Utakuwa hujanielewa nilichoongea.
Sijaongelea kuhusu JPM kama ni Rais anayependwa na wananchi wake au laa.
Nilichojaribu kueleza ni kuwa siyo hiari ya Rais aliyeko madarakani kutawala kwa kuitii Katiba, bali ni wajibu wake kwa asilimia 100, kwa kuwa Kabla hajaingia madarakani aliapishwa pale uwanja wa Taifa tarehe 5/11 /2015 na akakiri mwenyewe kwa kinywa chake kuwa ataitii na kuilinda Katiba ya nchi yetu.
Vitendo vyake vya kuisigina Katiba ya nchi waziwazi, vinatufanya waTz hivi sasa tuikumbuke sana hotuba ya hekima ya hali ya juu aliyoitoa Baba wa Taifa hili Mwalimu Nyerere, mwaka 1995, wakati aliposema kuwa Rais tunayemchagua ni lazima aitii na kuilinda Katiba ya nchi yetu aliyoapa kuilinda, Mwalimu aliendelea kusema kwenye hotuba hiyo kwa msisitizo mkubwa kuwa Rais asiyetaka kuitii Katiba ya nchi yetu Rais wa aina hiyo HATUFAI.........