Maandamano London: Another new episode

Maandamano London: Another new episode

Nawapongeza Wazanzibari waliopo Uingereza walioandaa Maandamano yatakayofanyika 10 Downing St, London SW1A 2AA kuanzia saa nne asubuhi siku ya Ijumaa tarehe 13/11/2015.

Lengo likiwa ni kutoa Shukran kwa Waziri Mkuu na Serikali yake ya Uengereza kuona haki inatendeka kwa Wananchi wa Zanzibar juu ya uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 25/10/2015.

Kibali kimetolewa na Parliamentary & Diplomatic Protection Command wakishirikiana na Scotland Yard Special Events.
Natoa Rai kwa watanzania wote kwa ujummla waliopo nje ya nchi wafanye hivi kama sehemu ya mchango wao wa kukuza demokrasia na kuhakikisha haki ya Wazanzibari inalindwa

Jumuiya ya kimataifa ina mchango mkubwa sana katika kuokoa hali ya kisiasa Zanzibar

Kwa huku nyumbani tutaendelea kushirikiana kuhakikisha Sheria na katiba ya zanzibar inalindwa na haki ya kidemokrasia ya wananchi visiwani haipotei



Aluta continua,Victory Ascerta....!

Ben Saanane

Kwa hiyo we Ben Saanane , umekuwa ndio msemaji wa cuf! Watu mkiishiwa jambo la kufanya mnakuwa na viherehere kama wakina mama wenye kupenda kusutwa. Ya kwenu yamewashinda mnakurupuka na ya wenzenu.
 
Last edited by a moderator:
hivi kwa uzi huu mleta mada CYBER CRIME UKITIWA NGUVUNI UTAMLAUMU MTU KWELI USIDANGANYIKE NA KYBOD KUWA ET HAUTAMBULIKI
cc
yereco nyerere
Tangu uijue cyber crime siku hizi hata mmeo akichelewa kurudi unamtishia kumshitaki kwa cyber crime.

Stop childish.
 
Kwa hiyo we Ben Saanane , umekuwa ndio msemaji wa cuf! Watu mkiishiwa jambo la kufanya mnakuwa na viherehere kama wakina mama wenye kupenda kusutwa. Ya kwenu yamewashinda mnakurupuka na ya wenzenu.

Ben ni Mtanzania na ana haki ya kuchangia chochote kwenye Taifa lake
 
Last edited by a moderator:
[h=2]nday, November 9, 2015[/h] [h=3]TAARIFA YA MAANDAMANO[/h]
zawalogo-346x272.jpg

Assalamu alaykum,
Kwa Niaba ya Zanzibar Welfare Association UK, inapenda kuwaarifu Watu wote watakaonafasika, kuhudhuria kwenye Maandamano yatakayofanyika 10 Downing St, London SW1A 2AA kuanzia saa nne asubuhi siku ya Ijumaa tarehe 13/11/2015.
Lengo ni kutoa Shukran kwa Waziri Mkuu na Serikali yake ya Uengereza kuona haki inatendeka kwa Wananchi wa Zanzibar juu ya uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 25/10/2015.
Kibali kimetolewa na Parliamentary & Diplomatic Protection Command wakishirikiana na Scotland Yard Special Events.
Ahsanteni
Mwenyekiti ZAWA UK
Hassan M Khamis

[h=1]KILA MZANZIBARI ALIYE IPIGIA KURA CCM AU MPAKA WAKATI HUU BADO ANAISAPOTI CCM ILI IBAKI MADARAKANI JAPO KUWA CCM IMESHINDWA UCHAGUZI AJUWE NA YEYE ANACHANGIA KUENDELEZA DHULMA NA KUFUNGWA KWA MASHEIKH NA KUTHALILISHWA KWAO NA KUENDELEZA DHULMA KATIKA NCHI YA ZANZIBAR UKAE UKIJUWA UTAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA,KUDHULUMIWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.[/h]
FREE ZANZIBAR PEOPLE FROM MKOLONI MWEUSI at 11:17 PM
Hayo maswali siku ya kiama hayatachagua wana ccm, ukawa, masheikh, waliopiga kura, waliotetea waliokamatwa, n.k kila nafsi itakumbana na maswali kwa mujibu wa matendo yake katika kutimiza malengo ya kuumbwa kwake. Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa yote ya dhahiri na ya siri
 
