Maandishi ya mwisho ya Ben Saanane

Maandishi ya mwisho ya Ben Saanane

Jamani mbona binadamu tumekuwa kama wanyama.Hata wanyama wana afadhali.Binadamu unashabikia kupotea kwa mwana wa mwenzio?Ama kweli mungu yupo .Kila mtoa kejeli mungu atamlipa kadri ya uwezo wake.Tuheshimu uhai wa binadamu wenzetu.
 
uchambuzi wa ben saanane una ibua maswali ya msingi kabisa kwa msomi yeyote asiye na mapenzi binafsi na mkuu
 
[HASHTAG]#tunamtaka[/HASHTAG] Ben.## hivi amepotea kabisa? Mola anawaona walotenda hayo.
 
Jamani mbona binadamu tumekuwa kama wanyama.Hata wanyama wana afadhali.Binadamu unashabikia kupotea kwa mwana wa mwenzio?Ama kweli mungu yupo .Kila mtoa kejeli mungu atamlipa kadri ya uwezo wake.Tuheshimu uhai wa binadamu wenzetu.
Hajapotea huyu. Tatizo la wanasiasa wetu ndiyo hili, vijana wanajitolea kuwapigia filimbi lakini wanawatelekeza. Wana CHADEMA hawana muda na mtu mfu ama aliyepotea sasa tunashughulikia kumsafisha Mungu wetu Mbowe na kumchafua Makonda, huenda Mungu si athumani Makonda akaamua kuja kuongeza nguvu CHADEMA kama Lowasa.
 
Kuanzia nilipoibua mjadala wa Uhalali wa Phd ya Mhe.Magufuli niliacha rasmi kumu-address kama Dr.Magufuli na kutumia Ndugu au Mheshimiwa tu hadi itakapothibitika ni Halali.

Nimesoma Hoja ya Prof.Kitila kuhusu PhD ya Magufuli.

Prof.Kitila ni Rafiki yangu sana.Yeye ni kaka yangu na ananichukulia kama mdogo wake.

Katika Kuchangia Mjadala wa PhD ameandika "UDSM hakuna namna mtu kupata Cheti Fake na huwa hatuangalii sura ya Mtu...". Kwa hiyo. .. "PhD ya Magufuli haina kasoro".

Vilevile kuna watu Mwanzo walisema masuala ya Machapisho hayana maana lakini cha ajabu wameweka waliyoita Machapisho ya Magufuli na pia kuweka Picha akiwa amevaa mavazi ya Graduation kama vile ndio Authentificatio
n ya PhD ya Magufuli.

Wengine wakaanza kusema Rombo ina matatizo hivyo niachane na PhD ya Magufuli.Utadhani kuhoji uhalali wa PhD ya Magufuli ndio kumeleta madhara Rombo.Wasomi wetu wengine wakoje?

Nataka kugusia hoja ya Prof.Kitila kuhusu kuwa hakuna namna ya kufanya Udanganyifu UDSM .

1-Prof.Kitila anaweza kuwa Mwaadilifu sana katika kusimamia taaluma na kazi yake kama Mhadhiri Chuoni.

Lakini ni kosa kubwa ku-assume kila mtu ni mwadilifu.

Tukienda hivyo tutaua nchi na ndio maana wengine tunasizitiza sana Kuimarisha Taasisi zetu na mifumo.

Hapo ni kama vile ku-assume kuwa kila mtu ni mpigaji.Hivyo tunasizitiza haja ya kuimarisha taasisi na mifumo ambayo itadhibiti mafisadi na watu wasio waadilifu baadala ya ku-assume kila mtu ni mtakatifu .

Kama watu waliweza ku-forge documents Serikalini na Kuchota Fedha Za EPA au ESCROW ni mechanism gani itakayozuia PhD za Mbeleko vyuoni kwetu hasa zinazohusu wanasiasa?

Tena katika mazingira yanayoashiria mbeleko kwa Mbebaji kumshusha aliyembeba nae akambeba kwa kumteua kushika ujumbe wa Bodi?

2-Kama Seif-Al Islam Mtoto wa Ghaddafi alikuja kuibuliwa kwa kashfa ya kuhonga na kupata PhD ya mbeleko Kule London School of Economics(LSE) sass UDSM ina mfumo gani thabiti wa kuepuka fraud kuliko LSE?

