Mabadiliko CHADEMA Makao Makuu

Mabadiliko CHADEMA Makao Makuu

Masatu,

Hebu tueleze wewe hiyo shule yako imekusaidia au kuisaidia nchi hii kivipi. Umefanya nini cha maana kwa huo usomi wako na umeona kama manyika naye akisoma kama wewe atakifanya hicho kitu. Manyika amefanya mambo makubwa kwa nchi hii na hiyo elimu yake kuliko nyie wenye masters na Phd zenu useless (wewe, kibunango na gembe kutwa kuongea mambo ya kijinga tu humu). Yaani kama usomi wenyewe ndiyo huo mnaomshauri naye akasomee halafu aje kuwa kama nyie (wasomi) mimi namshauri tu abaki kama alivyo kwa sababu sijaona tofauti yoyote kwenu.

Nyie kizazi cha kifisadi nyie we ngoja tu

Una jazba kweli... haya niambie wapi nimesema mimi ni msomi? Hayo makubwa aliyoyafanya "makubwa" ni yepi zaidi ya kupayuka ovyo kwenye media bila ya substance.

Unajichanganya kama ninayoandika humu ni ya "kijinga" how dare u r replying posts za "kijinga" hii inathibitisha wewe ndio mjinga zaidi!

Nyie kizazi "mpaka kieleweke" nyie ngoja tu
 
Dogo aende shule haraka iwezekanavyo he has a lot of potential!

Ila approach aliyotumia GT hapo juu....!!!!

Too harsh...wote tu binadamu tulioumbwa na Mungu!
 
Mnyika ni mwanaharakati asiyechumia tumbo; kuna vijana wengi ambao wakipata kanafasi kama hako hata asingeomba akasome;angetulia na elimu yake hiyo; lakini kwa chadema nafikiri utaratibu wao kiungozi walau unaangalia maslahi ya wanachama wake hasa ktk swala la elimu ambao hakika ndio ufunguo wa maisha; SO MNYIKA TWAKUSUBIRIA UBUNGO 2010 ukiwa na mambo hayo mapya; umefanya mambo mengi mno mpaka sasa
 
Mnyika ni mwanaharakati asiyechumia tumbo; kuna vijana wengi ambao wakipata kanafasi kama hako hata asingeomba akasome;angetulia na elimu yake hiyo; lakini kwa chadema nafikiri utaratibu wao kiungozi walau unaangalia maslahi ya wanachama wake hasa ktk swala la elimu ambao hakika ndio ufunguo wa maisha; SO MNYIKA TWAKUSUBIRIA UBUNGO 2010 ukiwa na mambo hayo mapya; umefanya mambo mengi mno mpaka sasa

Ubungo anakwenda kupoteza muda wake bure.
 
Tatizo dogo anashindwa kusoma alama za nyakati. Akina Zitto, Mdee et al wameenda shule anachoshindwa kuelewa kuwa hizi roller coaster politics za Bongo inafika wakati zinaparaganyika na baada ya hapo kila mtu na lwake na hapo ndio atakapoona umuhimu wa shule.

Awaangalie akina Dr Lamwai, Marando, Dr Tenga, Dr Limbu et al. Mambo ya siasa yalipoanza kuwaletea miyeyusho wakarudi kwenye fani zao na maisha yanaendelea.

Sasa ni muhimu dogo akajua kuwa hao Chadema wana enjoy their 15 minutes of fame kama ilivyokuwa kwa NCCR, TLP an CUF soon zitakapoisha ndio atajua kuwa hivyo vidingi vilikuwa vinamrostisha tu wakati hao akina Zitto haoo moto mwingi CCM....
 
Naona watu tuna -ve attitude;

Kwanza mtu kuacha uongozi ili akasome ndicho nilichokijua nakumbua ilishawahi kuongelewa humu hata kabla kwa wenye ubongo wa kutunza vema kumbu kumbu zao; na inaeleweka ameenda kusoma;
Naona huu ndiomuda muafaka; ana experience na TZ yote ametembea sana ingawa hiyo shule ilikuwa ndogo kuliko hata wengine hapa mna madegeree lakini LOGIC bwana du zero
Mnyika ameandika makala nyingi na kwa wale waliopitia pitia mambo haya ya wachache wanajua huyu mtu ana kitu fulani kichwani cha ziada kuliko hata maprofessor uchwara kibao wa bongo

Naombeni kama kweli mna nia ya dhati kulijenga taifa tuwape moyo vijana wenye asili ya upambanaji; sio mchumia tumbo yule angekuwa amechukuliwa na mafisadi zamani; alishawahi kumwandikia MSG RA kuwa =WEWE NI FISADI AKIWA BUNGENI; GT unaweza au wewe ndio wale wanaoenda pale kupiga magoti;
SO mie naona tumpe moyo akirudi jukwaani tutampokea na kumpa moyo kuendeleza mapambano ya maisha duni tuliyo nayo asilimia 85% ya WATZ
 
Huyu kijana tutamsemea, tutahisi hili na lile. Lakini kwa kuwa ni mwana JF yeye ndio atatueleza analokusudia baada ya kupokeza kijiti.
 
Naona watu tuna -ve attitude;

Kwanza mtu kuacha uongozi ili akasome ndicho nilichokijua nakumbua ilishawahi kuongelewa humu hata kabla kwa wenye ubongo wa kutunza vema kumbu kumbu zao; na inaeleweka ameenda kusoma;
Naona huu ndiomuda muafaka; ana experience na TZ yote ametembea sana ingawa hiyo shule ilikuwa ndogo kuliko hata wengine hapa mna madegeree lakini LOGIC bwana du zero
Mnyika ameandika makala nyingi na kwa wale waliopitia pitia mambo haya ya wachache wanajua huyu mtu ana kitu fulani kichwani cha ziada kuliko hata maprofessor uchwara kibao wa bongo

Naombeni kama kweli mna nia ya dhati kulijenga taifa tuwape moyo vijana wenye asili ya upambanaji; sio mchumia tumbo yule angekuwa amechukuliwa na mafisadi zamani; alishawahi kumwandikia MSG RA kuwa =WEWE NI FISADI AKIWA BUNGENI; GT unaweza au wewe ndio wale wanaoenda pale kupiga magoti; SO mie naona tumpe moyo akirudi jukwaani tutampokea na kumpa moyo kuendeleza mapambano ya maisha duni tuliyo nayo asilimia 85% ya WATZ
He he he !! Malunde-Malundi Kula tano mtu wangu
 
Naona watu tuna -ve attitude;

Kwanza mtu kuacha uongozi ili akasome ndicho nilichokijua nakumbua ilishawahi kuongelewa humu hata kabla kwa wenye ubongo wa kutunza vema kumbu kumbu zao; na inaeleweka ameenda kusoma;
Naona huu ndiomuda muafaka; ana experience na TZ yote ametembea sana ingawa hiyo shule ilikuwa ndogo kuliko hata wengine hapa mna madegeree lakini LOGIC bwana du zero
Mnyika ameandika makala nyingi na kwa wale waliopitia pitia mambo haya ya wachache wanajua huyu mtu ana kitu fulani kichwani cha ziada kuliko hata maprofessor uchwara kibao wa bongo

Naombeni kama kweli mna nia ya dhati kulijenga taifa tuwape moyo vijana wenye asili ya upambanaji; sio mchumia tumbo yule angekuwa amechukuliwa na mafisadi zamani; alishawahi kumwandikia MSG RA kuwa =WEWE NI FISADI AKIWA BUNGENI; GT unaweza au wewe ndio wale wanaoenda pale kupiga magoti;
SO mie naona tumpe moyo akirudi jukwaani tutampokea na kumpa moyo kuendeleza mapambano ya maisha duni tuliyo nayo asilimia 85% ya WATZ

Mkuu Malunde-malundi.
Niko pamoja na wewe dogo alikuwa anashusha nondo za uhakika.
J
 
Hapana mimi sikubaliani na GAME THEORY huyu kijana MNYIKa ana potential kubwa sana na ni hazina ambayo CHADEMA isithubutu kuipoteza. CHADEMA should take this boy to School kama CCM walivyompeleka Nape India; the sooner they do it the better awe na degree angalau moja mimi niko tayari kumchangia angalau kiduchu ,asikimbilie ubunge huo ataukuta atakapokuwa na confidence zaidi.


Unataka kusemaje??? Nini kilitokea UDSM? Nakumbuka 2005 wakati anajinadi tumpe jimbo la ubunge alisema angehitimu 2005? Sasa utasemaje awe na degree angalau moja, as if hana!!
 
Ni kijana muaminifu,muadilifu,mchapa kazi,mwerevu anayejiheshimu na kuheshimika ktk jamii yetu,anapenda kusikiliza, kujifunza, ana akili na hekima. Naamini kwa wasifu huu j.j.m ameelimika na kama suala ni degree basi atimize wajibu tu kwa kukamilisha wasifu wa kisomi wa kuhudhuria hadhara za kitaaluma madarasani ili jamii ijiridhishe juu ya usomi wake.

Mimi nimemkubali kama mwanazuoni kwa maono yake kimaandishi na mihadhara ya siasa na jamii. Ninarejea kumbukumbu zangu kuwa huyu j.j ni kama alishawahi kuwepo hapo udsm kabla ya 2005 ila sina hakika.

Tuendelee kujifunza j.j maana tuko wengi wa aina yako na sasa tunarudi madarasani taratibu ili ku shape fikra zetu na pengine tuwe silaha kali zenye kujenga na kuilinda nchi yetu tanzania kwa hoja na maarifa. Kidumu chama cha mapinduzi
 
Badala ya kukaa na kulumbana huku baadhi yetu tukionekana kufurahia wazi wazi suala la JJ kuachwa katika uteuzi huu mpya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, tungekaa na kujiuliza ni nini haswa kimesababisha JJ akaachwa katika hili.

Michango mingi hapa ni kama watu tunakurupuka na kumshambulia huyu kijana huku wengi wetu tukiona kufurahia wazi wazi, kwa nini wanadamu tunakuwa na roho za ajabu badala ya kutakiana mema tunakuwa twafurahia 'alleged downfalls' of others?

Kila mtu anaweza muongelea Mnyika kwa jinsi ambavyo anamfahamu, mimi ntasema Mnyika ni kisima cha 'knowledge.' Wengi tupo hapa tulipo kutokana na juhudi binafsi za Mnyika. He is what he is and we should respect that as it is. Maamuzi ya Chama juu ya Mnyika yana maana kubwa katika kujenga na si kubomoa.

Nawakilisha.
 
Watanzania tunasahau ya kwamba uongozi katika vyama vya kisiasa si 'birthright' ya kiongozi awae yoyote. Na kwamba katiak Chama abacho kinaendeshwa Kidemokrasia, mabadiliko katika Uongozi ni moja kati ya indicators kwamba ndani ya chama Demokrasia ipo.

Tunakosea sana kusema kwamba Mnyika katoswa kwani ukiangalia chama kina wanachama wengi na ni haki ya kila mwanachama kuweza shika nafasi mbali mbali za uongozi, na pia kutolewa katika hizo nafasi. Nafasi zote za uongozi ni dhamana tu.

Na pia jambo lingine la kulitilia maanani ni kwamba huitaji kuwa kiongozi wa ngazi fulani katika chama ili uweze kutimiza majukumu upasayo yatimiza ukiwa kama Mwanachama wa Chadema na Mtanzania. Maana unakuwa na majukumu kwa chama na pia unakuwa na majukumu kwa Taifa lako.

