Maandamano ya Chadema yatishia Serikali ya CCM madarakani

Mzee tulia kama huna cha kuandika ni bora ulale unaita wanasiasa dhaifu? Huna akili kabisa inaonekana huna hata elimu we kaumza
 
Ndugu zangu wanachadema, ni ukweli usiyofichika kwa sasa, serikali iliyoko madarakani(C**) imepagawa, haijui nini ifanye na wapi ikimbilie, hakika imeshikwa pabaya, hali ni tete. Kwa kuwa hala hala mti na ……………, na pia kifo cha nyani yawezekana akakurukia hata usoni
Nina angalizo kwa haya yafuatayo kwa siku chache zijazo
(i) Kama Tendwa (msajili wa vyama) atalazimishwa na bosi wake kukifuta chama cha CHADEMA kwa maslahi ya Taifa, je sisi wafuasi tufanyeje kwa hili
(ii) Kama viongozi wa CHADEMA watashitakiwa kwa kesi za uhaini, mimi na wewe tunafanyeje?
(iii) Mwisho kama vyombo vya habari vitaendelea kuchonganisha CHADEMA NA serikali hapa wewe unafanya nini?
Ndugu zangu msisahau kuwa tumewakamata nyeti zao ni vilio hivyo yakitokea haya tunafanya lipi? Toa ushauri kadiri utavyoweza.























































































































































































































































































kwa jinsi nilivyooangalia taarifa ya habari ni mapango mzima umesukwaq ili kukichafua chadema hoja ziko wazi waeleze hayo maneno ya vitisho na uchochezi yakoje huu ni mkakati maalmu uliopangwa wanakiogopa chadema kwa kuwa ndio sauti ya vijana wengi ambao ndio mtaji wa kisiasa hakuna cha uchochezi wanachokifanya sasa ni kutengeneza picha ya woga kwa watanzania wanafeli vibaya sana
 
Watu wenyewe hata mabomu mnaogopa, likipigwa moja watu wanakimbia wala hakuna hata mmoja anayesimama. Karibu sasa atasema basi na hapo ndipo mtakapo ona cha moto.
.

Nimeishuhudia sana hii, Watanzania ni waoga sana, naisubiri siku watanzania watakapoacha roho ya uoga na kuyasimamia wanayoyasema midomoni mwao!!
 
yaani wanakuwa wazembe mabomu yanalipuka yanaua watu halafu wanatukebehi eti sisi waoga wa mabomu? kuna siku yao wangoje tu!
 
CCM wanaweweseka sasa,maandamano na mikutano ya cdm yamewaumbua kwani ni dhahiri walichakachua matokeo!eti kipindi cha malumbano ya kisiasa kilichowekwa kisheria(kampeni)kimepita eboo!CDM hakuna kulala mpaka kieleweke,sasa tuhamishie harakati hizi kanda ingine mpaka wakimbie nchi....
 
kuna majina duniani humu hadi kipaka,ndo nani na yeye au ndo katibu mkuu mpya wa ccm?
 
CHADEMA accused of 'treason'

By ABDULWAKIL SAIBOKO, 4th March 2011 @ 12:00, Total Comments: 0, Hits: 196

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) has alerted state organs to treat seriously seditious statements being made by opposition Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) leaders, in a bid to save the country from unnecessary unrest.

And the Registrar of Political Parties, Mr John Tendwa has also issued a warning notice to CHADEMA against inciting violence.


CCM's Ideology and Publicity Secretary, Mr John Chiligati told a press conference on Friday in Dar es Salaam that the party has found Chadema's utterances inconceivable and that they were wondering as to why the law enforcers are remaining mum.


"There is a growing tendency among law enforcers to take lightly things that happen on the political stages, but the way we look at Chadema's move in the ongoing demonstrations and public rallies in the Lake Zone, the country's peace is at stake," he warned.


Mr Chiligati went further to condemn the move by Chadema leaders to incite chaos aiming at forcefully remove the sitting President, Mr Jakaya Kikwete from power, which is contrary to the country's constitution that was made on the basis of democracy.


