Maaskofu waipinga CHADEMA...

Maaskofu waipinga CHADEMA...

Msikurupuke jaman kuchangia na kuwalaumu maaskofu bila kufwatilia kile kilichosemwa.Hajawakemea chadema bali vyama vyote.Huyu jamaa namkubal sio mnafk hata kidogo

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Mwambieni huyo Askofu aende Lumumba akachukue Buku 7

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Kwan hivi vikosi vya ulinzi binafsi kuwepo nchini inamaana polisi au jeshi hawapo au!!? Sasa kuna tatizo gani chama Kama cdm kuwa na kikosi cha kujilinda? Mim binafsi sitaki kabisaaa habari za maaskofu wachumia Tumbo ndio maana kanisa langu ni sebureni kwangu..... Ilaaaaa!!
 
Asanteni maaskofu, msg sent ila sidhani kama itafanyiwa kazi na hawa watu maana vichwa vyao vigumu sana.
Hana lo lote. Hawa ndiyo maaskofu wa Baali. Kiboko yao Eliya.


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Hicho kikundi kipo.kwenye katiba ya Chadema.Viongozi wa dini wafanye tafiti badala ya kupotosha waumini wao

Hawana lolote ni unafiki tu na tabia ya kufikiri nusunusu! Kuhusu kushambuliliwa makanisa mbona waliwaambia waumini wao kuwa wayalinde makanisa? Huko sio kuanzisha vikundi vya ulizi?
 
hajatamka hata neno moja kuhusu chadema hapo. au mtu akisema vyama vya siasa anamaanisha chadema?

mkuu ligangaluma, inaonekana ameisema cdm kwa sababu wao ndio wametangaza rasmi kijilinda kwa kuanzisha kikundi red brigade ila tokea zamani kuna green gurd na blue gurd lkn askofu huyu hakuongea chochote ilona sawa tu. jamani mbona cdm mnaionea sana kuna nini?
 
Mimi naona tamko la Askofu ni sawa kabisa, na hakuna mahali anakoishutumu CDM. Ujumbe hapa ni uwa vikundi hivi havitajenga amani. Na CCM wakiwa waasisi, ambao wameamua kuvitumia sambamba na polisi kudhuru wananchi wasio na hatia, pale wanapohisi kuwa wamevutiwa na hoja za vyama vya upinzani ndio walengwa namba moja katika hili. Ingekuwa ccm hawatumii Green gurds kuuwa, kuteka, kumwagia tidikai, kuiba kura, kupiga n.k kungekuwa na haja gani ya kuwa na Red brigade? Ingekuwa polisi wanatoa ulinzi na kuhakikisha haki inapatikana kwa wote, kungekuwa wapi na haja ya brigadia hizi?

Saanane usishangae, MWEMA (IGP) Aliwaambia maaskofu na wachungaji waanzishe vikundi vya ulinzi kwenye mihadhara na ibada zao ili kujilinda na wa magaidi. Sembuse CDM yenye malengo mahususi kuchukua madaraka ya nchi? Hii ni kujisahau tu
Nono,

Nimekuelewa sana sana.Tulipiga kelele long time ago hata kabla ya katiba ya mwaka 2006 wakati CUF na CCM wakitunishiana misuli lakini hatukusikilizwa ikabidi nasi kuwa na ulinzi binafsi maana ilionekana order of the day
 
Last edited by a moderator:
Huyu ni mmoja wa maaskofu dhaifu waliopata kutokea nchini hatutaki kuwasema watumishi hawa lkn maadamu kaja acha imnyeshee ajifunze, uchaguzi uliomwingiza madarakani katika Dayosisi ya Dodoma ulileta manunguniko kutokana na uwezo wake kuwa mdogo kulinganisha na washindani wake haswa Mchungaji Mshana ambaye ndiye msaidizi wa Askofu,kinyunyu alipitiswa kwa sababu ya utu uzima wakidhani atakuwa na busara nadhani sasa inabidi walitizame vizuri apishe mtu mwingine kwenye nafasi ile tunataka askofu asiyejifungamanisha na wanasiasa watawalao kwa nguvu ya damu na kuwananga wafuasi wa vyama vingine.
 
Askofu KKKT atahadharisha uanzishwaji vikundi vya ulinzi

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Dodoma, Amon Kinyunyu, amesema kitendo cha viongozi wa vyama vya siasa ya kuamua kujianzishia vikundi vya ulinzi wa kujilinda kwenye vyama vyao, ni ishara tosha ya kuhatarisha amani ya Taifa.