Tuangalie na kukubali kwamba nyakati hazitobaki kama zilivyo na kamwe jana haitokuwa kesho...

Mabadiliko ya Kweli [Kuanzia Nyumbani]
 
Kwanza huyu kijana ni boara to the MAX. Articles zake mtu bora usome comments kwenye utamu. Ni ndefu na zinatia kidhungu dhungu,na zaidi ya yote hayo, Freeman Mbowe aliona bora ainvest in BALILE badala ya mnyika ambaye hata shule hakulipiwa na CHADEMA

Sasa ushauri wangu kwa mnyika:

Its never too late unaweza kwenda kusoma pale CBE then who knows baadae unaweza kupata ajira mjini lakini siasa huziwezi na hao unaodhani wanakupenda hawana nia ya kukuendeleza kisiasa

Hivi kati yako na Halima Mdee ulifikiri ungeweza kupita?

Mimi huo ndio ushauri wangu asubuhi hii na kwa sababu wewe ni member wetu humu JF naamini utakubali kupewa ushauri na memebers wengine...if the worst become worse unaweza kurudi kujijini ulikotoka ukalime...after all kilimo bado ni uti wa mgongo wa taifa hili
kijana ana elimu ya BBA evening programm ya UDSM na alikuwa mwanaharakati mzuri tu wakati yuko hapo na sio mtu wa kwenda CBE tena.
 
kijana ana elimu ya BBA evening programm ya UDSM na alikuwa mwanaharakati mzuri tu wakati yuko hapo na sio mtu wa kwenda CBE tena.


Ndugu Ochu,

Asante sana kwa kuweka sawa kumbukumbu! Maana 2005 kwenye kampeni za Ubunge, Kibangu (Kata ya Makuburi - Ubungo) alijieleza kwamba angehitimu pale Mlimani-UDSM mwaka huo huo. Sasa nilishtuka sana kuona anaongelewa kama vile hana first degree.

Wasiwasi wangu umeisha sasa. Maana ni vizuri vijana wakawa makini sana na hizi siasa za Tanzania. Zinadanganya sana na mwisho wa siku watajikuta wananunua "PhD" kama wenzao wanaopigiwa kelele kila siku.

Na kama anaenda kujiendeleza zaidi, namshauri aende tu kimya kimya kuliko kujitangaza (kisiasa) kwenye media kama tuliokwisha washuhudia na mwisho wa siku mambo yalipowawia magumu huko chuoni wakarudi kimya kimya.

Mnyika songa mbele. Watanzania si watu wa kuwatetea sana. Mwisho wa siku hao unaojidai kuwatetea na kuwaonea huruma saaaana, mwisho wa siku ndiyo watakaokuja kukucheka. Cheza siasa za bongo kwa akili.

Na kama ni kweli kwamba umeomba mwenyewe kuondolewa kwenye uongozi wa chama ili upate muda wa kujiendeleza umetumia busara, maana wahenga walisema "Mshika mbili moja humponyoka". Na mifano dhahiri unaijua wewe mwenyewe; haiko mbali nawe. Ni kama pua na mdomo.
 
Hata mimi kwa ufahamu wangu, JJ Mnyika ni Graduate wa UDSM. Issue ni jee aligraduate?. kama ni kupitia UD, wengi tumepita lakini sio wote waliograduate. Hata James Mbatia ni mwanaharakati ambae alianzia UD lakini hakugraduate.
Mwita Mwikabe aliyeula CHADEMA pia ni Graduate wa UDSM na aliwahi kuwa rais wa DARUSO ni mwanaharakati uchwala na oportunist, hivyo it wont bee long kabla CHADEMA hawajagundua wameuvaa mkenge.
 
