Pole sana mama kwa matatizo... ushaur jaribu kusahau yaliyopita na mambo mengine yataenda sawa.
Jaman wana jf kuuliza c ujinga. Huwa nackia tu ingia pm ndio nn hiyo pm?
Mpaka leo una watoto wanne wa wanaume wawili tofauti;
Je ushauriwe ili ukazae na mwanaume wa tatu?
Ukiona vipi jipange tu, maisha yako na wanao hayatakushinda.
bora ukosee kujenga kuliko kukosea kuoa au kuolewa
Poleni na majukumu ya kila siku wana JF, ikiwa ni mara yangu ya kwanza kuweka post, nahitaji msaada sana kutoka kwenu wazoefu kwenye ndoa, wana dini kimaombi zaidi .
Mimi ni mama wa watoto wawili, nimefunga ndoa miaka saba iliyopita, mwanzo kabisa maisha yangu ya mahusiano hayakuwa mazuri hata kidogo, first of all niliwahi kubakwa nikiwa na umri wa miaka 15, baada ya hapo niliishi maisha ya tabu sana mpaka nilipokuwa mkubwa na kuweza kujitambua.
Nillianza maisha ya mahusiano nikiwa na miaka 21 na mwanaume niliyetokea kumpenda na kuamini yeye ndio atakayenifuta machozi na huzuni zangu.
Mambo hayakuwa hivyo kwani miaka miatatu ya mahusiano yetu alienda oversizi na kuniacha na pia kuamua kukata mawasiliano kabisa. Nilibaki na kovu na maumivu niliyokosa tiba. Nilimtafuta bila mafanikio na kuamua kumove on na maisha yangu,ingawa ilikuwa ni ngumu sana.
View attachment 169831
Baada ya hapo nilikutana na mwamaume ambaye sikujua kama ni kweli nampenda kwani siku zote nilipokuwa nae nilikuwa namuwaza X wangu aliyeniacha bila kusema neno lolote.
Mwanaume huyu mwanzo sikumuelewa kabisa kwanza alikuwa mgomvi na mkorofi kwa watu dakika mbili alishabadirika haeleweki kama kinyonga ,police kwake ilikuwa ni kama nyumbani.
Nyimbo zake mara nyingi zilikuwa ni za kina Tupac ,Snopy D na wale aina ya magang star Ingawa alikuwa msomi na kazi nzuri,na maisha yake mpaka sasa bado miziki yake ndio hiyo ,starehe kwake hataki kuacha wala kupunguza.
Niliamini atabadilika ingawa nilikuwa nakwazika sana kuwa nae alinifundisha kunywa Pombe ,Ok nikawa mnywaji mzuri na ili niwe nae Kimapenzi niliona ninywe kwanza ndio nakuwa huru na hayo ndio yakawa maisha yangu..Tuliendelea na mahusiano ya muda mrefu hatimaye nilianza kumzoealakini si kumpenda ,
Tukiwa tayari ndani ya mahusiano nilishika mimba na tukakubaliana kuanza kukaa pamoja ,taratibu za mahali zilifanyika na nikahama rasmi lakini kwa sababu jamaa alikuwa mtu wa starehe alikuwa akiniacha na kurudi usiku wa manane amelewa mara anitukane na sikuona kama alikuwa ananithamini na hali yangu ya ujauzito chuki moyoni ikawa inazidi siku hadi siku.
Ingawa kuna wakati nilikuwa naona kama ananipenda .Baada ya kujifungua tulianza taratibu za ndoa lakini moyoni mwangu nikijua kabisa mwanaume huyu sina mapenzi nae hata kidogo.Na nilikuwa najiuliza kwanini nafunga ndoa?
Ingawa kuna vitu vingine vilikuwa kama najifosi kufanya. Tulifunga ndoa takatifu nakuanza kuishi kama mke na mme ,na mungu akatujaalia kuongeza mtoto mwingine wa kiume lakini system yangu ni mpaka ninywe ndio nakuwa na hisia za kuwa na mme wangu.
Ndani ya ndoa yangu nimekuwa nikiishi kwa kujifanya nampenda mme wangu ingawa hizo hisia sijawahi kuzipata hata kidogo ,nimekuwa nikilia na kujutia maamuzi yangu sina furaha ,ni mnyonge ,for the sake of my kids ndio napata faraja kidogo.