Askofu Kinyunyu amesema viongozi wa siasa wanaoanzisha vikundi vya namna hiyo ni kuashiria jinsi gani walivyokosa heshima kwa Mungu na kwa mamlaka ya serikali ambayo ina ulinzi na usalama unaolinda nchi kwa ujumla.

Alitoa kauli hiyo wakati wa hafla ya uzinduzi wa miradi ya mifumo ya miundombinu ya watoto ikiwamo ya maji, madarasa na vyoo vya kisasa iliyodhaminiwa na shirika la Compassion International Tanzania kwa kushirikiana na washirika wenza kutoka kwenye Makanisa ya Huduma ya Mtoto iliyofanyika katika viwanja vya Kanisa la Tag Miyuji mjini hapa.

Askofu Kinyunyu alisema kitendo cha vyama hivyo kuanzisha vikundi vya kujilinda, ni ishara ya kuleta machafuko ya amani ya nchi.

Pia alisema kitendo hicho kitawafanya vijana waliopo katika vyama hivyo kuendelea kuchukiana badala ya kupendana.

Alisema viongozi wa kisiasa hawana budi kutambua kuwa kwa kuanzisha vikundi hivyo ni kuzidi kujenga uhasama mkubwa utakaoiumiza jamii isiyohusika wakiwamo watoto, wanawake, wazee na walemavu.

“Hapa wanatakiwa kujua kuwa kitendo hicho ni ishara tosha inayoashiria kuanzisha vita ambayo washirika wakubwa ni vijana tunaowategemea kushika madaraka mbalimbali ya kiserikali na ya kisiasa,” alisema.

Askofu Kinyunyu amewataka viongozi wa vyama vya siasa kuheshimu amani iliyopo iliyobarikiwa na Mungu tangu kuumbwa kwa ulimwengu.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Compassion Intenrational Tanzania (CIT) hapa nchini, Mchungaji Joseph Mayala, alisema kitendo hicho ni sasa na uwekezaji kwa vijana wawe na roho ya ukatili badala ya upendo na amani.


Source: Home

NB:

..Askofu Mkuu wa KKKT Malasusa naye ametoa kauli inayoelekea kuwananga CDM.

..soma hapa chini:Home


Wakati wa mlipuko wa bomu Arusha katika kanisa la Olasiti raisi aliwashauri viongozi wa kidini kuweka ulinzi binafsi katika nyumba za ibada.Kwani makampuni bonafsi ya ulinzi ambayo tunayaona yakilinda mabenki na silaha za kivita Askofu hayaoni?Au hayo makampuni sio vikundi vinavyomilikiwa na watu binafsi?Askofu rudi ukajipange na uhakikishe umeisoma katiba ya Jamhuri ya muungano Tanzania,kama unataka kuingia katika siasa karibu lakini kwa dizaini vile unachungulia haipendezi njoo mzima mzima habari ya kuwa vugu vugu Mungu hapendi kama unakuwa moto basi amua kuwa moto
 
Maaskofu wengine ni uchwara! Hata kakobe ni Askofu! Pamoja na ukristu wangu kuna maaskofu wengine ni uchwara sana..hasa wale wanaojiita ASKOFU!
 
Nadhani imefika wakati tuwe straight tuachane na generalization. Hawa ni watu wawili kati ya Maaskofu wengi sana kwa madhehebu ya Tanzania. Tunashindwa nini kutaja majina yao? Kama wangesema huo ni msimamo wa dhehebu lao (ref. Malasusa kama askofu mkuu wa ELCT) basi tungesema maaskofu wa dhehebu so and so. Hii kauli ya kuunganisha watu wote katika chungu kimoja ni ukihiyo wa hali ya juu wa waandishi wetu wa habari.

CC: JokaKuu
 
Mwenye macho haambiwi tazama.

Maaskofu wamenena na kauli za Maaskofu huwa siyo za kukurupuka kama wengine watakavyotaka kuwaaminisha watu hapa.

Maneno ya Maaskofu yanadhihirisha ukweli wa maneno ya Rais, IGP na wapenda amani wengine nchini na kikubwa zaidi, kwa nini kauli ya Maaskofu imekuja baada ya CHADEMA kutoa tamko kuhusu Red brigade.

Kuna kitu wamefunuliwa na Mwenyezi Mungu na kukiona kile kilichoko nyuma ya dhamira za CHADEMA kutaka kuanzisha na kukiimarisha kikundi cha ulinzi.