Kwa Mujibu wa Academic Perfomance Center chuo kikuu cha London School of Economics kilishika nafasi ya pili kwa miaka kadhaa mfululizo kwa ubora duniani wakati UDSM ikishika nafasi ya 1618 kati ya Vyuo 2,000.

LSE iko vizuri kiteknolojia na kitaaluma katika kuzuia academic Misconduct kuliko UDSM lakini bado Seif Al-Islam alifanya.

3-UDSM imewahi kukumbwa na staff waliofanya Udanganyifu kwenye taaluma na Prof.Maboko aliwahi kuutangazia Umma.

UDSM hii hii imeshawahi kutoa wanafunzi waliofanya udanganyifu na baadhi yao kuvuliwa Degree zao.

Charles I . Ng'imba aliwahi kuvuliwa Digrii yake aliyoipata kwenye Graduation ya Tarehe 29 August ,1987.

Unasema haiwezekani?
4-Kuna hao walioleta machapisho waliodai ni Ya Magufuli na kudai kuwa alistahili PhD kwa sababu alishaandika tangu 2003.

Tena nimeona ameshirikiana baadhi na huyo Supervisor wake.
Sasa watuambie alifanya PhD by Publication?

Sweden ,Australia na hata Uholanzi(Najua Unafahamu) inaruhusiwa PhD by Publication.

Kwa faida ya mjadala tu: Ni kuwa PhD by Publication zinakusanywa paper zote na kuziandikia Covering Essay na jumla na paper iwe na maneno si chini ya 20,000 ikiwa condition na masharti mengine ya submission yapo constant.

Pia inazingatiwa ni paper ngapi umeandika mwenyewe na ni ngapi umeshirikiana(Co-Author).

Na katika kushirikiana ni ipi jina lako limekua la kwanza maana inabeba uzito wa synopsis.

Sasa Katika hizo Paper alizoweka the so called (Dr.!?) Chahali ni Tatu tu anazooneshwa kaandika yeye na zipo kwenye vijarida vya uchochoroni tu sio kwenye respectable Journals huko.

So swali la PhD Candidate huyu kuipata PhD kwa miaka 3 akiwa Part time Candidate kinyume na Prospectus halijajibiwa.

Ingawa Prof.Kitila umetoa maoni yako tu kama mchangiaji na Sio Authority ya UDSM au Supervisor wake(Ofcourse hawezi kujitokeza tena maana ni mteule wa Bodi) lakini naheshimu maoni yako uliyotoa kistaarabu bila matusi kama hao waliomtetea kwa vitisho na matusi kwa hoja zao za kula nae Canteen au kumuona amevaa vazi la graduation.

UDSM kama vilivyo vyuo vingine au taasisi nyingine nchini haina kinga thabiti dhidi ya Academic Fraud hasa zinazohusisha wanasiasa na vigogo serikalini.Hiyo hoja haijaleta uzito wa kutosha katika authentification ya PhD ya Mkuu wetu.

Tena nilicheka sana nilivyo-imagine jinsi kazi ya Literature Review ya Mkuu wetu ingefanana. With knowledge that Examiners may tolerate grammer idiosyncratic than any other mess.Sijui Lugha na VIVA ilikuaje. Don't joke! Ile lugha yake ile ...! Haya!

Hoja ya Prof.Buchweshwaija kuwa co-author kwenye paper yake kisha kuja kuwa Supervisor wake na kisha kuja kuwa mteuliwa wa Waziri aliyeteuliwa na yeye mwanafunzi wake tunaweza kuli-debate left-right-center hasa tunapoangalia mfumo wetu wa elimu na uadilifu.

Ofcourse nakiri kuwa wakati wa kuanza PhD yangu niliwahi kukuambia nilipata headache sana kuhakikisha kuwa napata Supervisor maahiri ndani yawanakamati.Maana uliwahi kufanya mchakato wa kujiunga na chuo hicho kabla hujajiunga Southampton University kwa PhD yako.

I knew as PhD candidate,Institution'll gain through my presence by gaining credibility,profile and funding. Why should I allow them to treat me as an inconvinient ,Incompetent fool? Si lazima nami niwe smart kujilinda?

So kwa Case ya Magufuli na SUP wake twaweza kui-debate kweli kuanzia co-authorship.

Sijui independence ya Mwanafunzi huyo ilikuaje hata kama ilikua ni Ph.D by Publication.

Ni vyema tu akajitokeza kutoa ufafanuzi au Chuo .Mbona lile la silaha alipohakiki hadi watu wengine walikua proud kuiweka picha yake na bastola kama Profile ya groups za Watsap?