Kila siku zinavyoenda nazidi kuchanganyikiwa mwenzenu nitaishi hivi mpaka lini nifanye nini ili nipate amani ya roho,? maana hii pretend sasa imenichosha. Nakosa usingizi usiku kucha.
Ni mengi ya kuelezea lakini kwa hapa moyo wangu unazidi kuwa mnyonge :angry:
Nisaidieni juu ya hili ,niombee
Mpaka leo una watoto wanne wa wanaume wawili tofauti;
Je ushauriwe ili ukazae na mwanaume wa tatu?
Ukiona vipi jipange tu, maisha yako na wanao hayatakushinda.
may dea ulifanya makosa mwanzo kabisa wa mahusiano yako ,hukuwa na fillings kabisa na matendo yake hukupenda na humpendi mpaka sasa ee mungu wangu dada tayari huyo ni mume wako wa ndoa ,nenda kanisani ombewa,na ww mwenyewe omba,hiyo ni spiritual husband linakusumbua na amini kupitia maombi mumeo atabadilika na ww utapata hisia za ajabu na kumpenda zaidi mumeo
pole sana anti kwa kuwa katika hali hiyo. Mimi ninachoweza kukuambia hiki kitu kipo na huwatokea watu wengi sana, chanzo chake kipo hivi wewe ulimpenda sana x wako na moyo wako uliuaminisha kuwa ni kweli una mpenda na ukaamini kuwa angeweza kuwa mume wako baadae pole kwa matokeo mabaya.
Ila napenda kukuambia kitu kimoja kwamba uruhusu moyo wako uyasahau yote yaliyopita kwani usipofanya hivyo nakwambia hautaweza kupata hisia zozote zakuwa na huyo mumeo kwani hadi sasa nikikuuliza kwanini unaumiza nafsi yako na kufikia kukosa usingizi, utakacho nijibu kuwa moyo wako na nafsi yako bado inakuaminisha kwamba yule aliyekupenda bado anakuhitaji sana na atarudi siku moja nakuambia hayo ndio mawazo yanayokujia na kukufanya ukose amani na hisia za mumeo kutoweka kabisa, kumbuka sasa upo katika ndoa hata kama haumpendi huyo mumeo navyofahamu mimi ni kwasababu tuu kuna hisia zinakuchochea x wako bado anakupenda kitu ambacho si cha kweli na kinabaki tuu ndoto na wewe umeshafungwa na ndoa tayari na huyo x hawezi kurudi hata akirudi hawezi kuwa na ww tena.
Nini cha kufanya.....
Jiulize kwanza wewe unahisi unachokitaka kitokee kinawezekana? Utagundua hakitawezekana kabisaa na kama nafsi yako ukiiruhusu kuwa hakitawezekana tena hasa kuwa na x wako tena basi utakuwa muda mzuri sana wa wewe kujitambua na kuamua sasa kuitengeneza ndoa yako ikawa imara.
Cha kwanza.
Acha pombe.,, wewe achana na kunywa pombe kabisa ili upate muda wakuangalia nini ukifanye utakapo weza kuacha pombe wewe unaweza ukamfanya na mumeo akaacha kabisa pombe.
Zungumzia maisha yenu na familia
nguzo na msingi mzuri mlio nao kwa sasa ni kuwekeza katika familia nikiwa na maana muwajengee watoto wenu msingi mzuri wa maisha yao kwenye elimu ili wao waje kuwa muunganiko wenu.
Anza kujishughulisha wewe kwanza.
Mwanamke anauwezo mkubwa sana wa kumbadili mwanaume. Hebu fikiria kama mumeo anarudi nyumbani kalewa anakukuta na wewe umelewa unadhani utakuwa na hisia na mumeo au yeye sanasana mnapigana mnatapika na kuchafua hata maramoja huwezi kupata hisia na utahisi ndoa ina kutesa kumbe wewe ndio chanzo cha kujitesa mwenyewe hilo ni tatizo lako wewe ndio chanzo cha kujitesa.
Ninachoweza kukwambia kwa sasa wewe ndio chachu ya kumbadili mumeo na akakupenda na wewe uka mpenda sana na mkajenga familia bora na yenye upendo na asijekudanganya mtu kuwa eti wewe ulimpenda fulani huwezi tena penda mtu mwingine noooooooo mapenzi huanzia popote pale hata kanisani msikitini kwenye gari na moyo huweza kutengeneza upya kama utauruhusu kufanya hivyo nakutakia kila la kheri
Poleni na majukumu ya kila siku wana JF, ikiwa ni mara yangu ya kwanza kuweka post, nahitaji msaada sana kutoka kwenu wazoefu kwenye ndoa, wana dini kimaombi zaidi .