Wasifu wa Mnyika hapa chini. Ushauri tu, kwenye masuala ya elimu, kama umeamua kuongelea ulivyopasua O-level, inatakiwa pia uongelee points ulizopata A-level na university. Kama mambo huko kwingine hayakuwa mazuri sana inakuwa safe kuacha kuongelea masuala ya umepata points ngapi. Ukiongelea ya form four, watu wanauliza A-level je? Unakuwa umefungulia maswali mengi badala ya kuyapunguza. Kama ni interview mtu anakuja na maelezo kama hayo, obvious nitakuwa interested kujua huko kwingine ilikuwaje?

John John Mnyika ama "JJ" kama wengi wanavyopenda kumwita, alizaliwa Dar es salaam Agosti 21 mwaka 1980 akiwa ni mtoto wa tatu katika familia ya Bwana John Dalali na Bi Lucia Mduma. Alipata malezi bora chini ya familia hii ya kikatoliki yaliyomjenga kiakili na kimsimamo huku mama yake akiwa ni chachu ya yeye kujiamini, kujitahidi, kuwa na moyo wa upendo kwa kila mtu na kuheshimu watu wenye mitazamo na imani mbalimbali.

Alianza safari yake ya kielimu katika shule ya msingi ya Chang'ombe mazoezi na kumalizia katika shule ya msingi Mbuyuni katika jiji la Dar es salaam. Alishika nafasi ya kwanza katika mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi na kuchaguliwa kujiunga na shule ya vijana wenye vipaji maalum ya Ilboru iliyoko mkoani Arusha. Hata hivyo wito wa kuwa padre ulimsukuma kijiunga seminari ya Maua iliyoko Moshi mkoani Kilimanjaro.

Akiwa seminari alijifunza kuishi maisha ya kujinyima, uadilifu na unyenyekevu kama alivyokuwa mtakatifu Fransisko wa Asizi na watawa wakikapuchini kwa ujumla. Aidha maisha ya seminari yalijenga zaidi ari yake ya kufanya kazi kwa bidii hususani katika kilimo na shughuli mbalimbali za uzalishaji mali. Alihitimu kidato cha nne mwaka 1998 kupata daraja la kwanza nukta saba yaani "division one-points seven" huku akiwa na alama A katika masomo tisa.

Pengine kipindi kilicholeta mabadiliko ya kimtazamo na kujenga dira ya maisha yake ni kile alichokuwa akisubiri kujiunga kidato cha tano baada ya kuwa ameshahitimu kidato cha nne. Katika kipindi hiki aling'amua adha ya ukosefu wa ajira kwa vijana na fursa finyu kwa vijana katika kujikwamua kimaisha na hasa kutokuwepo mipango ya makusudi ya kuwaendeleza vijana nchini licha ya wingi wao, nguvu zao na vipaji vyao kuwa tunu kwa mustakabali wa taifa. Kwa hivyo alijiingiza kwenye harakati za kumkomboa kijana kupitia asasi ya National Youth Forum (NYF). Aliomba kwa mafanikio kujiunga na shule ya sekondari Tambaza ili kubaki Dar es salaam kuendeleza harakati alizokwisha zianza.

Akiwa Tambaza aliendelea na harakati za vijana kupitia NYF na akawa pia mwenyekiti wa mkoa wa chama cha wanafunzi wakatoliki "Tanzania Youth Catholics Students", TYCS ambapo alifanya mengi ya kukumbukwa ikiwa ni pamoja na kubuni kampeni ya matumaini katika TYCS na akajifunza kwa vitendo kuwa uongozi ni utumishi.

Ni katika kipindi hiki - mwaka 2000, ambapo yeye na vijana wenzake wengi wao wakiwa ni wanafunzi wa sekondari walipoanzisha Taasisi ya Dira ya Vijana Tanzania "Tanzania Youth Vision Association" almaarufu kama TYVA na yeye kuchaguliwa kuwa katibu mkuu wa kwanza wa Taasisi hii.