"It should be made clear that CCM is not worried over the ability of Chadema to remove President Kikwete from office, that is a mere dream which will not be achieved since Mr Kikwete came into power after he had scooped majority votes in a democratic, free and fair election," he said.


Mr Chiligati added further that the party's only fear was the fact that Chadema's move to sow seeds of hatred to the people over their government may in a short or long run spark waves of chaos and in the end plunge the country into anarchy.


"If Chadema leaders are really dismayed by the situation the country is going through now, let them use their members of parliament, through their opposition wing to advise the government on the appropriate measures to be taken to address these issues, short of that we will perceive them as a group of greedy persons who want to hold the country's leadership through backdoors," he noted.


Mr Chiligati condemned the Chadema Secretary General, Dr Wilbroad Slaa for spearheading deliberate moves to mudsling President Kikwete, knowing that the election campaign's season ended last year, in which he was defeated by him.


"Dr Slaa wants to be another Jonas Savimbi (former Angolan rebel leader) who always wanted to enter the state house by force, that attitude is not welcomed here and that is why we are calling for action to stop him," he said.


Mr Chiligati noted further that instead of the CCM's government seating down and charting ways through which they would implement the manifesto that made people elect them into power, they were made to be busy with silly agendas.


"Everybody knows that it is against the constitution and it is treasonable to ask people's support to remove a democratic elected leader through the so called 'people's power' that is why we (CCM) are wondering as to why Chadema are left to continue with their incitement," he said.


Commenting on the challenges that the government is facing, Mr Chiligati noted that the party and its government were working very hard to see to it that people's lives are improved.


"The Dowans issue is now in the High Court, we are looking on the possibilities of not paying the fine but Chadema are telling people that nothing is being done, as if the government and CCM have agreed to pay the money," he said.


He noted further that issues of hunger and increased food prices and other services were being dealt with accordingly, adding that some of the things were out of the government control, because they are caused by the looming world's financial crunch.


He added that despite being improper, the Chadema's nine days ultimatum to President Kikwete to ensure all the challenges facing the country are solved was a far fetched expectation which can not be achieved.


Meanwhile, ORTON KIISHWEKO reports that Mr Tendwa has said that he has powers to deregister the opposition party Chadema 'if pushed to the wall' by their 'breach of the Political Parties Act and the penal code through inciting the public.


He called on Chadema during an interview with 'Daily News on Saturday' to relent on what is viewed as instigating the public against the government.


This comes a day after some ministers also called on the party to stop what they termed as instigating uprising against the government.


Mr Tendwa said the letter he recently wrote to the party was just a primary procedure.


He said that on Monday, they would have a political advisory council meeting, which will advise the Registrar and the government on all matters concerning the political situation in the country.


"I can take them to court for breach of Political Parties Act 2009 or instigation, which is a criminal offence where an individual can be fined or imprisoned for not less than one year," he said, adding that the registrar has powers to deregister the party if they don't become sober.


"I warned them in writing as the law prescribes. We don't care about their demonstrations as that is their legal right, but instigating people against a government is breach of law and political parties act.


"If you say what is happening in Libya should come to this country that is treason, because you are telling people to mutiny against the government," he explained.


Mr Tendwa also said that giving a president an ultimatum is a treasonable offence, noting that it may lead to something else if the president does not adhere to such.
 