Maaskofu wametimiza wajibu wao kama Mwenyezi Mungu anavyo waasa wakemee maovu katika jamii kwa nguvu zao zote.

siyo maaskofu wa nchi hii mkuu .
 
Askofu KKKT atahadharisha uanzishwaji vikundi vya ulinzi

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Dodoma, Amon Kinyunyu, amesema kitendo cha viongozi wa vyama vya siasa ya kuamua kujianzishia vikundi vya ulinzi wa kujilinda kwenye vyama vyao, ni ishara tosha ya kuhatarisha amani ya Taifa.

Askofu Kinyunyu amesema viongozi wa siasa wanaoanzisha vikundi vya namna hiyo ni kuashiria jinsi gani walivyokosa heshima kwa Mungu na kwa mamlaka ya serikali ambayo ina ulinzi na usalama unaolinda nchi kwa ujumla.

Alitoa kauli hiyo wakati wa hafla ya uzinduzi wa miradi ya mifumo ya miundombinu ya watoto ikiwamo ya maji, madarasa na vyoo vya kisasa iliyodhaminiwa na shirika la Compassion International Tanzania kwa kushirikiana na washirika wenza kutoka kwenye Makanisa ya Huduma ya Mtoto iliyofanyika katika viwanja vya Kanisa la Tag Miyuji mjini hapa.

Askofu Kinyunyu alisema kitendo cha vyama hivyo kuanzisha vikundi vya kujilinda, ni ishara ya kuleta machafuko ya amani ya nchi.

Pia alisema kitendo hicho kitawafanya vijana waliopo katika vyama hivyo kuendelea kuchukiana badala ya kupendana.

Alisema viongozi wa kisiasa hawana budi kutambua kuwa kwa kuanzisha vikundi hivyo ni kuzidi kujenga uhasama mkubwa utakaoiumiza jamii isiyohusika wakiwamo watoto, wanawake, wazee na walemavu.

“Hapa wanatakiwa kujua kuwa kitendo hicho ni ishara tosha inayoashiria kuanzisha vita ambayo washirika wakubwa ni vijana tunaowategemea kushika madaraka mbalimbali ya kiserikali na ya kisiasa,” alisema.

Askofu Kinyunyu amewataka viongozi wa vyama vya siasa kuheshimu amani iliyopo iliyobarikiwa na Mungu tangu kuumbwa kwa ulimwengu.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Compassion Intenrational Tanzania (CIT) hapa nchini, Mchungaji Joseph Mayala, alisema kitendo hicho ni sasa na uwekezaji kwa vijana wawe na roho ya ukatili badala ya upendo na amani.


Source: Home

NB:

..Askofu Mkuu wa KKKT Malasusa naye ametoa kauli inayoelekea kuwananga CDM.

..soma hapa chini:Home

uaskofu ni wake na mke wake na watoto wake na mawazo yake ni yake na ana haki ya kufanya hivyo lakini cc hatumjui na wala mawazo yake hayana mashiko kabisa yeye anatafuta bahati ya kuteuliwa kama lwakatare
 
hajatamka hata neno moja kuhusu chadema hapo. au mtu akisema vyama vya siasa anamaanisha chadema?
Kwanini aseme wakati huu ambapo CDM imeweka wazi kujilinda baada ya polisi kutowatendea haki.Labda kama ameyasema hayo wakati anasimikwa kuwa askofu tutamsamehe kwa kuwa ndo kwanza anaanza kazi, lakini kama alikuwepo hakuna namna ya kumtenganisha na wanafiki wengine.
 
Mbona hakuna walipotaja chama chochote. Ilivyokaa ni kuwa wanataka ujumbe ufike kwa vyama vyote na sio chama fulani
 
Tatizo la viongozi kama hawa ni UNAFIKI,Hawa ni mafarisayo wanaopenda kuvaa mavazi meupe wakati mioyo yao imekunjana na imeota fungus.Kwa nini mnashindwa kusema ukweli ya kwamba vyama vyote haviruhusiwi kuwa na vikundi vya ulinzi na kwa kuanzia Green Guard ifutwe ili na wengine wanaotaka kuanzisha wasifanye hivo? Mnahofia nini watumishi wa Mungu wakati Yesu aliteswa kwa ajili yetu sote?Mnamwogopa Mungu au Serikali? Siwaelewi hata kidogo! Ni kanisa gani mnaongoza la Mungu au la shetani?
 
Back
Top Bottom