Mimi ni mama wa watoto wawili, nimefunga ndoa miaka saba iliyopita, mwanzo kabisa maisha yangu ya mahusiano hayakuwa mazuri hata kidogo, first of all niliwahi kubakwa nikiwa na umri wa miaka 15, baada ya hapo niliishi maisha ya tabu sana mpaka nilipokuwa mkubwa na kuweza kujitambua.
Nillianza maisha ya mahusiano nikiwa na miaka 21 na mwanaume niliyetokea kumpenda na kuamini yeye ndio atakayenifuta machozi na huzuni zangu.
Mambo hayakuwa hivyo kwani miaka miatatu ya mahusiano yetu alienda oversizi na kuniacha na pia kuamua kukata mawasiliano kabisa. Nilibaki na kovu na maumivu niliyokosa tiba. Nilimtafuta bila mafanikio na kuamua kumove on na maisha yangu,ingawa ilikuwa ni ngumu sana.
View attachment 169831
Baada ya hapo nilikutana na mwamaume ambaye sikujua kama ni kweli nampenda kwani siku zote nilipokuwa nae nilikuwa namuwaza X wangu aliyeniacha bila kusema neno lolote.
Mwanaume huyu mwanzo sikumuelewa kabisa kwanza alikuwa mgomvi na mkorofi kwa watu dakika mbili alishabadirika haeleweki kama kinyonga ,police kwake ilikuwa ni kama nyumbani.
Nyimbo zake mara nyingi zilikuwa ni za kina Tupac ,Snopy D na wale aina ya magang star Ingawa alikuwa msomi na kazi nzuri,na maisha yake mpaka sasa bado miziki yake ndio hiyo ,starehe kwake hataki kuacha wala kupunguza.
Niliamini atabadilika ingawa nilikuwa nakwazika sana kuwa nae alinifundisha kunywa Pombe ,Ok nikawa mnywaji mzuri na ili niwe nae Kimapenzi niliona ninywe kwanza ndio nakuwa huru na hayo ndio yakawa maisha yangu..Tuliendelea na mahusiano ya muda mrefu hatimaye nilianza kumzoealakini si kumpenda ,
Tukiwa tayari ndani ya mahusiano nilishika mimba na tukakubaliana kuanza kukaa pamoja ,taratibu za mahali zilifanyika na nikahama rasmi lakini kwa sababu jamaa alikuwa mtu wa starehe alikuwa akiniacha na kurudi usiku wa manane amelewa mara anitukane na sikuona kama alikuwa ananithamini na hali yangu ya ujauzito chuki moyoni ikawa inazidi siku hadi siku.
Ingawa kuna wakati nilikuwa naona kama ananipenda .Baada ya kujifungua tulianza taratibu za ndoa lakini moyoni mwangu nikijua kabisa mwanaume huyu sina mapenzi nae hata kidogo.Na nilikuwa najiuliza kwanini nafunga ndoa?
Ingawa kuna vitu vingine vilikuwa kama najifosi kufanya. Tulifunga ndoa takatifu nakuanza kuishi kama mke na mme ,na mungu akatujaalia kuongeza mtoto mwingine wa kiume lakini system yangu ni mpaka ninywe ndio nakuwa na hisia za kuwa na mme wangu.
Ndani ya ndoa yangu nimekuwa nikiishi kwa kujifanya nampenda mme wangu ingawa hizo hisia sijawahi kuzipata hata kidogo ,nimekuwa nikilia na kujutia maamuzi yangu sina furaha ,ni mnyonge ,for the sake of my kids ndio napata faraja kidogo.
Kila siku zinavyoenda nazidi kuchanganyikiwa mwenzenu nitaishi hivi mpaka lini nifanye nini ili nipate amani ya roho,? maana hii pretend sasa imenichosha. Nakosa usingizi usiku kucha.
Ni mengi ya kuelezea lakini kwa hapa moyo wangu unazidi kuwa mnyonge :angry:
Nisaidieni juu ya hili ,niombee
Hapa naona mtihani
ha why ?