KERO Mabasi ya Mikoani yameanza kutoza nauli zaidi ya kiwango kilichowekwa. Mamlaka husika fuatilieni

KERO Mabasi ya Mikoani yameanza kutoza nauli zaidi ya kiwango kilichowekwa. Mamlaka husika fuatilieni

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Sasa kumekuwa na uhuni wa MABASI yote ya MIKOANI kutoza nauli kubwa bila nauli husika kwendana na viwango vya huduma.

Basi linatangazwa kama VVIP ila nje ya Bus kuwa jipya na choo ndani hamna jipya zaidi. Viti vimebanana mno wala havipo comfortable.

Juzi nimelipia ticket 2 kwaajili ya wazazi wangu sababu ni wazee nilitaka wasafiri comfortable Bus kutoka Mbeya kwenda Dar kampuni ya ABC bus lao wanasema ni VVIP - PRESIDENTIAL SEAT nauli Tsh 70,000
Wazee wamefika Dar wapo hoi wanalalamika viti vimebanana mnoo, wamefika miguu imevimba na mifupa inawauma.

Hii sio sawa na thamani ya pesa hamna.

LATRA watoe muongozo sifa za gari ya VVIP inapaswa kuwa na idadi gani ya viti na nafasi kati ya kiti cha mbele na nyuma kiasi gani.

Pia hata huduma za Vyoo vya kwenye haya magari sio rafiki kwa wanawake na haja kubwa...

LATRA itoe muongozo kwa kampuni inayoagiza gari za VVIP na kutoza nauli kubwa zijiandae na huduma kuendana na nauli husika na mazingira ya kusafiri comfortable iwe kipaumbele

Kinachoendelea kwasasa ni uhuni na utapeli na kuibia nauli wateja

Hamna sababu ya kulipa pesa za zaidi kwaajili ya choo tu

LATRA wafuatilie na watoe muongozo!
 
Acha kualamika nunua alphard kwa ajili ya familia yako !!!!
 
Bongo basi likiwa na choo tu ndani au wahudumu wa kike wanasema ni VIP. Kuna haja ya kujifunza zaidi VIP package inakuaje, kutangaza vituo na kutugawia maji ile sio VIP treatment.
 
Wazee hata ukiwapakiza kwenye ndege akifika lazima alalamike maumivu ya miguu, mgongo na uchovu kwa kuwa wao kukaa chini kwa muda mrefu ni tatizo kwao kutokana na kuchoka kwa viungo!!
 
Hili la viti kubanana sijajua ni kwanini limekuwa hivi, angalau ABC, mabasi mengine viti vimebana sana, kunyosha miguu ni tabu kubwa.
 
Mabasi ya kichina yanayokuja bongo mengi yapo hivyo, mwenzako wa mbele akirudisha siti nyuma hata kidogo Tu lazima akubane magoti, Kwa wazee lazima mgongo uume maana siti zimenyooka kama rula.
 
Hizo bus wala sio uongo uliyosema ni kweli tupu..!! Wengi wanalalamika seat ndogo zinabana hakuna cha luxury ni upuuzi mtupu..!!
 
Back
Top Bottom