Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,183
- 10,913
Ili kubadili mwelekeo wa Marekani dhidi ya Israel washawishi wa kiyahudi Marekani wamepeleka kikundi cha wajumbe wa Congress mjini Jerusalem kuzungumza na waziri mkuu wa nchi hiyo,Benjamin Netanyahu.
Katika mazungumzo hayo Netanyahu amewambia wajumbe hao kuwa ushindi wa Israel huko Gaza umebaki wiki kama tatu tu mbele na utapatikana kwa kuingiza vikosi vya IDF eneo la Rafah ili kuwapta viongozi wa Hamas.
Akawaambia wajumbe hao kwamba jeshi la Israel tayari limeshamuua Hamas namba 3 na namba 4 kati ya 10.Karibuni hivi itawaua namba 2 na moja.
Kwa kutamka hayo ni wazi kuwa Netanyahu anaweweseka kutokana na ugumu wa kupigana na Hamas na amesahau kuwa malengo ya uvamizi wake kwa Gaza ilikuwa ni kuwarudisha mateka nyumbani na kuwamaliza Hamas wote eneo hili.
Kuua namba moja mpaka kumi ya Hamas haikuwa miongoni mwa malengo makuu na kwamba kuua viongozi hao hakutamaliza Hamas na wala si mara ya mwanzo katika historia ya vita vyake na makundi kama hayo huko nyuma ambapo haikuwezekana kuwamaliza kabisa.
Wafuatiliaji wa mienendo ya kivita wanaamini kuwa viongozi hao wa Hamas hawapo wote Rafah na kwamba wameshatawanyikia maeneo mengine ya Gaza kama walivyopenya wapiganaji kadhaa kutoka kusini na kuingia maeneo tofauti ya jimbo hilo ambayo Israel ilikwishachoka kuyapiga na kuondoka.
Hali hiyo inafanya vita hivyo visiwe na ratiba ya kumalizika kwa wiki au miezi ya karibuni ijayo.
Silaha pekee ya matumaini anayotumia Israel kwa sasa ni kutumia chakula kama silaha ya kivita lakini kwa silaha haijawezekana kuwasambaratisha wapiganaji hao.
Katika mazungumzo hayo Netanyahu amewambia wajumbe hao kuwa ushindi wa Israel huko Gaza umebaki wiki kama tatu tu mbele na utapatikana kwa kuingiza vikosi vya IDF eneo la Rafah ili kuwapta viongozi wa Hamas.
Akawaambia wajumbe hao kwamba jeshi la Israel tayari limeshamuua Hamas namba 3 na namba 4 kati ya 10.Karibuni hivi itawaua namba 2 na moja.
Kwa kutamka hayo ni wazi kuwa Netanyahu anaweweseka kutokana na ugumu wa kupigana na Hamas na amesahau kuwa malengo ya uvamizi wake kwa Gaza ilikuwa ni kuwarudisha mateka nyumbani na kuwamaliza Hamas wote eneo hili.
Kuua namba moja mpaka kumi ya Hamas haikuwa miongoni mwa malengo makuu na kwamba kuua viongozi hao hakutamaliza Hamas na wala si mara ya mwanzo katika historia ya vita vyake na makundi kama hayo huko nyuma ambapo haikuwezekana kuwamaliza kabisa.
Wafuatiliaji wa mienendo ya kivita wanaamini kuwa viongozi hao wa Hamas hawapo wote Rafah na kwamba wameshatawanyikia maeneo mengine ya Gaza kama walivyopenya wapiganaji kadhaa kutoka kusini na kuingia maeneo tofauti ya jimbo hilo ambayo Israel ilikwishachoka kuyapiga na kuondoka.
Hali hiyo inafanya vita hivyo visiwe na ratiba ya kumalizika kwa wiki au miezi ya karibuni ijayo.
Silaha pekee ya matumaini anayotumia Israel kwa sasa ni kutumia chakula kama silaha ya kivita lakini kwa silaha haijawezekana kuwasambaratisha wapiganaji hao.