Kumekucha........ wazanzibar mliopo Uingereza fanyeni kweli pazeni sauti zenu muitetee Zenji yenu
 
Wazanzibari na Watanganyika wengi walioko Uingereza wamejilipua. Kwa sasa wanaishi kama Wasomali, Wasudani na Waeritrea.

Wadanganyeni waandamane ili wakakutane na mikono ya Maafisa wa border force kwenye underground entry, buses and demonstration!

Kuna hatred kubwa sana kama ya Waunguja na Wapemba kiasi kwamba wamechomeana kwenye ofisi za uhamiaji.

Kwa faida ya maisha yao, kama kuna mtu ana matatizo kuhusu status ya uhamiaji ni vizuri akaepuka maandamano hayo, otherwise, atajikuta kwenye matatizo.

Ninatoa ushauri kwa vile ninawapenda Watanzania wenzangu.

Don't hang the messenger!

Unachekesha sana ,haya maandamano tumewa invite jumuiya nyengine watuunge mkono kama za wasomali, Palestine, charities, time organized hatuja kurupuka, kwa taarifa yako, hii nchi inafuata sheria, na kwa sasa hao UK border hawana uwezo na kinyume cha sheria kufanya kama hivyo unavyo Sena.

Mimi nipo UK miaka 15 nani mzanzibari, kama msomali, kama British, vitu hivyo no kawaida mkuu, kama kidume na wewe njo uwombe ukimbizi.
 
Its not the first time kwa hawa wapenda waarabu kujifanya wanauchungu na Zanzibar bytheway impact ya hayo makobeano ni kama susumizi kwenye msafara wa TEMBO. HAPA KAzi TU

Eti hapa kazi ? Bila ya bishahara ya walimu ?
 
Tutatuma ffu asubuhi na mapema kuzuia...

Hivi Kov hajajua hili? si alikataza hadi mwamko wa siasa uishe mioyoni mwa watu... Wazanzibar hawapandi sana kuelewa amri za wakuu
 
Bora waandamane labda ccm wataona aibu wamuapishe Maalim Seif
 
Wazanzibari na Watanganyika wengi walioko Uingereza wamejilipua. Kwa sasa wanaishi kama Wasomali, Wasudani na Waeritrea.

Wadanganyeni waandamane ili wakakutane na mikono ya Maafisa wa border force kwenye underground entry, buses and demonstration!

Kuna hatred kubwa sana kama ya Waunguja na Wapemba kiasi kwamba wamechomeana kwenye ofisi za uhamiaji.

Kwa faida ya maisha yao, kama kuna mtu ana matatizo kuhusu status ya uhamiaji ni vizuri akaepuka maandamano hayo, otherwise, atajikuta kwenye matatizo.

Ninatoa ushauri kwa vile ninawapenda Watanzania wenzangu.

Don't hang the messenger!

Nimejikuta nacheka sana kwa ukweli huu.

Alafu wanatoa onyo kwa wana ccm na kumtaja Mungu, hapo wameenda mbali.

Nao wakiamua kuwachochea kwa hao hao wa Scotland yard maana kiuraia kweli wengi wamedanganya ni watakomaje.

Simu moja boda kontrol inawamaliza.

Wanajisahau kwa kutaka ubabe na chenji ya chama watumiwe wale, tumbo kwanza.
 
11219663_10205322714691282_4701558228154669459_n.jpg



Kamati kuu ya Uongozi wa ZAWAUK iliomaliza kikao chake tarehe 08/11/2015 kwenye Ofisi zake zilizopo Manor park huko East London. Moja katika maazimio yaliofikiwa ni kuandaa Maandamano yanayohusiana na Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar.
 
Back
Top Bottom