Mkuu, inawezekana ukawa sahihi kabisa. Ila nina wasiwasi sana na usahihi wa mawazo ya JK (kama kweli ndivyo anavyodhani), kuwa, kushiriki na mafisadi kutamsaidia kushinda uchaguzi ujao kwa urahisi. Nionavyo ni kuwa atapata shida sana akijiunga nao.
Kwa yaliyotokea Dodoma, nadhani JK hakuonyesha kwa kiasi kikubwa kuwa upande wa Mafisadi. Lakini pia hakuonyesha kuwa upande mwingine wowote. Ninavyohisi mimi ni kwamba, kadiri muda unavyosogea kuelekea kwenye uchaguzi ujao (2010), mafisadi watajitahidi sana kuhakikisha kuwa JK anaonyesha wazi yuko upande gani (wao au wa wapinzani wao). Hapo nadhani ndipo anapotakiwa kupaona sasa. Maana Mafisadi watamsumbua sana kuhakikisha wanajua mustakbali wao kisiasa. La sivyo wanajua kuwa watakuwa wamekwisha kisiasa.
- Mkuu Recta, heshima mbele sana ndugu yangu ninaheshimu sana hoja zako, lakini ushindi wa kikao cha siasa hutambuliwa na kupitishwa kwa agenda za ule mkutano wa siasa,
- Mafisadi walienda Dodoma wakiwa na agenda mbili, moja ni kumuondoa Six na pili kupitisha Azimio la kikao, la kwanza hawakufanikiwa lakini wamefanikiwa kumdhoofisha not olny Six, ila wapiganaji wote kwa sababu baada ya kile kikao kuisha ni makosa makubwa sana kuikosoa serikali na CCM unapokuwa kiongozi under CCM tiketi, ambalo ndio hasa Mafisadi wanted kwenye agenda yao ya pili ambalo lilipita likishuhudiwa na Mwenyekiti wa CCM,
- Toka hivi vita vianze kati ya wapiganaji na mafisadi, ukweli ni kwamba Mafisadi wamekuwa wakishinda hata wanaposhindwa hushinda anyways na siku zote wao humtumia Muungwana, kwa mfano:-
1. Lowassa alipokimbia kazi yake ya PM, alitakiwa kufikishwa kwenye sheria, lakini ni huyu huyu rais aliyemtetea kwamba hakukosea au umesahau mkutano wake na wazee wa Dar? Sasa who won hapa mkuu mafisadi au wapiganaji?
2. This time wapiganaji wakajaribu kupitisha agenda ya kuwathibiti mafisadi, look kwanza Makamba akaikwepesha na kujaribu kutoiweka hiyo Agenda, alipobanwa sana ikawekwa mezani tena dakika za mwisho, huyu huyu Muungwana akaizungusha zungusha, ikaishia makelele mengi ya kina Anna Abdallah na Kingunge, hakuna tamko rasmi la kikao on the ishu, nani aliyeshinda hapa mafisadi au wapiganaji?
3. Jambazi Nyari ambaye ni linked na mafisadi akaachiwa kati kati ya kikao cha NEC, baada ya ugomvi mkubwa ndani kikao kuhusu wabunge wa Arusha ambao walikamatwa kwa shinikizo la hao hao mafisadi, again hakuna tamko rasmi kuwapinga mafisadi na huku jambazi linked na mafisadi limeachiwa, nani aliyeshinda hapa Mafisadi au wapiganaji?
4. Uongozi wa UV-CCM, wapiganaji walimshauri Muungwana, asiruhusu mafisadi kugombea nafasi yoyote ile ya uongozi huo, tizama yaliyojiri, kwanza Nape akango'lewa na mafisadi asigombee, NEC kwa shinikioz la mafisadi ikaamua Mwenyekiti tu wa UV-CCM ndio atoke visiwani lakini nafasi zingine zigombewe na wote, kama mafisadi walivyotaka, sasa nani aliyeshinda hapa mafisadi au wapiganaji?
5. Oscar na kugombea ubunge wa Biharamulo, again baada ya vuta nikuvute huko NEC mafisadi wakampitisha kuwa mgombea wa ubunge, again nani aliyeshinda hapo mafisadi au wapiganaji?
6. Now juzi ndio haya, marufuku kwa kiongozi wa CCM kuishambulia CCM au serikali nje ya vikao vya chama, nani aliyeshinda mkuu sio hao hao mafisadi? Sasa mind you kwamba Mwenyekiti wa vikao vyote hivi ni Muungwana, sasa how could you say kwamba hajaonyesha yuko upande gani? Wakati hizi facts ziko wazi na clear kwamba anawaogopa? Mkuu baada ya hiki kikao cha juzi sasa ninaamini tena kwa 100% kwamba Muungwana anawaogopa zaidi hao mafisadi na yuko radhi kula nao ili ashinde uchaguzi na wapiganaji watakuwa ni wendawazimu kuamini tofauti!
Respect.
Field Marshall Es!