Baada ya kumaliza kidato cha sita mwaka 2001,alijiunga na chuo cha diplomasia cha jijini Dar es salaam katika kozi ya itifaki na mahusiano ya jamii. Baadaye aliajiriwa na Redio Tanzania Dar es salaam (RTD) katika kitengo cha PRT na kufanya kazi ya utangazaji kwa mwaka mmoja. Akiwa RTD bado aliendelea na harakati za vijana kupitia NYF mpaka taasisi hiyo ilipofutwa na serikali. Aliendelea pia na harakati za utetezi wa wanafunzi kupitia mtandao wa wanafunzi Tanzania 'TSNP'ambayo yeye ni mmoja wa waanzilishi wake.

Alijiunga na chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM) mwaka 2002 kusoma shahada ya kwanza ya utawala wa biashara (BBA) katika programu ya jioni. Sambamba na masomo ya jioni katika chuo kikuu cha Dar es salaam, ameendelea kuwa muajiriwa wa United Nations Association (UNA) kama mratibu msaidizi wa mradi wa ushiriki wa vijana unaotekelezwa na kitengo chake cha vijana (YUNA) katika wilaya kumi nchini Tanzania.

Pia pamoja na ajira na masomo, ameendelea kushika nafasi kadhaa za uongozi na kufanya shughuli mbalimbali. Mwaka 2003 alibuni na kuratibu programu ya maboresho na marekebisho ya TYVA ambayo yamesaidia asasi hiyo kupata uongozi thabiti, ofisi, miradi, mipango ya muda mrefu na uwezo wa kiundeshaji. Aliongoza kama mwenyekiti wa Taifa wa Taasisi hii mpaka alipoamua kujiuzulu mwezi januari 2005 ili kuweza kuingia kwenye siasa. Amejiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kuteuliwa kuwa mkurugenzi wa Taifa wa vijana wa chama hicho.

Pamoja na wadhifa huo, bado anaendelea kuwa mjumbe wa bodi na mjumbe wa kamati mbalimbali za kitaifa na za kimataifa za asasi na taasisi kadhaa zinazohusika na masuala ya vijana.

Ameandika na kuwasilisha tafiti na mada kadhaa kuhusu masuala mbalimbali zikiwemo za ukosefu wa ajira kwa vijana, ukuzaji wa vipaji vya vijana na mfumo mwafaka wa elimu Tanzania ambayo aliiwasilisha kwenye mkutano wa wabunge wa jamhuri ya muungano Tanzania.

Amefanya kazi pia kama mnukuzi wa warsha za kuwajengea uwezo wabunge wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, nafasi ambayo imempa fursa ya kujifunza masuala mbalimbali ya Bunge ikiwemo uchambuzi wa bajeti, utendaji wa Bunge na usimamizi wa mahesabu.

Ameshiriki warsha mbalimbali za ndani ya nchi na mikutano katika nchi sita. Alichaguliwa kuwasilisha hotuba ya vijana katika mkutano wa fungamano la asasi za Umoja wa mataifa uliofanyika Hispania.

Lengo lake la muda mfupi ni kuchangia katika kuongeza ushiriki na ustawi wa vijana Tanzania na lengo lake la muda mrefu ni kuchangia katika kuleta maendeleo ya jamii kupitia kipawa chake cha uongozi.
 
Ndugu wanaJF,
Heri ya mwaka mpya 2009.

Nimetuiwa ujumbe wa simu kuwa katika JF kuna habari hii ambayo nimeona niisemee.

Sio kweli kwamba John mnyika, aliyekuwa Mkurgenzi wa Vijana Taifa ameondolewa katika uongozi wa chama. Isipokuwa John amethibitishwa kuwa Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Kwa kuwa huwezi kuwa na Kurgenzi mbili kwa wakati mmoja, basi Kurgenzi wa Vijana imepata Mkurugenzi mpya ambae anasubiri kuthibitishwa na Kamati Kuu ya chama ambae ni Ndugu Halima Mdee(Mb).

