Nimegundua watanzania hatujui tunataka nini. Hatuna agenda hata hiyo ya mabadiliko. Kama hatuna dira ya tunakoelekea basi tutawapeleka akina Edward wakakalie viti vyao ili waendelee na BAU. Hakuna mabadiliko kama fikra zetu ni hizi.
Dr Slaa ameonyesha kukerwa na ufisadi kwa vitendo. Hongera sana Slaa. Lakini naona shutuma hapa zinazoelekezwa kwake. Yeye kaongea kwa data, ni wajibu wa watu waliotajwa kutueleza kwa data. Evidences alizotoa jana ukweli kama sisi watanzania tuko serious na nchi yetu basi tunapaswa tufikirie kwa dhati nafasi ya mgombea urais wa Chadema.
Kwa kuwa yeye jj flag bearer basi hana budi ajitokeze mbele ya watanzania ajibu tuhuma zile kwa evidence. Otherwise mihemko tulionayo itatupeleka Libya. At least kwa sasa ambapo hajajibu lolote Lowassa hafai kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano