Ndugu wanaJF,
Heri ya mwaka mpya 2009.
Nimetuiwa ujumbe wa simu kuwa katika JF kuna habari hii ambayo nimeona niisemee.
Sio kweli kwamba John mnyika, aliyekuwa Mkurgenzi wa Vijana Taifa ameondolewa katika uongozi wa chama. Isipokuwa John amethibitishwa kuwa Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Kwa kuwa huwezi kuwa na Kurgenzi mbili kwa wakati mmoja, basi Kurgenzi wa Vijana imepata Mkurugenzi mpya ambae anasubiri kuthibitishwa na Kamati Kuu ya chama ambae ni Ndugu Halima Mdee(Mb).
Naomba ifahamike kuwa John Mnyika Hajang'olewa CHADEMA. John ni mmoja wa hazina kubwa sana ya chama chetu na kwa muda mrefu ujao atakuwa tegemeo kubwa la chama na Taifa letu. John hajafanya makosa yeyote katika chama ya kustahili kuvuliwa uongozi. Amekuwa mwadilifu sana katika chama na ametoa mchango mkubwa sana katika ujenzi wa Demokrasia katika Taifa letu.
Mhe. Tunashukuru kwa ufafanuzi huu , kwani mengi yalisemwa na sababu nyingi kutolewa ku-justify tukio hili.