Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,186
- 10,922
Maandamano ya kumtaka Benjamin Netanyahu aachie madaraka na uchaguzi uitishwe yameiingia hatua ya juu leo pale waandamanaji kwenye mitaa tofauti ya Tel Aviv kuziba njia kuu za usafiri.
Hata hivyo Netanyahu pekee ndiye amekuwa na tamaa ya fisi ya kuishinda Hamas ambapo ametoa amri ya jeshi lake kuingia Rafah japo kumekuwa na makelele kutoka kila upande kumtaka asishambulie eneo hilo kwa hofu ya kusababisha vifo vingi na wengine wakiona anaweza akatibua hali ya vita kuwa vibaya zaidi.
Generali mstaafu wa jeshi la anga la Jordan kwa upande wake amelitahadharisha jeshi la Israel juu ya uwezekano wa kupata hasara kubwa kwa jeshi lake na kwa wananchi bila kupata mafanikio ya kuwafuta Hamas.Katika tamko lake generali huyo amesema mahandaki yamejaa Gaza yote lakini yale ya Rafah yametengenezwa kwa utaalamu zaidi na si rahisi kuyapenya.
Habari nyengine ni taarifa iliyotolewa na kikosi cha Islamic Jihadi ambacho kimerusha kwenye chaneli yao ya telegramu wakidai siku ya leo wamepiga kikundi cha askari wa IDF maeneo ya kambi ya wakimbizi ya Al maghazi iliyopo katikati ya Ghaza
kutokea kwa shambulio hilo kubwa eneo ambalo Israel imeshapita na kutangaza ushindi pamoja na tahadhari ya generali mstaafu wa Jordan na ukimya wa Misri kuelekea utekelezwaji wa amri ya kushambulia Rafah kunatoa picha kuwa kuna kipigo kikubwa kitatokea kwa jeshi la Israel na ambalo ndilo litakalomaliza vita na kumuondoa Netanyahu madarakani.
Hata hivyo Netanyahu pekee ndiye amekuwa na tamaa ya fisi ya kuishinda Hamas ambapo ametoa amri ya jeshi lake kuingia Rafah japo kumekuwa na makelele kutoka kila upande kumtaka asishambulie eneo hilo kwa hofu ya kusababisha vifo vingi na wengine wakiona anaweza akatibua hali ya vita kuwa vibaya zaidi.
Generali mstaafu wa jeshi la anga la Jordan kwa upande wake amelitahadharisha jeshi la Israel juu ya uwezekano wa kupata hasara kubwa kwa jeshi lake na kwa wananchi bila kupata mafanikio ya kuwafuta Hamas.Katika tamko lake generali huyo amesema mahandaki yamejaa Gaza yote lakini yale ya Rafah yametengenezwa kwa utaalamu zaidi na si rahisi kuyapenya.
Habari nyengine ni taarifa iliyotolewa na kikosi cha Islamic Jihadi ambacho kimerusha kwenye chaneli yao ya telegramu wakidai siku ya leo wamepiga kikundi cha askari wa IDF maeneo ya kambi ya wakimbizi ya Al maghazi iliyopo katikati ya Ghaza
kutokea kwa shambulio hilo kubwa eneo ambalo Israel imeshapita na kutangaza ushindi pamoja na tahadhari ya generali mstaafu wa Jordan na ukimya wa Misri kuelekea utekelezwaji wa amri ya kushambulia Rafah kunatoa picha kuwa kuna kipigo kikubwa kitatokea kwa jeshi la Israel na ambalo ndilo litakalomaliza vita na kumuondoa Netanyahu madarakani.