CCM: Kikwete si Mungu
• Kapteni Chiligati asema hawezi kumaliza matatizo yote

na Baraka Kimwanga


amka2.gif
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejibu mapigo ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwamba Rais Jakaya Kikwete hana uwezo wa Kimungu, kutekeleza ahadi zote ndani ya siku tisa zilizotolewa na viongozi wa juu wa CHADEMA.
Chama hicho ambacho kimeamua kujibu hoja za mikutano ya hadhara ya viongozi wa CHADEMA walioko kwenye ziara ya mikoa ya Kanda ya Ziwa, kimesema Rais Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa CCM, hutekeleza majukumu yake kwa kufuata mwongozo na mipango ya serikali na sheria za nchi, lakini si kwa shinikizo la CHADEMA.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM taifa, Kapteni John Chiligati wakati wa mkutano wake na vyombo vya habari, uliofanyika katika ofisi ndogo ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam.
Alisema CCM imelazimika kuvunja ukimya na kutoa kauli hiyo baada ya kubaini kuwa viongozi wa CHADEMA na wabunge wao wamekuwa wakifanya maandamano na mikutano ya hadhara kwa kutumia lugha za kichochezi na kuwahamasisha wananchi kuleta vurugu nchini.
Chiligati alisema kitendo cha CHADEMA kumpa siku tisa Rais Kikwete ili atekeleze matakwa ya wananchi si cha kiungwa. Alisema CHADEMA walipaswa kuyawasilisha maoni yao kupitia njia sahihi kuliko kupitia maandamano na mikutano ya hadhara ya lugha za uchochezi.
"Rais ni baba wa familia ya Tanzania lakini kumpa siku tisa atekeleze matakwa yote haiwezekani, maana yeye si Mungu, bali ni binadamu na ana mipango endelevu kwa taifa letu. Hebu CHADEMA wawe waungwana," alisema Chiligati.
Alisema tangu kumalizika Uchaguzi Mkuu mwaka jana, CHADEMA imekuwa ikitumia lugha ya uchochezi na kuwapotosha wananchi kuhusu masuala mbalimbali yanayolikabili taifa kwa sasa.
"Hatuna tatizo na maandamano yao Kanda ya Ziwa, maana hata sisi CCM huwa tunafanya lakini wenzetu wanatumia lugha za uchochezi na kutaka kuivuruga amani, sasa kama hawajakubali matokeo ni vema wakajipanga kwa uchaguzi wa mwaka 2015," alisema Chiligati.
Akizungumzia hotuba ya rais aliyoitoa Februari mwaka huu, Chiligati alisema Rais Kikwete alionya na kukemea kauli hizo kwa kusema zinavunja sheria na Katiba ya nchi.
"Katu hatuko tayari kuvumilia kuona hali inaharibika kwa kauli zao hasa ya wembe ule ule mpaka kieleweke, hakika huku ni kuendelea kuchochea vurugu na nchi isitawalike," alisema Chiligati.
Pamoja na kuonya juu ya kauli za CHADEMA, Chiligati alisema kufanya maandano ni haki ya raia kikatiba ili mradi asivunje sheria za nchi, lakini hali ni tofauti kwa maandamano ya CHADEMA kwani yametawaliwa na lugha za uchochezi.
Chiligati alisema CCM ina uwezo wa kujibu mashambulizi ya CHADEMA kwenye mikutano ya hadhara, lakini kwa sasa uchaguzi umepita na kinachotakiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali katika kutekeleza ilani yake ya uchaguzi.
Kada huyo wa CCM alimtaka Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa na Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, kuacha kutafuta umaarufu kupitia matukio na majanga yanayolikumba taifa kwa kutoa kauli za kibabe ambazo alidai zinaashiria uvunjifu wa amani ya nchi.
"Wanapohamasisha wananchi wafanye kama Tunisia na Libya, je, wanajua watu wangapi wamepoteza maisha kwa hili? Katu CCM tunasema hapana na haliwezekani.
"Tunajua Dk. Slaa hakubaliani na matokeo lakini atambue CCM ndiyo ilishinda na kama anataka kuwa Savimbi wa Tanzania hili halina nafasi, atafute nchi nyingine lakini si Tanzania," alisema Chiligati.
Akizungumzia milipuko ya mabomu iliyotokea Februari 16, mwaka huu alisema CHADEMA wanapotosha ukweli juu ya tukio hilo kwa kutoa ripoti yao majukwaani badala ya kusubiri timu za wataalamu zilizoundwa.
Tangu kuanza kwa mikutano hiyo maarufu kama Operesheni Sangara, CHADEMA imeonekana kugusa hisia za maisha ya wananchi wa kipato cha chini na kuwahamasisha kutaka mabadiliko kwa njia ya demokrasia.
Kuhusu hali ya chakula, Chiligati alisema hotuba ya Rais Kikwete ilitoa dira ya kukabiliana na hali ya maisha na chakula, hasa katika kukabiliana na janga la njaa nchini.
Alisema serikali imekuwa sikivu na hivi sasa imachukua hatua za dharura kukabiliana na mgawo wa umeme na upandaji wa bei za vyakula.
Dowans na CHADEMA
Katibu huyo wa Itikadi, alisema CHADEMA wamekuwa wakipotosha ukweli kuhusu suala hilo ambalo ni la kisheria na kulifanya la kisiasa zaidi.
"Suala la kisiasa huenda kisiasa lakini CCM kupitia kamati ya wabunge wetu, tulishatoa dira kwa serikali ili kukwepa tozo la sh 94 bilioni na ni lazima watambue suala hili linatokana na mahakama ya kimataifa na si CCM," alisema Chiligati.
Alisema na kuwashutumu viongozi wa CHADEMA huku akiwaita wapotoshaji wa suala hilo, kwani wanachokifanya ni kujenga chuki dhidi ya serikali ya CCM.
Dk. Slaa atoa mpya
Wakati huo huo waandishi wetu, Sitta Tumma na Janet Josiah, kutoka Misenyi wanaripoti kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amesema ni heri wampige risasi na kumuua badala ya kutaka kumnyamazisha na kumziba mdomo katika suala zima la
kuikosoa serikali.

