Maandishi ya mwisho ya Ben Saanane

Maandishi ya mwisho ya Ben Saanane

Mpuuzi wa mwisho kabisa wewe, wewe ni nani? Umewahi kumuumba hata binadamu mmoja? Unajua value ya ubinadamu wewe? Angalia yupo Mungu aliyetuumba sote, asije akakupindua kichwa chini miguu juu kama anavyompindua Makonda leo, kila unalolifanya liwe baya liwe zuri malipo ni hapa hapa, what goes around comes around ndugu.
Wewe pamoja na Huyo Mungu unayemwamini mnahitaji ushauri wa kisaikolojia.

Unaposema what goes around comes around ina maana Ben alikuwa ni mtakatifu? Vipi kama yaliyomtokea ndio comes around take?.....unauhakika gani alipatwa na baya?
 
Jamani we are talking about someone's life. A human being Siyo mbwa paka au panya. A human being. God's creation kwa mfano wake. Tuwe waangalifu sana maana we are touching God Himself. Haya shauri zenu
Tunaweza kuongea hata kwa karne nzima na Ben asionekane tena.........Tukubaliane na hali iliyopo.
 
Kuna nchi za wenzetu waliostaarabika, China,Marekani,Uingereza, Israel, Japan n.k. akipotea raia mmoja tu wako tayari kuingia gharama yoyote hata kama ni kwenda vitani ili kutetea uhai/utu wa raia huyo bila kujali ni wa chama Twawala au Pinzani!!!
The Bible says that One Soul is equivalency to 10,000 worlds.
Then unaweza ukaona jinsi nafsi moja ya bin-adamu ilivyo na thamani!!! Halafu jitu moja kutoka CCM linapuuza na kukebei kupotea kwa Ben Saanane! Huo ni wendawazimu...........!
Acha urongo mkuu huko marekani watu wanapotea kila siku na wengine kufariki kila uchao mbona hatuoni ayo maandamano? Ata ivo naamini ben yupo safe na anaendelea na shughuli zake za kila siku amechoka na usanii wa Chadema ameamua kusepa ki aina amemfuata Dr. Canada.
 
Wewe pamoja na Huyo Mungu unayemwamini mnahitaji ushauri wa kisaikolojia.

Unaposema what goes around comes around ina maana Ben alikuwa ni mtakatifu? Vipi kama yaliyomtokea ndio comes around take?.....unauhakika gani alipatwa na baya?
Watu hawamuoni muda mrefu umepita halafu unatoa kauli za kejeli, angalia ndugu yangu yasije yakakurudia ukajutia mdomo wako, waswahili wanasema mdomo unaponza.
 
Watu hawamuoni muda mrefu umepita halafu unatoa kauli za kejeli, angalia ndugu yangu yasije yakakurudia ukajutia mdomo wako, waswahili wanasema mdomo unaponza.
Kama mngekuwa na nia ya dhati ta kumtafuta Ben au kushurutisha mamlaka husika zimtafute Ben, basi mngeitisha maandamano na migomo ya kutosha hadi Ben apatikane na sii kubwabwaja maneno nyuma ya keyboard.
 
Kama mngekuwa na nia ya dhati ta kumtafuta Ben au kushurutisha mamlaka husika zimtafute Ben, basi mngeitisha maandamano na migomo ya kutosha hadi Ben apatikane na sii kubwabwaja maneno nyuma ya keyboard.
Hakuna anayebwabwaja hapa
 
Hebu acheni kutumalizia MB zetu kizembezembe
Wewe ni Nani.....
Na kwa nini unauliza humu JF
Jalada lake limefunguliwa Police, hivi umewauliza wamefikia wapi......!!!????
Kwa nini hukumtafuta Baba yake ambaye aliisha Ripoti Police, au umesahau kwamba Baba yake alimsihi Mbowe aseme aliko mwanae. Wewe kimekushinda kipi kwenda kuulizia Mrejesho wa Baba na Familia kwa ujumla?...( Maana Baba MTU huenda aliisha nong'onezwa akatulia tuliiiii...ajabu Wewe na ushakunaku wako unakuja kujaza server ya JF bure)
Anyway, kama huifahamu familia Ina maana hata Mbowe huwezi kumpata maana yeye anasema tukae kimya ili watesi wake wasije kuamua kumdhuru, sasa kamuulize amefikia wapi..!? au bado anakula fungate na Wema Sepetu!??
Ukiona tabu huko kamuulize yule Binti Mwenzi wake alietuambia mwanzoni kwamba Mr. yuko kwenye mission maalum wapi sijui but atarudi, yaani yule atasema kama ile mission imekamilka au imeongezewa Muda au wako ndani ndani wanatii kiu kwa raha zao au VP?
Wote hao hawasumbuki na Ben, mpaka yule Binti...ajabu wewe na kiherehere chako ndio unajiulizisha au wewe ni...
Aaaah maana jina lako nalo linaacha maswala ,Mombasa kunasifa yake yakhe...!
huna adabu
 
