zaidi nje ya Tanzania na kuifanya advertising network kubwa mkapiga pesa ndefu ya matangazo.
Tanzania kampuni chache sana wanafaidika na matumizi ya Business Intelligence (BI) lakini miaka michache sana karibu kila kampuni makini ya biashara na taasisi za kisiasa na serikali hapa Tanzania na duniani kote watalazimika kutumia hii teknolojia ya BI kwa ajili ya kufanya strategic decision. Hata sasa tayari makampuni makubwa ya simu hapa ndani (TZ) yana hangaika kuimarisha Datawarehouse zao kwa ajili ya BI.
Siasa: wanasiasa duniani kote wana hangaika na data za kijamii kama za JF na Facebook au Twitter ili kuweza kufanya kampeni mitandaoni za kuwabadili mawazo wapiga kura wao wakilenga makundi ya kijamii kiumri na kijiografia. Mfano hii kashifa ya FB kutoa data kwa kampuni flani zilizo tumika ktk kampeni za uchaguzi USA. Hapa Tanzania JF ina nguvu sana ktk siasa na watu hutoa maoni huru guvyo inaweza kutumika ktk tafiti za kampeni.
Ni rahisi sana kutambua mawazo au mahitaji ya vijana kupitia michango yao au vitu wanavyo share kupitia thread hata zile 'tunazoita za kijinga' za chit chat au MMU. Huku utaona mahitaji ya vijana na matatizo yao kama unataka kuanzisha kiwanda cha bidhaa za wakubwa chumbani n.k.
Kama unaifanya forum flani ya JF kuweza kuunganishwa na device au application zingine za watu binafsi kupitia JF API na kutumika na application na home device kama vile mfano wa Alexa inavyokusanya data Amazon au Apple Siri inavyokusanya sehemu nyingine kwa kulipia huduma basi JF inaweza kujiongezea kipato kwa kutoza watumiaji wa huduma yaani subscribers. Humu kuna taarifa nyingi sana za matukio na biashara kama kule kwe burudani, JF doctor, JF matangazo madogo madogo ya biashara, Breaking news n.k.
Mfano hapo kwenye breaking news kampuni za media zinaweza kujiunga kupitia API kama sehemu ya kupata news tip kisha kuwatuma waandishi wao walio karibu na tukio. Sasa hapa atakae ingia JF website kawaida na wa mobile app yenu inakuwa bure kabisa kama ilivyo hivi sasa lakini hawa watakao tumia API yenu wanalipia wanapo nunua API key iwe wana renew service kwa kila baada ya muda flani.
Sababu hawa wanapata huduma maalumu kibiashara kwa upendeleo. Na sisi wa kawaida tunatumika kuwafaidisha ninyi JF kwenye JF kutumika kama advertising network hivyo hatulipii kama ilivyo sasa.
Hawa nasema huduma maalum ya upendeleo sababu hivi sasa inawezekana kabisa mtu anaefuatilia kitu flani JF kikampita bila kusoma au akakiona siku kadhaa zimepita. Na notification zinaweza kuwa nyingi sana ni rahisi kuziondoa bila kupitia zote lakini kwenye API zinakuwa filtered kupata specific subject au keywords flani na muda flani kutokana na mtakavyo implement API na mtumiaji atakavyo chagua features wakati anafanya configurations. Hii sijui niifananishe na Microsoft Azure Events Handler au Azure Events Hub.
Unaweza kuona hii idea ni bado sana kufanya kazi kwa bongo lakini ifanyeni kama vile mtu anavyonunua kiwanja/shamba kisha miaka michache anasifiwa aliona mbali sana, alifanya investment kubwa kwa gharama ndogo sababu alikuwa ahead of time.
Kuna siku utakuja kuombwa structured data za mambo flani na taasisi kubwa za kimataifa kama za UN au google kwa malipo flani ndipo JF mtakumbuka huu ushauri wangu. Pengine hadi sasa tayari mmeshaombwa data.
Mniwie radhi kwa makosa (typos) mengi ya kuandika sababu ya keypad na screen ndogo ya simu, pia mtiririko mbaya wa hoja lakini nafikiri nimeeleweka.