Slaa alisema yupo tayari kufa kwa ajili ya kupigania maendeleo na ukombozi wa taifa.Tamko hilo alilitoa juzi kwenye mkutano wa hadhara wakati alipokuwa akihutubia maelfu ya wakazi wa Wilaya ya Misenyi mkoani Kagera, uliofanyika katika viwanja vya Kanyigo, ikiwa ni hitimisho la maandamano makubwa na ya amani katika mikoa minne ya Kanda ya Ziwa.
Akisisitiza alisema: "CHADEMA tunaposema ukweli wao wanasema sisi ni wachochezi, lakini hatutakubali kunyamazishwa labda wanipige risasi na siogopi kupigwa risasi nife nikipigania ukombozi wa Watanzania."
Dk. Slaa alikwenda mbali zaidi na kumpuuza Waziri Ofisi ya Rais, Sera na Mahusiano, Steven Wassira, kwa kusema waziri huyo ni mdogo sana kujibishana naye, hivyo si saizi yake.
"Nilimsikia jana (juzi), mtu mmoja anaitwa Wassira naye anaikoromea CHADEMA kuhusu maandamano yetu Kanda ya Ziwa, eti anasema tukizidi anaweza kuyazuia.
"Napenda nimwambie Waziri Wassira kwamba si saizi yangu...Rais Kikwete anasema maandamano ni haki kikatiba, Wassira anasema anaweza kuzuia
maandamano, wapi na wapi?" alisema Dk. Slaa ambaye alikuwa mgombea urais katika Uchaguzi Mkuu uliopita.

Dk. Slaa pia ametoa tamko zito la kuitaka serikali ya Rais Jakaya Kikwete kuhakikisha fedha zinazodaiwa kuibiwa katika kampuni ya Kagoda, Mwananchi Gold, Meremeta, Tangood na Deep Green zinarejeshwa na kuingizwa kwenye bajeti ijayo ya mwaka 2011/2012.
Alisema anataka kuona fedha hizo zinaingizwa kwenye bajeti hiyo ya fedha itakayopitishwa na Bunge Julai mwaka huu, ili ziweze kuwanufaisha Watanzania na si vigogo baadhi, vinginevyo chama chake kitachukua hatua, kwani Watanzania wamegeuzwa kama kuku wa kienyeji.
Alisema mabilioni hayo ya fedha yaliyoibiwa na wajanja yakirudishwa yanaweza kujenga shule, vituo vya afya na hospitali zote pasipo wananchi kuchangishwa michango ya ujenzi wa miradi hiyo, hivyo kufikia Julai mwaka huu, fedha hizo ziwe zimeingizwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2011/2012.
"Waziri Mkuu Mizengo Pinda alikwishawahi kusema bungeni kwamba yupo tayari kukatwa shingo kuliko kutaja fedha za Meremeta zilikokwenda na
matumizi yake.

