Mabadiliko CHADEMA Makao Makuu

Habarindiyohiyo

JF-Expert Member
Aug 11, 2008
263
13
Mabadiliko CHADEMA Makao Makuu: Mwikabe aula, Mnyika atoswa

Mabadiliko yafanywa CHADEMA Makao makuu, baada ya kujitoa CCM Mwita Mwikabwe abahatika kwa kuteuliwa mkurugenzi wa sera ya utafiti. Katika utuezi huo, John Mnyika ametoswa kuwa mkurugenzi wa Vijana na nafasi yake imechukuliwa na Halima Mdee(Mbunge wa Viti Maalum). Wengine waliokumbwa na mabadiliko hayo ni Regia Mtema, aliyetolewa uafisa vijana na nafasi yake kuchukuliwa na Ali Chitanda. Regia ameteuliwa kuwa Afisa wa Mafunzo nafasi ambayo ilishikiliwa na Dady Igogo ambaye ameteuliwa kuwa afisa Sheria. Aliyekuwa afisa sera na utafiti Danda Juju yeye amepelekwa Bunge na Halmashauri. Mabadiliko hayo hayahusishi wakurugenzi wengine kama Benson Kigaila, Erasto tumbo na wengine ambao wote wanaendelea na nafasi zao kama kawaida kama inavyoonyeshwa kwenye tovuti ya chama hicho Tovuti ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Uteuzi huo umeaanza mara moja

............ndiyohiyo
 
Last edited by a moderator:
Mabadiliko CHADEMA Makao Makuu: Mwikabe aula, Mnyika atoswa

Mabadiliko yafanywa CHADEMA Makao makuu, baada ya kujitoa CCM Mwita Mwikabwe aula kwa kuteuliwa mkurugenzi wa sera ya utafiti. Katika utuezi huo, John Mnyika ametoswa kuwa mkurugenzi wa Vijana na nafasi yake imechukuliwa na Halima Mdee(Mbunge wa Viti Maalum). Wengine waliokumbwa na mabadiliko hayo ni Regia Mtema, aliyetolewa uafisa vijana na nafasi yake kuchukuliwa na Ali Chitanda. Regia ameteuliwa kuwa Afisa wa Mafunzo nafasi ambayo ilishikiliwa na Dady Igogo ambaye ameteuliwa kuwa afisa Sheria. Aliyekuwa afisa sera na utafiti Danda Juju yeye amepelekwa Bunge na Halmashauri. Mabadiliko hayo hayahusishi wakurugenzi wengine kama Benson Kigaila, Erasto tumbo na wengine ambao wote wanaendelea na nafasi zao kama kawaida kama inavyoonyeshwa kwenye tovuti ya chama hicho Tovuti ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Uteuzi huo umeaanza mara moja

............ndiyohiyo

Mkuu,

Sijasoma katiba ya CHADEMA, hivyo ningetaka kuuliza ni nani kafanya hayo mabadiliko? Je ni Mwenyekiti wa CHADEMA au ni kikao cha chama?

Kijana wetu Mnyika amefanya nini mpaka kuondolewa? Kwa mawazo yangu strategically sidhani kama Mnyika alikuwa effective. Alikuwa anajihusisha mno na propaganda; ukizidisha inafika mahali watu wanachoka na hawasomi tena.

CHADEMA wangemsaidia Mnyika kwa kumpeleka kusoma shule ya maana, naamini ni mchapa kazi na hivyo akipunguza mapungufu yake anaweza kuwa effective.
 
Mkuu,

Sijasoma katiba ya CHADEMA, hivyo ningetaka kuuliza ni nani kafanya hayo mabadiliko? Je ni Mwenyekiti wa CHADEMA au ni kikao cha chama?

.


Katika chama hicho uteuzi wa wakurugenzi hufanywa na kamati kuu ya chama kwa mapendekezo ya sekretariati.

Maafisa wa chama hicho huteuliwa na sekretariati.

Kamati kuu ya chama hicho huwa chini ya Mwenyekiti wa Taifa, wakati Sekretariati inaongozwa na Katibu Mkuu wa chama.