Naomba ifahamike kuwa John Mnyika Hajang'olewa CHADEMA. John ni mmoja wa hazina kubwa sana ya chama chetu na kwa muda mrefu ujao atakuwa tegemeo kubwa la chama na Taifa letu. John hajafanya makosa yeyote katika chama ya kustahili kuvuliwa uongozi. Amekuwa mwadilifu sana katika chama na ametoa mchango mkubwa sana katika ujenzi wa Demokrasia katika Taifa letu.
 
Nani alitegemea kitu tofauti na hicho alichokiandika GT???Huyu mkulu ana tatizo la kuruhusu emotions kumtawala either anapofikiri au anapoandika.Huu ni upungufu mkubwa kwa mtu yeyote makini.
BTW;
Vipi kijiwe cha kwa January kinaendeleaje?
 
Hata mimi kwa ufahamu wangu, JJ Mnyika ni Graduate wa UDSM. Issue ni jee aligraduate?. kama ni kupitia UD, wengi tumepita lakini sio wote waliograduate. Hata James Mbatia ni mwanaharakati ambae alianzia UD lakini hakugraduate.
Mwita Mwikabe aliyeula CHADEMA pia ni Graduate wa UDSM na aliwahi kuwa rais wa DARUSO ni mwanaharakati uchwala na oportunist, hivyo it wont bee long kabla CHADEMA hawajagundua wameuvaa mkenge.
Wakulu Heshima Mbele!

Kuna wakati Flani nilikuwa Mbele kumsahauri sana mdogo wangu Jojn Mnyika Nini Cha kufanya,Hasa kuhusiana na shule.Na niliyasema haya kwa kuwa niliwahi kusikia kwamba hakumaliza masomo yake ya BBA pale Mlimani na alikuwa akisuasua sana .Tusubir sababu rasmi za kusimamishwa kwake ila nvyojua watampa kazi nyingine,Otherwise CCM watamchukua kijana na kumkabidhi kazi!

Kuhusu Mwita Mwikabe na John Mrema.
Hawa Wawili walikuwa wapinzani sana kipindi Mwita Rais na Mwikabe ni waziri mkuu wa DARUSO.Nakumbuka ilikuwa ikitupa sana taabu kipindi hicho kama Chama kujua nanai atatusaidia wakati migomo ikitokea,Mrema alikuwa ni mtu waCHADEMA na mwita alikuwa upande wetu na hii ni kwa kuwa tu tuliweza akumtoa chama cha NCCR na kumvuta kwetu .


Ila kimsingi mwita alikuwa ni mwanachama wa NCCR na sikumbuki kama alishawahi kurudisha kadi ya Chama hicho.Wote Mwita na john ni Ma-opportunist na hawajui wako CHADEMA kwa ajili ya nini na kwa Maslahi ya nani.

Kuna thread moja ahapa nilishawahi kusoma ikieleza kuhusu mapandikizi ya CCCM katika vyama hivi,Mwita ni mmoja wao na ukianalia kwa undani zaidi hakuna wapinzani wa kweli na wote hawa kina zitto wanakaa pale ili kujiwekea mazingira mazuri kimaisha na hawana lolote.Ulisahwai kuona wapi mtyu anatolewa katika CHama na anahama?Hii inaonehsa ni mtu anayependa Madaraka na siyo kusaidia watanzania

Kinachohitajika ni umoja wa kitaifa tu kutatua matatzio ya watanzania.Kila jimbo lijiunge na kuweka mikakati yao na wasitegeemee mbowe wala Slaa kuja kutatua matatizo yao.Kama tukiweza kuwa na watu wa aina ya wanaTARIME au Mbeya basi tutashinda .Na ushindi utachngiwa na kuwapa mbinu ya nini cha kufanya ili wajikomboe.

Huwa siku zote nasita kusema kwamba Chama au Muungwana wameshidnwa kuwapa watanzania maisha bora,bali ni watendaji wa serikali waliokosa ubunifu ndiyo wanalipeleka Taifa hili kubaya.
 
Back
Top Bottom