"Kwa maana hiyo, nataka kufikia Julai mwaka huu serikali iwe imezirudisha na kuziingiza kwenye bajeti itakayopitishwa na Bunge, la sivyo hatutaelewana...na fedha hizi zikirudi ni sawa na 1/5 ya bajeti yote ya nchi, tunataka zirudi," alisema Dk. Slaa.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu huyo wa CHADEMA, fedha zilizoibwa Meremeta sh bilioni 155 na mabilioni mengine kupitia Kagoda, Deep Green na Mwananchi Gold zikirejeshwa zitasaidia nchi kupata maendeleo.
Awali alisema sh bilioni 25 kati ya bilioni 40 za Kagoda zilichukuliwa na Rostam Aziz siku moja kwenye matawi sita ya Benki ya CRDB, lakini Rais Kikwete anasema hajui zilipo fedha hizo.
Juzi CHADEMA na viongozi wake akiwamo Mwenyekiti wa chama, Freeman Mbowe, mawaziri kivuli, walihitimisha kwa kishindo kikubwa kazi yao ya maandamano katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, ambayo yalilenga kupinga kulipwa kwa Kampuni ya Dowans, ongezeko la gharama za umeme, maisha magumu kwa Watanzania na mauaji ya raia huko Arusha Januari 5, mwaka huu.
Chama hicho kikuu cha upinzani kimepanga kufanya maandamano hayo ya amani nchi nzima, baada ya kumalizika vikao vya Bunge Aprili mwaka huu.
Pinda Kagera
Naye Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliwasili mkoani Kagera jana zikiwa ni siku chache tu tangu CHADEMA wapite na kufanya mikutano yao.
Akiwa Kagera Pinda ametaka apatiwe taarifa za Mkaguzi Mkuu na Mdhibiti wa Fedha za Serikali (CAG) kuhusu matumizi na mapato ya kila halmashauri ili apate picha kamili ya matumizi ya fedha za serikali.
Pinda alitoa kauli hiyo baada kuwasili mjini Bukoba, mkoani Kagera kwa ziara ya siku nane ambako atakagua shughuli mbalimbali za maendeleo kwa kutembelea wilaya zote za mkoa huo.
Alisema serikali inatuma fedha nyingi mikoani na katika halmashauri kupitia miradi mbalimbali lakini matokeo halisi ya fedha hizo hayaonekani katika maisha ya Mtanzania wa kawaida.
"Mkoa wa Kagera umepata sh bilioni 10 kwa ajili ya miradi ya DADPS na ninyi mna wilaya saba, maana yake ni kwamba kila wilaya ina zaidi ya sh bilioni moja na ushei, lakini kama fedha hii haionekani imefanya nini, hali inatisha," alisema Pinda.
Kuhusu elimu, alisema mkoa unakabiliwa na tatizo la mimba, hali ambayo alisema hairidhishi kutokana na idadi kubwa ya wasichana waliopata ujauzito.
"Katika mwaka 2009/2010 jumla ya watoto 339 waliacha shule kutokana na ujauzito na kati yao 70 ni wa shule ya msingi… hii inatisha, ongeeni na wazazi na walimu, lakini zaidi watafuteni wakosaji, wakiwekwa ndani hata watu 10, basi watajua kuwa hili ni baya," alisisitiza.
Aliitaja mikoa mitano ya mwisho ambayo iko chini ya wastani wa kitaifa wa pato la mtu ambalo limefikia sh 693,470 kwa mwaka; ni Kigoma ulioko nafasi ya 17 ukiwa na wastani wa pato la mwananchi la sh 483,158; Shinyanga wa 18 (sh 455,000); Kagera wa 19 (sh 453,235); Dodoma wa 20 (sh 414,597) na Singida ambao ni wa mwisho ukiwa na wastani wa sh 373,694.
Katika ziara hiyo ya kikazi, Pinda alizindua barabara ya Zamzam na kuzungumza na wakazi wa Manispaa ya Bukoba katika Uwanja wa Mayunga (Uhuru Platform).
 