Inaelekea huyo dogo ameshindwa kabisa kuongoza vijana wa CHADEMA ndio maana sasa ameteuliwa mpambanaji Halima Mdee. Huyo Mnyika sasa anasugua Benchi

......ndiyohiyo
 
Mabadiliko CHADEMA Makao Makuu: Mwikabe aula, Mnyika atoswa

Mabadiliko yafanywa CHADEMA Makao makuu, baada ya kujitoa CCM Mwita Mwikabwe aula kwa kuteuliwa mkurugenzi wa sera ya utafiti. Katika utuezi huo, John Mnyika ametoswa kuwa mkurugenzi wa Vijana na nafasi yake imechukuliwa na Halima Mdee(Mbunge wa Viti Maalum). Wengine waliokumbwa na mabadiliko hayo ni Regia Mtema, aliyetolewa uafisa vijana na nafasi yake kuchukuliwa na Ali Chitanda. Regia ameteuliwa kuwa Afisa wa Mafunzo nafasi ambayo ilishikiliwa na Dady Igogo ambaye ameteuliwa kuwa afisa Sheria. Aliyekuwa afisa sera na utafiti Danda Juju yeye amepelekwa Bunge na Halmashauri. Mabadiliko hayo hayahusishi wakurugenzi wengine kama Benson Kigaila, Erasto tumbo na wengine ambao wote wanaendelea na nafasi zao kama kawaida kama inavyoonyeshwa kwenye tovuti ya chama hicho Tovuti ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Uteuzi huo umeaanza mara moja

............ndiyohiyo
Yale yale ya CCM kuwazawadia akina Tambwe
 
"Mwikabe aula, Myika atoswa"....najiuliza huko Chadema ni kipi hicho ambacho watu 'wanakula' mara wanapopata nafasi ya uongozi? ifike mahali jamani mjitofautishe na CCM ma mambo ya 'kuula'!
 
Inaelekea Mnyika amechuka study leave kama alivyowahi kudokeza hapo nyuma.

Inawezekana ni study leave ama ameomba awe na muda zaidi katika kujiandaa kuchukua jimbo la Ubungo ambalo CCM wanataka kumsimamisha Nape Nnauye kupambana naye!!
 
Uongozi ni dhamana, leo unao, kesho hauna. Mimi nadhani Mnyika hajatoswa, bali ni mabadiliko ambayo hutokea katika kuongeza tija. Hata kesho na kesho kutwa Mdee naye ataondoka atakuja mwingine. Alikuwepo Mtei, akaja Makani (Bob) na sasa Mbowe.
 
Labda ni katika kuweka sawa mambo, maana lile tukio la Mbeya Vijijini haliwezi kupita hivi hivi.
 
Yale yale ya CCM kuwazawadia akina Tambwe


Mwikwabe hajateuliwa mkurugenzi, nimeangalia hapa kwenye sekretariati Sekretariati ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo hakuna kurugenzi ya sera na utafiti. Huyu atakuwa ameteuliwa kuwa afisa kwenye idara ya sera na utafiti. Vipi mabadiliko hayo hayajagusa ofisi yetu ya makao makuu Zanzibar?

Kuna mtu ana historia ya kila aliyeteuliwa tumjue kwa undani?

Namfahamu Halima Mdee.

Mwita Mwikabwe ndio nani?

Ali Chitanda?

Dady Igogo?

Regia Mtema?

Danda Juju?


Tujue elimu yao, wamewahi kuongoza wapi? na hata makabila yao-manake isije ikiwa ni wachaga watupu
 
Chadema boresheni chama kwa ushindani makini ila chungeni mamluki.Nadhani mabadiliko hayo yatakuwa na tija kwa mustakabali wa chama kinachotaka kuongoza dola.Mamluki ni sumu mkiruhusu wapenyeze Chadema.
 
Chadema boresheni chama kwa ushindani makini ila chungeni mamluki.Nadhani mabadiliko hayo yatakuwa na tija kwa mustakabali wa chama kinachotaka kuongoza dola.Mamluki ni sumu mkiruhusu wapenyeze Chadema.

KUKUBWA ni kuwa wanapaswa kuwa makini, kwani wakizuia mamluki ndani ya chama wajue na nje wapo kwani hujasikia ya Waislamu walioibuka na kudai Chadema wanaudini wakasahau CUF?
 
