Maaskofu waipinga CHADEMA...

Maaskofu waipinga CHADEMA...

Askofu huyu amelidharirisha kanisa la kilutheri,ni afadhari angeanza kwa kutangaza kwamba yeye ni mwanachama wa chama fulani ningeelewa.
Nijuavyo mimi kiongozi yeyote wa dini anatakiwa kusimamia haki na ukweli na kukemea pale inapobidi lakini akiongozwa na misingi ya haki,mbona hakusema lolote kuhusu mateso wanayoyapata wapinzani pale wanapotendewa isivyo.Lile bomu la Arusha kwenye mkutano wa CHADEMA alisema nini au hiyo siyo uvunjifu wa amani.Sikutegemea kuwa na watu wa aina hii ya wachumia tumbo ktk kanisa kama Lutheran,Nimeamini hizi ni siku za mwisho,na sitashangaa tena kuona makanisa yanapigwa mabomu maana mabomu siyo tatizo, tatizo ni kuunda kikundi cha kujilinda.
 
Kichwa cha habari hii si sahihi..! Askofu hakuipinga CHADEMA pekee ila vyama vyote
vya siasa ikiwepo CCM na CUF. Usiandike kishabiki!!!
 
Siku hizi ndo maana imani watu zimepungua na hii ni kutokana na matamko ya viongozi wao na ndo maana siku hizi ukiwa kiongozi wa dini watu wanachukulia kama hiyo ni ajira yako sawasawa na Mwalimu au mfanyakazi mwingine yeyote Tofauti na Zamani viongozi wa dini walikuwa waadilifu siku hizi madawa ya kulevya yanapitia kwenye mkondo wa taasisi za Dini.
 
Alitakiwa kwenda mbali zaidi ya hapo kama ameamua kuacha altare na kujiingiza kwenye siasa.
Alitakiwa avitaje vikundi kwa majina, vilianza lini, na vinayemtumikia ni nani!.

Ni ukosefu wa umakini kulaumu vikundi vya ulinzi huku akiacha vacuum ya ulinzi katika vyama, wakati anajua wazi yanayotendeka na walinzi rasmi-Polisi.
Huyu alitakiwa aombwe aongelee suala la Mwangosi kwanza, ndipo athubutu kulaani vikundi vya ulinzi.
Hapa ndiyo utajua mipaka ya kazi hizi inamaanisha nini!

kwa maneno kama hayo yatokanayo kwa mtu kama huyo kitakuja kukustajabisha nini unapozisikia habari zao za kutumia vyeo vyao na majumba hayo ya kuabudia kufanya biashara za unga na zile za nyumba za Ngono
 
Yatasemwa mengi kuhusu vikosi hivi, lakini naona wote wanasema tu kama vile kufurahisha genge.
Hakuna mwenye jeuri ya kuzuia vikosi hivi visiwepo hasa Red Brigade ambayo kumbe ipo kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA. Kwanza kutoiunda ni kukiuka katiba ya chama hicho, tena ni muhimu hasa wakati huu ambapo watu washaambiwa WAPIGWE TU.

Baba Askofu, unasemaje kuhusu WAPIGWE TU?
 
hao si ndiyo wanaopokea michango ya Mafisadi , nilishaacha kuwaamini kitambo sana , ni wanafiki mno ! Siku hizi nimeamua kufanya ibada zangu nyumbani , siwezi kushirikiana na watu wa hivi .
 
Alitakiwa kwenda mbali zaidi ya hapo kama ameamua kuacha altare na kujiingiza kwenye siasa.
Alitakiwa avitaje vikundi kwa majina, vilianza lini, na vinayemtumikia ni nani!.

Ni ukosefu wa umakini kulaumu vikundi vya ulinzi huku akiacha vacuum ya ulinzi katika vyama, wakati anajua wazi yanayotendeka na walinzi rasmi-Polisi.
Huyu alitakiwa aombwe aongelee suala la Mwangosi kwanza, ndipo athubutu kulaani vikundi vya ulinzi.
Hapa ndiyo utajua mipaka ya kazi hizi inamaanisha nini!
mbona wao makanisa yalipokuwa yanachomwa waliunda vikundi vya kulinda makanisa.
 
Maaskofu na siasa wapi na wapi jamani?
Wao wachunge kondoo za Bwana wasijepote waulizwe na wakakosa cha kujibu!
 
Kama kweli kuna askofu alietoa kauli hii bas alitoa kauli ya kipu.mbavu.
 
Mwenye macho haambiwi tazama.

Maaskofu wamenena na kauli za Maaskofu huwa siyo za kukurupuka kama wengine watakavyotaka kuwaaminisha watu hapa.

Maneno ya Maaskofu yanadhihirisha ukweli wa maneno ya Rais, IGP na wapenda amani wengine nchini na kikubwa zaidi, kwa nini kauli ya Maaskofu imekuja baada ya CHADEMA kutoa tamko kuhusu Red brigade.

Kuna kitu wamefunuliwa na Mwenyezi Mungu na kukiona kile kilichoko nyuma ya dhamira za CHADEMA kutaka kuanzisha na kukiimarisha kikundi cha ulinzi.

Maaskofu wametimiza wajibu wao kama Mwenyezi Mungu anavyo waasa wakemee maovu katika jamii kwa nguvu zao zote.
 
kwa tafsiri yako vyama vya siasa ni CHADEMA! Basi kazi ipo kwa jumuia ya magamba: lakini kumbuka kuwa waumini wake huyo askofu ndio CHADEMA na red brigade pia.
 
Yatasemwa mengi kuhusu vikosi hivi, lakini naona wote wanasema tu kama vile kufurahisha genge.
Hakuna mwenye jeuri ya kuzuia vikosi hivi visiwepo hasa Red Brigade ambayo kumbe ipo kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA. Kwanza kutoiunda ni kukiuka katiba ya chama hicho, tena ni muhimu hasa wakati huu ambapo watu washaambiwa WAPIGWE TU.

Baba Askofu, unasemaje kuhusu WAPIGWE TU?

Waridi wame-hack account yako nini?Siamimi macho yangu.
 
Hawa ndio maaskofu wetu wa kichina wasio na upeo mbona igp wao aliwaambia waunde kamati za ulinzi na usalama na hatukuongea.
 
Ukisoma biblia utawaona watumishi wa Mungu wa kweli walivyofanya kazi ya Mungu bila upendeleo hata wengine iliwaghalimu maisha yao kwa kuwakosoa watawala pale walipokosea,soma habari za Yohana mbatizaji,Yeremia,Daniel,Yohana aliyeandika kitabu cha ufunuo na wengine wengi,Walisimamia kweli bila kujali cheo au mamlaka ya mtu aliyokuwa nayo bali walipeleka ujumbe wa Mungu kama ulivyo na Mungu aliwatetea kwa uweza wake.
WAKO WAPI WATUMISHI WA NAMNA HII KTK KIZAZI HIKI?
Watumishi wa siku hizi wanaangalia upepo unasemaje wasije wakawaudhi watawala wakawagomea kwenda kwenye harambee za majengo ya ibada.Hii imesababisha heshima za watumishi kushuka na ndo maana wengine wamehusishwa na kashfa za madawa ya kulevya maana tabia ya Ki-Mungu ndani yao haijitokezi nje ili waumini wao waione.
Ni kawaida siku hizi kusikia kiongozi wa dini kafungiwa mlango wa nyumba ya ibada na waumini wake,mara kamwagiwa tindikali, mara kanisa limechomwa moto na mengine mengi,na Mungu hawaadhibu wanaofanya hayo,hii inatokana na nyumba za ibada kupigwa IKABODI(utukufu wa Mungu kuondoka) kwa sababu ya maasi ya makuhani wanaosimama kwenye madhabahu hizo kuwa ndumilakuwili,hawamtumikii Mungu bali wanaangalia nani kasema,anatoa sadaka kiasi gani na hivyo kutoa hukumu zilizopotoka.Viongozi wa dini wajitafakari upya na kuchagua kumtumikia Mungu au mamoni.
 
Askofu hakutaja chama chochote tusimlaumu. Ila ni vema akafanya utafiti kwanini vikundi hivi vinaanzishwa? Jeshi la polisi ambao wajibu wao ni kulinda usalama wa raia wameshindwa kutimiza wajibu wao? Je ni kinyume cha sheria mtu au kikundi au taasisi yoyote kujilinda? Ni dhambi kujinda? Hayo ndiyo tunahitaji kufahamu watanzania.
 
Askofu ni Askofu, anatakiwa kuhubiri habari za Mungu.

CHADEMA ni CHADEMA, jukumu lao ni kuhakikisha watanzania wanakombolewa kutoka kwenye utumwa wa serikali ya ccm
 
Hicho kikundi kipo.kwenye katiba ya Chadema.Viongozi wa dini wafanye tafiti badala ya kupotosha waumini wao

Mimi naona tamko la Askofu ni sawa kabisa, na hakuna mahali anakoishutumu CDM. Ujumbe hapa ni uwa vikundi hivi havitajenga amani. Na CCM wakiwa waasisi, ambao wameamua kuvitumia sambamba na polisi kudhuru wananchi wasio na hatia, pale wanapohisi kuwa wamevutiwa na hoja za vyama vya upinzani ndio walengwa namba moja katika hili. Ingekuwa ccm hawatumii Green gurds kuuwa, kuteka, kumwagia tidikai, kuiba kura, kupiga n.k kungekuwa na haja gani ya kuwa na Red brigade? Ingekuwa polisi wanatoa ulinzi na kuhakikisha haki inapatikana kwa wote, kungekuwa wapi na haja ya brigadia hizi?

Saanane usishangae, MWEMA (IGP) Aliwaambia maaskofu na wachungaji waanzishe vikundi vya ulinzi kwenye mihadhara na ibada zao ili kujilinda na wa magaidi. Sembuse CDM yenye malengo mahususi kuchukua madaraka ya nchi? Hii ni kujisahau tu
 
comments za hii thread zinadhihirisha wazi kuwa chadema sio chama cha kidini.
Ingekuwa arusha hili kanisa lake lingekosa sadaka wikiendi hii mpaka askofu aachane na kauli za kimagamba
 
Back
Top Bottom