Mwisho wa kumnukuu

Je, huenda post hii ndio ilikuwa sababu ya kutoonekana kwake hadi leo?
Kwa hiyo na wewe una maana gani kuendelea kusambaza hii post ambayo haina la maana??? Malengo yako ni nini? Wewe sio mtu mzuri kwa Taifa la Tanzania. Haaayaaaaa..............
 
[HASHTAG]#BringBackOurBen[/HASHTAG] vs [HASHTAG]#WelcomeMadamSepenga[/HASHTAG]
 
Kama kuna mtu rais alistahili kumpoteza basi ingekua kipanya, umeona anavyo mchora magu na kidevu chake?
 
Tatizo ushabiki umezidi
kabisa. napata shida sana kila nikipiga picha PhD kwa papers kwa miaka mitatu na paper hizo hazijachapishwa mahala pa kueleweka na kukubalika. ina maana ni rahisi kiasi hicho kupata PhD chuo kikuu cha Dar es Salaam? yani baada ya kusoma hii hoja ya saanane naanza kupata wasiwasi mkubwa sana na PhD ya huyu mkuu. nataka nifuatilie kwa undani kabisa hili suala nami angalau nijiridhishe. na kipindi hicho chote huyu bwana alikua ofisini full time kama waziri plus shughuli za ubunge. hii inaweza kuchochea wasiwasi zaidi. 3 yrs kwa mtu wa aina yake?? big NO
 
kabisa. napata shida sana kila nikipiga picha PhD kwa papers kwa miaka mitatu na paper hizo hazijachapishwa mahala pa kueleweka na kukubalika. ina maana ni rahisi kiasi hicho kupata PhD chuo kikuu cha Dar es Salaam? yani baada ya kusoma hii hoja ya saanane naanza kupata wasiwasi mkubwa sana na PhD ya huyu mkuu. nataka nifuatilie kwa undani kabisa hili suala nami angalau nijiridhishe. na kipindi hicho chote huyu bwana alikua ofisini full time kama waziri plus shughuli za ubunge. hii inaweza kuchochea wasiwasi zaidi. 3 yrs kwa mtu wa aina yake?? big NO
maswali ni mengi ila majibu hakuna
 
Kwa hiyo na wewe una maana gani kuendelea kusambaza hii post ambayo haina la maana??? Malengo yako ni nini? Wewe sio mtu mzuri kwa Taifa la Tanzania. Haaayaaaaa..............
wewe unawakilisha kundi la watu dhaifu kifikra hadi kimatendo. shame on you
 
Mwisho wa kumnukuu

Je, huenda post hii ndio ilikuwa sababu ya kutoonekana kwake hadi leo?
Hebu acheni kutumalizia MB zetu kizembezembe
Wewe ni Nani.....
Na kwa nini unauliza humu JF
Jalada lake limefunguliwa Police, hivi umewauliza wamefikia wapi......!!!????
Kwa nini hukumtafuta Baba yake ambaye aliisha Ripoti Police, au umesahau kwamba Baba yake alimsihi Mbowe aseme aliko mwanae. Wewe kimekushinda kipi kwenda kuulizia Mrejesho wa Baba na Familia kwa ujumla?...( Maana Baba MTU huenda aliisha nong'onezwa akatulia tuliiiii...ajabu Wewe na ushakunaku wako unakuja kujaza server ya JF bure)
Anyway, kama huifahamu familia Ina maana hata Mbowe huwezi kumpata maana yeye anasema tukae kimya ili watesi wake wasije kuamua kumdhuru, sasa kamuulize amefikia wapi..!? au bado anakula fungate na Wema Sepetu!??
Ukiona tabu huko kamuulize yule Binti Mwenzi wake alietuambia mwanzoni kwamba Mr. yuko kwenye mission maalum wapi sijui but atarudi, yaani yule atasema kama ile mission imekamilka au imeongezewa Muda au wako ndani ndani wanatii kiu kwa raha zao au VP?
Wote hao hawasumbuki na Ben, mpaka yule Binti...ajabu wewe na kiherehere chako ndio unajiulizisha au wewe ni...
Aaaah maana jina lako nalo linaacha maswala ,Mombasa kunasifa yake yakhe...!
 
Muulize mchumba ake aliyetuambia kuwa anajua alipo!
 
Back
Top Bottom