Inawezekana ni study leave ama ameomba awe na muda zaidi katika kujiandaa kuchukua jimbo la Ubungo ambalo CCM wanataka kumsimamisha Nape Nnauye kupambana naye!!

Hayo ya study leave na kujiandaa uchaguzi wa jimbo la Ubungo umesema wewe. Huyo hawezi kushinda hata uenyekiti wa kijiji nini ubunge. CHADEMA wangefanya vizuri zaidi kama wangemteua Mwita kuwa mkurugenzi wa vijana- kwa kuwa amewahi kuongoza vijana wa DARUSO na UVCCM, na pia anatoka kabila la wapambanaji wakina Chacha Wangwe. Halima Mdee angepelekwa kurugenzi wa wanawake.


.......ndiyohiyo
 
Hayo ya study leave na kujiandaa uchaguzi wa jimbo la Ubungo umesema wewe. Huyo hawezi kushinda hata uenyekiti wa kijiji nini ubunge. CHADEMA wangefanya vizuri zaidi kama wangemteua Mwita kuwa mkurugenzi wa vijana- kwa kuwa amewahi kuongoza vijana wa DARUSO na UVCCM, na pia anatoka kabila la wapambanaji wakina Chacha Wangwe. Halima Mdee angepelekwa kurugenzi wa wanawake.


.......ndiyohiyo

huo ndio ukabila tunaousemea na kuupiga vita kila siku na sasa umeuonyesha mwenyewe wewe mwanachama wa chadema
 
Mabadiliko CHADEMA Makao Makuu: Mwikabe aula, Mnyika atoswa

Mabadiliko yafanywa CHADEMA Makao makuu, baada ya kujitoa CCM Mwita Mwikabwe aula kwa kuteuliwa mkurugenzi wa sera ya utafiti . Katika utuezi huo, John Mnyika ametoswa kuwa mkurugenzi wa Vijana na nafasi yake imechukuliwa na Halima Mdee(Mbunge wa Viti Maalum). Wengine waliokumbwa na mabadiliko hayo ni Regia Mtema, aliyetolewa uafisa vijana na nafasi yake kuchukuliwa na Ali Chitanda. Regia ameteuliwa kuwa Afisa wa Mafunzo nafasi ambayo ilishikiliwa na Dady Igogo ambaye ameteuliwa kuwa afisa Sheria. Aliyekuwa afisa sera na utafiti Danda Juju yeye amepelekwa Bunge na Halmashauri. Mabadiliko hayo hayahusishi wakurugenzi wengine kama Benson Kigaila, Erasto tumbo na wengine ambao wote wanaendelea na nafasi zao kama kawaida kama inavyoonyeshwa kwenye tovuti ya chama hicho Tovuti ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Uteuzi huo umeaanza mara moja

............ndiyohiyo

Haya mambo ya kusema fulani AULA ndio yanayorudisha nyuma maendeleo ya nchi. Nafasi sio za kuwapa watu ULAJI. Na wanaochaguliwa wakihamua kula kweli mnawaita mafisadi.
 
Nadhani siku za Nyuma kuna mahala Mnyika alisema ana mpango wa kuachia ngazi

Pia,Halima Mdee yuko fiti.Halafu kama Kweli CCM wanataka kumsimamisha Nape huko ubungo apambanae na Mnyika basi tuseme CCM washalikosa hilo jimbo
 
As long as its for the good thing... Hongereni sana; wasiwasi wangu ni kwamba Mnyika is a very intelligent guy and you can't just drop him and excpect everything will be fine... unless yeye mwenyewe amekubali. Na huyu Mwikwabe kaja lini... kaijua Chadema lini... kakubalika na vijana lini... hata akamaliza na ka-probartion lini... hadi leo kupewa dhamana hiyo?? Ina maana hakuwamo mtu wa maana before him?

Naomba mungu usiwe ule mwanzo wetu tuliouzoea wa wapinzani na replacement circus... Chadema mmeanza mapema sana kugawana vi-miraba vyenu, ngoma ya kitoto haikeshi!!!
 
Haya, nimeshaondoa hayo mambo ya kuula. Mi nilijua kuula maana yake ni kubahatika kumbe kuna maana tofauti kabisa

.......ndiyohiyo
 
Back
Top Bottom