Tatizo kwa CCM ni kujidanganya ya kuwa walishinda uchaguzi mwaka jana na hushinikiza ya kuwa uchaguzi ulikwisha jambo ambalo siyo kweli................................................bila ya kuuunda tume ya kimataifa na kuchunguza jinsi NEC na TISS walivyovuruga uchaguzi uhalali wa CCM kuongoza haupo na madai ya "treason" ni kujidanganya wenyewe....................................

Hata ukiwapeleka watu mahakamani na wewe unatetea dhuluma ya JK na wabunge wake kujisimika madarakani kwa misingi ya dhuluma dhidi ya wapiakura hutafanikiwa kuishinda nguvu ya umma inayodai mabadiliko ya kweli na ya haraka kulinusuru taifa kutoka minyororo ya mafisadi............................
 
Chadema wasakamwa, wadaiwa wahaini
Imeandikwa na Theopista Nsanzugwanko; Tarehe: 4th March 2011 @ 07:36 Imesomwa na watu: 1160; Jumla ya maoni: 2








WANASIASA na taasisi mbalimbali nchini wamepinga maandamano yanayoendeshwa na Chadema kuhamasisha wananchi kuipinga Serikali na kuiondoa madarakani kuwa ni uhaini na inapaswa kushitakiwa.

Aidha, wamemtaka Msajili wa Vyama vya Siasa, kuangalia uwezekano wa kukisimamisha au kukifuta chama hicho kwa usalama wa Taifa na kudai kuwa maandamano hayo ni chanzo cha vurugu na kuvunjika kwa amani, ambazo ni dalili zinazopaswa kuchukuliwa hatua za kiusalama haraka ili Taifa lisiingie katika machafuko ya kisiasa.


Katika siku za karibuni Chadema imekuwa ikifanya maandamano na mikutano ya hadhara kwa lengo la kupinga ufisadi serikalini, hali ngumu ya maisha inayotokana na kupanda kwa bei ya vyakula, malipo kwa Kampuni ya Dowans na tatizo la umeme.


Wakizungumza na wanahabari Dar es Salaam jana, Wanaharakati wa Haki za Watu Wenye Ulemavu nchini, walisema kinachofanywa hivi sasa na vyama vya siasa na wanasiasa kuzunguka nchini kuhamasisha wananchi wakubali kuondoa Serikali halali madarakani, kinaweza kusababisha madhara makubwa.


Walipongeza hotuba ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa wiki iliyopita na kupinga maandamano yanayoendelea katika mikoa tofauti na kusema madhara hayo waathirika wake ni jamii ya watu wenye ulemavu.


Msemaji wa wanaharakati hao, Abubakar Rakesh, alisema wanampongeza Rais kwa kuona kwamba amani ya Watanzania ambayo ni tunu inaanza kutoweka kwa kusema kwake na kuwaondoa hofu Watanzania, imeonesha jinsi anavyowajali wananchi wake.


"Uzoefu na ushahidi unatuonesha, kwamba nchi nyingi duniani zilizokabiliwa na migogoro na uvunjifu wa amani, wahanga wakubwa wa kupoteza maisha ni watu wa jamii ya walemavu, hivyo tunamwomba Rais aendelee kukemea lakini pia asiyumbe katika kulinda amani ya nchi yetu," alisema Rakesh.


Walimtaka Rais Kikwete pamoja na kuendelea kukemea hali hiyo, lakini pia asiyumbe katika kulinda amani ya nchi na kuhakikisha kuwa Katiba iliyopo inaheshimiwa na kila mmoja, kwani Katiba ya nchi si ya chama.


