Mabasi haya mnayakumbuka?

Mabasi haya mnayakumbuka?

Write your reply...Umesahau Kiswele DAR SONGEA
 
Igesa Line
Kwacha
Safina
Widambe
Makete

Haya mabasi wakati yanaanza kuwika nilikwepo Iringa miaka ya 1989. kabla ya hapo kulikuwa na yale mabasi ya zamani ya carrier juu, Yalipokuja haya ndo ilikuwa hizi new model za mizigo inakaa chini tukiyaita MKATE. we acha makonda na madereva wa hayo mabasi waliwatafuna mabinti kule Iringa, maana demu akipanda mle lilivyo tu achomoiiiiiii hahahahaha
Mkuu hii widambe wamiliki ni hawa akina widambe wa Ilembula au? Je miaka ya Nyuma walikuwa na magari makubawa maana mi nimewakuta na Coaster kadhaa na walipigwa pigwa mawe kwa wizi sidhani kama hata wana baiskeli
 
Happy nation sauti ya Manka eti nayo historia???? Hii biashara ni sawa na kusomesha mchumba
 
1. KWACHA nimekumbuka warrant kwenda shule
2. Mwafrika nimekumbuka safari yangu ya kwanza kusafiri peke yangu
3. Railway nimekumbuka safari ya kishule toka Iringa kwenda Mazengo Dodoma
4. Kamata nimesafiri nayo sana toka Songea kwenda Dar
5. Binkleb Bus Service (BBS), Safari zangu za Songea Dar
6. Kiswele Songea Dar na wakiingia SOngea ile mihoni ya kushindana kati ya Kiswele na Zainabs
7. Scandinavia SOngea Dar, Dar Mbeya
8. Tawaqal Safari za Songea Dar, Iringa
9. Special Coach... Safari za Songea Dar
10. Ruvuma Line hata hakudumu wallah... alilipeleka basi kwa PARADISO kutambika lakini wapiii
Nimekumbuka miaka hiyo ya1980s mabasi ya mkoa yalikuwa yanapita manzese,niliishi pale kituo kilikuwa manzese msufini,aidha kulikua na mgahawa mmoja uliitwa msumbiji hotel mmiliki alikuwa meneja wa timu ya Simba marehemu Abrahman Hamisi Muchacho.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwinyihijas bus service,Dar mlandizi Ruvu,tajiri alikua anakaa mwananyamala,anatembea kwa mguu na kikapu cha kusukwa kwa ukili,Viatu vyake kandambili,mzaramo wa bagamoyo. 1980-81.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi ni lazima wamiliki wa mabus kwa nje waonekane choka mbaya?? Kuna mmoja namfahamu tajiri wa lindi ana mabus meengi ya dar,lindi na mtwara lakini ajabu kwa kutembea kavaa katambili na kushinda kavaa misuli sio ajabu na ndio kawaida kwake..
 
1. KWACHA nimekumbuka warrant kwenda shule
2. Mwafrika nimekumbuka safari yangu ya kwanza kusafiri peke yangu
3. Railway nimekumbuka safari ya kishule toka Iringa kwenda Mazengo Dodoma
4. Kamata nimesafiri nayo sana toka Songea kwenda Dar
5. Binkleb Bus Service (BBS), Safari zangu za Songea Dar
6. Kiswele Songea Dar na wakiingia SOngea ile mihoni ya kushindana kati ya Kiswele na Zainabs
7. Scandinavia SOngea Dar, Dar Mbeya
8. Tawaqal Safari za Songea Dar, Iringa
9. Special Coach... Safari za Songea Dar
10. Ruvuma Line hata hakudumu wallah... alilipeleka basi kwa PARADISO kutambika lakini wapiii
Umenikumbusha madereva wa Songea Dar enzi hixo Tawaqal unamkuta Giriki, Kiswele unawakuta Yogi, Okalla na Rwambo, Zainabs unamkuta Shida na Special coach unamkuta John Africa na Mapunda......dah ilikuwa ni moto chini!
 
yutong,
Igesa Line, Kwacha, Scandnavia na Comfort Video Coach

Hayo niliyowekea red yalikuwa ndo mabasi yangu ya DAR- Iringa. Hiyo ya kwenye bluu yalikuwa mabasi maarufu sana kati ya Dodoma/Mpwapwa na Dar bila kuwasahau Champion.
Umenikumbusha Mhagama aka baba Omary dereva wa Comfort!
 
Basi leo ngoja niwarudishe enzi za 1980's na 1990's wakati huo nchi ikiwa haijauzwa. Palikuwa na mabasi ya Layland CD wakati huo Scania ndo dili. Mnakumbuka Mabasi haya?

Igesa Line
Kwacha
Safina
Gold Line
Widambe
Mwaafrika
Makete
Siri Yako
Super Star
Railway
Kamata
Bin Klebo Bus Service
Kiswele
Sharuks
Air Msae
Air Chalinze
No Challenge
Air Shengena
Zainab
Scandnavia
Special Video Coach
Tawaqal
Comfort Video Coach
Living Light
Yarabi Salama
Safari Master
Big Mayai
Jupiter
Mbarak
Ruvuma Tours Line
Matema Beach Coach

Unakumbuka nini hapo?
Nyota ........Dar to Iringa!
 
Umenikumbusha madereva wa Songea Dar enzi hixo Tawaqal unamkuta Giriki, Kiswele unawakuta Yogi, Okalla na Rwambo, Zainabs unamkuta Shida na Special coach unamkuta John Africa na Mapunda......dah ilikuwa ni moto chini!
Hivi ni dereva gani ambaye ilikuwa kama ni gari mpya inapiga route ya Songea ukiongozana na gari anayo endesha anakata taa za breki.

Ukianza kutoka Njombe kwenda Songea kwenye zile kona na milima unajua jamaa akanyagi breki kumbe taa haziwaki ukijaribu kumfata kwa kasi lazima upige chini barabara ya Njombe Songea ni nyembamba na ina kona na milima mikali.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom