Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,495
- 51,090
Katika zunguuka yangu vijiweni Dar es salaam, Wananchi wanahasira kali sana juu ya ukosefu wa maji Jijini.
Wananchi wanasema Maji wakati mwingine yanakosekana kwa wiki nzima.
Kinachowakera zaidi ni kuwa wamekuwa wakitumia gharama kubwa sana kununua maji na hivyo kufanya maisha yao kuwa magumu maradufu.
Wananchi wanasema, Wameivumilia serikali kwenye mambo mengi sana ikiwemo kuvuruga uchaguzi serikali za mitaa mwaka 2019, Kuvuruga uchaguzi mkuu, Kuwatoza tozo kubwa, Ukatili wa kisiasa, Kuendesha zoezi la wamachinga kihuni. Sasa wanasema hili suala la Maji limewafika shingoni hali ni mbaya.
Inadaiwa Wananchi wanazungumza uwezekano wa kufanya maandamano makubwa ya kudai maji nchini.
Wananchi wanakumbushia kuwa kwenye rasimu ya Warioba MAJI ILIKUWA NI HAKI YA MSINGI ya mwananchi, wanasema kuwa kukataa katiba mpya maana yake ni kukataa wananchi wasipate hayo maji.
Katika mazungumzo yao, wananchi wanasema wanahitaji majibu ya suala la maji haraka sana la sivyo watatoka barabarani na ndoo za maji na magudulia ikiwa ni ishara ya kuonyesha kudai maji!
Wazazi wanalalamika watoto wanaenda shule bila kuoga, Watu wanalalamika wanashindwa kujisitiri chooni vyema sababu ya maji. Watu wanahoji hii nchi ni nchi ya namna gani?
Wakati huo wanahoji, Inakuwaje serikali inatumia matrilioni ya hela kununua ndege halafu inashindwa kujenga miundo mbinu bora ya maji kwa ajili ya jiji la watu milioni 8?
Haya mdogomdogo tutafika. Serikali ijiabdae kwa majibu, Mabomu ya machozi, virungu na bunduki havitoweza kuzuia watu wenye kiu!
Wananchi wanasema Maji wakati mwingine yanakosekana kwa wiki nzima.
Kinachowakera zaidi ni kuwa wamekuwa wakitumia gharama kubwa sana kununua maji na hivyo kufanya maisha yao kuwa magumu maradufu.
Wananchi wanasema, Wameivumilia serikali kwenye mambo mengi sana ikiwemo kuvuruga uchaguzi serikali za mitaa mwaka 2019, Kuvuruga uchaguzi mkuu, Kuwatoza tozo kubwa, Ukatili wa kisiasa, Kuendesha zoezi la wamachinga kihuni. Sasa wanasema hili suala la Maji limewafika shingoni hali ni mbaya.
Inadaiwa Wananchi wanazungumza uwezekano wa kufanya maandamano makubwa ya kudai maji nchini.
Wananchi wanakumbushia kuwa kwenye rasimu ya Warioba MAJI ILIKUWA NI HAKI YA MSINGI ya mwananchi, wanasema kuwa kukataa katiba mpya maana yake ni kukataa wananchi wasipate hayo maji.
Katika mazungumzo yao, wananchi wanasema wanahitaji majibu ya suala la maji haraka sana la sivyo watatoka barabarani na ndoo za maji na magudulia ikiwa ni ishara ya kuonyesha kudai maji!
Wazazi wanalalamika watoto wanaenda shule bila kuoga, Watu wanalalamika wanashindwa kujisitiri chooni vyema sababu ya maji. Watu wanahoji hii nchi ni nchi ya namna gani?
Wakati huo wanahoji, Inakuwaje serikali inatumia matrilioni ya hela kununua ndege halafu inashindwa kujenga miundo mbinu bora ya maji kwa ajili ya jiji la watu milioni 8?
Haya mdogomdogo tutafika. Serikali ijiabdae kwa majibu, Mabomu ya machozi, virungu na bunduki havitoweza kuzuia watu wenye kiu!