Je unahisi haina la maana? Au kwa kuwa hakuwa akikuhusu kwa lolote lile, utajua kuwa kupotea kwake kuna maana iwapo angepotea MTU wa muhimu kwenye familia yako, anaweza kwako lisiwe la maana lakini kwa watu wengine lina maana kubwa sana.
hivi umekula maharage ya wapi? mimi nimesema kupotea kwake sio kwa maana???? usichanganye mada, mimi nilizungumzia huyo aliyeleta hilo andiko at this moment ana nia gani???? kwa maswali zaidi wasiliana na polisi ili uwape taarifa ulizonazo kuhusu jambo hilo. bye.
 
huna adabu
The teh teh teh.
Anyway, nilikuwa natania kwenye sentence yangu ya mwisho, nashukuru kwa kuelewa hilo. Sasa naomba majibu kwa hoja zangu
1. Mbowe anasemaje/anashughulikia VP suala LA kutoweka huyo Dogo
2. Kwa nini Mzazi wa Dogo alimtaka Mbowe aseme alipo mwanae
3. Yule Binti anayedaiwa kuwa Mwenzi wake alitutangazia kupitia Facebook, kwamba Dogo yuko kwenye Mission na atarudi, sasa atuambie kulikoni?
4. Suala hili liko Police, wamefikia wapi na upelelezi
Lengo ukweli ujulikane yu hai, au kafariki/kauawa, katekwa, kajificha/kafichwa au nini kilichompata na kinanani ni wahusika. Baada ya kujua alichoafanyiwa na kuwajua waliomfanyia ndio tutaanza kutafuta sababu.
Ujue tunaweza kusumbuka na Post zake, kumbe alikamatwa ugoni MTU akammaliza akafuta ushahidi, au labda alichukuliwa Msukule basi twende kwa Mchungaji Gwajima....
 
Limeibuka kundi kubwa kutoka Chama Tawala linashambulia wanaomtaka Mhe.Magufuli ahakiki vyeti vyake.

Beatrice Condrad umejenga hoja vizuri. Sitakushambulia au sitakujibu.Nina sababu maalum.Na unajua....!

Ila tu nitahadharishe tu wale viongozi na makada wa CCM na baadhi ya Watendaji serikalini waliosimamia ajenda yako ya kumshambulia James Mbatia kwa kuwa ameunga mkono hoja ya kumtaka pia Rais Ongoze Uhakiki wa Vyeti.

Ni jambo la Ajabu watu wanamtaka Mbunge aongoze zoezi la Uhakiki wa Vyeti wakati kuna Rais ambae alikua kinara katika Kufanya usafi,Kinara wa kuhakiki Silaha,Tulipomkomalia suala la kodi alijitokeza ikatangazwa Bungeni nae atalipa kodi,tulipotangaza hili suala la mishahara liangaliwe haraka sana Rais akatangaza Mshahara wake umepunguzwa(Hajatoa hadharani vielelezo kama alivyoahidi,Pengine hakusema ukweli). Huko alilenga kuonesha yeye kuwa ni mtu wa mfano.Hakuna waliomtaka mbunge aongoze na kuwa mstari wa mbele badala ya Rais.

Inashangaza sasa leo mnataka kuleta Falsafa au itifaki(Protocal) ya Bata Kutanguliza watoto Mbele au Falsafa ya Mbuni kufukia kichwa Mchangani akabiliwapo na hatari akidhani eti anajificha adui asimuone wakati mwili wote uko nje.

Iweje suala la Uhakiki wa Vyeti aliloasisi Rais Magufuli na kulisemea kwa ukali sana sambamba na kuonesha kuchukia Vilaza anarudi nyuma na badala yake alipopata fursa ya kufafanua PhD yake iliyowatia watu mashaka yeye akaitumia fursa hiyo kuongoza rhumba la ngoma za asili pale chuo kikuu cha Dar Es Salaam? Jana alikwepa kabisa suala la uhakiki wa vyeti.Kwani yeye hajipendi?Jitihada zake jana zinazidisha mashaka zaidi.

Mbona Waziri Mwigulu Nchemba alitoa Ufafanuzi? Caesar's wife must not be accused.

Tunataka watu watoke na ufafanuzi wa Uongo halafu tuwavue nguo kwa nyaraka.Maana tunajua hawana utetezi zaidi ya kuingia kwenye mapishi.Fabrications!

Sasa eti Mbatia ambaye anapaza sauti kutaka zoezi la uhakiki liwe kwa wote na Rais awe kinara wa Uhakiki watu mnataka yeye aongoze uhakiki halafu Rais aongoze Ngoma za utamaduni na kuja kuhakiki baadae au asihakiki kabisa?

Hii tabia ya kuokoteza tuhuma ili kuondoa watu kwenye mjadala haitamnusuru Raia namba moja katika kadhia hii.

Kuna kiongozi nilimuonya juzi hapa akae kimya asubiri zamu yake maana tupo ngazi za juu zaidi kiitifaki kwenye taaluma na uongozi katika suala hili la uhakiki.

Unaweza kuta katika picha hii hapa chini kwa mfano kuna mtu mmoja anajifanya hatujui historia yake na suala hili la uhakiki anajaribu kupambana ili kufifisha mjadala na Rais Magufuli asiongoze uhakiki kwa kuwa anajua itifaki ikizingatiwa wakifika kwa wakuu wa mikoa yeye hatapona.

Wakati Wenzake walikua wanasoma yeye zake ilikua usingizi tu.

Kwa utaratibu wake huu chuoni kama inavyooonekana pichani Kwanini usisome kozi ya miaka 3 kwa muda unaolingana na muda wa Mwanafunzi wa Shule ya Msingi kuanza La kwanza hadi kuhitimu ?

Utakuta mtu kama huyo alikua akikurupuka hapo usingizini anaenda mjini kushughulikia Usajili wa Chama kipya cha CCJ.

Kwanini SUP zisimuhusu?
Unadhani atafurahia zoezi hili la Uhakiki wa Vyeti lianzie kwa Rais kisha liende kwa Wateule wake? Ataponea wapi huyu?

Ana haki ya kushambulia yeyote anayeongelea suala la Rais kuhakiki vyeti vyake.

Hao wanaokomaa kusoma hapo Pembeni (Pichani) huko walipo kwa sasa ni Mungu anajua.

Ila naendelea kuonya kila mtu anayeibuka kutushambulia na kutetea PhD ya Mhe.Magufuli ajikague kwanza .

Hatutaki lawama baadae kuwa kuna mtu amedhalilishwa. Mtetee kwa hasara zako mwenyewe .At your own risk !

Please don't cheapen this post or entire debate by your sophomoric criticism,entitled as you may be .

Cheers..... But ,

[HASHTAG]#MagufuliHakikiPhDyako[/HASHTAG]

[HASHTAG]#MagufuliVerifyYourPhD[/HASHTAG].

A Luta Continua,Victory Ascerta.....!

Ben Saanane
 
Mmmhh..kama ndo ujumbe huyo ndo ulikuwa wa mwisho, tayari kuna ukakasi na kupotea kwa saanane!
 
....very possible post hii ya Ben iliyojibiwa na Kitila ndio iliyofanya kitila kupewa shavu la uwaziri...na pia labda ndio sababu ya prof. Maboko kupewa shavu Tacaids....just thinking loud....serikali hii ya kimagumashi kila anayepewa shavu kuna sababu....ukiondoa of course vigezo vya kitaaluma..

Maandishi ya Ben Saanane



Mwisho wa kumnukuu

Je, huenda post hii ndio ilikuwa sababu ya kutoonekana kwake hadi leo?
 
kuna siku watu fulani huwa wanakurupuka....oh Ben kapotea kapotea

saa hizi wanakula nyama na familia zao

wakikamatwa na issues zao fulani, wanamtumia Ben kama mtaji

Come Back Ben, we miss you
 
Back
Top Bottom