Katibu wa Kamati ya Amani Umoja na Mshikamano wa Kitaifa (UPF), Risasi Mwaulanga, alisema wanachofanya Chadema ni uhaini wa wazi, kwani umma utakapokasirika utapata hamasa na kugomea sera ya chama tawala na kuacha kushiriki shughuli za maendeleo.


"Vyombo vya usalama vinatakiwa kuchukua hatua dhidi ya Mwenyekiti wa Chadema na Katibu Mkuu wake wakamatwe na kufunguliwa mashitaka ya uhaini, ikiwa ni pamoja na Bunge kutoa onyo kwa wabunge wake na Msajili kuangalia vifungu vya Katiba kuona uwezekano wa kukisimamisha au kukifuta chama hicho," alisema Mwaulanga.


Pia aliwataka wananchi kupuuza mikutano yao ya hadhara bila kujali itikadi, kujenga ushawishi wa kutengwa na taasisi mbalimbali hadi watakaporekebisha mustakabali wa siasa zao za uchochezi nchini .


Mwenyekiti wa TLP, Augustino Mrema, alisema maandamano hayo yanahamasisha wananchi kuiga mifano ya nchi za Kaskazini mwa Afrika, ambazo chanzo cha maandamano na hatimaye vifo yametokana na vyama vya upinzani.


"Maandamano hayawezi kutuondolea matatizo tuliyonayo, bali yatasababisha maafa makubwa yasiyoweza kulipika, kama ilivyotokea kwenye nchi nyingine duniani, ni wazi tunaweza kuiondoa Serikali iliyoko madarakani kwa kutumia njia za kikatiba na kisheria kwa ridhaa ya wananchi kwa kura zao," alisema Mrema.


Aliwasihi wapinzani wenzake kuwa kwa kutumia njia sahihi wana uwezo wa kuingia madarakani, ndiyo maana walipata asilimia 40 ya kura za urais na wana wabunge na madiwani.


"Wapinzani tuko bungeni, kwenye halmashauri za miji, serikali za vijiji na vitongoji, kwa nini tusitumie fursa hizo? Baada ya uchaguzi siasa zihamie bungeni na kwenye mabaraza ya halmashauri na miji na si kuishia maandamano na mikutano tu," alisema Mrema.


Alisema wapinzani wana wenyeviti katika kamati mbalimbali za Bunge, hivyo wanaweza kupambana na ufisadi na wakishindwa ni uzembe wao, kwani hawana kikwazo, aliwataka kukamata mafisadi na kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria kwani ufisadi hauwezi kuondolewa kwa maandamano.


"Kwa mfano mimi nilishakabidhiwa vitabu vya ukaguzi kutoka kwa Mkaguzi Mkuu wa Serikali vinavyoonesha kwenye halmashauri za miji kuna ubadhirifu wa kutisha, kuliko hata ubadhirifu unaodaiwa kufanywa na Dowans," alisisitiza Mrema.


Aliwataka Watanzania wasidanganywe na kufananisha Tanzania na nchi nyingine kama Libya na Misri, kwani matatizo hayafanani na nchini tatizo ni umasikini, hali ngumu ya maisha, umeme na ufisadi, wakati nchi hizo zingine, matatizo yao ni mfumo mbaya wa kiutawala tofauti Tanzania.




Jumla Maoni (2) Maoni Nashukuru sana kwa mpinzani wa kweli na mwenye busara Mh. Agustino Mrema kwa kuliona hili linalofanywa na wanasiasa wa Chama cha Chadema na kuwapa Watanzania wenzake tahadhari kubwa, Ndugu zangu, Mh. Slaa na Mh. Mbowe, hivi ni kweli mnawapenda Watanzania wenzenu kwa kuwashawishi hayo mnayoyafanya? Nina Imani kwa ukomavu wenu wa kisiasa mnaelewa wazi athari kubwa na mbaya iliyo mbele kwa hayo mnayoyatazamia. Sie sote ni Watanzania na wazalendo wa kweli wa nchi yetu, nawashauri msitumie mikutano yenu kuwashawishi Watanzania kuichukia serikali ilikuwa madarakani kwa ridhaa ya Watanzania wengi. Nawatakia mzee Slaa na Father Mbowe, siasa njema na zenye mabadiriko kimtazamo. Maoni Nimegundua kuwa wananchi wengi wa Tanzania hatuelewi vitu gani ambavyo tukivifanya vinavyoweza kutuletea maendeleo nchini,kwa umbumbu huu watanzania wengi wanadanywa kwamba maandamano tena ya jasba kwamba huleta maendeleo bila kujua kuwa maandamano ya watu wenye hasira na jazba huzaa uvunjifu wa amani ambayo ndio kitovu kikuu cha nchi kupata maendeleo,ukitaka kujua ukweli huu angalia nchi ambazo zimekumbwa na mizozo ya kivita kwa muda mrefu jinsi walivyo na hali ngumu ya maisha.Ni hatari nchi kuingia katika machafuko kwani kila kitu husimama ,hakuna shule,hakuna cha huduma za afya,uzalihsaji mali mashambani na viwandani ,hakuna kinachotoka wala kuingia nchini kwa ajili ya kuinua uchumi badala yake hata kile kidogo kilichopo hutumika na serikali katika kukabiliana na hali mbaya ya hatari inayokuwepo ya machafuko.Watanzania wengi tumezaliwa nchi ikiwa na amani sasa tumelewa na amani hiyo kiasi kwamba tunatamani machafuko nchini,eeh Mungu tuokoe na balaa hii ya machafuko Tanzania ,tujalie kuwa kuwa na amani siku zote ipitayo akili na fahamu zetu ili tuendelee kufurahia mema na baraka na neema tele tuliyopewa na MOLA MUUMBA WETU AMINA.
 
PHP:
                                                                                                                                                                                                                                                        WANASIASA na taasisi mbalimbali nchini wamepinga   maandamano yanayoendeshwa na Chadema kuhamasisha wananchi kuipinga   Serikali na kuiondoa madarakani kuwa ni uhaini na inapaswa kushitakiwa.     

Aidha, wamemtaka Msajili wa Vyama vya Siasa, kuangalia uwezekano wa   kukisimamisha au kukifuta chama hicho kwa usalama wa Taifa na kudai kuwa   maandamano hayo ni chanzo cha vurugu na kuvunjika kwa amani, ambazo ni   dalili  zinazopaswa kuchukuliwa hatua za kiusalama haraka ili Taifa   lisiingie katika machafuko ya kisiasa.

Tatizo kwa hizi ngebe ni kuwa..............."did Jk really won the last election?"..........the answer is a big no..................then how can you talk of treason while we have an impostor masquerading like a president?
 
nasikitika sana napoongozwa na serikali oga na isiyoweza chukua hatua inabaki inalalama tu.kiukweli jk yupo fear angekuepo bwana mkapa ujinga huu usingefanyika wa lengo la maandamano 1 na ku add mengine.hamjiulizi kipindi icho slaa mbowe walikuwa wapi? Ukweli wanajua shughuri ya mkapa.mapinduzi tz ni ndoto. Sababu dar ndo kitovu ila ndio kuna wanafiki wengi washabiki wa kisiasa.mikoa mingine nayo mbwembwe wakipigwa mabomu siku 1 kesho hawajitokezi tena. Huko wilayani ndo hata haiwezekani watu waoga sana maandamano ya amani ni tofauti ya mapinduzi hawawezi pata mtu watz wanapenda kuishi sana
 
Sawa kabisa tunajua umetumwa ucheck joto sasa kwa taarifa yako mwaka huu hautaisha kama ataendelea na uongozi wake kama anaendesha familia yenye watoto wa kambo
 
hakuna sehemu ambapo mapinduzi hayawezekani. Ni suala dogo tu la kuwaelimisha wananchi ili wamjue mbaya wao (CCM)! Kwa sasa CCM bado imewekeza kwenye ujinga wa watanzania na hawataki CHADEMA wawaelimishe ili waendelee kuwa-fool!
 
Back
Top Bottom